Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Hata Dr Slaa ana data zake anasema alishinda uchaguzi.

Hayo matokeo ya Mag3 wala hakuna jipya uki-google utayapata matokeo zaidi ya mia wewe mwenyewe utaamua uchukue yapi ambao yanakupendeza.

Nikikuuliza unamjua mkuu wa tume ya uchaguzi Zanzibar aliyetangaza hayo matokeo ututajie hata jina hujui. Kazi yako kufuata mkumbo tu.

Kuna sehemu huko nyuma nilikwambia kuwa itendee haki jf,

Hivi wewe mwenyewe umesema wazi kuwa gogu inakupatia hizo takwimu za uchaguzi, sasa iweje upate takwimu za chaguzi hizo na kisha ushindwe kupata majina ya wenyeviti wa chaguzi hizo?

Lazima upevuke ndugu!

Kimsingi Qualification za mjadala huu, ndiomaana sometimes unapuuzwa na ukijibiwa basi mjibuji aliona hana kazi kwa mda ule!
 
Kuna sehemu huko nyuma nilikwambia kuwa itendee haki jf,

Hivi wewe mwenyewe umesema wazi kuwa gogu inakupatia hizo takwimu za uchaguzi, sasa iweje upate takwimu za chaguzi hizo na kisha ushindwe kupata majina ya wenyeviti wa chaguzi hizo?

Lazima upevuke ndugu!

Kimsingi Qualification za mjadala huu, ndiomaana sometimes unapuuzwa na ukijibiwa basi mjibuji aliona hana kazi kwa mda ule!

Ni kweli mie mnywa kahawa tena ni kichwa cha madrassa.
 
Nitajitahidi kutafuta kwenye hifadhi za kumbukumbu,

Mshume Kiyate inafahamika wazi kuwa alikuwa rafiki wa karibu na mzee, nitajitahidi kupata picha zao pia.


Ha haa haaa, mimi na wewe nani wa kupuuzwa humu ukumbini.

Wanaukumbi hebu msomeni wenyewe huyu jamaa anajifanya mtoto wa Julius Kambarage.

Cc.. gombesugu, THE BIG SHOW, Kadogoo,
 
Last edited by a moderator:
Ha haa haaa, mimi na wewe nani wa kupuuzwa humu ukumbini.

Wanaukumbi hebu msomeni wenyewe huyu jamaa anajifanya mtoto wa Julius Kambarage.

Cc.. gombesugu, THE BIG SHOW, Kadogoo,

Nini chaajabu kwako hapo?

Ninaposema Mwalimu Nyerere ni Mzee wangu, Joseph Warioba ni mzeee wangu, Paul Boman ni Mzee wangu, Joseph Butiku ni Mzee wangu, Abdul Sykes ni Mzee wangu, Kingunge Ngombalemwiru ni Mzee wangu, unaelewa nini hapo?

Usiwe mkubwa wa mwili na umri tu lakini akili za kijiko cha chai!

Mohamed Said anaposema Shehe Hassan Bin Amir ni mzee wake unaelewaje?

Wewe unaposema Abdul Sykes ni mzee wako unaelewa maana yake!

Nilishasema huna Qualification za kujadiliana na mimi, nakustahi kwakuwa ni binadamu unaepumua!

Kimsingi nakupuuza! Na sitakujibu kwa upuuzi wako huo!
 
Last edited by a moderator:
Mzee Mohamed Said nimefarijika sana hili haujalikanusha,wapo baadhi ya wanajamvi wasiotaka kushughulisha akili zao walitaka Nyerere awachekee Masheikh waliotaka kuyumbisha usalama wa nchi.

Yericko,
Huyo anazungumza ni Mohamed Omari Mkwawa.

Dk. Ghassany kaweka yote kama yalivyokuwa ili
historia ikae sawa kwa wasomaji wa kitabu chake.
 
Last edited by a moderator:
quote_icon.png
By Ritz
Yericko Nyerere,

1} Mzee wako alipokuwa hai alikuelezea chochote kuhusu wazee wa kariakoo katika harakati za kutafuta uhuru.

