Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Thread za nini mimi nataka utufahamisha Nyerere ndiyo ameleta amani Tanzania ambayo haikuwepo?
Kuna tofauti kubwa sana kati yako na WildCard, wewe umezoea ubishani wa kwenye Mihadhala ya kina Mazinge kwamba Yesu alikuwa Muislamu, wakati mwenzako anakufundisha namna ya kureson.
 

Najua mkiishiwa hoja mankimbilia kutukana matusi. Mimi sina alergy ya kutukanwa. Ndio maana naitwa Zali la Mentali.

Mpumbavu huamini kila neno bali mwenye hekima hutafakari kila neno!
 
 

So assassination ndo the only kipimo cha kutokuwa Kibaraka???????
 
 
Last edited by a moderator:

Nguruvi3,

Nakushukuru kwa maelekezo.

Kama nilivyokufahamisha jana,yakuwa hii shughuli bado ni pevu mno. Naona na sasa imeingia ile kitu ya moto mwingi...Zali la Mentali a.k.a Mchimba Chumvi. Nahisi huyo jamaa mtaweza kufahamiana nae kwa uzuri, kwa kuwa anatumia "lugha nyepesi" kwenu nyinyi kufahamu. Sisi wengine lugha zetu ni za Kibilatii na Ukhalat mwingi,kwa hiyo inakuwa taabu mno nyinyi kutufahamu.

Tuendelee na mnakasha.
 


Sheikh Said, itoshe tu kusema nyaraka ulizopata zilisema Balozi Royall alihutubia Bunge. Kujitahidi kujitetea katika hilo hutaweza na kama ni kosa, basi halikuanzia kwako bali kwenye chanzo chako cha taarifa ambacho nacho hakikupaswa kuripoti kwa namna hiyo. Hata hivyo nawe pia ulitakiwa ujiridhishe tofauti hizo mbili.
 

Hivi mnapata wapi ujasiri wa kusema Nyerere alichukia wizi, rushwa, uporaji wa rasilmali za nchi, udini na ukabila? Utawala wake vitu hivyo vyote vilishamiri na kuota mizizi.

Kuhusu wizi yeye ndiye aliyeasisi wizi hapa Tanzania. Alinyang'anya mali za watu kwa kisingizio cha ujamaa. Huu ulikuwa wizi wa mchana kweupe. Mali alizozinyang'anya akawapatia makada wa chama chake ili waziendeshe. Makada hawa wakaanza kuiba mali ya umma na kufilisi mali karibu zote zilizotaifishwa. Huu ni wizi wa pili aliouasisi ambao sasa hivi tunauita ufisadi.

Kuhusu rushwa kipindi chake ilikuwa ni ya hatari sana. Ulikuwa huwezi kupata huduma hata za msingi kama unga, sabuni, mchele bila kulanguliwa. Ilikuwa ukitaka kununua tuseme gunia la unga lazima upate kibali ambacho huwezi kupata kama huna connection ya kada.

Kuhusu uporaji wa rasilimali za nchi yeye amepora sana rasilimali za Tanzania na kuzisambaza maeneo mengine barani Africa kwa ajili ya crusade yake. Ni vigumu kuweza kukuta kuna vita ilipiganwa wakati ule barani Africa bila yeye kuwa na mkono wake kwa njia moja au nyingine. Vita za Zanzibar, Uganda, Burundi, Rwanda, Nigeria n.k kote huko ana mchango wake na alikuwa anatumia kasma ya kodi za Watanzania kufadhili vita hizo matokeo yake taifa la Tanzania likabaki taifa maskini la kutupwa wakati lilikuwa na kila rasilimali za kuliwezesha kuwa taifa lenye neema. Watanzania wengi wamekufa katika vita hizi zisizokuwa na kichwa wala miguu na matokeo yake mataifa hayohayo yaliyotumia rasilimali zetu kufikia malengo yao leo yanatudharau na yenyewe yamepiga hatua kubwa ya maendeleo ukilinganisha na sisi.

