Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Wewe ndiyo unajichanganya wapi tumesema tunataka upendeleo tutake upendeleo kwa nani hili iweje.

Mohamed Said anaelezea historia ya Wazee wetu nyie roho zinawauma hakuna sehemu yeyote ambayo mmelazimishwa kuikubali.

Ndiyo maana mkashauriwa na nyie andikeni historia ya wazee wenu.
historia ya wazee wenu mbona mnaongezeachumvi ya upotoshaji?
mara oo nyerere kafundishwa siasa na wazee wenu, mara kaenda sokoni hana hata senti akitaraji kupewa japo thumni yakununulia pilipili hoho sokoni, mara kafundishwa kuvaa na wazee wenu, mara hakujua kiswahili vizuri, ..............
mkuu Ritz umesahau hayo yote mliyasema?
 
Hivi kwako wewe GRADUATE ni nini mpaka mtu atimize vigezo gani? huwezi kusema Ibn Battuta siyo GRADUATE.

Ritz; Baada ya salamu; Kwangu mimi "u-graduate" ni kigezo tuu watu wamebuni ili kuhalalisha matumizi wa tija ya watu katika Nyanja Fulani. Mara nyingi haina uhusiano na Intelligent Quetient (IQ)-kama spelling ni sawa, ambayo haswa ndiyo tunu mtu anapewa na Muumba wake.

Kwa maana hiyo, mtu kuwa graduate (all levels)haina maana ndiye mbora na mwenye IQ kubwa kuwashinda wenzie. Ukipitia kwa mfano wale wagunduzi wa Cordoba-spain na hawa walioanzisha branch kabisa za mathematics (Aljebra) yote ni zawadi ya IQ. Au Wamisri wa kale walianzisha calendar ya siku 365/yr based on appearance ya stars, hii ni zawadi ya IQ. Babu anawapatanisha wajukuu waligombana na kuhasimiana huku wao ni Maprofessa mpaka wanamkubali kuwa babu hapa Kaongea, ni suala la IQ. Hii ndiyo muhimu. Lakini kwa vile ni vigumu kuwapima kikamilifi watu kwa hili ndio maana madaraja ya elimu yanatumiwa ambayo kimsingi mimi sikubaliani nayo, ila sijui MBADALA.
 
Barubaru,
Sasa unachobisha ni nini? Nimesema Anna alisoma Canada na nilimtembelea kule. That is a fact. So did Madaraka. Wewe kauli yako ni kwamba Nyerere hakusomesha wanae. Uwongo. Mimi nimemaliza form 4 Aga Khan mwaka 1967. Sikuchaguliwa kwenda form 5 kwa sababu ya jeuri yangu. Nikaondoka kwenda Marekani ambako nimesoma Howard University hapa Washington. D.C. Sasa unajaribu kusema nini? Kuna mdogo wangu naye alimaliza form 4 akaja kusoma University of Maryland. Sasa hapo kwako issue ni nini? Unasema unajua mengi sana juu ya familia hiyo lakini unachoandika hapa ni uwongo na ngano za vijiweni. Ndio maana nikakukumbusha kuwa mtu wa Phd unahitaji kuwa mbobeaji kwenye utafiti na unachoandika hakikisha kina mantiki. Hayo ya vijiweni waachie wenyewe. Nina marafiki wengi tu enzi hizo air force waliochukuliwa jeshini baada ya form 4 na kwenda kusoma Canada. Sasa sijui hapo unataka kusema nini. Hata marehemu Ditopile, huyu alikuwa class mate wangu, alijiunga jeshini baada ya kumaliza form 4 pale Aga Khan kwa hiyo sioni ajabu kwa John Nyerere kujiunga na jeshi baada ya form 4. Ni wengi tu waliofanya hivyo.

Jasusi,

Nakupa pole sana kwa kutaka kupotosha ukweli. Siku zote marubani wa Air force ni lazima wawe form six na sio form four nao walianzia cheo cha cadet sio private. Kwa zamani kujiunga jeshi ilikuwa hata darasa la saba alikuwa anakubaliwa lakin kwenye taaluma kama Urubani tena wa fighter lazima awe form six . Sasa yeye aliingia kwenye kozi hiyo wenzake wote wakiwa form six yeye form four je hapo napo unaona ni kawaida hiyo?
Canada wamekwenda wengi jeshini ambao wengine ni mafundi wa ndege ambao walikuwa kule Angus Ontario .

Lakin kubwa carleton kuna Kozi nyingi kuanzia certificate, diploma mpaka Ph.D. sasa be specific ni level gani kwani kwenye Degree hakuna jina lake.

