Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 17,005
- 20,425
- Thread starter
-
- #12,921
Hujaibadili, Bado inasomeka muasisi wa Taifa ni Julius K. Nyerere, Muasisi wa TANU ni Julius Nyerere,Wild Card,
Kama kubadilika ndiyo nishaibadili.
Leo historia ya TANU na Nyerere mwenyewe watu wanaisoma vingine.
Haya ndiyo mabadiliko yenyewe.
Mkuu dhuluma ipi mlodhulumiwa?Hayo maneno ungemwambia Joseph Selasini Mbunge wa Rombo Chadema.
Wapi mie nimewachukia Wakiristo acha kuniwekea maneno mdomoni dini yangu inanikataza kuwachukuia watu wa dini zingine kwani sikuwaumba mimi.
Mimi kuelezea dhulma tulizofanyiwa wewe tafsiri yako ni kuuchukia Wakiristo.
Hujaibadili, Bado inasomeka muasisi wa Taifa ni Julius K. Nyerere, Muasisi wa TANU ni Julius Nyerere,
Hilo linathibitishwa na kukaziwa na maamdishi yako pia hasa unaposema, Kadi namba Moja(1) ya TANU ni ya Julius K. Nyerere,
Vivyohivyo inazidi kukidhihirisha ukuu wa uasisi wa TAifa pale wewe mwenyewe katika maamdishi yako unaposema rais wa kwanza wa Tanganyika/Tanzania ni Julius Nyrerere.
Hilo halitafutika wala kuwa badiliko la kikemia au kiumbo ndugu yangu Mohamed Said.
Ngano zako zitasimama Kama ngano za Mohamed Said, kamwe hazitageuka kuwa historia ya kweli ya uhuru wetu.
Mohamed
Huhitaji kujua zaidi yaliyomo mwenye kitabu changu kiitwacho "Vita dhidi ya Ugaidi"?
wickama,
nadhani unajua kuwa sie wamanyema wawili uzito
wetu unatosha kuzamisha jahazi na kina kasulwa
ni ndugu zangu...
Sasa ile mie kusema "nilijua" sikukusudia wewe.
Nilikusudia wote watakaosoma kitabu changu.
Hili la uislam limerefushwa kuliko kusudio lenyewe
na baya zaidi ndio mwiba wenyewe.
Ama kuhusu yericko ulosema sawa tunawajibika kumtia
ghera na huo ndiyo utu.
Sheikh Mohammed Said,
Salaam sana.
Hapa pana mambo mengi mno yenye kuleta rabsha kiduchu na vichekesho vingi. Nafikiri unakumbuka ile bayana yangu ya awali kwako,sababu nilichelea kuingia mambo kama haya ya udini,kutaja majina na kuwaadhiri jamaa zetu toka family mbalimbali tunazozistahi na mikanganyiko mingi saana,na matokeo yake tupo nje kabisa na hii mada/shutuma dhiki yako.
Imekua kama mtego wa panya sasa,anangia alokuwamo na asokuwamo!ahaha!!
Nimecheka pasi kiasi na yale majibu ulotoa kuhusu hiyo habari ya mmanyema mkristo. Nafikiri Sheikh Mohammed labda kitambo hujenda tembea pale Ujiji kuona "mabadiliko". Mimi binafsi pia pana pahala kwingi nahitaji nikatupie jicho Insha Alaah penye uhai na maajaliwa.
Hii habari ya makabila, ama kwa hakika imenichekesha kiduchu hasa ulipotaja Wangazija Wakristo. Unajua pale Comoro siku hizi pana wale "Wangazija pori" ambao huenda pale "kununua baraza" na kujinasibu Ungazija pasi kiasi. Ukizungumza na Bwana Ahmed Rajab atakuchekesha zaidi juu ya habari hizi.
Nafikiri hata ndugu zetu wa kiZaramo zamani nao walikua na dasturi na ustaarabu kama huo wa kukaribisha "wabweshu" na kuita "udugu wa khiyari". Tena walikua wakifanza na sherehe kubwa mno siku ya kutimiza huo "udugu". Napenda saana tamaduni na mapenzi yalokuwapo zamani baina yetu.
Sijui lini utapata fursa tuwekee na habari za mapinduzi ya Zanzibar,hasa wale wamakonde wa Kipumbwi,Ushongo na Sakura walotumiwa kuua ndugu zetu na kumuweka madarakani yule Mnyasa alokuja Unguja mtoto wa mgongoni(yaleyale ya Musharaf kuja Pakistani mtoto wa mgongoni halafu kuwafanzia watu hadaa). Ndugu na jamaa zetu wengi walitolewa roho na yule dhalim.
Uncle yangu Commando Amour Dougheish,ndo alokua akamkamate yule Mnyasa toka pale Ikulu na kumpeleka pale Idara ya habari - Rahaleo, halafu atangaze kuwa nchi isharejeshwa na imo mikononi kwa wananchi wenyewe. Wallahi,lile jambo mpaka leo najuta halikufanikiwa.
Basi Insha Allah tuendelee na mnakasha.
