Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Duh! ajabu na kweli! mimi nilidhani huwa unaelimika na post za mzee mchochezi Mohamed Said peke yake! nampa hongera sana Wickama naona anaweza kukuongoa kwenye makucha ya muovu!

Tatizo lako wewe mambo unayachukulia kishabiki sio kila analoongea mpinzani wako unalipinga hatakama linaukweli wewe uko huku kwaajili ya kupinga tuu hata kama umeona ukweli wickama sio wa kihivyo kuna mambo mangapi anayaongelea mzee MS na Wickama anayakubali mbona wewe hukumshangaa Wickama wewe kapambane na ZALI LA MENTALI niache nipumue mkubwa
 
Boko haram, ni lini ulimtangaza Wickama kama mpinzani wako?ninachokijua mie nikwamba ulitangaza kwamba unajifunza mambo kutoka kwa mchochezi Mohamed Said tu! sasa leo unabadili msimamo?
 

Ritz,
Tena hapo nimejizuia kweli kweli. Sote ni wafu watarajiwa. Haijalishi kama mtu amekufa kwa kuzama, au kugongwa gari lakini katu tusitumie kifo cha mtu kama adhabu fulani vile inayostahiki. Nimejizuia sana tu.
 
Boko haram, ni lini ulimtangaza Wickama kama mpinzani wako?ninachokijua mie nikwamba ulitangaza kwamba unajifunza mambo kutoka kwa mchochezi Mohamed Said tu! sasa leo unabadili msimamo?

Gwalihenzi, unajua maana ya upinzani? kunapost moja Wickama aliituma akaulizwa na kama sijakosea Jokakuu kwamba mbona unawapa nguvu hawa jamaa mimi hapo nilishindwa kuelewa hata boss wako Nguruvi3 ali comment hiyo issue wickama kwanini aseme hivyo kwa maana hiyo hata Nguruvi akikosea asiambiwe?
 
Mimi napata tabu kukuelewa wewe. Mohamed ameshatuambia kuwa Nyerere amekutana na Sykes mara ya kwanza mwaka 1953. Lakini Nyerere alikuwa mwanachama wa TAA kabla ya hapo. Sasa kabla ya kukutana uso kwa uso wangefahamiana vipi? Kupitia mitandao na e mails na skype? Au mabango ya Abdulwahid Sykes yalikuwa yamesambazwa nchini kote kama mlivyofanya na Kikwete katika uchaguzi wa 2010?
 
Nguruvi3 ni boss wa nani? naamini Nguruvi3 ni "independent thinker" na wala hahitaji kuwa boss wa mtu yeyote labda kazini kwake na wala sio hapa JF, hiyo ndio tabia ya "intellectuals". Wewe Boko haram kwa sababu ya uelewa wako mdogo ndie uliyeanza kuumba maboss hapa, na bila aibu wala kutumia akili ukaamua kumfanya mchochezi Mohamed Said kuwa boss wako na wajinga wenzako ambao hamtaki kutumia akili zenu!
 

Swala la kutoa majengo Morogoro wala Waislam hawaitaji kushukuru hata Wakirsto pia aliwapa majengo kule Mbeya.

Kuhusu Msikiti wa Dodoma unataka Waislam wamshukuru Mkapa badala ya Gaddafi?

Waislam wanaojitambua wataendelea kumuona kam Mkapa ni kiongozi aliofanyia dhulma kubwa Waislam wa Tanzania.

Tunachokikumbuka kutoka kwa Mkapa ni shinikizo la paroko Lwambano na serikali ya Mkapa iliwakamata Masheikh, Wazee wa Kiislam, Maimamu na Wahadhiri na kuwaweka ndani.

Polisi walivamia Msikiti wa Mwembechai wakavurumisha mabomu ya machozi wanawake waliumizwa vibaya kisha kudhalilishwa.

Rais Mkapa chanzo cha mauwaji ya Mwembechai taingia aondoke madarakani hatujashuhudia tena askari akiamriwa "piga yule" " na yule" bado (hajafa) mwongeze na kweli polisi anafyatua risasi kuwalenga shabaha na kuuwa Waislam.

