Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Mohamed Said,

Unachosema ni kweli kabisa mimi takupa kisa kimoja wala hakina muda mrefu.

Pale Msikiti wa Kichangani Magomeni kulikuwa na mzee mmoja walikuwa wanamuita makoti amefariki mwezi uliyopita makazi yake yalikuwa hapo hapo Msikitini.

Kipindi cha mwisho wakati mgonjwa kuna kauli alikuwa anazitoa anaelezea unyama waliokuwa wanaufanya Zanzibar wakati wa mapinduzi huwezi amini yule mzee watu wengi walimchukia hata wale waliokuwa wanamsaidia.

Yule mzee alikuwa ni Mmakonde walitokea Tanga kwenda Zanzibar.

Bora yule mzee angekaa kimya wala watu wasingejua.
 
Last edited by a moderator:

Haahaaa ooooho safi sana,

Nimefurahi sana kusikia kuwa safari yako Berlin ilianzia Tanga,

Huenda hii ndio ulikuwa mwanzo wakuzuru mataifa!

Mimi safari yangu ya WTC na Pentagon ilianzia ITV pale chini ya Godwin Gondwe,

Nakumbuka vema ilikua nia jioni nikamfuata Dada Sauda Simba Kilumanga na kumwelezea kile nilichonacho na akanifikisha kwa Gondwe,

Kisha Mr Gondwe akaniambie nifike saa 10 alfajiri tayari kwa kipindi "live" kinachochukua saa moja,

Ilikuwa ni siku ya maadhimisho ya mashambulizi ya Pentagon!

Baada ya kipindi kile ndipo safari za magharibi zilipojongea hadi Pentagon na WTC!
 

Yericko Nyerere,

Siku zote mtu muongo kazi sana kuwa na kumbukumbu.

Wewe juzi tu umetuambia Marekani walikupa mualiko baada ya kuandika kitabu chako cha ugaidi.

Leo tena umekuja na habari mpya za ITV sijui hicho kipindi ulikuwa unaongea nini wakati kwa mujibu wa maelezo wako kitabu chako bado hakijatoka kipo ubalozi wa Marekani.

Kumbuka leo mwezi wa tano unakatika ulisema humu ukimbini kuwa utaenda TBC kuchukuwa hotuba ya Nyerere inauzwa.

Yericko unatuchanganya ndugu yangu.
 
Last edited by a moderator:

Ritz
,
Ndipo hapo ninapowaeleza jamaa zetu kuwa wao wanaisoma
historia ya mapinduzi.

Sie tunaishinayo.
 


Anajichanganya mwenyewe tuh,haeleweki mara alialikwa mara alijipeleka ili mradi apate tuh la kuongea,
Kuishiwa kubaya sana...
 

Ritz unamatatizo sana ya kuelewa!

Hivi kufanya mahojiano na kituo cha runinga ni lazima kitabu kiwe tayari kimechapwa?

Sasa nakujuza upya kuwa nilifanya hahojiano na ITV nikiwa na mswaada wa kitabu hicho, hata Ubalozi waliniona kupitia ITV ndipo wakanifuata na ushirikiano wetu ukanza hadi mwaliko wa Pentagon!

Soma vizuri maandishi yangu hapo juu ndugu yangu!

Kinachonishangaza nikuwa Ritz wewe ni mmoja wa wakongwe hapa jf, lakini uwezo wakung'amua mambo haupandi wala haupungui!

Yani Ritz yule wa mwanzo ni yule yule wa leo!

Jamani tuwe waungana tuitendee haki jf, tutumie maarifa yatokayo hapa kwakukuza fikra zetu sio kila siku upo vilevile!
 
Last edited by a moderator:

Small minds discuss people like Ritz, whilist big mind discuss ideas...
 
Last edited by a moderator:

Yericko,
Hujui kitu.

Hujawa na makamo ya kuandika ukasomwa.
Hapo chini ni mimi namzungumza Ali Nabwa:

''But strange never at any one time did he mention to me that he had just been released from prison. I only came to know about that many years later when I met Jim Bailey and he handed me a manuscript ‘Tanzania the Story of Julius Nyerere.' I met Jim Bailey in early 1990s.