Kwa uwadilifu wa Nyerere nilitegemea watoto wake wangepita katika proper channel kama wananchi wengine lakin ndio hivyo tena. Uadilifu wake upo wapi?. Jiulize aliwalipia mwenyewe au alitumia pesa za wananchi wake kusomesha watto wake kwa njia za mkato mkato?

mwisho watoto wangu wapo hapo Silver spring , mary land na insh'Allah Ijumaa mosi nitakuwa hapo likizo ya siku tatu.

Tumia facts katika kuandika kwako na sio hisia. Nimekuuliza vipi niku PM majina ya graduates wote wa Carleton kuanzia 1073 -1990 uona kama unayonena ni sahihi?
 
Wickama,
Nitakuwa sina uadilifu ikiwa mimi naandika historia ya wazee wangu
naeleza makubwa walofanya katika kupigania uhuru halafu aje mtu
mwingine na yeye aeleze historia kama ya kwangu kisha mie nimpinge.

Siku zote nikisema na nyie andikieni historia za huko makwenu ili ijulikane
badala ya kunipinga.

Hii ya kutembea kwa miguu mwaka 1950 kutoka Usambaa hadi Tanga mie
nimeipenda sana nimefananisha na ile historia ya Mzee Said Chamwenyewe
aliyekuwa anapandabaiskleli kutoka Dar es Salaam hadi Rufiji akiuza kadi za
TANU.

Huu ni mwanzo mzuri.


Sawa MS; Baada ya Salaam, At last utaona jinsi ambavyo inawakera watu kupata impression kuwa ONE family is being amplified juu ya Watanzania wengine. You are a good writer MS. No doubt. Lakini mzee MS umeruhusu sana prejudice in your sights. NINA UHAKIKA KAMA NYERERE wazazi wangeingia in this country kama Mamluki wa kwenda KUUA wahehe na wasambaa kule Lushoto, saa hizi your books zingekuwa zimejaa idadi (estimates) za hao ambao BABU au BABA yake Nyerere aliua huko kwenye ajira yake ya kuwauwa Watanganyika. But you have with caution just said wazazi wa Fulani waliingia kama MAMLUKI. Ukafanya stahiki ya heshima kwa familia husika ukaishia hapo. Lakini unapokuja kwa yule unayemchukia inabidi hata aliye mpa Matango siku Fulani iwe historia ya Kitaifa. Hutumii mizania ya HAKI. One guy whose family started its establishment with the blood of Tanganyikans on its hand (we know what mercenaries DO) is being elevated at the expense ya another person whose fault is to have a different faith other than yours.

No wonder you see reaction ya people like Zumbe, kwa vile THERE IS NO WAY ON EARTH DAR ALONE AS A CITY/TOWN WOULD HAVE WON INDEPENDENCE WITHOUT THE RESOURCES OF THE UP COUNTRY REGIONS, NO WAY. On the other hand ukiwajibu watu simply kuwa NA NYIE ANDIKENI WHILE YOU CHURN OUT MATERIALS WHICH RIDUCULE the very people who brought hope and joy in their distant lands, I find you to be too assuming. In fact you sound RUDE.
 
Ritz; Baada ya salamu; Kwangu mimi "u-graduate" ni kigezo tuu watu wamebuni ili kuhalalisha matumizi wa tija ya watu katika Nyanja Fulani. Mara nyingi haina uhusiano na Intelligent Quetient (IQ)-kama spelling ni sawa, ambayo haswa ndiyo tunu mtu anapewa na Muumba wake.

Kwa maana hiyo, mtu kuwa graduate (all levels)haina maana ndiye mbora na mwenye IQ kubwa kuwashinda wenzie. Ukipitia kwa mfano wale wagunduzi wa Cordoba-spain na hawa walioanzisha branch kabisa za mathematics (Aljebra) yote ni zawadi ya IQ. Au Wamisri wa kale walianzisha calendar ya siku 365/yr based on appearance ya stars, hii ni zawadi ya IQ. Babu anawapatanisha wajukuu waligombana na kuhasimiana huku wao ni Maprofessa mpaka wanamkubali kuwa babu hapa Kaongea, ni suala la IQ. Hii ndiyo muhimu. Lakini kwa vile ni vigumu kuwapima kikamilifi watu kwa hili ndio maana madaraja ya elimu yanatumiwa ambayo kimsingi mimi sikubaliani nayo, ila sijui MBADALA.

Intelligence Quotient~IQ.

Tuendelee na mnakasha hujue wa magharibi wanawachukuliwa watu kama Ibn Battuta siyo GRADUATE kutoka na elimu zao ukiangalia mtu kama Ibn Battuta alikuwepo miaka 1304 mpaka 1369 vitu alivyofanya ni vikubwa sana.