2} Tupe ushahidi kuwa Chifu Maliale ndiyo aliyetoa pesa za kumpeleka Mwalimu Nyerere UN.

3} Kabla Mwalimu Nyerere ajafariki ameishawahi kuuwambia ni nani aliyekuwa rafiki yake kipenzi wakati yupo TANU. /QUOTE]




MAJIBU

1) Swali hilo linajibiwa na nukuu ya mwalimu Nyerere niliyoiweka kwe uzi maalumu pale juu.



2) Kama ulifuatilia vema mjadala wangu na Mohamed Said juu ya kisa hicho nilisema mwezi kesho nitakwenda Butiama nitajitahidi walau kupata picha ya msaada huo wa Chifu Marealle

3) Sikumuuliza na hakuwahi kuniambia, lakini mimi ninajua kuwa alikuwa Mzee Mshume

Swadakta,

Wanakumbi mtaamua wenyewe hapa tena Yericko anajinasibisha kuwa Julius Kambarage ndiyo baba yake walikuwa wakiishi pamoja.

Siku zote ukiwa muongo unapoteza kumbukumbu, tawaletea kisa kingine cha huyu dogo analazimisha nasaba.

Anaenda mbali zaidi kuwa Nyerere alikuwa akimuadithia habari za marafiki zake kina Mshume Kiyate kwenye viwanja vya Ikulu, ha haa haa teh teh!
gombesugu, Jasusi,
 
Last edited by a moderator:
Swadakta,

Wanakumbi mtaamua wenyewe hapa tena Yericko anajinasibisha kuwa Julius Kambarage ndiyo baba yake walikuwa wakiishi pamoja.

Siku zote ukiwa muongo unapoteza kumbukumbu, tawaletea kisa kingine cha huyu dogo analazimisha nasaba.

Anaenda mbali zaidi kuwa Nyerere alikuwa akimuadithia habari za marafiki zake kina Mshume Kiyate kwenye viwanja vya Ikulu, ha haa haa teh teh!
gombesugu, Jasusi,

Bado unazidi kuonyesha ulivyo na upeo finyu,

Watanzania mamia wamekuwa wakimiminika Nyumbani kwa Hayati Mwalimu Nyerere, najiuliza sana, Niini kinachokustua nikisema nitakwenda kupata picha hiyo?

Hhivi wewe huna uwezo wa kwenda Butiam nyumbani kwa Hayati Mzee Nyerere na ukapata data yoyote unayoitafuta tena data yenyewe ni picha?

Mimi kila mwaka huwa nakwenda kuhiji pale kaburini, ukitaka wasiliana na mimi twende wote mwezi wa sita kesho kutwa tu!



Pole sana! Naishia hapo juu ya hili sitakujibu
 
Last edited by a moderator:
Bado unazidi kuonyesha ulivyo na upeo finyu,

Watanzania mamia wamekuwa wakimiminika Nyumbani kwa Hayati Mwalimu Nyerere, najiuliza sana, Niini kinachokustua nikisema nitakwenda kupata picha hiyo?

Hhivi wewe huna uwezo wa kwenda Butiam nyumbani kwa Hayati Mzee Nyerere na ukapata data yoyote unayoitafuta tena data yenyewe ni picha?

Mimi kila mwaka huwa nakwenda kuhiji pale kaburini, ukitaka wasiliana na mimi twende wote mwezi wa sita kesho kutwa tu!



Pole sana! Naishia hapo juu ya hili sitakujibu

Bora ukimbie maana mipini ikikuwa inakuja tena kupitia mabandiko yako mwenyewe unanadhani watu wajinga humu unaweza kuongea pumba zako bila kuhojiwa.

Mbona haujawaambia wanaukumbi habari za Mshume Kiyate, Nyerere alikuwa akikuadithia wapi kwenye viwanja vya Ikulu au Butiama.

Yericko usikimbie mnakasha watu wanataka utupe habari za mzee wako.

Cc.. Ben Saanane,
 
Last edited by a moderator:
Yericko Nyerere,

Dawa siyo kukimbia jibu hoja wewe ndiyo umejinasibisha na Nyerere kama mzee wako mbona unakuwa tena mkali ukihojiwa.