Jim Bailey was the proprietor and executive editor of ‘Drum' a photo-journalistic magazine published in South Africa and distributed in almost all English speaking African colonies. Drum was a very popular magazine. Its popularity only waned after most of African countries gained their independence and the new leadership in Africa seemed to be enjoying founding fault with the publication.

Drum was banned in many African countries for various reasons, from publishing nude pictures (scanty dressed girls) to not observing the right etiquettes when reporting ‘sensitive' government matters. I was introduced to Jim Bailey by Ally Sykes.

Jim Bailey had a manuscript and wanted someone to go through it and give recommendations on the work. It was a book of collection of old photograph with captions and articles in between from Bailey's African Photo Archives in Johannesburg . Bailey travelled from Johannesburg to Dar es Salaam to see Ally Sykes and show him the manuscript.

Ally Sykes recommended me to Jim Bailey and it was in this way that I met him and he gave me the manuscript to read. It was through this manuscript that I came for the first time face to face with Nabwa's pen through his Prison Letters.

The letters introduced Nabwa's mind to me in a way that I can not find words to describe. In those letters Nabwa's pen was not writing but weeping and whipping. The words from Nabwa's pen were taking me to a different world which even in my wildest imagination I never thought existed. The first letter written in 1973 from Central Police Station Dar es Salaam shocked me. In that letter Nabwa described intimidation and torture by the police in the style replica of the Ton Ton Macouts of Papa Doc's Haiti .

That was not all among those arrested with him was Badru Said. This was a person I knew, an uncle of a friend of mine. In Nabwa's sense of humour in the letter he says it needs a Dickens to describe the squalor of the cell he was in. The letters which followed were all from Condemned Section Ukonga Prison with the exception of one from Muhimbili Hospital where he was hospitalised.

I remember reading those letters I some times found myself laughing not because the paragraph was in any way amusing but for the mockery and absurdity of it all. But that alone would not have made me laugh. It was that cynicism banking on satire which made me laugh at the tragic events unfolding instead of shading tears. Nabwa's pen ‘entertained' me in a way that I had not experienced before.

In his analysis of the personalities which people were made to believe were symbols of justice and principles Nabwa's pen removed the charade and the camouflage to reveal their true colours and identity. Nabwa's letters were a potpourri of short biographies, dossiers, profiles, hit list of ‘enemies' and method of their execution. In the Prison Letters Nabwa's pen exposed the atrocities which took place in Zanzibar after the revolution and analysed the arrogance, mediocrity and sheer myopia of the leadership.

Bailey had this to write on the letters:

''When I came by the letters of Ali Mohamed Ali – a Comorian islander, formerly manager of the Dar es Salaam branch of the East African Publishing House – written from Ukonga Gaol in Dar es Salaam , describing gaol conditions, they turned my stomach. I checked them against the story of a totally independent former prisoner in Ukonga. They tallied. I checked them against the record of a former Ugandan prisoner. They tallied. I discussed them with a former senior member of Tanu in Dar es Salaam . He confirmed that those were the conditions. I did not publish them since it would have put paid to any chance of publishing again in Tanzania.''

After finishing reading the manuscript I wanted to meet Nabwa and give him his letters as I knew he would not have copies and he would love to have them back. At that time he was Personal Assistant to the Vice President Dr Omar Ali Juma. I was able to get Nabwa's telephone number through an acquaintance at Masomo Bookshop in Zanzibar and I called him. If Dar es Salaam has Saigon Club, Zanzibar can boast of Masomo Bookshop at Mkunazini. One can fix anything from there.

I travelled to Zanzibar and I met Nabwa. About ten years had passed since we saw each other. Nabwa was happy to see me and was beside himself when I presented the envelope full of photocopies of his prison letters. He wanted to know how I came by them. Typical of him Nabwa began asking me if I could recognise the personalities behind he initials and innuendos he had used in the letters instead of real names. I told him some I could. Nabwa revealed to me the true identities of the characters. Some of them were people personally known to me.

