As much as you people want to prove me wrong kwa kejeli na dhihaka, I will bring this to the light.
Lazima uelewe kuwa Mohamed ameonyeshwa kuwa mzigo aliobeba umeandikwa na mtu mwingine.
Hicho ndicho chanzo cha yeye kushindwa kuelewa tofauti ya ''Addresing na addressed''.
Mwanakijiji ameeleza vizuri sana.Mohamed amekiri kuwa kwa ''taarifa' alizokuwa nazo habari ndivyo kama alivyosema.
Pili, kwa kutambua maudhui ya alichokisema tulimwambia Mohamed asiseme ''kahutubia'' bunge bali semina au kinginecho.
Mohamed akaja na tarehe 15 May 2003. Tena akisema kama tungefanya tafiti tusingeuliza swali la namna hiyo.
Hakuishia hapo akazidi kutoa kashfa na kejeli kwa kutambua kuwa alikuwa sahihi.
Sasa ninyi mnaosema kuhusu maudhui, mnasema kitu gani wakati mhusika ametoa tarehe?
Tatu, katika mada yake kuna tukio na wahusika. Tukio ni kuhutubia bunge, wahusika ni wabunge na balozi.
Kwa mtu mwenye weledi lazima atajiuliza wanaofanya tukio hilo liwe katika mizania iliyopo ni akina nani?
Jibu ni wabunge na balozi. Mohamed kumtaja balozi na bunge haikuwa bahati mbaya ilikuwa ni makusudi kuonyesha sheria hiyo kandimizi kwa waislam ilivyoshiinikizwa.
Nne, kwavile bunge halikukaa siku hiyo na kwavile balozi hakuhutubia bunge, maudhui yote yanakuwa hayana maana.
Hayana maana kwasababu tukio limekosa viunganisho viwili muhimu, bunge na balozi.
Kwamba hakuna uhusiano wa dhahiri kati ya sehemu hizo mbili katika tarehe 15 May 2003.
Tano, tumeona mada halisi iliyoandikwa ambayo Mohamed ameinukuu. Technically hata kama ametaja aliponukuu, hapa jamvini amekuja na hoja kuwa ni paper yake na wala hakusema sehemu ya paper yake alinukuu kutoka kwa bwana fulani.
Hilo halina tatizo, tatizo linatokea pale ambapo anabeba dhamana ya maneno yale ambayo ni Tarehe 15 May 2003.
Mwisho, bila yeye kufanya utafiti kuhusu taratibu za bunge na itifaki za kibalozi, Mohamed akabeba mkoba hadi Ibadan akakalisha watu kitako na kueleza kisicho cha kweli. Kisicho cha kweli kwasababu leo watu wa Ibadan wanajua kuwa balozi anaweza kuhutubia bunge la Tanzania kitu ambacho hakijawahi kutokea.
Kwa mfano rahisi sana wa mitaani, mbunge X alimtukana mwenzake Z wakiwa katika baa wanakunywa.
Hilo ni tukio litakaloandikwa katika vijarida vya udaku. Lakini Mbunge X aliposema 'F' ndani ya bunge basi bunge zima lilizizima na nchi nzima kulaani. Kwanini? Jibu ni kuwa ametumia tukio(mkutano wa bunge) na wahusika(wabunge) ndani ya bunge(eneo) kusema neno baya.No one is talking about his/her topic any more.
Huu ni mwendelezo wa exaggerations za Mohamed (rejeeni post 13112 ya Mag3 ).
Sijui kwanini hamuoni mantiki iliyopo.
Mohamed amekashfu sana sisi wengine kuwa mahakimu kiruka, hatukafanya tafiti japo kidogo, atatuweka kwenye kundi alisoloweza kulisema n.k. Mbona hamjamtaka aombe radhi kuhusu hayo baada ya ukweli kujulikana mnajitahidi kushambulia walioweka ukweli wazi.
Mkoba wa Ibadan una tarehe Baru baru acha utetezi wa mitaani, mwenye mada hakuja na utetezi alikuja na tarehe tena akiwa ame-bold kuonyesha msisitizo na uhakika.
Nafikiria Mtu aseme Rais Mandela wa Nigeria amehutubia UN mjini Carcas venezuela kuhusu Malaria, ati tukubali tu kwasababu kuna neno malaria! Hell no!