Mbona Jasusi, tunamuhoji mambo ya ndani ya Nyerere pamoja na familia yake anatoa ushirikiano kama mwanafamilia.

Wewe unataka kumuhoji Mohamed Said, kuhusu wazee wake anakujibu pamoja na kutoa kejeli kuwa wazee wa vibarazani wanywa kahawa na watu wa madrassa.

Wewe tumekuomba tu kwa faida ya wanaukumbi tujuze Nyerere alikuwa anakuadithia wapi habari za Mshume Kiyate.

cc.. gombesugu, Jasusi,
 
Last edited by a moderator:
Mzee Mohamed Said nimefarijika sana hili haujalikanusha,wapo baadhi ya wanajamvi wasiotaka kushughulisha akili zao walitaka Nyerere awachekee Masheikh waliotaka kuyumbisha usalama wa nchi.

Ngongo,
Tatizo la Baraza la Wazee wa TANU na Nyerere halina
uhusiano hata chembe na usalama wa nchi.

Ilikuwa ni hofu tu kuwa Waislam wakiwa na nguvu kama
ile waloonyesha wakati wa kupigania uhuru ukristo utakuwa
mashakani.

Waislam walimpenda sana Nyerere.
Isome historia niliyoandika hili liko wazi kabisa.
 
Juu ya Karume

Ninachofahamu kwa kabila ni Mnyasa,alikuwa mfanyakazi wa bandari (kuli) na alikuwa mwanachama mtiifu wa ASP,

Kuingia kwake madarakani kulitokana na ASP chama kilichoungwa mkono wazalendo wengi napia kiliungwa mkono na Tanganyika (Julius Nyerere),

Karume hakuingia mtaani kupambana na Sultan, Siku ya mapinduzi yeye alikuwa Dar,

Karume alikabidhiwa madaraka mizi sita baada ya mapinduzi, hilo lilitimia kutokana na juhudi za Julius Nyerere kumshawishi Okello akabidhi madaraka kwa chama kinachoungwa mkono na wengi, kumbuka Okello hakuwa na chama chochote cha siasa!

Hapo swadakta.. Narudi kidogo kwenye uhuru wa Tanganyika., Hili pia ningependa na Mzee wetu Mohamed Said alitolee ufafanuzi. Katika mojawapo ya maandiko ya wanazuoni nguli wa Zanzibar niliyopata kuyapitia kwa umakini mkubwa yanaelezea namna ambavyo Baba wa Taifa, akiwa katika TANU alivoanza kuwa na mgogoro na baadhi ya wazee wa kiislamu.

Anaeleza kuwa, mara tu baada ya Uhuru, mwalimu alikutana kwa siri na baadhi ya viongozi wa juu wa kanisa katoliki, hasa maaskofu na waliliweka Taifa la Tanganyika chini ya usimamizi wa Bikira Maria, na hii ikafanywa kuwa formal kabisa.

Baadae alipowaomba kuzikabidhi shule za makanisa chini ya Serikali haikuwa vigumu kwa kuwa tayari walikuwa "wanazungumza lugha moja". Tukio hili la kuliweka taifa chini ya Bikira Maria lilifanywa kwa siri kubwa, lakini kwakuwa ndani ya Serikali walikuwepo viongozi wa kiislamu kama vile akina Mzee wetu Mkwawa (R.I.P), Zilivuja na kuwafikia baadhi ya masheikh wakubwa Tanganyika hasa wa Tabora na Dsm..

Hawa wasingekubali kunyamaza, na huo ukawa mwanzo wa maelewano tete kati ya mwalimu na wenzake wa TANU, hasa wale waislamu. June 1962, masheikh hawa waliamua kuonana na Mwalimu ili kuweka wazi madukuduku yao.. Hata hvo, yasemekana mwalimu alikuwa na baadhi ya masheikh ambao "wangemtetea popote hata kupinga imani zao", na hata katika mazungumzo hayo, walisimama kidete kumtetea mwalimu.

Sina shaka hili pia lilihusishwa na uundwaji wa BAKWATA, na waliotengeneza BAKWATA ya mwanzo walikua hawa ambao waliiva katika chungu kimoja na Mwalimu, wakati wengine walipinga vikali uanzishwaji wake.


