Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Na kweli hili hata mimi nimeliona, sasa hivi anakuwa mwangalifu sana. Lakini nimejifunza kitu, si vizuri
kukaa kila mara na watu wanaokusifu tu au kukusikiliza bila kuhoji....Unaishia kuwa arrogant.

Na ukishakuwa arrogant na ukawa na darsa la aina hiyo wanameza kila kitu, kama Warioba hakuwa
anafahamika kabla ya kuwa Waziri Mkuu watu wanameza, Kigoma Malima alianzisha namba za Mtihani
watu wanameza
, Nyerere aliingia Dar 50's watu wanameza, Utafiti uliopinda Watu wanameza n.k n.k.

BTW: Ameshakuweka kwenye "shit" list yake
?

nafikiri kama utatumia busara kidogo na kutazama ni lini namba zilianza kutumika katika mitihani ya Tanzania na kuachana na kuandika majina na kutazama wakti huo nani alikuwa waziri wa Ilmu utaligundua hilo. Kwani Hata wizara ya ilmu ya Tanzania watakusaidia hilo wala haliitaji mjadala. Ila kwa mimi nakwambia ilikuwa kipindi Prof malima akiwa waziri wa Ilmu. Fanya uchunguzi utaligundua hilo.

Suala la Warioba naye yupo hai unaweza ukamuuliza tu kwani miongoni mwa aliosoma nao darasa moja Chuo kikuu (marhum Brigadia mang'enya ) mimi niliwahi kumuuliza kuhusu huyo hakuwa na jipya zaidi ya ukabila tu ulimbeba kama ilivyokuwa kwa akina Nyirabu na wengine kutoka mkoa huo enzi za JKN.
 
Mohamed Said
Nakusoma, mzee wetu. Inawezekana kabisa huna chuki na wala hukuwa na nia ya kupandikiza chuki. Lakini ukweli uliopo ni kuwa wafuasi wako wanatumia mafundisho yako na ku-develop hatred. Kila kitu sasa hivi ni kuangalia majina tu. Hassan vs Peter!

Nafikiri unafikiri tofauti.

Zinazojitokeza hapa ni chuki dhahir kabisa za watu wa upande wa pili wanaoamini kuwa JKN hawezi kufanya kosa lolote na hakufanya makosa jambo ambalo si kweli. Tunaamini kama mwanadamu amefanya mengi mazuri na mabaya pia.

sasa wengu huko Tanzania wamejikita kuandika mazuri ya JKN ikiwa pamoja na kutia hata chumvi sasa akitokea mtu kuandika mabaya ya JKN ndio hapo unaona kinachodhihiri hapa.

Huu ni mpasuko huko Tanzania na ulipandwa zamani. sasa hivi kila kitu kinatazamwa kwanza kwa imani kabla kujua uhalisia.

 
mohamed said ni mdini endelevu

Ndugu zangu tuwe nadesturi yakuukubaki ukweli hata kama unauma kwani itatusaidia kujua mengi.Mohamedi said kasema kweli lakini Yericko Nyerere analet mambo yasomali tofauuuuuti kabisa.Tukikwambia kwanini somalia iko vile hutakubali kama kawaida yako.Ukitaka somali iwe shwali waruhusu waanzishe sheria za kiislam jambo ambalo U.S.A hawalitaki wakihofu kua maficho yamagaidi.Hapo sasa mambo ndo kama unavyoona.
 
Wickama,

Huyu Alhaji Mzee Shekue wa barabara ya 12 nakumbuka mwaka jana walikuwa taasisi moja na mzee wangu mmoja kwenye safari ya hijja.

Nimefurahi kusikia ni mmoja wa wadau wa Zahrau, muda mrefu sijafika Tanga vipi Shamsi maarifa nao wanaendeleaje na harakati za kujenga shule.
Ukimtaja Mze Shekue unanikumbusha mbaali sana enzi za akina Sheikh Abdullah Ayub na nduguye Mohamed Ayub.
 
Kadogoo,

Mbunge wa Chadema Joseph Roman Selasini Shayo kutoka Rombo ametetoa shutuma nzito bungeni kuwa UDOM kuna udini.

Kauli hiyo inawalenga Prof Idris Kikula na Prof Shaban Mlacha kwa sababu wao ni Waislam.

Nilipenda majibu ya Juma Nkamia alimwambia mkuu wa chuo angekuwa Liymo wala usingesema hayo maneno ya mambo ya udini.

Halafu kuna watu wanasema Waislama hawabaguliwi Ebo!!

Wanafiki wote kimya.
Mimi nafikiri wenzenu walitakiwa waangalie Chuo kikuu chochote hakiendeshwi na watu wawili tu kuna safu za juu za uongozi kama mkuu wa utawala , mkuu wa taaluma na wengine ambao chuo kidogo wanakuwa 7 lakin kama UDOM nafikiri watakuwa zaidi ya 10.

sasa angalieni katika hao viongozi 10 wa juu kabisa wa chuo hicho waislam ni wangapi? ndio mseme kama kuna Udini au vipi?.

naombeni jibu kwa mnaokijua chuo hicho na safu yake ya uongozi





 


But Dont get me wrong, just t clarify

I do not condone any violent au terrorist act kwa jamii au watu wowote, in the name of anything.


Violence is violence, act of terror is act of terror, it has no justification whatsoever.



Mkuu

I know, Its not about supporting its about using brain to know that what Americans are doing is not right at all, even terrorist are divided,those in Afghanistan are bad but those in Iran are good terrorist.

