Nimejaribu kupitia hoja za bwana JF, pamoja na kuangalia maelezo ya bwana Mohammed Said,pia nimekisoma kitabu cha bwana Mohamed Said,(MAISHA NA NYAKATI ZA ABDULWAHID SYKES 1924-1968) nilichokiona mimi,nimeona hoja za msingi ambazo bwana Mohamed Said amesimamia na katika hiki kitabu chake utangundua mambo mengi juu ya udhaifu wa hoistoria ya Tanganyika.Pamoja na hayo yote bwana JF anaonekana ni mtu asieweza kutoa hoja kwani kila jambo yeye analifananisha na waislam wa Somalia,nataka nimsaidie kitu kwamba kuna tofauti ya muislam na uislam, kama vile tunavyoona baadhi ya makanisa Marekani yakiruhusu ushoga na kufungisha ndoa mashoga,mimi naamini hili ni matakwa yao wala halifungamani na mafundisho ya kikristo, na hatuwezi kwamba hapa napo wanaruhusu ufedhuli kama huo,kwa maana hiyo kama bwana JF hajui chanzo cha migogoro ya watu wa Somalia ni vizuri atafute ukweli wa chanzo cha machafuko ya Somalia,then ndio aweze kutoa mifano hai inayolandana....
Kwanza kabisa niseme najibu kama Nguruvi kwasababu sijui bwana JF ni nani. JF inawachama zaidi 50,000.
Umesema vizuri sana kuwa kuna Uislam na Waislam. Waislam wanaweza kuwa waumini au waislam kama jina.
Bwana Barubaru ana kauli yake ninayoipenda sana. Si kila mwislam ni muumini lakini kila muumini ni mwislam.
Kwa mantiki yako Mohamed Said ni Mwislam lakini si kila asemacho ni Uislam. Sheikh Amir alikuwa Mwislam kwahiyo kama kulikuwa na tatizo ni Nyerere basi ni Amir na Nyerere na wala si ukristo na Uislam kama ulivyoanisha vema sana.
Na hakika tukushukuru sana baadhi yetu kwa kuliona hilo. Ndiyo maana tunasema kila siku kuwa Historia ya Tanganyika ni ya Watanganyika na wala si Waislam ingawa katika Utanganyika kuna waislam, wakristo, wasioamini na wapagani.
Sasa ukikubali kuwa kuna Uislam na Waislam basi utakubaliana nasi kuwa harakati za uhuru zilichangiwa na waislam na siyo Uislam kama ambavyo zilichangiwa na jamii nyingine.
Kuhusu Somalia, nadhani unakosa mantiki ya wachangiaji wengi. Suala la Mohamed ni kuwa Uislam unashambuliwa kwa kuwashambulia Waislam. That being the case, tunasema si kweli kwasababu hata kule ambako Uislam ni 99 au 100% bado kumekuwa na matatizo na hapa ni mfano wa Somalia.
Kwamba, wao baada ya kuwa waislam kwa zaidi ya 90% bado hilo halikufanikiwa kuwanunganisha kwasababu ndani yake hakuna Uislam kuna waislam ambao hawakuzingatia Uislam na hivyo kutafuta sababu zingine na kujigawa katika koo.
Kwa mukatadha huo wanaiangalia Somalia nje kama waislam, wakibaki wenyewe wanasahau Uislam wanakimbilia Koo zao na hapo ndipo hoja ya Uislam na Uumini inapoingia. Mimi binafsi nimefuatilia historia ya Somalia na utashangaa nikikuambia habari nyingi za Bosaso ambako ni mji unaofanana sana na Dar es Salaam.
Mohamed, naye kaanza hilo kwa kusema ni waislam. Halafu anawagwa waislam wa Dar es Salaam, kisha anamalizia waislam Wazulu, wanubi na Wamanyema. Ndio Maana hataki kumtaja Ali Ramadhani Mndengereko kwasababu anatumia kalam yake kwanza kama Mwislam kwa namna ile ile ya Somalia.
Halafu anasema wa Dar es Salaam kama wasomali wanavyosema wa Mogadishu, Baidoa na Bosaso. Halafu anasema wanubi, Wamanyema na Wazulu kama ambavyo wasomali wanasema wasengeli na wabaidoa. Ndio mantiki ya kuingia kwa hoja ya Somalia.
Ni kwasababu ulizotoa, Mohamed hana haki wala sababu ya yeye kuwa Uislam na Waislam,anayo haki ya kuwa muislam na uislam kama yeye na si kama jamii. Ni makosa kufikiri kuwa maandishi yake ambayo yamejaa upotoshaji wa kina na dhahiri ni maandishi ya waislam. Uislam unasimama kama dini ukiwa na miongozo yake na wala hauhitaji chapuo la mtu.
Endapo umesoma ''historia'' ya Mohamed na kujiridhisha sana kuwa ndiyo yenyewe, hiyo ni haki yako na wala hakuna mwenye haki ya kuhoji haki yako. Lakini basi haki yako ina mapaka, usitake kuaminisha wengine haki yako kama ndiyo haki ya watu wote.
Na hii ni fursa nzuri sana kwako kumfahamisha Mohamed kuwa anapoongea kama waislam ni makosa kwasababu ndani ya waislam kuna waislam na waumini sasa anaongelea kundi gani, kwa capacity gani aliyopewa na nani?
NB
**Usisahau kutafuta phrase na spelling for spinning**