Hebu wanazuoni wangu naombeni mnichambulie vizuri hii habari ya Bikira Maria kufanywa msimamizi wa Taifa na mgogoro kati ya mwalimu na masheikh., pana ukweli ama ni porojo za kwenye gahawa?
Kwako
Yericko.
Mohamed Said,
Ritz,
Nguruvi na wengine wote...
 
Tunataka source ya hizo takwimu zako,
Hatupo hapa kuangalia mapambo yako ya majedwali bila kutupa references na sources za statistics zako,
Tuna akili zetu timamu sisi...
Upo sahihi mkuu, lakini naomba umshauri ndugu yetu Ritz naye atuletee source ya taarifa hii nyeti;
Alichokifanya Nyerere baada ya uhuru Kilichofuata baada ya kupatikana uhuru ilikuwa ni kukamatwa, kuwekwa kizuizini na kuhamishwa kwa masheikh na Waislamu wengine waliodhaniwa kuwa wanapinga utawala wa Nyerere.
Mashuhuri miongoni mwao walikuwa: Abdillah Schneider Plantan, Sheikh Abdulkarim Abdulwahid, Maalim Popo Saleh, Suleiman Masudi Mnonji, Ali Migeyo, Mufti Sheikh Hassan bin Amir, Sharff Hussein Badawiy, Shariff Mwinyibaba na Shariff Adnan
Wengine ni Bilali Rehani Waikela, Sheikh Jumanne Bias, Maalim Matar, Abdalah Mwamba, Sheikh Hashim Haji Abdallah, Sheikh Nurdin Hussein, Salum Abdallah Popo, Sheikh Mzee Ali Comoriam, Sheikh Al Amin Maftah, Rajab Kiguu cha Mbuzi na wengine wengi.
Lakini ukweli ulikuwa kwamba si wote katika wale waliokamatwa na kuwekwa kizuizini walijihusisha na siasa. Baadhi yao walikamatwa kwa sababu tu walikuwa wakishirikiana na wale waliodhaniwa ni wapinzani wa Nyerere.
Maalim Matar na Shariff Adnan walifungwa jela kwa sababu tu walihusika na msikiti wa Badawiy mjini Dar es Salaam ambako Sheikh Hassan bin Amir, wakati huo akichukuliwa kuwa ndiyo roho ya waumini wa Tanganyika, alikuwa ikiendesha madrasa yake kila magharibi pale msikitini.
Shariff Hussein na nduguye Mwinyibaba walihamishiwa Kenya, walikotoka si kwa sababu walikuwa wamejishughulisha katika harakati za kuipinga serikali, ila lakini kwa sababu walikuwa waangalizi wa msikiti wa Badawiy.
Sheikh Mzee Ali Comorian alitiwa kizuizini kwa sababu kila mara alikuwa akifuatana na Sheikh Hassan bin Amir kama vile alikuwa kivuli cha sheikh. Huenda kile kilichomfanya Nyerere kuwatia kizuizini masheikh na wengine kuhamishwa ni kufuata ule msemo wa Biblia usemao, 'yule ambae hayuko nasi basi ni dhidi yetu'.
Jinsi siasa na za Tanzania zilivyobadilika na jinsi Nyerere alivyoanza kuonesha uadui dhidi ya Waislamu kulimsikitisha sana Abdulwahid. Alishindwa kuelewa uhasama huu ulikuwa unatoka wapi. Alihisi kuwa anahusika na yale yaliyokuwa yanawapata Waislamu. Mawazo haya yalimzonga kama jinamizi. Kwa ufahamu wake alikuwa akidhani matatizo yote ya udini walikuwa wameyashinda toka miaka ya 1950. Mwaka 1953 Abdulwahid akiwa Muislamu na akiungwa mkono na Al Jamiatul Islamiyya aligombea kiti cha urais wa TAA na Nyerere, Mkatoliki.
Abdulwahid alishindwa uchaguzi ule. Waislamu hawakuuchukulia uchaguzi ule kama uchaguzi kati ya Muislamu na Mkristo. Kilichotazamwa ni uwezo wa wagombea.
Nyerere alikuwa amemzidi Abdulwahid na kwa ajili hii alichaguliwa kuiongoza TAA. Abdulwahid alikumbuka ugomvi wa Sheikh Suleiman Takadir wakati ule Mwenyekiti wa Baraza La Wazee wa TANU. Sheikh Takadir aliwaonya Waislamu wachukue tahadhari kwani Nyerere atakuja kuwapendelea Wakristo wenzake pale atakaposhika madaraka. Kama walivyofanya Waislamu wengi, Abdulwahid alimuunga mkono Nyerere na kumpinga Sheikh Takadir.
Wakati ule Abdulwahid aliamini kama Waislamu wengi walivyoamini kuwa Sheikh Takadir alikuwa anataka kuleta siasa za kibaguzi ambazo alikuwa anaziegemeza katika dini. Abdulwahid aliona udini aliokuwa anataka kuuleta Sheikh Takadir lilikuwa jambo ambalo lingeiletea hatari Tanganyika.
Abdulwahid alikufa mwaka 1968 wakati nchi ikiwa imegubikwa na hasama za chinichini kati ya Waislam dhidi ya serikali ya Nyerere ambae sasa alikuwa amehodhi madaraka yote katika serikali.
Umoja wa kitaifa, moja ya maadili ambayo yeye(Abdulwahid ) aliyapigania katika maisha yake yote katika siasa ulikuwa unahatarishwa. Halikadhalika umoja wa Waislamu ulikuwa unaelekea kuvunjika. Kulikuwepo na kuwekwa kizuizini kwa masheikh chini ya Preventive Dentation Act of 1962.