Umetaja University of Cordoba ni baadhi ya vyuo vilivyoleta mapinduzi ya elimu duniani wakati huo Ulaya na Marekani bado kuna giza kubwa la ujinga.

Kimsingi Islamic Scholar hawakubariki kwenye nchi za magharibi ingawa wao ndiyo wameleta elimu kubwa huko kwao.
 
Yericko Nyerere,

Wanaukumbi ndiyo wataamua, wapi nimeleta matusi na kejeli naona "mipini" imekuchanganya sana nionyeshe wapi nimekutukana? kwa faida ya Wanaukumbi nashindilia Mpini mwingine halafu utasema matusi.


Wanaukumbi nadhani mnajionea wenyewe hapa anatujuza kuwa huyo Sheikh Issa amefariki mwaka 1953 hapa chini baada ya kufa akafufuka...waalahi bayana zako ndiyo zinakutukanisha na mimi siwezi kukaa kimya umekutana na kichwa cha madrassa mnywa Gahawa, haha haa aaa Shariff gombesugu, upo Alhy Baabu soma chini hapa.


Sheikh Issa Bin Amir amefariki mwaka 1953 halafu alifanya mkutano na Nyerere mwaka 1954...ha ha haaa
gombesugu, Jasusi, Kadogoo,

Shariff Ritz,

Salaam.

Unajua mimi huwa sipendi malumbano yaso maana,nilishakuambia awali yakuwa hawa jamaa zako unawaweza wewe mwenyewe.

Nimeingia tu hapa ndo nakutana na huu mpini ulompiga nao jamaa wa rohoni!ahaha!! Yaani nimecheka pita kiasi!!

Huyo Mzee wa watu wa Kizaramo ati anakwenda kuvua akiwa na miaka 87!ahaha!! Hili jambo haliingii akilini asilan!

Sisi soote tunajua Wazee wetu khasa wa KiAfrika wanapofikia umri na miaka hiyo wanavyochoka bin taaban...halafu mtu huyohuyo ende akavue na akirejea awe Mufti na wakti huohuo awe ati anajishughulisha na shughuli za kisiasa!?ahaha!!

Halafu baada ya kufariki maskini,ghafula akafufuka na kuanza upya kujishughulisha na shughuli za kisiasa!?ahaha!! Nijuavyo mimi miujiza hiyo walikua wakifanya baadhi ya MaNabii tu!

Unajua mimi juzi pia nilipitia upya baadhi ya vitu hapa,na pia nikachungulia hiyo khabari kiduchu. Nilichofanza nikamwandikia kwa kistaarabu Yericko kumuuliza kama alikusudia Sheikh Hassan Bin Amir,sababu niliona hiyo miaka/umri hai-tally na yale maelezo tulopewa. Lakini nafikiri hakutambua maskini kwanini nilikua namdodosa vile! Matokeo yake akaniletea majibu fulani ya kifedhuli na huku akisisitiza hiyo khabari!?

Jaribu ku-imagine kama hiyo khabari au kosa hilo angelifanza Sheikh Mohammed Said;ungeona jinsi gani Nguruvi3 na ndugu yangu Mag3 shughuli yao ya kebehi na kashfa ingechukua atleast a week minimum Wallahi!

Nipa fursa kuna jamaa inanilazim kumnyooshea maneno japo kiduchu.

Haina neno tuendelee na mnakasha,ndo viroja vya Jamii Forum hivyo.

Ahsanta.

Cc;The Big Show,Nambokola,Sheikh Farid,Mag3,Nguruvi3
 
Wanajamvi,
kuna habari za kufuja mali za EAMWS, mnajua zilisababisha nini na zilifanywa na nani?

Abdul Wahid na Sheikh Amir kuna mahali wanakutana katika chama nje ya TAA na TANU.
Mnajua ni wapi na ni nani kiongozi wa taasisi hiyo?

CC Zumbemkuu, Mag3, JokaKuu, Shariff Ritz, al maarufu Gombesugu, Jasusi, Wickama

Muheshimiwa Nguruvi3,

Hakikisha safari hii, unapokuja na hii "khabari yako mpya" unaleta na vielelezo vya kutosha(sources zako,links,vitabu,barua ama chochote cha kusadikika kitaaluma). Maana tumechoka maneno matupu.

Au pia kama utaweza kututajia majina ya hao walokutuma kuleta uchafuzi na ufataani huo hapa jamvini.

Fuatisha mfano wa mwenzio Sheikh Mohammed said,japo mnamfanyia kebehi na tashtit,lakini mwenzenu atleast ana kitabu chake mkononi,kwa hiyo tunajua wapi pa kumuanzia.