Now looking back I am happy that I was among those privileged to read Nabwa's revelations of injustices in Zanzibar before he became a celebrity of sorts and his writings major topic of discussion in the corridors of power. The atrocities which no one had the courage to speak about them publicly for almost forty years were laid bare for all to read through Dira the paper which Nabwa founded in 2004.

Dira was the first free newspaper in Zanzibar since the revolution. The ripples from Nabwa's pen were electrifying. Dira became a paper eagerly awaited by the public including Zanzibar leadership each week. Its circulation rose each passing week. Nabwa's pen was lifting the lid in broad daylight. The stories of treachery, rape, murder, homosexuality, forced marriages by members of the Revolutionary Council and their cronies in Zanzibar were all there with names, places and accomplices for all to read and pass judgement.

Those who had demonised the Sultan had no tongue to defend their own ‘upright' track record. The young generation began to ask questions and in the answers they saw the leadership in power and the revolution in a different light all together.

Nabwa's pen helped the young generation to understand why those in power abhorred democracy and were constantly haunted by the ballot box. They now knew why the leadership in the government shivered at the prospect of losing power. The young generation now realised why the leadership would go to any length to cling to power even to the extent of committing more atrocities just to remain in power through massive vote rigging.

What more the young generation realised why those in power were trying to build a dynasty. The government did not have the courage or the strength of character to contradict Nabwa's pen. The only way out for the ruling clique was to harass Nabwa, revoke his citizenship and muzzle him by banning Dira. But government's revenge upon Nabwa had come too late as to some extent Nabwa's pen had completed its mission.

The last time I saw Nabwa was at his Dira office at Vuga. I had gone there to congratulate him for the work he was doing through the paper. I called him when Dira was banned and his citizenship revoked. I had a pressing matter which I wanted to discuss with him. I asked him if we could meet in Dar es Salaam . He told me that if he leaves the isles, Zanzibar Government will not let him in again. That was Nabwa. Much as he was haunted through intrigues Nabwa was not a person to be cowed. He challenged those in power to take him one on one. The authorities did not have the stomach for that.''
 

Jasusi,

Najua wewe na wenzio mna allergy na Vitabu/sources za Wanataaluma wa akili za Madrassa,kwa hiyo haina haja ya kukusumbua akili zako nyingi kwa kukupatia hizo credible sources zangu kuhusu Biafra Conflict. Endelea tu na hiyo Ilm yako kutoka kwa hao Slave Masters.

Hiyo Dinner ya Nyerere Clan sio ilonichafua,naipenda mno maana najua ilikua ni yale madikodiko ya Mshume Kiyate. Kama ungelisoma uzuri ile post yangu ungeona yakuwa kilichonitafir na ile dinner table talk yenu...yakuwa watu wanachinjana na huyo Nyeyere wako akishiriki halafu ati mnapongezana!? vipo vitu vya kuleta maskhara hapa jamvini,lakini sio inapohusu masuala ya bin-Adam kutolewa roho zao!

Shamte alichaguliwa kihalali kwenye uchaguzi wa 1961.

The results of of June 1961 election saw ZNP&ZPPP alliance with 13 seats and ASP secured 10 seats.
The Alliance formed the first internal Self Rule Government with Mr. Mohammed Shamte as The Chief Minister.

Zanzibar was given full Independence in Dec 10th. 1963. The first Governmemt was formed by a Coalition of ZNP&ZPPP. Mr Mohammed Shamte,of the ZPPP became the first Prime Minister and Sultan Al Khalifa Jamshid Ibn Abdullah remained as the Head of State.

On Dec 16th. 1963,Prime Minister Mohammed Shamte,as Head of the Independent and Sovereign Government of Zanzibar,delivered a speech what was to be a historic speech to the United Nations General Assembly in New York.....and the rest is "History"!

Huyo Nassor Moyo wako; ni mojawapo ya viroja na vitimbi vya hayo maafa ya 1964...Seremala kugeuka Waziri na yule mtengeneza matofali kugeuka Field Marshal!? Wala si MZanzibary. Kama yuhai nipa salaam na sikose kumuuliza akutajie uzuri kwao ni wapi!? Yawezekana ni mwenzio wa huko huko Mara!?