Baadhi ya masheikh waliotiwa gerezani walikuwa watu waliomuunga yeye mwenyewe mkono wakati anaunda TANU. Baadhi yao aliwashawishi kumuunga mkono Nyerere na TANU katika kile kipindi kigumu cha harakati za kudai uhuru. Mwanakamati wa Kamati Ndogo ya Siasa ya TAA, Mufti Sheikh Hassan bin Amir, kiongozi wa ngazi ya juu kabisa kwa Waislamu alikuwa amekamatwa na kuondolewa nchini na kurudishwa kwao Zanzibar kwa amri ya Nyerere. Sababu iliyotolewa ya kukamatwa kwa Sheikh Hassan bin Amir ilikuwa alikuwa ati 'akipanga njama ya kupindua serikali'.
Sheikh Hassan bin Amir alikuwa kati ya Waislamu wachache ambao walithubutu kusimama kidete dhidi ya serikali na kutoa mawazo yake kuhusu jinsi serikali ilivyokuwa ikiwakandamiza Waislam. Kabla hajafa Abdulwahid alikuwa akifikiwa na habari kuwa Nyerere alikuwa alikuwa akiendesha kampeni makini sana ndani ya chama kuwafuta Waislamu ndani ya TANU.
Abdulwahid alikuwa anafahamu matokeo ya kuvunjika kwa umoja wa Waislam. Yeye alikuwa anajua vyema nguvu ya umoja wa Waislamu wakati walipokuwa wanapigania uhuru wa Tanganyika.
Abdulwahid halikadhalika alikuwa anafahamu nguvu ya wale waliokuwa nyuma na njama zile za kuwagawa Waislamu katika makundi hasimu. Vilevile alikuwa anatambua hofu na watu wote waliokuwa nyuma ya njama zile.
Alifahamu kuwa wale aliowapokea na kuwatia katika harakati za kudai uhuru sasa walikua na hofu na Uislam. Kama Uislamu ulitumika kuwaondoa wakoloni Uislam hautashindwa kuwatoa wao madarakani. Uislam ikiwa itkadi ya kupinga ukoloni sasa ilikuwa ni tishio kwa Ukristo katika Tanzania huru.
Kabla hajafariki dunia Abdulwahid alifanya mazungumzo na Nyerere. Mazungumzo haya baina ya Abdulwahid na Nyerere yalifanyika katika miezi ya mwisho ya mwaka 1968 wakati mashekhe na Waislamu mashuhuri wanasombwa na kutupwa gerezani. Abdulwahid na Nyerere walikuwa wametoka mbali. Watu hawa walikuwa marafiki wa zamani. Huenda kama isingelikuwa kwa msaada wa Abdulwahid historia ya TANU na ya Nyerere mwenyewe zingechukua mkondo tofauti.
Mazungumzo haya yalikuwa muhimu kwa Abdulwahid kwa sababu kwa kiasi fulani alihisi anahusika na yale yaliyokuwa yakiwasibu Waislamu, wale kutoka Dar es Salaam. Taarifa za Waislamu kukamatwa usiku na kuwekwa kizuizini zilikuwa zikimfikia karibu kila siku. Abdulwahid hakuweza kujifanya kuwa haathiriki na matokeo yale. Baadhi ya watu ambao Nyerere alikuwa anawatupa gerezani walikuwa watu ambao yeye Abdulwahid binafsi walimuunga mkono wakati anaanza siasa na watu ambao aliwashawishi wamkubali Nyerere wakati wa kuundwa TANU.
Abdulwahid alimwambia Nyerere huenda yeye akawa hana hisia wala uhusiano wowote na watu ambao yeye anatia sahihi wakamatwe na kutupwa gerezani. Lakini kwake yeye hao ni jamaa zake anaokutananao ama msikitini au mitaani. Yeye kama mtu anayeishi miongoni mwa Waislamu na zile familia zao alikuwa anaelewa majonzi yao.
Abdulwahid alimwambia Nyerere kwamba watu wale wanajua kuwa yeye, Abdulwahid ndiye aliyesamsaidia Nyerere wakati akiwa mgeni mjini Dar es Salaam, watu wakamjua na kumkubali na hivyo kuja kuweza kufika hapo alipofika.
Abdulwahid alimwambia Nyerere kuwa ndugu na jamaa za wafungwa wale wanamjia wakimbembeleza amsihi Nyerere awatoe ndugu zao jela. Abdulwahid alimwambia Nyerere kwamba kule kuwatia watu kizuizini ni uonevu kwa sababu wale watu hawana uwezo wa kupindua serikali yake.
Kwa sauti ya masikitiko Abdulwahid alimaliza maelezo yake kwa kumwambia Nyerere 'Naondoka hapa nikiwa nataka kuamini kuwa wewe Julius Nyerere, leo hujatugeuka.' Kwa maneno hayo Abdulwahid aliaga na kuondoka.
Alichosikia Nyerere kuhusu Abdulwahid baada ya maneno yale ilikuwa taarifa ya kifo chake jioni moja Jumamosi tarehe 12 Oktoba, 1968. Mkewe Mama Maria Nyerere, alizirai aliposikia habari zile za msiba. Alikuwa Abdulwahid ndiye aliyewapokea yeye na mume wake mara ya kwanza walipokuja Dar es Salaam.