Natumai utanifahamu ndugu yangu.

Ahsanta.

Cc;Ritz
 
Intelligence Quotient~IQ.

Tuendelee na mnakasha hujue wa magharibi wanawachukuliwa watu kama Ibn Battuta siyo GRADUATE kutoka na elimu zao ukiangalia mtu kama Ibn Battuta alikuwepo miaka 1304 mpaka 1369 vitu alivyofanya ni vikubwa sana.

Umetaja University of Cordoba ni baadhi ya vyuo vilivyoleta mapinduzi ya elimu duniani wakati huo Ulaya na Marekani bado kuna giza kubwa la ujinga.

Kimsingi Islamic Scholar hawakubariki kwenye nchi za magharibi ingawa wao ndiyo wameleta elimu kubwa huko kwao.

Ritz; Tatizo la ndugu zetu wa magharibi sio kukudhulumu sifa yako kwa sababu wewe sii dini yake. Tatizo lao ni UCHOYO wa KUGAWANA SIFA. Wanapenda KUPATA CREDIT WAO. Aliyempandisha mzungu wa kwanza Mt. Kilimanjaro ni Mchagga, yet utasikia, THE FIRST MAN TO CONQUER KILIMANJARO WAS ..... yule mchagga hatajwi. Mzungu aliyeona chanzo cha mto Nile infact alipelekwa na wenyeji, No name of Africans (utamuharibia credit), Vasco Da Gama aliongozwa pale Pangani kuwa ili afike India inabidi akaondokee Mombasa. Na jinsi ya kufika India akaelekezwa (no names of helpers, I.....discovered). Kuna mahali nilisoma (sikumbuki vizuri, lakini ilkuwa Ufaransa, wakati wa vita Fulani, kulikuwa na battalion ya kiafrika ambayo ilifanya kazi sana dhidi ya maadui (possibly Germans, not sure) hadi maadui ikabidi watimke. Lakini ilipofika sasa kuwa majeshi ya wakombozi yanaingia ule mji waliokuwa wanaupigania na kuufia, ile battalion ya akina MANGI ilipangwa mwisho. Nani ulaya ya wakati huo anataka kusikia credit za kukombolewa na akina Shemahonge???? Ni hulka Ritz, hawa jamaa hata angekuwa ustadh mwenzio, huenda bado ataficha tuu kuwa hiyo paper aliyotoa kwenye mhadhara wewe ulichangia. Waulize watanzania wanaofanya nao UTAFITI wanavyolizwa!!!!!!
 
Sawa Kadogoo; Mimi nilikuwa nafata kile nachoona dunia sasa inakifanya. Uingereza waandishi (mapaparazi wameeshaambiwa wawaache WATOTO WA MAREHEMU DIANA WAISHI KIBINAFSI. Clinton kweli anachambuliwa na hata mpenzi wake uliyemtaja, Lakini MWANAYE, yaani CHELSEA Clinton anapewa stahiki ya maisha yake kama mtu binafsi. Mabinti wa Obama hali kadhalika. Watoto sio wanasiasa. Labda mtu kama Makongoro tumkwae humu JF kwa siasa zake sio za babaake. Isitoshe Kadogoo, kama mwanao leo unamwambia "shule imepatikana kenya..... unaondoka kesho kwenda kusoma". Yeye muda wa kukuchimba wewe kama mzazi kuhakiki kuwa mipango yote ya kumtafutia shule ni halali au haramu ataianza vipi? Ndiyo maana nikaona atalaumiwa asiyestahili lawama. Ila kama wewe unaona ni tija wanachokifanya Jasusi na mwenzie kuchimbua undani wa watoto wa Julius sina hoja juu yako. Ulikuwa ushauri tuu.

WICKAMA,
nimekuelewa Mkuu, watoto wasihusishwe na madudu waliyofanya Baba zao uko sawa kabisa! ila kumjadili kiongozi kama Mwalimu kwa mazuri na mabaya yake sidhani kama nikosa! kwani ktk mjadala huo huenda pakapatikana fundisho litakalosaidia kutengeza pale walipoharibu ndio maana Waislamu wa nchi hii wanaitaka Serikali kuunda tume huru kuchunguza madai yao ya dhuluma walizofanyiwa tangu na utawala wa awamu ya kwanza mpaka leo! lakini la kusikitisha madai yao yamekuwa kichekesho mbele ya wa TZ wenzao hasa Wakristo wanaoitaka Serikali isikubali kusikiza madai ya Waislamu na la kushtua zaidi ni Serikali kukubali maoni na matakwa ya Wakristo mifano ipo mingi lakini mfano mmoja;

Baada ya mauaji kufanyika ktk Msikiti wa Mwembechai mwaka 1998 chini ya Serikali ya Mkapa, Waislamu ktk baraza la Idi waliombwa na Rais Mkapa kuthibitisha madai yao kisayansi na alipopewa, majibu yake ni Serikali yake haiwezi kupuuza maoni ya Wakristo na madai ya Waislamu kuyatupa kapuni!