Kuhusu udini hilo nimeshalieleza sana na mpaka sasa hakuna mtu aliyejibu hoja zangu hivyo sina haja ya kurudia kwamba Nyerere alikuwa zaidi ya mdini. Alikuw mmadhehebu kwa kuupendelea Ukatoliki dhidi ya dini zingine na madhehebu mengine ya Kikristo na alifanikisha hali hiyo kwa kutumia kodi za wananchi kuwawezesha Wakatoliki ili wawe na nafasi ya kuwa juu zaidi ya wengine. Kitendo cha yeye kumpigia debe Mkapa Mkatoliki mwenzake na kuwawekea kiwingu Wakristo wengine wakati ule wa Uchaguzi ambapo Mkapa alipita ni dhahiri kwamba huyu jamaa hana hata soni kwenye kuupendelea Ukatoliki waziwazi. Maana kama angekuwa na soni basi angesema angalau awache kipindi kile atawale Mkristo mwingine ambaye siyo Mkatoliki kwani walikuwepo wengi tu wenye uwezo wa kutawala na hasa ukichukulia kwamba yeye kama Mkatoliki amekaa pale Ikulu zaidi ya miongo miwili.

Kuhusu ukabilia huyu jamaa alikubuhu kwa hilo. Neno Erro hapa Tanzania linatumika kuwatambulisha Wanajeshi na polisi kwani alikuwa amewajaza Wakurya kule kila kona. Huu ulikuwa ni ukabila wa waziwazi. Ukabila mngine wa hatari aliouasisi na mpaka leo bado unaisumbua CCM ni ule wa kuyatenga makabila makubwa kama Wahaya, Wachaga, Wasukuma, Wanyakyusa katika nafasi nyeti za uongozi kwenye nchi hii, hasa kwenye ulingo wa siasa kwa sababu ya inferiority complex yake ya kutotaka kukaa na watu waliomzidi ujuzi na maarifa karibu nao ili yeye ndio aonekane kama mjuzi wa kila kitu na wengine wote ni watu wa kujifunza kutoka kwake.

Kusema kwamba mwalimu aliongozwa na sheria za nchi huu ndio mzaha wa mchana kweupe. Yeye alikuwa dicteta wa kuburuta kila kitu. Alikuwa yeye ndiye sheria na sheria ni yeye. Hata kwenye hotuba zake aliwahi kuthibitisha hili pale aliposema kwamba alimtia ndani jamaa mmoja aliyetamba kwamba aliiweka mfukoni serikali yake na alimtia ndani bila kufuata sheria za haki za binaadamu. Kilichomuokoa yule jamaa ni Kanisa Katoliki lilipomuombea kwa Nyerere ili amuachie. Na huu ni uthibitisho mwingine kwamba Kanisa Katoliki lilikuwa linaendesha nchi hii kwa remote control kupitia Nyerere. Mifano ipo mingi hapa ya yeye kutoheshimu utawala wa sheria. Alipiga marufuku mashindano katika ngazi ya Urais na ikawa ama unamchagua yeye au kivuli wakati katiba ya nchi ilikuwa inatoa haki kwa wote kuweza kuchagua au kuchaguliwa. Hii ni dhambi kubwa aliyotutendea Watanzania. Alikua anatishia watu kijinga mno. Kwa mfano aliwahi kusema kwamba mmeniita majina mengi lakini hilo la haambiliki litaondoka na mtu. Kwa maana hiyo alikuwa tayari kuua mtu kwa ajili tu ya kuambiwa haambiliki, jina ambalo alilistahili kwa kila hali. Bado kuna mifano mingi ya Watanzania waliouawa, kuwekwa kizuizini bila kufuata kanuni za sheria n.k
 


'Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake' The Bible
 
Jasusi,

Jibu swali Nyerere wakati anatoka Musoma kuja Dar es Salaam alikuta kuna vita au huko alikutoka ndiyo watu walikuwa wakatana mapanga.
Hata Kenyatta alivyokabidhiwa uongozi na Jaramogi alikuta hakuna msuguano na vita vya kikabila Kenya. Lakini baada ya utawala wake wa kikabila tulishuhudia matunda yake 2007.
 
Kuna tofauti kubwa sana kati yako na WildCard, wewe umezoea ubishani wa kwenye Mihadhala ya kina Mazinge kwamba Yesu alikuwa Muislamu, wakati mwenzako anakufundisha namna ya kureson.


MUSLIM CIVILIAN- BASED DEFENCE...

"VEMA,MMETUHUKUM TUNYONGWE NASI TUMEKUBALI.TUMEKUBALI KWA SABABU NI SISI WENYEWE TULIOENDEA MAJI YA DAWA YA NGARAMBE KWA HIARI YETU;KWA SABABU HATUKUONA HAKI YA KUTAWALIWA NA NYINYI WAHUNI,NA KWA SASA KWA KUWA MMENIPATA,BASI NINYONGENI HARAKA SANA KUSUDI JINA LANGU LIBAKI LIKIKUMBUKWA KWAMBA NILIKUWA MMOJA WA NILIYEPIGANIA NCHI YANGU...