Ahsanta.
mzee ms you have earned my deepest respect for this courage. Na kwa kweli this is maturity at its best. There are no enough words to describe it. Thank you.
Mimi ni mkristo lakini mpka leo nalaumu Marekani na vita hii na naipinga kwenda kutumia drones zao Pakistan, somalia Afghan na sehemu nyingine, hata juzi kwenye Boston Bombs niliwaonea huruma wamarekani na felt very bad for kid and those who lost thier lives and i got to think that what they went through is what Pakistan,somalia and other countries go through almost daily and to top up wamerikani wana wabomb na drone zao, i empathize with Iraq and Afghan people. But i have never looked at it as Muslims being oppressed, but i look at it as a Powerfull nation kuonea taifa dogo.
So huo ni udini when you look at it as Muslims being oppressed.
Watu gani hao wanaoisoma historia ya TANU, Tanganyika vingine. Unaweza kuendelea kujifariji kwa namna hiyo hadi mwisho wa maisha yako hapa duniani. Kitabu kile hata kama kingeandikwa na Abdu kwa namna ulivyokiandika bado kingebaki ni simulizi tu. Kitabu kipo tangu 1998 kimekuja kuwa gumzo humu JF mwaka 2013! Historia ya TANU haiwezi kuokotwa kwenye vikabrasha vya familia moja. Mtu mmoja akajifungia chumbani kwa mkewe, akaibuka na historia ya sisi kuamini kama mazuzu.Wild Card,Kama kubadilika ndiyo nishaibadili.Leo historia ya TANU na Nyerere mwenyewe watu wanaisoma vingine.Haya ndiyo mabadiliko yenyewe.
Muheshimiwa Mwanakijiji
hivi ndugu yangu wewe binafsi kwa mtazamo wako unakubaliana na mawazo ya baadhi ya wanajamvi hapa,watanzania kadhaa pamoja na Serikali hapo kuwa Waislam wana matatizo na dhiki kadhaa za kihistoria na inalazim Serikali iwatengee sikio japo la upande mmoja kujua kinachowasibu?
Sijui kama unakubaliana na ile kauli ya Bwana W. Mkapa ya kuthibitisha na kuwa wengi kati ya Waislam wana matatizo na dhiki zilizosababishwa na kurithiwa toka kwa wakoloni?
Unakubaliana na mimi kuwa Sheikh Mohammed Said alipoandika Historia ya Tanu/Tanganyika, hakuwa na madhumuni potofu au kukusudia uchochezi kama mnavyodai bali labda ni khitilafu kiduchu na dhahama tu za kitaaluma na kiuandishi na pia hakukusudia nia dhalili dhidi ya nchi yake na wananchi wenzie.
Nashukuru, na niwie radhi kama kuna masuala nimekuuliza tena. Najaribu kuangalia kama mpaka hapa mnakasha ulipofikia labda kuna majambo umeyaona na umepata kubadili fikra zako japo kiduchu.
Ahsanta.
Gombesugu,
Hayo hapo chini ni baadhi ya maneno niliyoandika katika pitio la kitabu ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru'' cha Dk. Harith Ghassany:Kwakipindi kirefu historia ya mapinduzi ya Zanzibarilikuwa ni ile historia rasmi ambayo imeathiri historia nyingi Afrika. Viongoziwa Afrika wanapenda ile historia itakayowakweza na kuwaonyesha wao katikamwanga wa kupendeza.
Vinginevyo historia hiyohaitakiwi.
Wazalendo wenyewe hawakuwa na hamu ya kuandika historia hii na watuwa nje walioandika historia ya mapinduzi ya Zanzibar hawakupata kuifanyia hakihistoria ya Zanzibar labda kwa ugeni wao na kwa kuyaamini maelezo yaliyokuwa"wazi" kwa wakati ule, mfano mkubwa ukiwa ni kule kuamini kuwa mapinduzi yaZanzibar yalipangwa na makomredi wa Umma Party. Hapajakuwapo udanganyifu mkubwa katika uandishi nautafiti kama huu.
Dkt Ghassany amekiweka chanouwanjani bila kawa. Akizungumza na Abdushakur Aboud wa Sauti ya Amerika DktGhassany amesema kuwa historia ya Zanzibar ni historia ya kujijuwa maisha yakeakiwa mjukuu wa babu wa mababu Muomani na mabibi wa Kimanyema na Kimwera –mchanganyiko wa damu ya Kiarabu na Kiafrika.
Hii kwa hakika ndiyo historia yawananchi wa Zanzibar.
Ni tabu sana kumpata huyo Muarabu Zanzibar kila umuonaeMuarabu basi ana mjomba na shangazi Mwafrika.
Maadui wa Zanzibar wakiweka mkazo katika ubaguzi warangi na kuwafitinisha Wazanzibari. Ukweli huu ndiyo chanzo cha matatizo yoteyaliyoikumba Zanzibartoka vyama vya siasa vilipoanza katika miaka 1950 na matatizo yaliyosababishamauaji ya mwisho yakiwa mwaka 2001.Ilikuwakatika barza yetu ya kawaida ya kunywa kahawa na kula pweza huku tukijadilihistoria ya Tanzaniaambako siku moja Mzee Mkwawa alinambia, "Mohamed nataka nikuambie kitu.