Ahsanta.
 
Kwa muda mrefu nimekuwa nafuatilia thread hii lakini sikutaka kuchangia chochote, Maandiko ya Mohamed Said na uchambuzi wa Ndg Yerico Nyerere wote wameweza au hawakuweka kukidhi haja za wasomaji ambao kwa bahati mbaya wanaamini andiko la Mohamed Said ama kinyume chake.

Kitu kimoja ambacho wakoloni na watafuta maslahi waliweza kukifanya au wameweza sasa, ni kuwachonganisha waisilamu na wakristo. Hili halikufanyika hapa Tanzania tu bali hata pengine pote Duniani.

Hapa, nichangie tu kuthibitisha uchochezi huu ambao ulianza miaka mingi na bado unaendelea. Haya ni maneno ya Sheikh Thabit Kombo Jecha.

".............African Association iliundwa mwaka 1933 kwa msingi madhubuti wa kuaminiana na kukubaliana waafrika wote wa shamba na mijini, lakini ilipita katika vizingiti vingi kabla ya serikali kuitambua.Kama unavyojua, wakati huo waafirika wengi hawakuwa na elimu wala maarifa ya kuongoza Association kama sheria zilivyokuwa zinataka.. Kwa sababu hiyo waafirika wakakubaliana kwa kauli moja kuwa uongozi wapewe waafirika wenye mwanga wa elimu na wenyekujua mipango ya Association. Ikatokea kwamba wakati ule waafirika waliokuwa wanajua mipango ya Association na wenye kujua kusoma kidogo wakawa wenzetu wa Kikristo tu. Kwa hiyo tukakubaliana kumuweka Raisi wa chama hicho Mwl. Augostino Ramadhani, na mwandishi Bwn Paul Seme Sindi, na Bwn Fedha Ndg William Lyimo.. Katibu msaidizi Sajin Athuman Juma; Yeye alikuwa askari katika vita vikuu vya kwanza , na kwa sababu hiyo alijaliwa kuerevuka kidogo.

Kwa muda wa mwaka mmoja tu African Association ilikwisha pata zaidi ya wanachama 56,000, na mimi nikiwa mmoja ya wanachama hao.Michango mingi ilitolewa kwa hiari kabisa, na chama kikashamiri. Nguvu hiyo ikawatisha wazungu na waarabu, ambao hawakupenda umoja wetu, na tofauti za dini zikatumbukia kutuvuruga. Waisilamu wakashawishiwa kutoka katika chama kwa kutishwa kwamba madhali viongozi wote wa chama hicho ni wakiristo, basi na wao siku moja watabatizwa.. Kulikuwako taratibu za kuimba nyimbo za siasa za kuhamasisha umma, na watotot wa kike wawili, Damarias Njelwa na Grace Lyimo, walikuwa wakitunga nyimbo za siasa kwa sauti zinazo fanana na zile za kanisani, na viongozi wote wa African Association katika hadhara hiyo wakavua kofia. Wakati huo Damarias na Grace wote walikuwa viongozi wa Association. Tena kwa kawaida ya dini ya Kiisilamu wanawake hawachanganyiki na wanaume, na kitendo cha wale akina mama kilionekana kama kihoja hivi. Basi ule ushawishi ukakolea , na waisilamu wengi, hasa Washirazi, wakaondoka taratibu bila hata ya kutoa taarifa. Na mimi niliacha chama cha African Association kwa sababu hiyo iyo, lakini walikuwako waisilamu wengine walioendelea na chama"

Maelezo haya nimeyanukuu kutoka kwenye kitabu cha 'MASIMULIZI YA SHIKH THABITH KOMBO JECHA" kama kilivyoandikwa na Minael-Hosanna O. Mdundo Ukurasa wa 43-44.

Katika maelezo haya na mengine, Thabit Kombo, anaeleza jinsi wakoloni walivyoweza kupenyeza fitina za udini ili kuvuruga umoja harakati za waafirika kujenga umoja ili kuupinga unyonyaji wa wakoloni. Hapa, Thabiti Kombo, mmoja ya Wazanzbar waliopata kushika nafasi kubwa kabla na baada ya uhuru, anatubu na kukiri hiana hii ambayo ilimtumbukiza yeye mwenyewe hata akaamua kuachana na African Association.