Kati ya mwaka 1993 na 1994 Padre Lwambano aliiamrisha Serikali ya Mwinyi kuwakamata wahubiri wa Kiislamu kwa kusema Yesu si Mungu na Waziri Lyatonga Mrema alitangaza vita dhidi ya Mashehe kwa kusema atawavua majoho na kuwapiga ngumi! muda mfupi baadae Shehe Kassim Bin Jumaa wa Msikiti wa Mtoro akakamatwa na kuwekwa kizuizini na kuachiwa akiwa kadhoofika na baadae kufariki!

La kusikitisha Mzee Mwinyi alisema dola iwashughulikie Waislamu na wengi baadhi yao waliishia Magerezani!
Sikuambii ni Mashehe wangapi waliwekwa kizuizini enzi za awamu ya kwanza na dhuluma walizofanyiwa hasa kupigwa marufuku jumuiya yao muhimu ya EAWMA! aidha sikuambii nini madhila wanayopata sasa Waislamu chini ya awamu hii ya Rais Kikwete!
Lakini bado ndugu zetu Wakristo wanaona dhuluma hii dhidi ya Waislamu ni uongo wa kutunga au mchezo wa kuigiza! na zaidi pale tunaposhuhudia vyama pinzani hasa Chadema kuungana na Serikali inapokuja issue ya Waislamu! mwenye macho haambiwi tazama! mwenye masikio na asikie!
 
Intelligence Quotient~IQ.

Tuendelee na mnakasha hujue wa magharibi wanawachukuliwa watu kama Ibn Battuta siyo GRADUATE kutoka na elimu zao ukiangalia mtu kama Ibn Battuta alikuwepo miaka 1304 mpaka 1369 vitu alivyofanya ni vikubwa sana.

Umetaja University of Cordoba ni baadhi ya vyuo vilivyoleta mapinduzi ya elimu duniani wakati huo Ulaya na Marekani bado kuna giza kubwa la ujinga.

Kimsingi Islamic Scholar hawakubariki kwenye nchi za magharibi ingawa wao ndiyo wameleta elimu kubwa huko kwao.



Ritz; Wakati mwingine wanakubali. Soma hii stori

Institute of Arabic and Islamic Studies

Huyu astroner wamempa heshima ya kuita bonde Fulani kwenye uso wa Mwezi JINA LAKE
 
Mohamed Said,
Msiba wa Mzee Ally Sykes umetugusa sote tunaojua mchango wake ktk harakati za kupigania uhuru wa nchi hii! kwaniaba yangu binafsi kwanza nakupa pole wewe binafsi na kutufikishia ktk familia na ndugu wa Marehemu Allah awape subra na Imani! kwani hakika kwake tulitoka na kwake tutarejea!
Shekh MS, umetoa mchango muhimu ktk kufundisha historia ya mashujaa wetu na hasa waasisi wa vyama vilivyopigania uhuru wetu lakini cha kusikitisha kifo cha Mzee Ally Sykes pamoja na viongozi wote waandamizi na wastaafu kuhudhuria msibani, hakuna gazeti hata moja lililoripoti msiba na mazishi ya Mzee Ally Sykes?
 
Juhudi za Kuanzisha Chuo Kikuu cha Kiislamu chini ya EAMWS, 1964


APRILI 1964 ujumbe wa hali ya juu wa EAMWS ndani yake wakiwemo Sheikh Hassan bin Amir, Sheikh Said Omari Abdallah, Tewa Said Tewa, Katibu wa EAMWS Abdul-Aziz Khaki na mzee wa TANU Mzee Mwinjuma Mwinyikambi; Makisi Mbwana, Issa Mtambo, Omari Muhaji na Saleh Masasi waliondoka kwenda ziara ya nchi za Waislamu kutafuta msaada wa kujenga Chuo Kikuu cha Kiislamu na kuanzisha uhusiano na nchi za Kiislam.

