Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Ni nukuu ndefu kidogo lakini isome ni muhimu:

Kisa Cha Julius Kambarage Nyerere, 1952

Mwaka wa1952 Julius Kambarage alikuja Dar es Salaam kama mwalimu katika St. Francisí College, Pugu. Nyerere alikuwa na Mwapachu huko Makerere na wakawa pomoja Tabora mwaka wa1945 na baadaye nchini Uingereza kwa masomo ya juu. Mwapachu na Nyerere walikaa bweni moja walipokuwa wanafunzi Makerere wakati ambapo Kasella Bantu na Nyerere walifundisha pamoja hapo Tabora.

Kasella Bantu alikuwa na msimamo usiotetereka katika kupinga ukoloni. Alijiuzulu kufundisha na kwenda Dar es Salaam kujiunga na Tanganyika Broadcasting Corporation (TBC). Inawezekana Nyerere kwa kufuatia harakati za TAA, alisikia habari za Abdulwahid kupitia kwa Mwapachu alipokuwa bado yuko Uingereza. Katika hotuba ya kuwaaga wazee wa Dar es Salaam, (wazee wa Kiislam waliomuunga mkono wakati wa kudai uhuru) aliyoitoa tarehe 5 Novemba, 1985 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Nyerere aliwaambia waliohudhuria kuwa Kasella Bantu ndiye aliyempeleka nyumbani kwa Abdulwahid na kumtambulisha.

Hii ilikuwa mara ya kwanza Nyerere kuzungumza hadharani kuhusu kufika kwake Dar es Salaam na ilikuwa mara yake ya kwanza kuihusisha hadharani historia yake, ya TANU na jina la Abdulwahid .[1]

Nyerere alikuwa mgeni kabisa mjini Dar es Salaam na kama ilivyokuwa mazoea, Kasella Bantu alimpeleka Nyerere kwa Abdulwahid kumtambulisha na vilevile akutane na watu wengine maarufu wa pale mjini. Mbali na Dossa Aziz aliyekutana na Nyerere kwa muda mfupi katika mkutano mkuu wa TAA Aprili 1946, Kasella Bantu mwenyewe na Denis Phombeah, hakuna mtu mwingine mbali ya hao hapo makao makuu ya TAA aliyewahi kusikia habari za Nyerere.

Abdulwahid, Nyerere, Ally, Dossa Aziz, Mhando, Rupia, Dunstan Omar na wengine walikuwa wakikutana kila Jumapili nyumbani kwa Dossa Aziz Congo Street au nyumbani kwa Abdulwahid, Stanley Street. Hizi ndizo zilikuwa baraza mbili ambazo wazalendo walikuwa wakikutana kujadili mustakabali wa Tanganyika.

Majadiliano ya siasa miongoni mwa vijana hawa sasa yalivuka kutoka manungíuniko ya ndani ya nchi na kuingia kujadili masuala ya kimataifa ya mlengo wa kushoto na hasa kuhusu kuwa na utawala wa Waafrika Tanganyika. Nyerere alimwona Abdulwahid kama mtu mwenye akili sana, asiye na choyo na mtu wa kupendeka. Abdulwahid alimuona Nyerere, kama mtu aliyeelimika sana na mwenye ustadi katika majadiliano.

Nyerere alipata nafasi ya kuifahamu dunia vizuri na kupata msimamo wa siasa kutokana na uhusiano wake na Fabian Society, wakati alipokuwa mwanafunzi Uingereza. Mijadala mizito sana ilijitokeza katika vile vikao vya kila Jumapili wakati akili na ujuzi wa siasa wa Abdulwahid vilipopambana na uhodari wa majadiliano wa Nyerere. Wakati ule Nyerere hakuwa na wa ujuzi wowote katika siasa ukimlinganisha na Abdulwahid. Wakati African Association Tabora kiliposhiriki katika mgomo wa mwaka 1947 Nyerere hakujihusisha na harakati zile za wafanyakazi ingawa yeye ndiye alikuwa katibu wa chama.