Violence is Violence hamna wakifanya Ireland (IRA)wanatizamwa kwa jicho jengine lakini wengine wanapigania dini.

heheheh funny
 
Ngoma inogilee,sindimba imepamba moto..
Mwanakiijiji amehamia kwenye makabila sasa..
Kweli mfa maji haachi kutapa tapa,enhe sasa atueleze takwimu hizo uwiano wake ukoje?
Wapi kapata takwimu hizo,au ndio histohisia zake?
 
Suala la Warioba naye yupo hai unaweza ukamuuliza tu kwani miongoni mwa aliosoma nao darasa moja Chuo kikuu (marhum Brigadia mang'enya ) mimi niliwahi kumuuliza kuhusu huyo hakuwa na jipya zaidi ya ukabila tu ulimbeba kama ilivyokuwa kwa akina Nyirabu na wengine kutoka mkoa huo enzi za JKN.
Ahli yangu Barubaru! ushabiki usikuondoe katika hali ya fikra au usikufanye ukawa dhalili kwasababu tu ukisema Mohamed kakosea utakuwa umekufur.

Hili suala la Warioba nadhani hukusoma au hukuelewa Mohamed alisema nini na alilenga nini.
Kwa kukumbusha Mo alisema kuwa ni wakati wa mwinyi ambapo Nyerere aliingilia kati uandaaji wa baraza la mawaziri. Aliwaacha watu wenye sifa na kumchukua Warioba ''mtu aliyekuwa hana credential yoyote na ASIYEJULIKANA'' kuwa waziri mkuu.

Tulimuonyesha Bio ya Warioba na kukumbusha tu huyu aliwahi kuwa Attorney wa serikali na AG.
Unafahamu kuwa AG ni kati ya vyeo ambavyo mtu huwezi kukosa kuvielewa.
AG anaingia bungeni kwa wadhifa wake na ndiye mshauri wa kisheria wa serikali bungeni achilia mbali huko kazini kwake.

Warioba alikuwa mbunge na wakati anachaguliwa alikuwa Waziri wa sheria. Narudia waziri wa sheria.
Mohamed anaposema Warioba alikuwa hajulikani ni tusi, dhararu, dhalili kwa warioba na kwake kama mwandishi.

Mohamed anasema alikuwa hajulikani katika cabinet! hivi kweli waziri wa sheria anaweza kufanya kazi zake katika viunga vya minazi au kwenye vijiwe vya pombe na chai. Real!
Nawe unasimama kabisa bila aibu hapa jamii forum kutetea upotoshaji huu wa kina unaostahili kukemewa na watu wote wenye akili.

Unaweza kusema Warioba umesoma naye na hakuwa na lolote amebebwa. Angalia kama hajavuka mipaka?
Nadhani umekolea chuki kiasi cha kuona busara kama najisi. Haifai ndugu yangu, rudisha moyo.

Na zaidi ukweli ulipowekwa hadhwran Mohamed hajasema na nakuhakikisha hatasema lolote kwasasababu ukweli unasiamama wenyewe na anauona. By the way Mzee Warioba yupo hai na Mohamed huwa haongei na watu tulio nao, anasubiri muda mufaka kwake.....
 
Ndugu zangu tuwe nadesturi yakuukubaki ukweli hata kama unauma kwani itatusaidia kujua mengi.Mohamedi said kasema kweli lakini Yericko Nyerere analet mambo yasomali tofauuuuuti kabisa.Tukikwambia kwanini somalia iko vile hutakubali kama kawaida yako.Ukitaka somali iwe shwali waruhusu waanzishe sheria za kiislam jambo ambalo U.S.A hawalitaki wakihofu kua maficho yamagaidi.Hapo sasa mambo ndo kama unavyoona.



Mkuu

Nilisoma zile point za kwanini somali kwanini somali nikashangaa sikujua nini kinafananishwa Alshabab waliposhika nchi miaka kadhaa tuu nchi ikatulia lakini Americans wakaaanza zile chokochoko zao zile...............
 
Ninaposema historia imebadilika mabadiliko yeynyewe ndiyo haya.
Si kama tutabadilisha uasisi wa Nyerere katika ujamaa na vijiji vyake
kuasisi CCM nk. nk.Historia hii ya vijiji vya ujamaa hakika hana mpinzani ila hii ya kuasisi
TANU ndiyo panapo maneno ya kuzungumza.
Na hakika historia haiwezi kubadilika kuwa yeye alikuwa kiongozi wa kwanza wa TANU na alikuwa Rais wa Kwanza wa Tanganyika.
Historia haiwezi kubadilika kuwa A.Sykes aliwahi kuwa rais wa TANU au rais wa Tanganyika.
Historia haiwezi kubadilika kuwa K.Sykes alikuwa katibu wa AA na Cecil Matola alikuwa Rais wa AA.

Ndio uzuri wa historia, inatoa hukumu bila upendeleo au kificho. Hata kama itafinyangwa vipi bado kuna sehemu historia itamsota kidole anayeifinyanga.
 
Mohamed Said,

Unakijua kisa cha chifu Adam Sapi na Mwalimu Nyerere mwaka 1958 kabla ya uhuru?

Je kisa cha baada ya kuachishwa uspika na kuteuliwa kuwa waziri wa wanyama/maliasili?

Ikiwa wavijua visa hivyo kuna hoja muhimu nataka tuijenge hapo!
 
Ukimtaja Mze Shekue unanikumbusha mbaali sana enzi za akina Sheikh Abdullah Ayub na nduguye Mohamed Ayub.