Wapo waisilamu wachache wanao amini Nyerere aliwabagua waisilamu, hili wameliweka km sehemu ya imani yao. Ni ngumu kuwaeleza na kuwaondoa kwenye hoja hii. Jambo moja nawaomba, ni afadhali wasithubutu kupoteza muda wao kuiaminisha Dunia ya waisilamu inayokuja, kwamba Nyerere alikuwa mdini. Yerico amejitahidi kupingana na hoja hizi za udini wa Nyerere, nami nampongeza kwa udadavuzi wenye weleji mkubwa wa vihistoria hivi muhimu, hata hivyo ni jukumu zaidi la Mohamed na maswahaba zake kujichimbia na kutafuta ukweli wa upande mwingine na uongo wa hayo wanayoamini.

Nawasilisha.
 

Asante sana ndugu yangu kwamchango wako na simulizi hiyo nzuri ya mzee wetu Thabiti Kombo,

Ningeomba nisahihishe kidogo katika simulizi hiyo,

AA iliundwa mwaka 1927 na sio 1933,

Rais wake wakwanza alikuwa Mwalimu Cesil Matola na Katibu wake alikuwa Klest Sykes,

Mwaka 1933 ndipo Mwalimu Cesil Matola alipofariki na chama kikashikwa na Klest na waambata wengine!

Nimefurahi sana kusikia kuona mzee wetu Thabiti Kombo ni sehemu ya wanachama wa AA!

Safi sana!
 

Barubaru,

Waalyka Salaam Al Akhiy.

Wallahi,mchana huu ndo napitia hizi posts hapa,nakuta yale madhila alokufanzia huyo Yericko katika yale majibizano yenu.

Unajua hawa jamaa mila,taratibu na dasturi zao ni tafauti saana na sisi. Ndo maana mimi binafsi hii Topic naiepuka mno. Na pia nalijaribu kumpa wasia kiduchu huyo Yericko kuwa haya majambo kwetu sisi wengine ni sensitive mno,nilidhani angefanya hishma japo kiduchu lakini naona wameshindwa.

Kama umepitia zile posts za jana,nilijibizana nae kiduchu mno tena kwa makhnatha tu maana nilihisi alitaka kunianzia mimi vile vituko vyake. Ati yeye nae anataka kujaribu kunikhadith khabari za yale maafa ya 1964!?ahaha!!

Embu fikiri,hawa jamaa mpaka kesho ati wanaamini yakuwa huyo "Field Marshal" "alipindua" Zanzibar kwa ngumi kavu kavu na masumbwi mazito mno!? Na kumbuka yakuwa wana ushahidi kutoka papers za CIA!?ahaha!!

Lakini lazim niseme;huyo Yericko alinichekesha kiduchu pale aliposema ati mojawapo ya sifa kubwa za huyo "Field Marshal",ilikua kitoweo chake ni mapaka!ahaha!! Nasikia na hii pia CIA wamethibitisha!ahah!!

Pana mengi mno Al Akhiy,lakini Insha Allah tutafika nao taratibu...Falyafrahu Qalilan Wa Yahku Kathiran!

Naona jana umetaja kiduchu khabari za Shangani na Mwera...nilihisi tunafahamiana tangia nilipoingia hapa na kuona hiyo picha yako. Lakini tusijuane sana hapa jamvini maana italazim tuwe wazito kiduchu kunena tutakayo baina yetu!ahaha!!

Nakupa hints kiduchu; pale Shangani Al Marhum Ali Amrani na nduguye Said Amran na Mama yao Hobo alifariki kitambo maskini. Hapo Kianga ndipo khaswa umefika, pale ndani kiduchu Mwangarani unapakumbuka,Al Marhum Bwana Salum wa Mkunazini ndo alokua akishughulika kule mwishoni!? Pale Mwera Legeza Mwendo na Maili Sita vipi!? Kwenye ule Msikiti wa Kianga kabla ya kuvuka kidaraja pia paliuliwa jamaa wengi hiyo siku ya maafa.