Kutokana na urafiki huu pakawa na kuheshimiana na mapenzi makubwa baina ya Abdulwahid na Nyerere. Kila Jumapili Nyerere alikuwa akisafiri kutoka Pugu hadi Dar es Salaam kuhudhuria baraza lile lililokuwa likijadili siasa za Tanganyika. Baada ya kikao, Dossa Aziz au Dunstan Omar alimrudisha Nyerere kwa gari hadi Pugu. Hivi ndivyo Nyerere alivyokuja kuingia ndani ya TAA makao makuu na hatimaye akaja kupendekezwa kugombea cheo cha juu kabisa cha uongozi wa chama mnamo Aprili, 1953.

Uongozi wa TAA ulimpendekeza Julius Nyerere ili kukiimarisha chama kwa kuwa na Waafrika wenye elimu ya juu ndani yake. Ilibakia kwa Nyerere kukubali au kukataa. Kujadili siasa haikuwa sawa na kuongoza chama kilichokusudia kunyakua madaraka kutoka kwa serikali ya kikoloni. Hivi vilikuwa ni vita dhidi ya ukoloni na ilibidi mtu ajitayarishe kwa lolote ambalo lingetokea.

Nyerere alikuwa mwalimu wa Kikatoliki aliyekuzwa katika makuzi ya kunyenyekea kanisa na serikali. Vilevile Nyerere alikuwa chini ya ulezi wa Father Richard Walsh, aliyempatia nafasi ya masomo Scotland. Inasemekana Father Walsh alikuwa na ëushawishi wa kutosha juu ya maisha na fikraí za Nyerere.[1]Alimlea Nyerere na akamsaidia kupata nafasi ya kusoma nje ya nchi.

Katika hali kama hii haikutarajiwa kwa Nyerere asimame kuipinga serikali. Kanisa lilimtarajia afanye kazi ya ualimu katika moja ya shule zake nchini Tanganyika. Nyerere alikuwa ndiyo kwanza amerudi kutoka masomoni Uingereza mwaka uliopita na alikuwa anataka kutulia aanze maisha. Vijana wenzake wa mjini aliowakuta katika siasa pale Dar es Salaam kama Abdulwahid na mdogo wake Ally, na Dossa Aziz walikuwa watu wenye uwezo wao na wakiishi ndani ya mji wao ukilinganisha na yeye mgeni, tena amekulia kijijini.

Nyerere alijua yeye akiwa Mkristo, kamwe hangeweza kujijengea nguvu ya siasa katika mazingira yale ya Dar es Salaam ya miaka ya 1950 ambako siasa zilitawaliwa na Waislam. Kwa sababu hii, Nyerere alisita kukubali shauri la kuongoza TAA.

Uongozi wa TAA ulitambua thamani ya elimu ya Nyerere na uwezo wake wa uongozi kwa chama na nchi yenyewe hapo baadaye. Abdulwahid pamoja na viongozi wenzake wa TAA waliamini kwamba kuwa na Mwafrika aliye na elimu ya juu kama rais wa chama kungeimarisha uongozi wa TAA na kutoa sura nzuri machoni mwa serikali ya kikoloni na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa uliokuwa ukitembela Tanganyika. Nyerere amenukuliwa kusema kuwa ilikuwa dhamira yake kufundisha kwa muda kisha aingie kwenye siasa.[1]Hatimaye Nyerere alishawishiwa kukubali kuchukua jukumu la kuongoza TAA.

Miaka mingi baada ya Tanganyika kupata uhuru, Abdulwahid aliulizwa kwa nini hakuliondoa jina lake kwenye ule uchaguzi wa mwaka 1953 ili kumpalilia njia Nyerere achukue uongozi bila kupingwa. Abdulwahid alijibu:

''Kulikuwa na upinzani mkubwa dhidi ya Nyerere wakati huo na baadhi ya wanachama ndani ya kamati yangu mwenyewe ya utendaji walikuwa wakinishinikiza nisikubali kushindwa hivi hivi. Nilikuwa mgombea niliyependwa na kuondoa jina langu kungevuruga uchaguzi. TAA kilikuwa chama cha kisiasa chenye nguvu kilichokuwa kikiamini katika uchaguzi wa kidemokrasia. Uongozi wa chama ulikuwa upatikane kwa ushindani wa uwezo na sifa njema za uongozi. Tulimchagua Nyerere kugombea kwa sababu tulikuwa na imani naye nami nilikuwa mmoja katika wale walioamua hivyo.''[1]
 

Mwalimu Nyerere alikuwa peke yake tu hana wenzake.
 