Shukran sana ndugu yangu Barubaru. Mzee Shekue, Mwinshashi, na wengine 6 tunajitahidi kuunda taasisi inayolenga kuboresha elimu na maendeleo ya jamii ya hapa kwetu. Ipo nia njema sana kutoka vijana wa Tanga walioko ma-ofisini na hata nje ya nchi. Lakini hii haituisubiri itatukuta na infact ndiyo iliyodumaza watu wetu kujitoa kwenye mkasa huu. Kila aliyekuja toka alikotoka, aliahidi, akirudi tuu mamboo safiii wazee hawa wakasubiri hadi ujana umeisha. Hii tumeikataa na kusema tuanze bila ahadi za watu. Nime notice tatizo kubwa ni kutofuatilia mambo au kuyaogopa kuwa bila fulani kuwapo tutakwama ofisi ile na wakati mwingine kutoyapa uzito stahiki. Huu uoga ukiondoshwa watu wataamka sana. Tatizo lingine ni kutopangilia mambo kwa daraja linalostahiki. Barubaru kuna vyuo hapa vya kiislamu (sitavitaja) nimeshuhudia mwanafunzi bora wa mwaka na nidhamu (tena graduand) anayehitimu kozi ya ualimu anapewa zawadi ya kijipakti cha tende (mjini zinauzwa 1000/) hata cheti cha kutambua umahiri wake hakuna. Nilizuia machozi. Hakuna chuo cha kikiristo kinachoweza kufanya mzaha kama huu (mwanafunzi bora apewe kipande cha skonzi!).

Tukirudi kwenye kundi la mzee Shekue, nilipewa jukumu la ku-draft katiba na namshukuru Mungu tumefanikiwa. Tupo kwenye process ya registration. Hii shughuli imezorota kwa sasa kwa vile niko masomoni na japo niliwaomba waendelee, wao wameamua kunisubiri nimalize kozi tusonge mbele. Ila harakati zipo.

Ritz, Zahrau panaendelea vizuri Masheikh Mbwana na hata Akerballi ni jirani yangu. Mwaka jana tuliondoka na convoy kubwa sana kuelekea Moshi, huko walikuja matawi ya nchi nzima kuwatia nguvu na kuwasisimua wenzetu wa Msikiti wa Pasua ndipo palisomwa maulid. Shamsi al Maarif inaendelea vizuri na afya ya Mudir Mohammed bin Bakar inazidi kuwa nzuri. Tunashukuru Mungu. Lushoto ndiko shughuli pevu, kuna Shule nyingi. Shule ya Soni Islamic hii ni ya wazazi wa pale Soni, wengine tunaipa tafu tuu. Tatizo liko kwenye quality ya waalimu na registration ya wanafunzi. Sio nzuri sana. Huwezi walaumu kwa vile nayajua mazingira waliyoanzia. Ila wanasonga mbele. Kwa sasa hata wavulana wana bweni.

Kwa assessment yangu mimi saidieni sana wilaya ya Handeni na Pangani. Mwenye nia njema na uwezo huko ndiko haswa kwa kulenga. Hali sio nzuri. Mkiniona wakati mwingine nakuwa mkali ni kwa sababu miji yote hiyo nimeitembea na huwa inaniuma sana nikihisi nguvukazi ya maana ikielezwa kusiko na tija. Lakini yote ni maisha. I hope nimewapa update ya mkoa huu.
 
Mohamed Said,

Unakijua kisa cha chifu Adam Sapi na Mwalimu Nyerere mwaka 1958 kabla ya uhuru?

Je kisa cha baada ya kuachishwa uspika na kuteuliwa kuwa waziri wa wanyama/maliasili?

Ikiwa wavijua visa hivyo kuna hoja muhimu nataka tuijenge hapo!

Yericko,
Sivijui visa hivyo.

Ningependa kuvisikia.
 
nafikiri kama utatumia busara kidogo na kutazama ni lini namba zilianza kutumika katika mitihani ya Tanzania na kuachana na kuandika majina na kutazama wakti huo nani alikuwa waziri wa Ilmu utaligundua hilo. Kwani Hata wizara ya ilmu ya Tanzania watakusaidia hilo wala haliitaji mjadala. Ila kwa mimi nakwambia ilikuwa kipindi Prof malima akiwa waziri wa Ilmu. Fanya uchunguzi utaligundua hilo.

Suala la Warioba naye yupo hai unaweza ukamuuliza tu kwani miongoni mwa aliosoma nao darasa moja Chuo kikuu (marhum Brigadia mang'enya ) mimi niliwahi kumuuliza kuhusu huyo hakuwa na jipya zaidi ya ukabila tu ulimbeba kama ilivyokuwa kwa akina Nyirabu na wengine kutoka mkoa huo enzi za JKN.

Nyirabu ni Mkurya, Warioba hakuwa Mzanaki kama Nyerere kwa hiyo suala la Ukabila halipo. Na hapa kwenye Kitabu chake anasema kipindi Warioba anateuliwa kuwa Waziri Mkuu hakuwa akijulikana wakati iko wazi tayari alikuwa mwanasheria Mkuu wa Serikali na kwa hivyo anaingia moja kwa moja Bungeni, utasemaje mtu huyo hafahamiki?

Na hilo la Mtihani tulishalimaza siku nyiingi. Kaka yangu (alikuwa mtoto wa jirani yetu na hivyo tulikuwa kama ndugu) amemaliza darasa la saba kwa mara ya kwanza 1980 kabla hajarudia na alitumia namba za mtihani, na tena haya wakiongea na Kaka yangu wa kuzaliwa nawasikia kabla hata uvumi huo unaousema haujasikika.