Unajuamimi nimehusika sana katika mapinduzi ya Zanzibar?"
NilimuangaliaMzee Mkwawa kwa makini.
Fikra yangu ya utafiti na uandishi ishashtuka haipo tenausingizini.
Mzee Mkwawa aliendelea, "Mimi ndiye niliyekuwa nikiwavushaWamakonde kutoka Kipumbwi kwenda Zanzibarkuipigia kura ASP na wakati wa mapinduzi mie ndiye niliyewavusha Wamakondekwenda kuipindua serikali ya Jamshid."
Sasa moyo wangu ukaanza kudunda kwanguvu.
Naisemesha nafsi yangu, "Huyu mzee anajua uzito wa maneno haya?"
Tuishiehapa.
Watu gani hao wanaoisoma historia ya TANU, Tanganyika vingine. Unaweza kuendelea kujifariji kwa namna hiyo hadi mwisho wa maisha yako hapa duniani. Kitabu kile hata kama kingeandikwa na Abdu kwa namna ulivyokiandika bado kingebaki ni simulizi tu. Kitabu kipo tangu 1998 kimekuja kuwa gumzo humu JF mwaka 2013! Historia ya TANU haiwezi kuokotwa kwenye
vikabrasha vya familia moja. Mtu mmoja akajifungia
chumbani kwa mkewe, akaibuka na historia ya sisi kuamini
kama mazuzu.
TANU imeundwa na kuasisiwa mwaka 1954. Mwalimu amekuwa kinara wake tangu mwaka huo hadi 1977. Miaka 23 mfululizo. Abdu hakuwahi kuwa kiongozi mkuu wa TANU wakati wowote ule katika uhai wake. Kama kuna ukweli mwingine kuliko huu basi hiyo haitakuwa TANU labda TAA. Historia ni lazima iambatane na tarehe na matukio halisi sio mambo ya kufikirika kama ilivyo kwenye DINI na misahafu yake. Hakuna kinachoweza kuibadili historia.Yericko,Hayo yote uliyosema ni kweli kabisa na wala mimi sijapinga hilo.Tatizo ni kuwa huwezi kuishia hapo.Utakaposoma sasa historia ya TANU ndipo hapo utakapokutanana Abdu Sykes, ndipo hapo utakapokutana na Chief David KidahaMakwaia.Vipi unakutanananao?Kitabu kitakuambia kuwa kabla ya Abdu kuonana na Nyerere 1952fikra ya kumpata kiongozi mpya wa TAA na kisha kuunda TANUalizungumza na Chief Kidaha 1950.Akili ya msomaji akifika hapo itamuuliza ehe ikawaje Abdu na ChiefKidaha?Hapo anasonga na kurasa za kitabu anasoma yale ambayo kwake nimageni kabisa - ni mambo mapya.Ninaposema historia imebadilika mabadiliko yeynyewe ndiyo haya.Si kama tutabadilisha uasisi wa Nyerere katika ujamaa na vijiji vyakekuasisi CCM nk. nk.Historia hii ya vijiji vya ujamaa hakika hana mpinzani ila hii ya kuasisiTANU ndiyo panapo maneno ya kuzungumza.
Tujihadhar jaman na hizi thread kwani hazijengi zaidi ya kubomoa,
Ila hapo kwenye NECTA ninaweza nikaamini maana nakumbuka uzembe uliopitiliza wa NECTA uliofanywa mwaka jana ktk mitihani ya Islamic knowledge, Hapo sina ubishi kwa kile alichokieleza mzee Mohamed Said na wadau wengine.
Watu gani hao wanaoisoma historia ya TANU, Tanganyika vingine. Unaweza kuendelea kujifariji kwa namna hiyo hadi mwisho wa maisha yako hapa duniani. Kitabu kile hata kama kingeandikwa na Abdu kwa namna ulivyokiandika bado kingebaki ni simulizi tu. Kitabu kipo tangu 1998 kimekuja kuwa gumzo humu JF mwaka 2013! Historia ya TANU haiwezi kuokotwa kwenye vikabrasha vya familia moja. Mtu mmoja akajifungia chumbani kwa mkewe, akaibuka na historia ya sisi kuamini kama mazuzu.
Wild Card,
Sina ugomvi na fikra yako.
Lakini nitakueleza jambo moja.
Kitabu hiki kimependwa sana.
TANU imeundwa na kuasisiwa mwaka 1954. Mwalimu amekuwa kinara wake tangu mwaka huo hadi 1977. Miaka 23 mfululizo. Abdu hakuwahi kuwa kiongozi mkuu wa TANU wakati wowote ule katika uhai wake. Kama kuna ukweli mwingine kuliko huu basi hiyo haitakuwa TANU labda TAA. Historia ni lazima iambatane na tarehe na matukio halisi sio mambo ya kufikirika kama ilivyo kwenye DINI na misahafu yake. Hakuna kinachoweza kuibadili historia.