Sio kweli unashambuliwa personal uoga wako tu, wewe na mzee Mohamed Said, nani anashambuliwa personal.
Wewe unaweza kujiona unaweka hoja za maana kumbe ni majitaka watu wanashindwa Kufyonza Ilm.
Nani alikudanganya Palestine ni ya waislam peke yao?
Mwl Nyerere alikuwa anaitetea Palestine kutokana na Bethelem na Nazareth pamoja na Jerusalem, Yesu alizaliwa wapi?
Tarudi baadae kufyonza Ilm.
Ahaa kumbe basi Palestina si waislam watupu! hilo nilikuwa nalifahamu na nimeliandika sana hapa.
Niliweka kwa vile wapo wanaoamini kuwa Palestina wanaonewa kwasababu ya Uislam na si haki zao kama raia wa dunia. Unafahamu kisa cha Bait al Muqadas kwa ufupi tu.
Sasa hapo unaniunga mkono kuwa Nyerere hakusimama na wapalestina kama waislam, wala Polisario kama waislam kama ambavyo alisimama kidete kuhusu Kaburu na Mreno. Nadhani unaelewa.Kipi cha ajabu akisimama kidete kuhusu zanazibar kama basi alifanya hivyo? Kwanini ionekane ni udini?
Nilidhani pia ungekuja na majibu naona hakuna, nasubiri Big show huenda akaja na majibu.
Sitegemei kwasababu mtoa Ilm Mohamed hana majibu mwaka wa pili anaulizwa na anakimbia kimbia hovyo.
Kwanini nasema kuna ilm ya asali na ilim majitaka.
Nasema hivyo kwasababu lazima uwe na uwezo wa kuchambua mambo.
Nadhani nimekueleza kuhusu fikra na Theology. Kwasababu ya kufyonza ilm bila fikra kuna mtu kasema kumzuia mwislam kutenda jambo baya ni jambo zuri. Nilipomuuliza kwanini tukimzuia Mohamed asitende mambo mabaya tunaonekana wakorofi, akaingia mitini. Huyo kafyonza hakuwa na fikra
Kama utakubalina nami unatakiwa uwe na fikra vinginevyo utatangulizwa mbele ya maandamo wenzako wakiwa wamekaa na lap top wanaeleza kichapo chako na mateso yako. Sababu kubwa ni kukosa fikra
Mathalan, mtu akikutupia kitu na kusema Tanganyika ilifanya sensa mwaka 1957 bila kukuambia nani kafanya, halafu ikifanyika mwaka 1967 na kisha mwaka 1970, unaweza kufyonza kama Ilm lakini ujue hapo hakuna ilm ni maji ya uani yelipouliziwa manukato.
Hivi unakubali kuwa kuna ilm mtu akikuambia kuwa kiwanja kilichouzwa na waislam kikanunuliwa na waislam ni dhulma ya serikali. Kuna elimu mtu anapokuambia tafuta kichwa kimoja ua kwa siri! Kuna ilm mtu akikuambia kuwa kuua kunahitaji maulamaa hata kama anayeuliwa hana kosa au hatia.
Ilm inahitaji fikra si kufyonza tu spike lee.
Hata machungwa ya nyumbani Mtindiro unafyonza maganda unatupa, sasa wewe unameza kila kitu kwasababu ni chungwa!
Hebu waulize wenzako eti fikra maana yake nini? Ya znz naona mazito, naona nikupe shule ya Theology unasemaje?