Na nikuulize kitu kimoja ni nani aliyemteua Warioba kuwa Waziri Mkuu na Nyirabu Gavana?
 
Ukimtaja Mze Shekue unanikumbusha mbaali sana enzi za akina Sheikh Abdullah Ayub na nduguye Mohamed Ayub.

Barubaru,

Salaam. nafurahi na nakutazama sana bayana zako hapa jamvini. Nilifurahi kuna wakti ulitujuza yakuwa Almarhum Burhan Mtengwa alikuwa ni class mate wako. Mimi nilimfahamu uzuri kupitia kwa Dr. Ibrahim Msabah. Insha Allah Mola tamjaalia kauli thabit na Fir'daus huko alikotangulia.

Nijaalie fursa kiduchu ya kunipokelea bayana yangu hii adimu kwako.

Mimi kwa upande wa Mama yangu ni baina ya Unguja na Tanga. Ndo maana baadhi ya jamaa hapa wakizungumza na kutuchosha kwa kuitaja Tanga,basi mie husikiliza na kujichekea peke.

Hao wanaotaja kila kukicha hizo habri za Zahrau hata na Tamta yake;family yetu ndo baadhi ya waasisi na wafadhili mpaka kesho Allahmdulillahi. Zile shughuli za awali zoote za Islamic knowledge,Taqwa,Shura,Tahweed na mengineyo mengi babu zanguWazee wetu walikua ndo Wanazuoni,wanaharakati, washughulikaji na wenye kutakwa shauri kwa kila lilotaka kufanzwa.

Leo huwezi kuitaja au kuijua asili na waasisi wa Tanga mpaka kuna baadhi ya jamaa,family uzijue kwa kina. Huyo jamaa anayetaka watu wakamuulizie habari zake kwenye misikiti na baadhi ya maSheikh pale Tanga mjini mpaka Lushoto,yanini tufikie huko ya Illahi ya manani?

Nimekujuza haya machache,maana umenitajia baadhi ya jamaa zangu wa karibu na maswahib/ndugu wa karibu wa family yetu na pia hapa kuna watu kila kukicha wanatutisha na habari za Tanga.

Pamoja na kuwataja hao kina Sheikh Mohammed na Abdallah Ayoub,pia huwezi ikamilisha Tanga leo bila kuwataja kina Sheikh Shame Mbuyu wa Kwale,Bwana Vuzo Mnyimanzi wa Chumbageni,Sheikh Merei Islam Al Baajiry,Sheikh Ali Bin Muhammad Majisu,Sheikh Hemed Bin Jumaa Al Bukhry,Sheikh AbdilRahman Salim Jibran,Sheikh Maalim Pera Bin Ridhwan,Bwana Fadhil Bwanga na wengineo wengi mno. Halafu pia lazim hiyo Tanga uijue local politics zake tangu enzi ya Mwarabu, Mjerumani na enzi ya wenye mji wao. Na ujue vitongoji vya asili na tamaduni za pale,mfano;Kilindi,Vuga,Tongoni,Mnyanjani,Chumbageni,Pongwe,Mkwaja,Buyuni Kuu,Ngamiani,Chuda,Kwale,Chongoleani,Mwarongo na mambo mengi kadhaa wa kidhaa.
Kwa ufupi kwa wale wasokwisha kututajia habari za Tanga kama vile sisi wengine ni wageni hii ni home work yao. Na wakajaribu kumuuliza huyo Sheikh Shekue, nae atawafahamisha uzuri hayo majina na hizo sehemu kwa kina,kama nae anajua au ni mtu mwenye asili ya pale Tanga mjini?
Hizo sehemu za Donge,Sahare na nyinginezo si sehemu za watu wa asili ya pale. Ilikua ni viunga tu vya wazee wetu au makazi ya wageni walohamia pale Tanga,ambavyo nahisi ndivyo ilivyo sasa?

Nilistaajabu pale Nguruvi3 alipomtaka Sheikh Mohammed Said ati atake radhi kisa "alimwambia hilo neno usirudie tena". Nguruvi3 akadai ati hilo neno kwao Tanga ni tusi!? Si kweli asilani,nami nampa challenge huyo Nguruvi3 ataje Tanga ipi hiyo atokayo yeye,na anipe nasaba yake kwa kina. Au nae kahamishia tu pale Tanga na mila za kwao Tarime,kama ni hivyo itakua amezungumza kweli.

Tangia zamani haikuwa ati ni mughali kwa Mkristo,asokua na dini au mtaalamu yeyote kujua Quran,Sunah na masuala fulani kuhusu Uislamu. Haina maana yakuwa huyo mtu ati ni Muislamu. Na mfano wetu wa karibu hapa jamvini kuna huyu ndugu yetu Mwanakijiji. Yeye anajua mengi kuhusu Uislamu na Quran kutokana na sababu zake kadhaa japo anadai hana dini. Huku nje kuna wale so called Orientalists na wataalamu kadhaa hasa wa nchi za magharibi, tangia karne ambao ni Wakristo au Atheists,nao pia wanajua saana Quran na Uislamu kutokana na sababu zao kadhaa za kitaaluma na nyinginezo za kidhalim. Kwa hili tusipate taaabu kwa jamaa wengine kutaka ati kutupatia Islamic knowledge na hadith kadhaa za Mtume-SAW,hapa si pahala pake,na kama ipo haja basi ifunguliwe thread nyingine. Nachelea tusijetia udini uso kiasi hapa jamvini,kuwakera ndugu zetu wengine na pia tukaongezewa kashfa na tashtit kwenye Iman yetu. Mengi yalosemwa juu ya Uislam imeshatosha.