Unajua huyo Bwana Mohammed Salim nduguye Salim Ahmed,ameoa mmojawapo ya Aunt zangu. Na kwa sasa nafikiri wanapaendeleza uzuri pale Kianga. Insha Allah tutazungumza uzuri siku nyingine.
Nafurahi Al Akhiy Ritz kawawekea ule mpini mubashar kutoka kwa Ahmed Rajab. Nimecheka maana namjua Bwana Ahmed Rajab,hana stahamala akianza kutiririka na kalamu. Kamchambua japo kiduchu,lakini imesaidia kuwaonyesha jamaa hapa yakuwa huyo "Field Marshal" wao alikua ni mgonjwa wa akili na maarifa!ahaha!! "Rais wa Nchi" ati akishinda Rahaleo pale Radio kutwa kucha kutangaza makhanatha ya kutisha ndugu na jamaa zetu,bila ya maarifa yoyote!...Khabith mkubwa yule!

Nimesikitika kiduchu,maana naona huyo Mag3 ati kaleta taarifa yakuwa family ya huyo "Field Marshal" imekumbwa na njaa na madhila yaso kifani huko kwao Uganda. Sasa sijui ndo twatakiwa tuwachangie senti au vipi...kwa hili binafsi tasubiri amri toka kwa Al Akhiy Shariff Ritz ili atoe maelekezo na Fatwa yake!

Ahsanta.

Cc;Ritz
 

Yericko,

Mbona unaanza kutuletea maneno ya kutuvunjia hishma!? Unakuwa akili zako kama yule mwanaharamu wa Kiganda a.k.a "Field Marshal"!

Bila ya kujali mtazamo wako katika hiyo "Historia yenu" lakini kumbuka sisi wengine Family zetu zilimwaga damu pale! Na hili nilishakufahamisha awali tena kwa njia ya kistaarabu.

This is a little advice to you. Stop acting like you know everything. Please talk about sucking lollipops not what happened in Zanzibar 1964.

If you never hear the words manners and dignity it's much much more difficult to comprehend.

Most importantly,before you learn the word or concept,you never could know that you needed to learn it or that anything was missing.

Probably you are "a learned man". Then you should decide if what you learned is valid,or useful,or just propaganda as you go and after you understand it,not before hand.

A bad attitude is like a flat tire as you can't go anywhere until you change it.

I hope this help.

Shukran.

Cc;Ritz
 

Ritz,

Salaam Al Akhiy.

Hii mipini na bayana zako ni khatwari ilo salama! Nakusoma kwa utuvu mwingi.

Nakusifu saana,maana nimebaini yakuwa hawa jamaa takriban woote wapo hapa kwa ajili ya Crusade. Na pia wengi wao ni hao Chadema.

Ndo maana pale ajapo mtu na kuwaambia ati yeye ni "Muislam",na akaungana nao kuendeleza hizi dhuluma na kebehi zao hapa jamvini,basi wao hufarijika mno!

Embu jaribu ku-imagine hicho chama chao ndo kiingie madarakani,halafu Cabinet iwe na hawa kina Nguruvi3,Mag3,Mwanakijiji na huyo Yericko wao!?ahaha!! Wallahi,nchi zetu za ki-Afrika ni comedy tupu!ahah!!

Kwa sababu nimechungulia Threads mbalimbali kiduchu na kuona ule "mpambano" wako na wao na mipini yako adimu ukijibishana nao. Mimi binafsi hizo local politics hapo zimenitupa mkono maana ni kitambo sasa. Halafu hayo mambo yao ya Udini huku wakijivisha ngozi za Uzalendo na u-Atheist,mimi nakua sina asilan interest na topics kama hizo. Ndo maana huona mara nyingi najiepusha nazo mno.

Lakini Al Akhiy, mimi nakufahamu na ni vyema ufanyavyo. Maana nyinyi ndugu zetu mlo karibu nao na kuwajua kwa kina udhaifu wa nyoyo zao kuwanyooshea maneno japo kiduchu ni wajibu.