Kwenye Waislam siku zote wanafiki hawakosi.
 

alafu wakiambiwa ni ngano. Povu linawatoka
 

mkuu gwalihenzi angalia watu wakubishana na nao huyo Boko haram msamehe tu.. Naomba nielewe
 
Last edited by a moderator:

Shukran Ritz; Katika utawala huu wameuwawa waislamu arusha kwenye maandamo ya Chadema. Morogoro aliuwawa mwislamu pia katika mazingira yanayofanana. Mhesabu pia. Kwa hiyo statement yako ya mwisho siyo kweli na wala haizingatii uadilifu wa kiislamu. Unless kwako waislamu ni wale waliouwawa wakati rais ni mkiristo. Katika utawala huu amri ya piga yule iliondoa maisha ya pia mwandishi wa habari kule iringa. Kuficha na kuukana ukweli pia ni unafiki. Rules za engament za polisi ni sawa popote pale duniani. Kwanza Maspika; wananchi rudini ondekeni. Ikizidi, ni risasi za kuonya (hewani); Maji ya kuwasha/ rubber bullets; mwisho kama askari wanaona wao pia wako hatarini mnaachiwa risasi za moto. Uliza askari yeyote atakwambia. Haijalishi demonstration kaandaa pagani au saint. Ndio yaliyotokea hata ule mgodi wa Afrika Kusini. Ulizia utaambiwa vilevile wakati wakataji miwa wa kilombero waliuwawa na FFU, raisi alikuwa ni nani. Mwisho jeuri yako ya kusema bora umshukuru Gaddafi na sio Mkapa kwa msikiti wakati Gaddafi hakuwa anapajua Dodoma inaonesha dhulma na UDINI uliokujaa. Refer definition ya Mdini ambayo nimeitoa kila mara. Katika hilo la msikiti, nani alimfungia safari mwenzie. Epuka ukweli. Haina maana utageuka kuwa ni urongo. Zanzibar ilishaingia OIC, ni rais yupi aliyeitoa? taja dini yake. Msifiche madhaifu yenu juu ya kuwahofia wengine. Mbona Mkapa hakutaka mjadala juu ya kuitoa TANESCO kuwa university (alithubutu).

Ritz; Elewa siafiki watu kuuliwa. Lakini marais hawafiki kufyatulia waandamanaji marisasi uwanjani. Sasa kama unawawajibisha kwa yale yaliyotokea kwa mfano pemba, sharti pia uweke mizani na umlaumu na rais wa zenj na polisi kamanda wa zenj, haya yanakupa taabu kwa vile ni waislamu. Kama unao ushahidi kote huko kuwa waandamanaji walishatii amri ya polisi wakaondoka, kisha polisi wakawafata na kuwauwa majumbani mwao ulete. Bila hivyo nahisi tutakesha kwa vile naisoma dhamira yako barabara.
 

Nimekupa mtengo wa maswali yangu nashukuru umeingia dhumuni langu ilikuwa watu wakusome fikra zako dhidi ya Uislam na Waislam.

Ninakuacha na Suratul Anfal: Aya ya 55-59 ukipa wasaa jaribu kuipitia Inshaa'Allah.
 

Jasusi,

Mtu umekuwa Katibu wa TAA Tawi Makerere, Katibu wa TAA Tabora.

Halafu hujui jina la Katibu wa TAA Taifa.

Hii kali labda nikuulize wewe ni Katibu wa Chadema tawi la Marekani humjui jina Katibu wa Chadema taifa.
 
Jasusi,

Mtu umekuwa Katibu wa TAA Tawi Makerere, Katibu wa TAA Tabora.

Halafu hujui jina la Katibu wa TAA Taifa.

Hii kali labda nikuulize wewe ni Katibu wa Chadema tawi la Marekani humjui jina Katibu wa Chadema taifa.
Kwanza tuwekane sawa.
Chadema tawi la Marekani lina viongozi wake. Na mimi si mmoja wao. Pili, Mohamed ametuarifu kuwa Nyerere alifahamiana na Sykes mwaka 1953. Wewe unambishia?
 