Niwie radhi Al Akhiy,najua mengi humu tunasababishwa tunene pasi na mioyo yetu kutamani.

Ahsanta.

Cc; Ritz,The Big Show,Nguruvi3,Ami
 
Barubaru,

Salaam. nafurahi na nakutazama sana bayana zako hapa jamvini. Nilifurahi kuna wakti ulitujuza yakuwa Almarhum Burhan Mtengwa alikuwa ni class mate wako. Mimi nilimfahamu uzuri kupitia kwa Dr. Ibrahim Msabah. Insha Allah Mola tamjaalia kauli thabit na Fir'daus huko alikotangulia.

Nijaalie fursa kiduchu ya kunipokelea bayana yangu hii adimu kwako.

Mimi kwa upande wa Mama yangu ni baina ya Unguja na Tanga. Ndo maana baadhi ya jamaa hapa wakizungumza na kutuchosha kwa kuitaja Tanga,basi mie husikiliza na kujichekea peke.

Hao wanaotaja kila kukicha hizo habri za Zahrau hata na Tamta yake;family yetu ndo baadhi ya waasisi na wafadhili mpaka kesho Allahmdulillahi. Zile shughuli za awali zoote za Islamic knowledge,Taqwa,Shura,Tahweed na mengineyo mengi babu zanguWazee wetu walikua ndo Wanazuoni,wanaharakati, washughulikaji na wenye kutakwa shauri kwa kila lilotaka kufanzwa.

Leo huwezi kuitaja au kuijua asili na waasisi wa Tanga mpaka kuna baadhi ya jamaa,family uzijue kwa kina. Huyo jamaa anayetaka watu wakamuulizie habari zake kwenye misikiti na baadhi ya maSheikh pale Tanga mjini mpaka Lushoto,yanini tufikie huko ya Illahi ya manani?

Nimekujuza haya machache,maana umenitajia baadhi ya jamaa zangu wa karibu na maswahib/ndugu wa karibu wa family yetu na pia hapa kuna watu kila kukicha wanatutisha na habari za Tanga.

Pamoja na kuwataja hao kina Sheikh Mohammed na Abdallah Ayoub,pia huwezi ikamilisha Tanga leo bila kuwataja kina Sheikh Shame Mbuyu wa Kwale,Bwana Vuzo Mnyimanzi wa Chumbageni,Sheikh Merei Islam Al Baajiry,Sheikh Ali Bin Muhammad Majisu,Sheikh Hemed Bin Jumaa Al Bukhry,Sheikh AbdilRahman Salim Jibran,Sheikh Maalim Pera Bin Ridhwan,Bwana Fadhil Bwanga na wengineo wengi mno. Halafu pia lazim hiyo Tanga uijue local politics zake tangu enzi ya Mwarabu, Mjerumani na enzi ya wenye mji wao. Na ujue vitongoji vya asili na tamaduni za pale,mfano;Kilindi,Vuga,Tongoni,Mnyanjani,Chumbageni,Pongwe,Mkwaja,Buyuni Kuu,Ngamiani,Chuda,Kwale,Chongoleani,Mwarongo na mambo mengi kadhaa wa kidhaa.
Kwa ufupi kwa wale wasokwisha kututajia habari za Tanga kama vile sisi wengine ni wageni hii ni home work yao. Na wakajaribu kumuuliza huyo Sheikh Shekue, nae atawafahamisha uzuri hayo majina na hizo sehemu kwa kina,kama nae anajua au ni mtu mwenye asili ya pale Tanga mjini?
Hizo sehemu za Donge,Sahare na nyinginezo si sehemu za watu wa asili ya pale. Ilikua ni viunga tu vya wazee wetu au makazi ya wageni walohamia pale Tanga,ambavyo nahisi ndivyo ilivyo sasa?

Nilistaajabu pale Nguruvi3 alipomtaka Sheikh Mohammed Said ati atake radhi kisa "alimwambia hilo neno usirudie tena". Nguruvi3 akadai ati hilo neno kwao Tanga ni tusi!? Si kweli asilani,nami nampa challenge huyo Nguruvi3 ataje Tanga ipi hiyo atokayo yeye,na anipe nasaba yake kwa kina. Au nae kahamishia tu pale Tanga na mila za kwao Tarime,kama ni hivyo itakua amezungumza kweli.

Tangia zamani haikuwa ati ni mughali kwa Mkristo,asokua na dini au mtaalamu yeyote kujua Quran,Sunah na masuala fulani kuhusu Uislamu. Haina maana yakuwa huyo mtu ati ni Muislamu. Na mfano wetu wa karibu hapa jamvini kuna huyu ndugu yetu Mwanakijiji. Yeye anajua mengi kuhusu Uislamu na Quran kutokana na sababu zake kadhaa japo anadai hana dini. Huku nje kuna wale so called Orientalists na wataalamu kadhaa hasa wa nchi za magharibi, tangia karne ambao ni Wakristo au Atheists,nao pia wanajua saana Quran na Uislamu kutokana na sababu zao kadhaa za kitaaluma na nyinginezo za kidhalim. Kwa hili tusipate taaabu kwa jamaa wengine kutaka ati kutupatia Islamic knowledge na hadith kadhaa za Mtume-SAW,hapa si pahala pake,na kama ipo haja basi ifunguliwe thread nyingine. Nachelea tusijetia udini uso kiasi hapa jamvini,kuwakera ndugu zetu wengine na pia tukaongezewa kashfa na tashtit kwenye Iman yetu. Mengi yalosemwa juu ya Uislam imeshatosha.