Naona jamaa yako ati kaleta taarifa/barua ya madhila na njaa iso kiasi ilowasibu family ya yule "Filed Marshal" huko Uganda!? Mimi nangojelea Fatwa yako,je ina khalis!?aahaha!!

Napenda afanyavyo Sheikh Mohammed;maana anapumzika kwa utuvu na kuwaacha jamaa wakichacharika na kufurukuta kuleta vitabu vilotungwa na wenzao. Halafu wakimaliza yeye anarejea tena kiduchu na kuwatwanga naMpini mwingine, tena kwa ustaarabu na utaratibu laini kabisa!ahaha!! Wallahi,rah ilioje inakua kama vile niko Royal Theatre!ahaha!!

Ahsanta.

Cc;The Big Show
 
gombesugu,

..kabla mnakasha huu haujaendelea naomba niweke mambo machache sawa.

..kwanza, kwetu sisi watu wa BARA, kuna tofauti kati ya MUARABU na MZUNGU.

..MUARABU kwetu ndiye SLAVE MASTER kutokana na ushiriki wake ktk kukamata WATUMWA.

..MZUNGU yeye tunamtambua kama MKOLONI kwasababu alifika hapa na kuanzishwa utawala wa mabavu wa kikoloni.

..suala la pili ni kuhusu uhuru wa mwaka 1963, uchaguzi wa Zanzibar, pamoja na MAPINDUZI.

..Uhuru wa Znz wa mwaka 1963 haukuwa halali. kwetu sisi tunaufananisha na ule Uhuru wa kina Ian Smith wa Rhodesia.

..Uchaguzi uliofanyika na matokeo yake hayakuwa halali kwasababu chama kilichopata kura nyingi na viti vingi kilishindwa kuunda serikali.

..utaratibu wa uchaguzi wa Znz ulikuwa umetengenezwa kwa namna ambayo WAAFRIKA na chama chao cha ASP wasingeweza kushika madaraka na kuongoza serikali.

..ZPPP walitakiwa kuunda alliance na ASP,chama kilichoshinda uchaguzi,hatimaye kuunda serikali. sasa hapo unaona vyama vya Kiarabu, vilivyoshindwa uchaguzi, vimeungana na kuwatenga Waafrika walioshinda uchaguzi ktk kuunda serikali.

..Kwa msingi huo ndiyo utaona kwamba sisi watu wa BARA tunaona serikali ya Mohamed Shamte haikuwa halali, hata kama sheria za uchaguzi zilikuwa zinawaruhusu kufanya waliyofanya.

..Katika mazingira yale ya sheria za uchaguzi na vitimbi vya Waarabu kuendelea kuwakandamiza Waafrika basi MAPINDUZI yalikuwa lazima.

..Mwisho, vile unavyomuona Hassan Nassoro Moyo kama mtu wa kuja hapo Znz ndivyo hivyo hivyo na sisi watu wa BARA tunavyowaona Waarabu na utawala wao wa Kisultani kwamba nao ni "wakuja"/ "alien" ktk ardhi ya Waafrika.

..Baada ya kusema hayo sasa naomba kwa heshima na taadhima mnakasha huu uendelee.

cc: Ritz, THE BIG SHOW, Jasusi, Mag3, Kibunango, Kadogoo, Nguruvi3, Wickama, Barubaru
 
Last edited by a moderator:

JokaKuu,

Salaam. Nimependa hayo majibu yako.

Nitakujibu kiduchu tu;yakuwa haiyumkini asilan ati wewe JokaKuu uwe M'bara au MTanganyika zaidi kuliko mimi Gombesugu...hasha,asilan abadan! Na nina vithibitisho vingi mno kwanini nakuambia hivi. Labda muhimu ni kuwa sisi soote tunaishi na tuna asili ya hapa Afrika.

Usije kunipa kicheko kwa kutaka kunita Racist!?ahaha!!

Lakini iko siku nitakunyambuliana kiundani hapa hapa jamvini,ili ujue kwanini nalisema hivi.

Nakukumbusha yakuwa mimi si Mwarabu,bali mimi ni Mswahili.

Ahsanta na tuendelee na mnakasha ndugu yangu.
 

Umenena vema kabisa mkuu!
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…