Kama hajaelewa hapa basi tena...sikio la kufa...

Vipi ndugu yangu nikutie katika orodha ya askari wakati wewe hukujiandikisha kuwa askari?

Wale waliojiandikisha kuwa askari wakatolewa katika orodha ya wapiganaji.

Nakuja kuandika orodha yao unadai niwaweke hata wale ambao hawakuwa askari.

Hii kweli ni haki?
 
Mwalimu Nyerere alikuwa peke yake tu hana wenzake.

Huyo ni Superman au Hercules.

Haitaji mtu.
Kaja ana fedha ana ofisi ana wanachama, kaitisha mkutano watu wakamchagua.

Kisha akasema, ''Sasa nifuateni tudai uhuru!''
Wote wakamfuata.

Tena huyo ni mtu mgeni mjini.
 

samahani mzee wangu kwa kunielewa vibaya.. Labda ni namna tu ya uandishi wangu
"wachagizaji" nilimaanisha kina mohamed Iyombe na Balozi waendeshaji wa kipindi kile cha mwangaza wa jamii. Pamoja na kina Bilal Majuva na suleiman filambi ambao mlikuwa nao studio.


"Ustadhi" kwani ilunga sio ustadhi uhuni wangu upo wapi?

"mtu hatari" ni kutokana na matamshi yake yaliyomo kwenye dvd mbalimbali kama kuchochea kuuliwa kwa mapadri na maaskofu na waislamu HIVI MTU HUYO labda alistahili jina gani?

By the way nisivuruge mjadala nisamehe mzee wangu endelea na darsa pamoja kujibu hoja za watu wengine.
 
Hayo yamepita ndugu yangu tundelee na majadiliano.

Hebu tia neno kuhusu TANU kuasisiwa Pugu tena na
Nyerere peke yake.

Kweli hii itawezekana vipi?
 
ndugu yangu, sio kila mzungu ni padre,

hivi unamfahamu anaeiendesha hiyo tovuti?

Fanya utafiti ummfahamu kisha njoo tuendelee na mjadala huu

tujuze basi anayoiendesha hiyo tovuti ikiwa wewe ni miongoni mwa wale wasemao kweli.
Eti tanu iliasisiwa pugu??

Mmmmmmh
 
Hayo yamepita ndugu yangu tundelee na majadiliano.

Hebu tia neno kuhusu TANU kuasisiwa Pugu tena na
Nyerere peke yake.

Kweli hii itawezekana vipi?
Mohamed,
Unajua na sote tunajua kwamba Mwalimu amefariki bila kuanzisha tovuti yake popote pale. Kwa hiyo unaposema tovuti ya baba wa taifa unamhusisha Mwalimu Nyerere moja kwa moja na yaliyomo katika tovuti hiyo. Nilidhani wewe ni mwana historia makini lakini kumbe unaweza kuyumbishwa na majungu?
 
Huyo ni Superman au Hercules.

Haitaji mtu.
Kaja ana fedha ana ofisi ana wanachama, kaitisha mkutano watu wakamchagua.

Kisha akasema, ''Sasa nifuateni tudai uhuru!''
Wote wakamfuata.

Tena huyo ni mtu mgeni mjini.

Ni wapi pale Mwalimu Nyerere alitoa hizo claims?
 
Hayo yamepita ndugu yangu tundelee na majadiliano.

Hebu tia neno kuhusu TANU kuasisiwa Pugu tena na
Nyerere peke yake.

Kweli hii itawezekana vipi?