Niwie radhi Al Akhiy,najua mengi humu tunasababishwa tunene pasi na mioyo yetu kutamani.

Ahsanta.

Cc; Ritz,The Big Show,Nguruvi3,Ami

Unnecessary pomps from someone who thinks that because he was born in Dar or Tanga or Zanzibar then he is a better and more knowlegeable muslim than those muslims from Kigoma, Kondoa and Tabora. Pathetic "mipasho" style!
 
Nafikiri unafikiri tofauti.

Zinazojitokeza hapa ni chuki dhahir kabisa za watu wa upande wa pili wanaoamini kuwa JKN hawezi kufanya kosa lolote na hakufanya makosa jambo ambalo si kweli. Tunaamini kama mwanadamu amefanya mengi mazuri na mabaya pia.

sasa wengu huko Tanzania wamejikita kuandika mazuri ya JKN ikiwa pamoja na kutia hata chumvi sasa akitokea mtu kuandika mabaya ya JKN ndio hapo unaona kinachodhihiri hapa.

Huu ni mpasuko huko Tanzania na ulipandwa zamani. sasa hivi kila kitu kinatazamwa kwanza kwa imani kabla kujua uhalisia.


Barubaru
Nani ambaye amesema JKN hakuwahi kufanya makosa? Hizo chuki ni hisia zako tu. Sisi tunasema Nyerere ni Rais wa kwanza na muasisi wa TANU. Ni Rais wa kwanza wa Tanganyika na tunakataa kwamba alikuwa na mpango mahususi wa kuwahujumu waislam. Sasa haya wewe ndio unatafsiri kuwa tunawachukia waislam!

Barubaru, usipofushwe na udini. Wewe ni msomi hebu soma maoni yetu bila kutumia udini. Najua wewe kama mwarabu uliyekimbilia Oman labda huna huna ndugu au rafiki asiye muislam. Sisi wenzio tuna marafiki na ndugu wa dini zote na suala la kuwachukia watu kwa dini zao halipo. Ila tunachukia uongo/uzushi wenye nia ya kututenganisha.

By the way, on a personal note, naomba kujua jinsi unavyokuwa treated huko Oman kama mwarabu kutoka zanzibar, je kuna namna yoyote wanakubagua? Nimeuliza hivyo kwa sababu nimemsoma mtu hapa ambaye amesema wangazija wahamiaji huko Comoro wanaitwa wangazija pori. I just want to know whether you are facing similar hostile reception in Oman.
 
Last edited by a moderator:
Shukran sana Mwanakijiji. This is one of the best analysis. By the way Nyerere angekuwa mtu wa kanda na dini kama juhudi za hivi karibuni mbona Mara ingekuwa mbali? Wakiristo kibao, waislamu kiduchu, rais Mara, Prime Minister Mara, Mkuu wa Majeshi Mara mbona jamaa kila nyumba ingekuwa na vigae!!!!! Suala hapa ni KAZI. Anayetaka aende Lushoto. Waislamu tele, hard work bila kipimo, maendeleo yao hayana mipaka.

Asante kushukuru Wickama;

Kwa kweli nimesoma jinsi mambo ya Tanga yalivyo basi hadi nimesikia uchungu. Nimeishi Tanga maisha yangu ya utoto na ujana na kukulia miongoni mwa Waislamu. Nimesoma na Waislamu toka darasa la kwanza hadi sekondari. Sasa siyo kusoma tu hivi hivi lakini kuwa na urafiki wa karibu kiasi cha kwenda nao kwenye Maulidi ya Mtume, na utotoni hata kupiga nyimbo za daku - na unajua bana hakuna wanakofanya vizuri kama Tanga (sijui siku hizi). Ni Tanga ambako miye sikujua wapo Waislamu ambao walikuwa hawajaendelea; nimekua nikiwaona wanafanya biashara, wana maduka, wana mabasi (na hapa sizungumzii Waarabu tu - kina Mabrouk) la hasha nawazungumzia hawa weusi tii wenzetu. Tulipokuwa shule tukisoma pamoja niliwaona uwezo wao darasani; mtu mmoja darasani alikuwa best wangu na tulikuwa tukishandana sana aliitwa Saleh Khalfan (alikuwa ni mswalihina hadi mtu unaona wivu); baba yake Mzee Khalfan akiishi pale Majani Mapana karibu na duka la Chako ni Chako. Binti aliyekuwa anatutesa wote, mpole kwelikweli - Mwanahawa Salim alikuwa ni Binti wa Kiislamu; mwingine ambaye alikuwa anatuzingua darasa aliitwa Mpaji Juma akiishi pale kijijini cha Mwamboni (sijui kama bado kipo). Dada zangu wamesoma ile shule ya Jumuiya (pale karibu na stendi). Mwenyewe nikaenda kusoma Pangani. Kote huku - nisamehe kwa kutembelea kumbukumbu za zamani - niliishi nikiamini kabisa kuwa sisi sote tulikuwa tunashindana vizuri darasani na wenye kipaji walikuwa na kipaji - sikufikiria kabisa suala hili la dini. Na kweli niliwaona vijana wa Kiislamu wakipasua darasani vizuri tu na wengi wameenda mbali leo hii. Na niliwaona watoto wa Kikristu wakiharibu darasani na leo maisha yao yako duni vile vile.