ITAENDELEA....
 
Ndugu yangu gombesugu, macho ya binadamu hayana uwezo wa kuona mgongoni kwa mwenyenayo! ukiona hitilafu basi isahihishe bila kujali kama mwaka jana kulitokea nini. Lakini tukubaliane kitu kimoja kwamba hoja hujibiwa kwa hoja. Kama mtu akiiona hoja basi huo ndio utamu wa mnakasha. Lakini kuja jamvini kuwakarahisha watu wengine kwa kisingizio cha kumtetea mtu fulani hata bila hoja huo sio moyo wa kisomi. Kuhusu daraja la Nyerere, Mtume na Allah, nisamehe sana ndugu yangu, mimi sio mtaalam katika nyanja hiyo, na kuendelea kulijadiri hilo naogopa sana nisije nikakufuru au nikawaumiza watu wengine bila sababu. Katika mnakasha kuna kukwazika na mawazo ya watu wengine, busara ni kuyaheshimu mawazo hayo japo hata kama hukubaliani nayo. Lakini kusimama na kuyakejeli au kutukana siamini kama ni kuyanyamazisha.
Nakushukuru sana kwa kunivumilia.

Maulaga,

Salaam sana ndugu yangu.

Nashukuru mno kwa ustaarabu na maneno yako mema ulotumia. Huo ndo ubin-Adam na weledi wa hali ya juu.