Gamal Abdel Nasser alifurahishwa sana na ujumbe wa Tanganyika kiasi kwamba ingawa alikuwa katika matayarisho ya mapokezi ya Waziri Mkuu wa Urusi Kruschev, na ingawa ujumbe wa EAMWS ulikuwa wa kidini zaidi kuliko wa kiserikali, alikutana na ujumbe ule akaupatia ofisi, huduma za simu, na makatibu muhtasi ili waweze kutayarisha mipango yao kwa serikali ya Misri bila shida. Halikadhalika alimuagiza makamu wake Sharbasy afanye makubaliano na EAMWS kwa niaba yake.

Serikali ya Misri ilikubali kugharamia ujenzi wa chuo hicho. Mkataba wa makubaliano ukatiwa sahihi mjini Cairo kati ya Tewa Said Tewa kwa niaba ya EAMWS na Makamu wa Rais wa Misri, Sharbasy kwa niaba ya serikali yake.

Serikali ya Misri iliahidi kujenga Chuo Kikuu cha Kiislam ambacho kitamilikiwa na kuendeshwa na EAMWS. Gharama ya mradi mzima uliuwa pauni milioni hamsini na tano za Ki-Misri.

Baada ya kukamilisha kazi ile ujumbe ule uliondoka Cairo kuelekea Makka kufanya ibada ya hija. Baada ya kumaliza hija wajumbe wanne walirudi nyumbani na Tewa, Aziz Khaki, Sayyid Omar Abdallah wakaendelea na safari kwenda Aman, Jordan ambako walifanya mazungumzo na Mufti na Waziri wa Aukaf.

Kutokea hapo ujumbe ulikwenda Kuwait ambako ulikutana na Sheikh wa Kuwait kisha ukaenda Bhaghdad, Iraq na kukutana na rais wake, Abdisalama Arifek.

Kutoka hapo ujumbe ulielekea Beirut, Lebabon ambako ulifanya mazungumzo na viongozi wa harakati za Kiislam. Baada ya kutoka Beirut ujumbe ule ulirudi tena Cairo kwa ajili ya kukamilisha makubaliano ya kujenga Chuo Kikuu.

Tarehe 20 Mei, 1964 ujumbe ulirejea Dar es Salaam na kupokelewa na viongozi wa EAMWS na Waislamu kwa ujumla. Mkutano wa Halmashauri Kuu ya EAMWS ukaitishwa na Tewa Said Tewa akatoa taarifa yake kuhusu ujenzi wa Chuo Kikuu Cha Kiislamu. Siku ya pili Tewa akaitisha mkutano na waandishi wa habari na kutoa habari za kufurahisha za kujengwa kwa Chuo Kikuu Cha Kiislamu kwa vyombo vya habari na kwa Waislamu kwa ujumla.

Kwa mafanikio haya Tewa akawa amejichimbia kaburi. Matokea haya yalijaza hofu kwa viongozi wa Kanisa. Kampeni za chinichini dhidi ya Tewa binafsi na uongozi mzima wa EAMWS zilianza.

Mara baada ya ujumbe wa EAMWS kurudi kutoka ziara yake, Nyerere alifanya mabadiliko katika baraza la mawaziri na Tewa Said Tewa, Mwenyekiti wa EAMWS upande wa Tanzania akajikuta nje ya serikali.

Nyerere akamteua Tewa balozi wa Tanzania katika Jamuhuri ya Watu wa China. Mwezi Januari, 1965 Tewa alikwenda China kuanza kazi yake mpya. Inasemekana uteuzi wa wa Tewa kwenda China ulisababishwa na juhudi zake za kutaka kuwaunganisha Waislam kuwa kitu kimoja chini ya jumuiya moja yenye nguvu. Wakati ule ile mipango iliyopitishwa na mkutano wa Waislamu mwaka 1962 ilikuwa ikitekelezwa vyema, shule zilikuwa zimejengwa Ilala, Kigogo na Kurasini, Dar es Salaam; shule zilikuwa zimejengwa Ruvu na Maneromango. Shule hii ya Maneromango ilikuwa na umuhimu wa pekee kwa sababu hii ndiyo ilikuwa shule ya kwanza ya Waislamu kujengwa Uzaramo. Shule za upili zilikuwa zikijengwa Dar es Salaam, Kinondoni na Moshi, Kibohehe. EAMWS ilikuwa vilevile imetiliana mkataba wa makubaliano na serikali ya Misri kuipa scholarship thelathini na tano kila mwaka kwa wanafunzi wa Kiislamu kusoma Misri. EAMWS ilikuwa imejenga shule, misikiti, shule za ufundi na hosteli kwa ajili ya wanafunzi katika sehemu nyingi za Afrika ya Mashariki. Kwa hakika EAMWS ilikuwa ikifanya mambo ya maendeleo kwa Waislamu.