Na hili ni kweli siyo hapo Tanga tu; nimebahatika nami kupita sehemu kubwa ya nchi yetu. Ni mikoa mitano tu ambayo sikujaliwa kufika kabisa; Mtwara, Lindi, Rukwa (Katavi), Kigoma na Pemba. Sehemu nyingine zote nimefika; nimefika Mwera, Boza, Muheza, Maramba, Dunga, Ileje, Ndala, Unguja, Kisarawe n.k ni sehemu nyingi. Nimekuja kuelewa kitu kimoja ambacho Mohammed Said na wengine wenye kuamini histohia hii hawajajaribu basi kuangalia - maendeleo Tanzania yameenda kimaeneo zaidi (geographical). Kwamba kuna maeneo ambayo yamefanikiwa sana kutokana na historia yake bila kujali makabila yaliyomo ndani yake. Leo hii huwezi kushangaa kuwakuta Wahaya Waislamu waliosoma sana; huwezi kushangaa kukuta Wachagga Waislamu ambao ni wasomi vile vile n.k

Lakini cha kushangaza sana; utaona kuwa wanaodai kuwa Waislamu wamedhulumiwa hawawezi kuelezea mafanikio ya Waarabu Waislamu, au Wahindi Waislamu, au hata Wahindu wa Tanzania. Mfumo Kristu ambao unapendelea Wakristu unaweza vipi kuachilia Waislamu wa makundi mengine wakafanikiwa? Wanatolea mfano hapa wa kuvunjwa kwa EAMWS kama mfano mmoja wa jinsi Uislamu ulivyopigwa vita; lakini hawahawa hawawi wa kweli kusema kuwa Aga Khan (muasisi na mfadhili mkuu wa EAMWS) aliendelea kuwekeza Tanzania na mahusiano yake na utawala wa Nyerere hayakuingia mawaa hata chembe.

Kwangu mimi kurahisisha tu kudai kuwa haya yote ni kwa sababu Waislamu/Uislamu unapigwa vita.
 
Na hakika historia haiwezi kubadilika kuwa yeye alikuwa kiongozi wa kwanza wa TANU na alikuwa Rais wa Kwanza wa Tanganyika.
Historia haiwezi kubadilika kuwa A.Sykes aliwahi kuwa rais wa TANU au rais wa Tanganyika.
Historia haiwezi kubadilika kuwa K.Sykes alikuwa katibu wa AA na Cecil Matola alikuwa Rais wa AA.


Ndio uzuri wa historia, inatoa hukumu bila upendeleo au kificho. Hata kama itafinyangwa vipi bado kuna sehemu historia itamsota kidole anayeifinyanga.

Nafikiri kuna haja ya kuwapa wasomaji wapya mtiririko wa kwa nini mimi Mag3 ni moja kati ya watu waliowekwa kwenye "shit list" ya Mohamed Said kwa kumuita kwa jina lake halisi...muongo na mchochezi. Nanukuu madai ya Mohamed Said kwenye posti namba 914;
Mohamed Said said:
  • Kwa Dar es Salaam Nyerere aliingizwa katika siasa na Abdu Sykes. Hakuna mtu aliyekuwa anamjua Nyerere katika siasa za Dar es Salaam hadi Abdu alipomleta ofisi ya TAA New Street. Hiki wala si kitu cha kificho watu wote wa Dar es Salaam katika harakati zile za 1950 wanajua.
  • Hapana inawezekana huko alikotoka alifanya makubwa. Lakini kwa Dar es Salaam ambako ndiko hasa siasa zilikuwa kali hakuna aliyepata kusikia jina la Nyerere. Ukipenda pitia magazeti ya Zuhra ya mwaka 1950 upime hali ya siasa ilikuwaje.
Mtu anayeweza kutoa madai ya uongo kama hayo tumwiteje? Mwalimu Nyerere tayari alikuwa kiongozi wa AA mwaka 1945 akiwa Tabora na mwaka huo huo alifika Dar es Salaam na kukutana na viongozi na wanachama wa AA mojawapo akiwa Dossa Aziz. Sasa, kama Mwalimu Nyerere na Abdul hawakukutana ni wazi kumbe Abdul Sykes hakuwa kati ya vinara wa AA mjini Dar es Salaam...swali la kujiuliza ni je, Abdul alikuwa nani ndani ya AA kabla ya kuvamia ofisi za TAA mwaka 1948 kwa ngumi na mateke? Katika msingi huo huo dai la Mwalimu Nyerere kuingizwa katika siasa na Abdu Sykes, linatokea na kuanzia wapi?
Mohamed Said said:
Nyerere alimwona Abdulwahid kama mtu mwenye akili sana, kijana aliyejiweza kihali na mtu mwenye moyo mkubwa usiokuwa na hasad wala choyo. Abdulwahid alimuona Nyerere, kama mtu aliyeelimika vizuri kati yao na mwenye ustadi katika mijadala. Nyerere alipata nafasi ya kuifahamu dunia vizuri lau kama alikulia kijijini.

Zaidi Nyerere alikuwa amepata uerevu wa siasa kutokana na uhusiano wake na Fabian Society, wakati alipokuwa mwanafunzi Uingereza. Mijadala mizito sana ilijitokeza katika vile vikao vya kila Jumapili wakati akili na ujuzi wa siasa wa Abdulwahid vilipopambana na uhodari wa majadiliano wa Nyerere.

