Kwa faida ya wanajamvi hebu tuwekee huo ushahidi wa Selasini.
Kitabu cha Abdul Sykes kinamsaidia Muislamu kujua ilmu inayoitwa Fiqhul Waaqiy (Fiqhi ya kujua kinachoendelea duniani au sehemu ambayo Muislamu yupo).
Ukitaka asli katika Sunnah basi Mtume salalahu alayhi wasallam aliwaelekeza sahaba zake waende Ethiopia na sio Yemen, Syria,Rome au popote pale bali aliwaelekeza waende Ethiopia kwa kuwa kulikuwa na Mfalme muadilifu, hii inakuonyesha kuwa Mtume salalahu alayhi wasallam alikuwa akijua Fiqh waaqiy! alikuwa akijua kitu gani kinachoendelea Bara Arabu na Duniani kiujumla.
Ndiyo maana karibu Ma-Sheikh wote wa kueleweka aidha watakuwa wanafuatilia habari zinazoendelea ulimwenguni au watakuwa na vijana wao wanaofuatilia na kuwapasha habari kila siku.
Hata kiakili tu sijui ni Aalimu gani huyo atakayejifungia kwake na vitabu vya dini tu bila ya kujua yanayoendelea duniani! aalimu wa namna hii atatoa vipi fatwa wakati hajui kinachoendelea mjini mwake?
Usishangae ukija kugundua kuwa wanawazuoni maarufu wa Kiislamu wameshakipitia hiki kitabu cha Abdu Sykes au kama bado basi ujue wakati wowote mwanazuoni atakayetaka kujua fiqh waaqiy ya Tanzania ataelekezwa kitabu hiki.
Nafikiri unajichezea mwenyewe. Rudia tena post yangu. Soma kwa makini kuhusu issue ya majina.
Wimana,
Usemalo linawezekana sana.
Halikadhalika unaweza ukampata Mngazija Mkristo.
Sideeq: Ahsanteni kwa mawazo yako and of course I understand them. Mtume ni Mtume. Alitabiri tunayoyaona including watu kushindana kujenga majengo marefu. Of course unajua sana source yake ya kauli. Mkewe Mtume Bi Aisha (ra) alibainisha kuwa maisha yake yalikuwa ni kurani. Kurani inakataza kutafuta wengine makosa, kusengenya na hata definition ya hivyo vyote mtume alivieleza. maishani mwake Hakuna mahali Mtume (saw) anadekeza waislamu walalamike badala ya kuongeza tija katika maisha yao.
Kwa bahati mbaya sasa zipo species za waislamu ambazo life kwao ni kujenga chuki na malalamiko katika nafsi za jumuiya kiislamu tuu. Ukiwaambia haya tufanye nini. HAMNA JIBU. Mimi bado I STAND BY MY STATEMENT kuwa kama awali hukujijenga kiimani usitarajie eti kitabu hiki ndicho kiwe mtaji wa taqwa yako.
Sideeq tusonge mbele kidogo; mwenye kitabu hiki ndio achangie kujibu hili swali. Kama kitabu hiki kimekuongezea taqwa (uchaji Mungu) yako tutajie specific page na kisa ambacho hivyo vimekuzidishia ucha Mungu wako kiasi kwamba sasa, mahudhurio yako msikitini ni bora, zaka unatoa, unasaidia yatima na wenye shida kuliko siku za nyuma katika maisha yako. Hapa itajwe pg# na kisa husika sio nani murtad au kunguni au mission educated. By the way hakuna aliyewahi kukataa kuwa wazee wa kiislamu walikuwa bega kwa bega na Julius, Lakini huwezi kuitumia hiyo ili upate uhalali wa kuwatukana baadhi ya watu kwa majina kama "mission educated" wakati unapotaja ya waislamu wenzio hutaji "madrassa educated" huu ni ubaguzi na unafiki.
Sideeq; Review ya Prof. Glassman (wa Northwestern University) kuhusu kitabu hiki ilishabandikwa hapa. Aliyoyaongea hopefully, uliyasoma. Please, kama hujaisoma dont attempt kujibu bila kuitafuta katika hizi threads. Kwa muktadha wa hiyo review, sasa wanajamvi walete page # (mmoja kwa mmoja) na kisa husika ili tujiridhishe kuwa yaliyomo hayapatikani kwingine kokote ILA kwenye kitabu hiki peke yake.
Nakushukuru kwa kutaja hijra ya Ethiopia/Eritria kama ushahidi kuwa waislamu walishafadhiliwa na wakiristo katika madhila yao. Umefanya vyema kwa sababu baadhi ya waislamu wanakaribia kuaminishwa na some campaigns kuwa wakiristo shughuli yao kubwa maishani ni kudhulumu waislamu tuu. Hizi kampeni hazijui kuwa majumbani mwetu wakiristo ni shangazi au mjomba au hata wazazi. Nakuomba angalua pata ujasiri wa kusema NO to this satanic hatred.
Sasa Sheikh, kwa heshima yako nakusihi ufute ile kauli yako kuhusu Mmanyema Mkristo, nimekuinyesha mama zangu, wajomba zangu na bibi zangu Wamanyema Wakristo.
Wimana,
Usemalo linawezekana sana.
Halikadhalika unaweza ukampata Mngazija Mkristo.
Nanren,
Ulikuwa unazungumza na Ritz lakini nami umenitaja.
Kwa kuwa umenitaja nami nitakujibu.
Hakika nimesema, ''Alhammdulilah hakuna Mmanyema Mkristo.''.....
/QUOTE]
Sheikh Said, ndio maana nimekutaka utuombe radhi kwa upotishaji wako wa makusudi unaoufanya kwa sababu ya udini uliokujaa.