---SELEMANI MAMBA,,A MAJI MAJI HERO...

Watu walipigania nchi hii kwa huba na maslahi ya nchi yao,wala hawakuweka dini zao mbele,walikuwa waislam safi kabisa,walifanya hivyo kwa mapenz ya nchi yao ili waje kukumbukwa na vizazi vijazavyo kama wapigania uhuru wa nchi hii,hadi kunyongwa walinyongwa,cha ajabu historia hii ya kwao ikiafutwa kwa makusudi na kufifishwa eti kwa kuwa tuh wameonekana wana majina na iman za kiislam..!
Watu wakisema historia ya nchi hii kwa baadhi wa watu imefichwa kwa makusudi eti wanaitwa wachochezi..!,,wachochezi wakati wao wanausema ukweli unaofutwa kwa makusudi??
Haki siku zote itasimama tuh,hakuna wa kuificha..

Naona sasa unataka kutuingiza kwenye mijadala ya yesu mungu ama si mungu sio??hapa hatupo katika kikao hicho,fungua uzi kule kwenye jukwaa la dini...
 
Wacha wewe Mwanakijiji kujigaragaza kwenye tope!.
 
Kuna tofauti kubwa sana kati yako na WildCard, wewe umezoea ubishani wa kwenye Mihadhala ya kina Mazinge kwamba Yesu alikuwa Muislamu, wakati mwenzako anakufundisha namna ya kureson.

Kureson ndiyo nini? Mihadhala ndiyo nini? Haya ndiyo matunda za shule ya kata. Huyu ni mfuasi wa Chadema anategemea naye Chadema wakichukuwa nchi apewe uongozi...ha haa haaa!

Mungu tunusuru waja wako.
 
Barubaru,
Nimeshakupa tuisheni kuhusu makabila ya Kenya na Uganda, siyo machache sana kama unavyodai. Anyway, kuhusu ukoloni nakubali walitumia devide and rule, siyo Kenya tu hata Tanzania. Wewe unadhani ni kwa nini Nyerere alipiga marufuku utawala wa uchifu? Kwa sababu machifu walikuwa na ushawishi mkubwa sana katika makabila yao. Usingeweza kujenga taifa lenye umoja kwa kuendeleza utawala wa machifu. Hilo moja. Pili, katika harakati za uhuru wa Kenya, TANU kilishirikisha viongozi wa makabila mbalimbali, akiwemo Jaramogi Odinga, ambaye alimpisha kiti Kenyatta kwa heshima tu, Paul Ngei, Tom Mboya na wengine wengi. Kenyatta alikuwa na nafasi ya kipekee kujenga umoja wa Wakenya lakini yeye alipoingia mamlakani akaanza kuwapendelea Wakikuyu. Mikopo yote ya kibiashara walipewa Wakikuyu peke yao. Ardhi katika Rift Valley, Mombasa hadi Taveta, walipewa Wakikuyu. Kuna wakati mwaka 1973 ukifika Nairobi ukipiga simu kwenye ofisi za serikali ama unajibiwa Kiingereza au Kikikuyu. Hiyo ndiyo Kenya ya Kenyatta. Nyerere alimwita "tribal chief." Matokeo yake tuliyaona sote 2007. Ukitaka somo kuhusu udogo au wingi wa makabila ya Uganda na Kenya nijulishe tena.
 



Lakini Sheikh Said, naomba nikuulize pia; Je, Historia ya TANU 'iliyoandikwa Kivukoni', inaelezea Mchango wa Wakristo?
 

Mimi najazia kiduchu tulikuwa tunavaa makatambunga na tunafuruhia magwanji.

Mie naendelea kukusoma, Zali la Mentali, huku nimevaa miwani ya 3D.

Cc.., Kadogoo, gombesugu,
 
Last edited by a moderator:


Hatimaye umefunua rangi yako kamili, kumbe Mapinduzi ya Zanzibar yalikuathiri sana. Pole sana Mkuu.
Aliyefanya Mapinduzi Zanzibar naambiwa sio Karume baba, bali John Okello Mganda. Huyo Nyerere unayemwingiza hapa hakuunga mkono Mapinduzi ya Zanzibar tu bali aliwaunga mkono hata Wapalestina na Nchi zote za Kusini mwa Afirka.

Kwanini unakerwa na Nyerere kujihusisha na Mapinduzi ya Zanzibar pekee?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…