Uganda Tanzania Kenya
Shule 77 70 28
Misikiti 67 53 29
Shule za Ufundi 3 - -
Hosteli 1 - -
Chanzo: Utafiti
Baada ya Tewa kuondoka Bibi Titi Mohamed akachaguliwa kuwa makamu mwenyekiti wa tawi la EAMWS la Tanzania ili kuongeza nguvu makao makuu kwa kuwa mwenyekiti hakuwepo. Kutokuwepo kwa Tewa nchini kulileta ombwe ambalo ilibidi lijazwe. Ghafla palizuka uvumi kuwa Sheikh Abdallah Chaurembo alikuwa achukue uongozi wa EAMWS. Inasemekana nia yake ilikuwa ni kwanza kupata urais wa EAMWS na kisha achaguliwe kuwa Mufti wa Tanzania. 35 Uvumi huu ulidumu kwa karibu mwaka mzima hadi pale Tewa aliporudi kutoka Peking baada ya kujiuzulu ubalozi kuja kugombea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1965. Aliporudi Tewa alihojiwa na waandishi wa habari kuhusu uvumi ule na yeye jibu lake lilikuwa kuwa Muislamu yeyote mwenye sifa ya maadili mema ana haki ya kugombea nafasi yoyote katika uongozi wa EAMWS. Neno alilolitumia Tewa katika kumueleza mtu ambaye angeweza kuwaongoza Waislamu lilikuwa takwa, neno la Kiarabu kueleza mtu mcha-mungu.

Nikuanzia katika matukio haya ndipo tunaweza sasa kuanza kuchunguza jinsi Nyerere akiitumia serikali alivyoanza kuuhujumu umoja wa Waislamu kwa kutumia njama, hujuma za dhahiri na za kificho, magendo na kueneza uongo dhidi ya uongozi wa EAMWS, ambao ulionekana ni tishio kwa utawala wake. Wakati ule serikali nzima ilikuwa mikononi mwa Wakristo. Ukiwatoa Wazanzibari waliokuwa katika serikali ya muungano - Aboud M. Maalim, Waziri wa Biashara na Viwanda; Aboud Jumbe, Waziri Nchi; A.M. Babu, Waziri wa Ardhi, Makazi na Maji; Hasnu Makame, Waziri wa Habari na Utalii; Rashid Kawawa ambae alikuwa mtu wa karibu sana na Nyerere, waziri Muislamu katika baraza la mawaziri kumi na tano alikuwa Said Ali Maswanya, Waziri wa Mambo ya Ndani. Hali kama hii ya Wakristo kushika nyadhifa takriban zote za serikali ilikuja vipi? Jibu la swali hili linapatikana katika historia ya Tanganyika wakati wamisionari wa kwanza walipowasili nchini kuja 'kulistaarabisha bara jeusi' na halikadhalika katika historia ya TANU .


'Mgogoro' wa East African Muslim Welfare Society (EAMWS) wa Mwaka wa 1968
Uchochezi wa 'Mgogoro' wa BAKWATA

Kutokana na katiba ya mwaka wa 1957 lengo kuu la EAMWS ilikuwa ni 'kuutangaza Uislamu katika Afrika ya Mashariki'. EAMWS yenyewe ilikuwa ikijigamba kuwa uti wake wa mgongo ilikuwa ni tabligh, yaani utangazaji wa dini. Jumuiya hii iliyoanzishwa mwaka 1933 ilikuwa ya Waislamu wa mataifa yote katika uanachama na katika uongozi wake.

Katika uhai wake wa miaka thelathini na tano EAMWS ilijiweka mbali sana na siasa. Jumuiya hii ilishughulikia kuutetea na kuueneza Uislamu katika Afrika ya Mashariki. Lakini baada ya kutokea maasi ya Tanganyika Rifles mwaka 1964 yaliyopelekea viongozi wengi wa Kiislamu kuwekwa kizuizini, EAMWS ikawa imepoteza mwelekeo wake na kudhoofika. Baadhi ya matawi yaliyokuwa katika majimbo yakafungwa kwa woga na kukosa viongozi thabiti na kwa matawi mengine yalifungwa kwa sababu viongozi wake walikuwa wakichimbwa chinichini na serikali. Waislamu wengi walihisi vitisho vya serikali kwa hiyo waliogopa kuchukua uongozi wa EAMWS. Wengi waliogopa kuitumikia EAMWS kwa kuwa walihisi ofisi za jumuiya hiyo zilikuwa zikichukuliwa na serikali kama vituo vya upinzani dhidi yake. Kwa zaidi ya miaka mitatu toka ule mkutano wa mwaka 1963, EAMWS haikuweza kufanya mkutano wowote.