Ritz
Kwanza hizo percentages nina wasi wasi nazo. Huwa mna kawaida ya kupika na kuleta data from your own imaginations halafu mnazifanya ni factual data. Hivi umeisha andika hapa, baadaye data za 92% na 8% zitaanza kuonekana kwenye alnuur, na baadaye kwenye toleo la nne la Moh Said ilhali umezitengeneza wewe chumbani kwako.
Uchache au uwingi watu wa dini fulani hau-define udini.
Mzee Mwinyi, Rais Shein sio wadini
Lakini wewe na Moh said, mnaqualify kuitwa wadini japo nyie wanne wote ni waislam.
Statement kama "alhamdullilah, I have never seen a christian manyema" ya Moh Said, ni statement inayoashiria udini.
Haya lete data za maana zaidi tujadili.
Winama,
Inawezekana pia wapo Wanyagatwa Wakristo.
Sasa nifute kwa ajili gani ingawa sijamuona Mnyagatwa
Mkristo.
Mtu mmoja anaundaje chama? Anachotaka kutuaminisha Mzee Mohamed ni kuwa AA ni mali ya Sykes; TAA ni mali ya Kleist; TANU ni mali ya Abdu! Hakuna siku wala saa mzee Mohamed atakiri kuwa RAIS wa KWANZA na pekee wa TANU alikuwa Mwalimu. Hasad mbaya sana hii sijui inatokana na Umanyema au UDINI wake.
Nanren,
Sina chuki na Nyerere wala na Ukristo.
Yote niliyoeleza hapa JF ni kweli kadri
ya ufahamu wangu.
Ikiwa unadhani nasukumwa na chuki hiyo
ni bahati mbaya sana.
gombesugu,
Poleni sana Allah ataafu Inshaa'Allah.
Maradhwi na mitihani ni yetu sote tumeumbiwa sisi binadamu.
Karibu sana mie napata chai ya maziwa ya ngamia na mkate wa chila na vipopoo!
Ritz,
Nini maoni yako kuhusu anayoyafanya Sheikh Ponda? Huyu bwana ni shujaa wako kama alivyo kwa Sheikh Mohamed Said ?
WildCard,
Genocides za Rwanda, Burundi, Zaire, Angola, Liberia, Sierra Leone, New Guinea, Uganda, Haiti, Zimbabwe.
Haya mauaji walisabisha Waislam?
Sijataja mauaji ya zamani ya vita vya kwanza na vya pili.
Mohamed ''mission educated'' ni tusi lakini si la moja kwa moja. Ni kama vile marhum Ditopile aliposema watu wanafundishwa kula chapati.Wickama,
Mwenye kitabu ni mie.
Sijapata popote kusema kuwa kitabu hiki ni mashaf.
Wala haijawa kusema "mission educated" ni tusi.
Laiti kungekuwa na tusi humo mhariri asingeliacha.
Ama nia ya kitabu changu ni kuiweka historia mahali pake.
Hilo nini Waislam wanafanya baada ya dhulma hilo wala
halihitaji kuulizwa kwani liko peupe.
Ikiwa kitabu kimekuchoma hili nililitegemea na halinishangazi.
Sheik Ponda kafanya nini? kwani kesha hukumiwa? au nawewe Lwakatware wa Chadema ni shujaa kwako kama alivyo Ponda kwa Waislamu?
Mnakasha unasaidia sana,mimi nimesoma nikashangazwa na maneno ya Mohamed, he is not Mohamed of yesterday. Mohamed has come to terms with majority that he is entitled to his own opinion not the facts.Kwa mara ya kwanza umesema kitu cha kweli kimantiki; kwa ufahamu wako unayoyasema ni ya 'kweli'. Siyo kwamba ni kweli kwa vile ndivyo ilivyokuwa bali ni kweli kwa kuwa wewe unaamini hivyo. Kwa vile hujawahi kuona Mmanyema Mkristu basi unaamini hakuna Wamanyema Wakristu. Na hivyo unaweza kusimama na kusema "hakuna Wamanyema Wakristu"! Si kwa sababu hakuna bali kwa sababu wewe hujawaona.
Your whole narrative is based on this kind flawed reasoning; what you don't know you assume it is not there. Na unawafundisha wengine kuwa hakipo kwa vile wewe hukuiamini au hukijui kuwa kipo. Siku hizi mbili tatu napitia vitabu vya Iliffe na kulinganisha na madai yako na nashangazwa ujasiri ulio nao wa kupotosha maandishi ya Iliffe kwa kuingiza 'sihasa' zako. Kuna vitu viko wazi sana hadi inakera kwanini upande huu mwingine umeving'ang'ania kuwa ni kweli.
Mzee Mwanakijiji. Kwa vile hujawahi kuona Mmanyema Mkristu basi unaamini hakuna Wamanyema Wakristu. Na hivyo unaweza kusimama na kusema "hakuna Wamanyema Wakristu"! Si kwa sababu hakuna bali kwa sababu wewe hujawaona.....[/QUOTE said:Mwanakijiji, nimeshamthibitishia kuwa Wamanyema Wakristu nami nimetokana na hao. Ingawa "amekubali" ila ameongeza kabila lingine ambalo silijui na nikamwambia watakuja wenyewe wenye hilo kabila.
Kwa mara ya kwanza umesema kitu cha kweli kimantiki; kwa ufahamu wako unayoyasema ni ya 'kweli'. Siyo kwamba ni kweli kwa vile ndivyo ilivyokuwa bali ni kweli kwa kuwa wewe unaamini hivyo. Kwa vile hujawahi kuona Mmanyema Mkristu basi unaamini hakuna Wamanyema Wakristu. Na hivyo unaweza kusimama na kusema "hakuna Wamanyema Wakristu"! Si kwa sababu hakuna bali kwa sababu wewe hujawaona.....