Nimekupa mtengo wa maswali yangu nashukuru umeingia dhumuni langu ilikuwa watu wakusome fikra zako dhidi ya Uislam na Waislam.

Ninakuacha na Suratul Anfal: Aya ya 55-59 ukipa wasaa jaribu kuipitia Inshaa'Allah.

Ritz; Mbona unachomoa. Issue hapa ilikuwa kwamba baada ya Mkapa (huyu anafanya dhulma, ameuwa waislamu) ameingia rais hayo ya waislamu kufa hayapo tena. The momemnt ushahidi unaanza kuwekwa hadharani wewe unaniambia soma surah fulani ya Quran. Kwa kifup Ritz ni kuwa hizo aya nne ulizokimbilia zinaongelea jambo tofauti ndugu yangu (somo lake kuu ni kuwa: Sanctity of treaties has been enjoined and the Muslims commanded to observe them as long as the other party does not break them. Anfal 55 - 59) isome hii kwenye; Quran - Surah Al-Anfal - Maududi's Translation, Commentary and Summary. Ili tusidanganye watu hapa. Hakuna aliyevunja mkataba hapa. Wala usiseme nimekutega. Hamna samaki JF. Wewe hukujiandaa na ukweli kuwa wamekufa watu tena waislamu ndani ya huu utawala wa JK. Sasa soma hiyo report nyingine uone kama unaweza kuhimili kuilinda ile kau;li yako ya awali. Pia hukujua Kilombero walishauwawa wakata miwa wakati wa Mwinyi. Nakuongezea mwaka jana waliuwawa watu 26 Tarime. http://www.state.gov/documents/organization/186460.pdf

Ama kuhusu masuala ya taasisi tofauti za kidini kuomba na kupewa na mkuu wa nchi ni taratibu za nchi za nchi. Lakini kiongozi hawezi kuwapa au kuwanyima watu kwa sababu wakina fulani hawajaomba au mpaka waombe. Kama unalingine lete. Ukiweza omba msaada.
 

Jasusi,
Abdu Sykes alikutana na Nyerere 1952.
 

Wickama,

Ni tabu labda wewe kuniamini lakini kuhusu
BAKWATA niamini mimi ni "authority" katika
somo hilo.

Waislam kwa miaka mingi sasa hawashughulishwi
na BAKWATA.

Waislam wanahangaishwa na ustawi wao na katika
hili zipo taasidi nyingi nchi nzima zinajiendesha kwa
juhudi za Waislam.

Kwa hiyo si kweli kuwa Waislam wanaihitaji BAKWATA.
 
Mzee Mohamed,
Mwogope Mungu wetu. Yaani Mufti, Alhad Mussa Salum,..., sio watu? Hili la kutoikubali wewe BAKWATA limekuwa neema na baraka kwa nchi yetu. Hata CCM, CHADEMA, TEC, CCT, sio sote tunazikubali taasisi na asasi hizi.

Wild Card,
Kusema hakuna watu ni lugha.

Maana yake hawaungwi mkono na wengi.

Historia ya BAKWATA ni mbaya ndiyo maana
haikubaliki.

Ikiwa unadhani BAKWATA ina hadhi sawa na TEC
hakuna wa kukuzuia.
 

Naona unajichanganya mie nakueleza habari za polisi kuvamia Msikiti wewe unaniletea habari za Chadema kwa hiyo Chadema ni chama cha Wakirsto.

Nataka unipe orodha ya Makanisa mangapi yamevamiwa na polisi na kupigwa mabomu.

Nipe na orodha ya Maaskofu wangapi wamekamatwa na polisi na kufungwa.
 
Nimekupa mtengo wa maswali yangu nashukuru umeingia dhumuni langu ilikuwa watu wakusome fikra zako dhidi ya Uislam na Waislam.

Ninakuacha na Suratul Anfal: Aya ya 55-59 ukipa wasaa jaribu kuipitia Inshaa'Allah.

wewe ritz nawe unaubongo gani wa kumpa mtu mtego.. Hapo nachoona hujajibu hata hoja moja ya wickama
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…