Kweli akutukanaye hakuchagulii tusi; hapa akili na ujuzi wa Abdul eti unapambanishwa na uhodari katika ubishi wa Nyerere! Nini lengo la Mohamed Said hapa? Kwamba Nyerere pamoja na usomi wake wote hadi kuwa Mtanganyika wa kwanza kuwa na masters ya uchumi kutoka Edinburgh hakuwa lolote mbele ya Abdul mstaafu wa vita vya pili vya dunia?

Mohamed Said haishii hapa; kwa mbali nakumbuka alivyowahi kumponda, Dr. Vedasto Kyaruzi, msomi wa kwanza kuchaguliwa kuiongoza TAA mwaka 1950 Abdul akiwa katibu wake, nanukuu;
Mohamed Said said:
Kuhusu ''brains'' baba yangu ananiambia kuwa yeye na Abdu walianza kusomeshwa mashaf yaani Qur' an siku moja. Abdu kamaliza kabla ya wenzake wote na akaja kuwa ndiyo mwalimu wao maalim asipofika darasani. Cambridge alitoka first class.

Dar es Salaam ya 1950s ilikuwa nyingine. Kyaruzi "was playing second fiddle." Huu ndiyo ukweli wa siasa za miaka ile. Nani anamjua Kyaruzi?
Madai yale yale ya dharau katika harakati za kuwainua wazee wake wa Gerezani...eti who was Kyaruzi!... Dr. Vedasto Kyaruzi, Raisi wa kwanza wa TAA wa kuchaguliwa ambaye aliwapa hofu wakoloni hadi akapewa kifungo cha uhamisho mbali na Dar es Salaam. Katika misingi hiyo hiyo Mohamed Said aliwahi pia kubeza mchango wa Raisi wa kwanza muasisi wa AA mwaka 1929, Cecil Matola, na katika njama za kumpa sifa zote baba yake Abdul, Klest Sykes...swali la kujiuliza ni hivi jitihada zote hizi za nini? Anaendelea na nanukuu;
Babu yangu Salum Abdallah yeye alikuwa katika kamati ya siri ya TAA Tabora iliyokuwa ikiratibu harakati pale New Street na 1955 akawa rais muasisi wa Tanganyika Railway African Union (TRAU).

TRAU ilipigana bega kwa bega na TANU dhidi ya ukoloni.
Haya sasa, hapa katibu wa TRAU, msomi Balozi Christopher Kasanga Tumbo hata hatajwi; anatajwa tu baba, Rais muasisi wa Tanganyika Railway African Union, Salum Abdallah! Bahati mbaya katibu hakuwa Manyema wala Mzulu na hakuzaliwa Dar es Salaam. Tatizo linakuja kutokea wakati akina Mag3 wanapokosoa maandiko kwa kuhoji ukweli wa baadhi ya madai, jibu ni hili, nanukuu;
Mohamed Said said:
Nimesema na nyinyi andikeni mchango wa wazee wenu katika kupigania uhuru wa Tanganyika. Badala ya kushughulishwa na hili mmekazania kunishambulia mimi. Mimi nimekuelezeni kuwa hiyo haitasaidia kwa kuwa kitabu changu kimekubalika na kinasomeshwa vyuo vikuu vyote vyenye idara ya African Studies.

Kitabu changu kinasomwa vyuo vikuu vyote vinavyosomesha African history. Hivi ninavyoandika kitabu kinakwenda toleo la tatu. Wewe unazungumza kukipinga JF...Kitabu kipo Oxford, Cambridge, Harvard, Northwestern,
University of Dar es Salaam...Unajua hata nilipowaambia kuwa kitabu changu kimefanyiwa review na maprofesa wawili wa historia na review hizo zimo katika Cambridge Journal of African History walibeza.
The audacity of it all..."andikeni na nyie" Mtoa mada, Yericko Nyerere, akajaribu kutoa ushauri, nanukuu;
Naomba nikuulize swali Mohamed Said, mnakasha huu umekuonyesha mapungufu ya kitabu chako au haujakusaidia kwa lolote?
Jibu alilopewa ni hili nanukuu;
Yericko, Haujanionyesha upungu wowote katika kitabu changu. Kunisaidia mnakasha umenisaidia sana tena sana. Nimeelewa kwa nini hata Nyerere hakupenda historia ya wazee wangu ijulikane. Lakini kubwa limenidhihirishia lile nililokuwa nimefunzwa...1 ni sawasawa na 20...
???...Hapo ndipo tulipo, Mohamed Said hajaona upungufu wowote katika kitabu chake ingawa mnakasha anadai umemsaidia sana tena sana...kwamba sasa anaelewa kwa nini hata Nyerere hakupenda historia ya wazee wake ijulikane! Na mimi nasema kuwa, kama unayodai ni historia ya wazee wako ndio unayoiita historia ya TANU, basi kumbe hiyo TANU aliyoianzisha Abdul ni tofauti na TANU iliyozaliwa 7/7/1954 na kupigania uhuru wa Tanganyika hadi ukapatikana mwaka 9/12/1961.

  • Hakuna ushahidi wowote kwamba Abdulwahid Sykes aliwahi kuchaguliwa kuiongoza TANU tangu kuasisiwa kwake hadi uhuru unapatikana.
  • Hakuna ushahidi wowote kwamba Abdulwahid Sykes, aliwahi kusimama jukwaani akiinadi TANU tangu kuasisiwa kwake hadi uhuru unapopatikana.
  • Hakuna ushahidi wowote kwamba Abdulwahid Sykes aliwahi kuwa kiongozi wa juu wa TANU katika ngazi ya taifa, Jimbo, Wilaya hadi Kata.
 
Back
Top Bottom