Nami sitagusa wala kuongeza lolote katika hayo ulonena,zaidi ya kukwambia yakuwa nimefarijika mno kutambuana na muungwana kama wewe hapa jamvini.

Kabla ya kukuacha,takupa usia kiduchu. Hayo ulonena yakuwa "macho ya mwana-Adam hayana uwezo wa kumwonyesha yanyuma huyo alonayo". Hili ni kweli nami nakuunga mkono. Lakini taratibu hapa jamvini, pana jamaa waweza kutumia neno hilo hilo kukudhihaki yakuwa ati hujapitia au hujasoma mnakasha woote,sasa yanini kukurupuka au kuchangia hoja!...wenyewe wana msemo wao ati "umedandia Train kwa mbele" nafikiri!?

Nimekupa usia huo kwani mimi binafsi yalinikuta wakti najiunga na kuanza kuchangia hapa jamvini!

Nakutakia siku njema ndugu yangu natuendelee na mnakasha,kwa hishma na mahaba.

Shukran.
 
Jasusi,
Ninashangaa sana, unaposema ana PhD! Mkuu Barubaru hebu itendee heshima club ya PhD, hadithi za mitaani achia akina Al-akhyi. Come forward cogently and boldly. The street rumors belong to the street!

Muheshimiwa Nguruvi3,

Salaam.

Unafahamu nini maana ya Al Akhiy kwa utuvu,na kama unafahamu mbona unafanya tashtit zisizo maana "ndugu yangu wa Kicheba"!?

Napenda kukufahamisha yakuwa Al Akhiy Barubaru,siye pekee mwenye hiyo PhD hapa jamvini(kama PhD ndio kigezo chako cha kumuhishimu mtu na kumuona wa maana au msomi zaidi).

Hata hao "ma-Al Akhiy" unaowadharau na kuwabeza nao pia wanazo hizo "PhD zako" unazoziabudu.

Kama kuitendea haki "Club ya PhD",mbona unamuonea Barubaru peke yake!?

Kwani hujapata khabari kuna watu wa "Club" hiyohiyo ya PhD,wananyang'anya Wake za watu na kuwafanza Vimada wao...je ushawahi kuwaambia lolote!? Kumbuka udhaifu ni kwa mwana-Adam yeyote.

Hivi karibuni takujibu ile hoja yako,nisamehe nimezongwa na vijishughuli kiduchu.

Nashukuru kwa kunisikiza.
 
Juu ya Karume

Ninachofahamu kwa kabila ni Mnyasa,alikuwa mfanyakazi wa bandari (kuli) na alikuwa mwanachama mtiifu wa ASP,

Kuingia kwake madarakani kulitokana na ASP chama kilichoungwa mkono wazalendo wengi napia kiliungwa mkono na Tanganyika (Julius Nyerere),

Karume hakuingia mtaani kupambana na Sultan, Siku ya mapinduzi yeye alikuwa Dar,

Yericko Nyerere,

Naomba ufafanuzi japo kiduchu,hivi unafahamu nini maana ya neno "Kuli"!? Je pia unaweza kutofautisha vipi kati ya "Kuli" na "Hamali"!?

Kwa maelekezo yako hapo juu,je kila afanyae kazi Bandarini ni "Kuli"!?

Kwa "Historia" uliyofundishwa na unayoifahamu wewe,je Rais Karume alizaliwa wapi!?

Ahsanta kwa kunisikiza ndugu yangu.

Shukran.
 
Upo sahihi mkuu, lakini naomba umshauri ndugu yetu Ritz naye atuletee source ya taarifa hii nyeti;

Niwe radhi ndugu yangu maulaga, kwa kuchelewa kukujibu.

Source ya mipini hiyo imetoka kwa Mwalimu wetu wa historia Mohamed Said, pamoja na Masheikh na Wazee wetu ambao wengi wameishatangulia mbele ya haki mmoja wao tumemzika jana Ally Sykes.

Kama utapenda kufyonza Ilm zaidi bado wapo Wazee unaweza kumtafuta Mzee Abbas Sykes, Sheikh Bilal Waikela hawa wameishi zama hizo na Nyerere.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom