Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
Mzee Mwanakijiji, Mohamed Said, Nguruvi3, Jasusi,
..yaani hata kwenye winter la Edinburgh SCOTLAND Mwalimu alikuwa anadunda na kaptura, suruali ameijua alipokutana na wazee wa D'Salaam??
Companero,
..ile document uliyosema utatuletea vipi mkuu?
..au umeanza likizo mpya?
Tena kaweka wazi kabisa. Ndio maana nilisema lile bandiko lake la ukurasa fulani hapo nyuma sijui aliliweka kwa makusudi au bahati mbaya.
Limeonyesha hata Nyerere alivyokaa na akina Sykes kutafuta mstakabali wa Tanganyika siyo Waislam.
umeshindwa hoja unaanza kejeli na kashfa.Kinachofurahisha mpaka sasa hamjatoa historia mbadala iliyosahihi.Nyinyi mnapinga yaliyoelezwa na Mohamed Said.Haya basi leteni hiyo historia iliyo sahihi hamna.Mjadala mmeuanzisha wenyewe sasa unawatoa jasho.
Niko hapa kufahamisha ile historia ambayo wengi hawakuwa wakiijua.
Laiti kama nisingeandika historia hii...
Mengi muhimu yasingefahamika.
Labda tumuulize Bw. Said swali jingine la moja kwa moja: Je Dossa Aziz aliwahi kukutana na Nyerere au kushiriki na Nyerere mkutano wowote wa TAA kabla ya 1953? Wapi na Nyerere alishiriki kama nani?
Unakwepa kitu ulichokizungumza wewe mwenyewe? Umesahau uliposema uvaaji wa kaptula halikuwa jambo la ajabu kwa tanganyika?Naomba mimi ndugu zangu msinihusishe na hii historia ya ''kaptula.''
Kwa kweli hainipendezi na inanivunjia muruwa wangu.
Nihusisheni na historia ya kudai uhuru hilo ndilo somo ninalojua.
Naomba mimi ndugu zangu msinihusishe na hii historia ya ''kaptula.''
Kwa kweli hainipendezi na inanivunjia muruwa wangu.
Nihusisheni na historia ya kudai uhuru hilo ndilo somo ninalojua.
Hoja za kipuuzi huletwa na watu wapuuzi kama wewe. hivi kuna mjinga gani waleo utakaemdanganya na utumbo wako huu? nani asiyejua wapigania uhuru wa nchi hii ni waislam tangu ukoloni wa kijerumani, soma akina Abshiri, Hasan Omar Bin Makunganya na wengineo walionyongwa (mungu awarehemu) walivyopinga utawala wa wakoloni. narudia tena, hivi huoni hata aibu kuleta mada ya uongo kama hii? mchana kweupe na uongo weupe? Mirembe panakufaa sana wewe.
Vitu vidogo vidogo ambavyo kwa kweli linaua raha ya darsa.
Hiki si kitu kikubwa.
Nimeeleza kuwa Dossa kakutana na Nyerere Dodoma mwaka
1946 katika mkutano wa African Association.
.
Unakwepa kitu ulichokizungumza wewe mwenyewe? Umesahau uliposema uvaaji wa kaptula halikuwa jambo la ajabu kwa tanganyika?
Umesahau uliposema umeishi Scotland na umeona ni washamba tu?
Yani unakana vitu ulivyovitamka wewe mwenyewe hapa?
Hii inaenda katika kiini cha simulizi lako. Kama Dossa Aziz alikutana na Mwalimu mwaka 1946 kweli unataka watu waamini Dossa hawakuwa impressed na Nyerere huyu? au Mwapachu anapokutana na Mwalimu wakiwa masomoni habari za Nyerere hazijafika kwa wazee wao Dar?
Hivi umeuliza mzee John Rupia alisikia habari za Nyerere kwa mara ya kwanza wapi?
Mohamed,Nsame hawawezi kuandika chochote watu hawa.
Hiyo historia hawana.
Huko nyuma nilisema unaweza kuwaambia Wachina waandike
historia yao ya ''holocaust?''
Jibu ni kuwa hapana.
Kwa nini?
Kwa sababu hiyo si historia yao.
Ndiyo maana unaona wanalazimisha kila kitu kianze na Nyerere.
Sasa ukiwaeleza ukweli ulivyokuwa cha kwanza ni kuhamaki cha
pili kejeli na matusi.
Mzee Mwanakijiji Nguruvi3 Jasusi Mag3 Yericko Nyerere na mkuu Sweke wakuu mmejenga hoja za maana sana ila nasikitika maswali humu hayajibiwi kabisa inasikitisha kama mtu anashindwa kutetea kitabu chake,nazidi kujifunza hapa asanteni sana kwa hili darasa
Vitu vidogo vidogo ambavyo kwa kweli linaua raha ya darsa.
Hiki si kitu kikubwa.
Nimeeleza kuwa Dossa kakutana na Nyerere Dodoma mwaka
1946 katika mkutano wa African Association.
Kwani hili ni jambo muhimu kiasi swali linarudiwa mara kwa mara,
mara kwa mara...
Vitu vizito ninavyokuwekeeni hapa hamuulizi.
Nimeweka nyaraka kati ya Ally Sykes na Kenneth Kaunda 1953.
Kimya.
Nimeeweka hapa mkutano wa Abdu Sykes na Kenyatta, Kungu
Karumba, Bildad Kaggia...1950.
Kimya.
Nimeeleza mambo mengi.
Kimya.
Muhimu ni lini Dossa alikutana na Nyerere.
Nimeeleza Dossa alikuwa tajari sana na alisaidia mno TANU.
Dossa kafa masikini katika hali ya kutisha.
Hakuna maswali nini kilitokea.
Sasa hata kama nia ni kusema kuwa Nyerere akijulikana Dar es Salaam
pale TAA New Street basi ndiyo kweli kwa kujuana na Dossa Dodoma 1946
ndiyo atakuwa maarufu Dar es Salaam nzima?
Mnanistaajabisha sana.
Mohamed,
Hakuna mtu anayelazimisha kila kitu kianze na Nyerere. Lakini hata kama kila kitu kilianza na wazee wako wa Gerezani, hiyo ilikuwa ni chapter one tu katika kitabu kizima cha harakati za uhuru wa Tanganyika. Na katika chapta zote, baada ya kumaliza chapter one na wazee wako wa Gerezani, by the time unafika chapter seven, wazee wako watakuwa wameshasahauliwa kwa sababu dynamics za harakati zilikuwa zimeshabadilika na kupanuka Tanganyika nzima, ambako wazee wako wa Gerezani hawakufika, lakini Nyerere alifika. He no doubt was the star of the Tanganyika independence movement. Hiyo haiwezi kubadilishwa. He was chosen by history to play that role and he will forever remain so.
Kuna wakati Mugabe alikuwa analalamika sana kwamba anakuwa sidelined baada ya Mandela kutoka jela. Nilipata bahati ya kuongea na Mwalimu Nyerere juu ya malalamiko ya Mugabe. Mugabe alifikiri kuwa kwa sababu Zimbabwe imepata uhuru kabla ya Afrika kusini, yeye ndiye aliyepaswa kuwa kama prominent leader na amu-overshadow Mandela. Mwalimu alinijibu kuwa "historia ndiyo iliyom-assign Mandela the role of prominence" na hata Mugabe akilalamika kwa kiasi gani hawezi kubadilisha hiyo role ya historia. The same applies to Mwalimu and the wazee wa Gerezani.
Kwakuzingatia hoja yako ya awali kuwa Nyerere aliingizwa katika siasa na Abdu mwaka 1952, na kwakuzingatia kuwa Mwalimu Nyerere alikuwa hafahamiki na yeyote katika wale wazee wa AA na TAA,
Je mwaka huo 1946 Mwalimu Nyerere alihudhuria mkutano huo wa AA huko Dodoma kama nani na alikuwa akitokea kanda ipi?
Utajibu swali mtu lenye tija na maana.
Huwezi kujibu kila kitu.
Huwa vilevile sijibu kejeli na matusi.
Hebu tafakari haya hapo chini:
Hivi hatuwezi kutoka hapa tukasonga mbele katika mambo muhimu
yaliyopitika katika historia ya Tanganyika.
Mbona sipati maswali kuhusu watu muhimu sana lakini hata siku moja
hawakupata kusikika.
Mathalan.
Huyu Idd Faiz Mafongo alikuwa na umuhimu gani kiasi kuwa yeye akabidhiwe
kukusanya fedha za safari ya Nyerere UNO?
Huyu Idd Faiz ndiye alikuwa mweka hazina wa TANU 1954 na hapo hapo mweka
hazina wa Al Jamiatul Islamiyya...
Huyu Idd Faiz alihudhuria mkutano wa kwanza wa TANU pale Arnatouglo...
Huyu Idd Faiz na nduguye Idd Tosiri ndiyo waliomtambulisha Nyerere kwa Sheikh
Mohamed Ramia wa Bagamoyo ambae alikuwa ndugu yao.
Hawa walikuwa Wamanyema kizazi cha pili kuzaliwa Tanganyika.
Yote haya hamyaoni umuhimu wake.
Nyie ni Nyerere, Nyerere, Nyerere...
Hamtaki kujua habari za wale waliokuwa pamoja na yeye.
Ajabu sana.
Nini kinakutisheni?
Hapana mzee hili ni muhimu; wewe umekusanya historia ya wazee wako wa Dar tangu wakati Nyerere anakuja na tumeona baadhi ya video ambapo baadhi ya watu mbele zakow anasema kwa kejeli kuwa Nyerere alifundishwa kuvaa suruali na wazee hao na wewe hujakanusha. Ama unakubali kuwa ni kweli au hujathubutu kuwauliza wazee wako ili uwasahihishe hawa wanaosema hivi.
Inaelekea hili swali mmelipenda sana.
Soma nyuma nimetoa maelezo.
Hivi hatuwezi kutoka hapa tukasonga mbele katika mambo muhimu
yaliyopitika katika historia ya Tanganyika.
Mbona sipati maswali kuhusu watu muhimu sana lakini hata siku moja
hawakupata kusikika.
Mathalan.
Huyu Idd Faiz Mafongo alikuwa na umuhimu gani kiasi kuwa yeye akabidhiwe
kukusanya fedha za safari ya Nyerere UNO?
Huyu Idd Faiz ndiye alikuwa mweka hazina wa TANU 1954 na hapo hapo mweka
hazina wa Al Jamiatul Islamiyya...
Huyu Idd Faiz alihudhuria mkutano wa kwanza wa TANU pale Arnatouglo...
Huyu Idd Faiz na nduguye Idd Tosiri ndiyo waliomtambulisha Nyerere kwa Sheikh
Mohamed Ramia wa Bagamoyo ambae alikuwa ndugu yao.
Hawa walikuwa Wamanyema kizazi cha pili kuzaliwa Tanganyika.
Yote haya hamyaoni umuhimu wake.
Nyie ni Nyerere, Nyerere, Nyerere...
Hamtaki kujua habari za wale waliokuwa pamoja na yeye.
Ajabu sana.
Nini kinakutisheni?