Bw. Said naomba utuwekee nukuu yoyote iliyoko katika vitabu vya historia ambapo inasemwa au inadaiwa kuwa Nyerere alianzisha TANU akiwa PUGU tena peke yake. Au niulize kwa namna nyingine ni mahali gani historia imeandikwa kuwa Nyerere alianzisha TANU peke yake tena PUGU?
 
Kaka mtaje kwa faida ya wanaukumbi.

Ninachoweza kusema nikuwa, mwalimu Nyerere amefariki akiwa hana barua pepe, wale tovuti.

Hicho kinachotajwa kuwa ni tovuti ya Mwalimu Nyerere si kweli kuwa ni yake japokuwa ipo kwa jina lake,

Inaendeshwa na mtu mwenye uelewa mdogo juu ya Mwalimu ama mtu mwenye sababu zake kama alivyo Mohamed Said
 

Sawa tumekuelewa unachosema lakini bado ujamtaja huyo mtu mwenye uelewa mdogo.
 
Kinachonichekesha nikuwa tangu tuanze mjadala huu Mohamed Said amekuwa akitumia maandishi yake mwenyewe kama ushahidi wa hoja zetu, baada ya kuishiwa maandishi yake sasa amekimbilia kwenye viblogu vya mtaani nakuita ni tovuti ya Mwalimu Nyerere.

Inasikitisha sana kuona mwanahistoria anaesema anaheshimika ulaya na marekani anatumia ushahidi wa blogu ambayo hata mwenendesha blogu hiyo hajui nini anachokiandika.
 

Ukitafuta nukuu kwa maneno unayochagua na kutaka wewe kuwa mwenyewe nipe nukuu inayosema kadha wa kadha hutopata na ukitaka mfano mzuri search katika computer yako kwa maneno yaliyokuwa katika fikra yako.

Nimekuwekeeni nukuu kutoka tovuti ya Baba wa Taifa na hii nadhani ndiyo iliyokufanya uniulize swali hilo.Lakini ukiwa unataka kuthibitisha kuwa historia rasmi inataka ionekane kuwa Nyerere alianzisha TANU peke yake hebu anza na kitabu cha Kivukoni.

Nimeeleza hapa ukumbini kuwa mwaka wa 1987 jarida zima la Afrika Events lilikusanywa kwa sababu niliandika makala ''In Praise of Ancestors'' (March/April 1987) ambamo nilisema kuwa TANU iliasisiwa na Abdulwahid Sykes. Toleo lile zima lililotoka Uingereza lilikusanywa likachomwa moto.

Ushauri wangu kwako au kwenu msinitume mimi kukutafutieni vitu katika vitabu jitumeni wenyewe faida kubwa mtapata.
 

Bwana Nyerere kuwa makini sana unapozungumza na mimi.
Nakuomba pia nifanyie heshima katika lugha yako.

Mimi naweka hapa mambo ambayo nimeandika katika miaka
mingi ya utafiti na kwa hakika katika somo hili la historia ya uhuru
wa Tanganyika najichukulia mimi kama ''authority.''

Ikiwa unamjua msomi yeyote ambae anaijua historia hii kunishinda
ufahamishe ukumbi na maandishi yake apate kunukuliwa.

Kama nisemavyo wakati wote.
Mimi nimeingia humu si kwa nia ya kubishana ila kueleza yale yasiyofahamika
na wengi.

Hiyo tovuti si ya mtaani.
Tafadhali ipitie kisha ndiyo useme.

Ikiwa unaikana kuwa si ya Baba wa Taifa na haimuwakilishi tafadhali
ufahamishe ukumbi.
 

Mimi sikufahamu kuwa hiyo tovuti haina baraka na wahusika wakuu nikiamini kabisa kuwa imewekwa pale kwa niaba ya Baba wa Taifa.

Zaidi nimepata hata kuwaandikia kuhusu historia ya awali ya Nyerere kuwaambia kuwa hiyo walioweka si ya kweli na nikawaandikia historia kama ilivyokuwa.

Hawakunijibu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…