EAMWS ilipokuja kuitisha mkutano wake wa mwaka mjini Arusha mwaka 1966 kikajitokeza kikundi kutoka upande wa Tanzania kikidai EAMWS ijigawe, kila nchi iwe na mamlaka yake na ijitegemee yenyewe, yaani Tanzania, Kenya na Uganda zote ziwe mbalimbali. Kikundi hiki kilichokuwa kikidai utengano vilevile kikadai kuwa katiba ya EAMWS nayo iwe ya 'kizalendo'.

Hii ilikuwa na maana kuwa uongozi itabidi uifanyie katiba marekebisho ili kuiwezesha Tanzania kuwa huru ndani ya EAMWS. Wajumbe waliokuwa wanaona mbali kutoka Tanzania na wengine kutoka Kenya na Uganda, na kwa hakika mkutano mzima kwa ujumla walipinga kitendo hicho, wakidai kuwa kwa kufanya hivyo Waislamu wa Tanzania watakuwa wametengwa na umma wa Kiislamu wa Afrika ya Mashariki. Jambo hili likitokea, si tu litakuwa limewadhoofisha Waislam wa Tanzania peke yao, bali Waislamu wa Afrika ya Mashariki nzima. Wajumbe wa Kenya na Uganda walikuwa wanatambua kuwa kulikuwa na shinikizo kubwa kutoka serikali ya Tanzania kwa Watanzania kujitoa kutoka EAMWS. Halikadhalika ilikuwa inafahamika kuwa wajumbe wa Tanzania walikuwa wakifanya kazi chini ya shinikizo kali kutoka serikali ya Nyerere.

Haikuwa siri sana kuwa baadhi ya viongozi wa EAMWS walikuwa kisirisiri wakiandamwa na serikali. Lakini mkutano ule haukuzungumzia matatizo haya kwa kuwa hayo yalichukuwaliwa kama matatizo ya ndani ya nchi. Hata hivyo kwa ule moyo wa Kiislamu wa kuhurumiana, wajumbe wa Kenya na Uganda kwa faragha walionesha masikitiko yao kwa Tewa kuhusu ile hali iliyokuwa ikiwakabili Waislamu wa Tanzania. Wajumbe walipokuwa wakiondoka kurejea makwao, ilikuwa wazi kuwa serikali ya Tanzania ilikuwa ikiingilia kati EAMWS kiasi cha kuifanya jumuiya hiyo ishindwe kufanya kazi yake vyema na kupitisha maamuzi yake. Hali hii ilijidhihirisha wazi pale kwa kipindi kizima cha mkutano, makachero wa serikali walikuwa wamejitokeza kwa wingi mjini Arusha.

Haukupita muda ikadhihirika kuwa serikali ilikuwa imepania kuivunja EAMWS kwa kuwatumia Waislamu wachache walioteuliwa kwa kazi hiyo. Lengo likiwa ni kuanzisha taasisi mpya ambayo serikali itaweza kuiamuru. Ieleweke hapa kuwa kama ilivyokwisha elezwa hapo nyuma, serikali nzima ya Tanzania ilikuwa mikononi mwa Wakristo na watendaji hawa walikuwa wapo chini ya Kanisa. Hii ilikuwa na maana kuwa kilichotakiwa kuwepo ilikuwa taasisi ya Kiislamu ambayo Kanisa itaweza kuiamuru. Hii ilikuwa ni jambo lazima lifanyike ili kuwadhibiti Waislamu kama nguvu inayoweza kuleta mabadiliko ya siasa. Baada ya kuelewa hali hii ndipo sasa tunaweza kuuangalia kile kilichoitwa 'mgogoro' wa EAMWS ambao ulidumu kwa miezi mitatu ya mwisho ya mwaka wa 1968.

Ili tuweze kuuelewa vyema kisa kizima cha 'mgogoro' ni muhimu kwanza kuelewa chanzo chake, hadhi za wahusika wakuu na nafasi zao katika 'mgogoro' ule. Mwisho, ni muhimu kuweka bayana na kuchambua nafasi ya Julius Nyerere, serikali yake, chama cha TANU na vyombo vya dola katika 'mgogoro' ule. Hii itasaidia kuelewa kama kweli ulikuwepo 'mgogoro' katika EAMWS, au 'mgogoro' ulibambukizwa na watu katika TANU, serikali na ndani ya Waislamu wenyewe ili kuwadhoofisha Waislamu kwa nia ya kuwa usije Uislamu ukawa na nguvu katika Tanzania hivyo kuwawezesha Waislamu kushika madaraka ya nchi.

Mwaka wa 1967 Mwalimu Julius Nyerere alitangaza Azimio la Arusha hatua ambayo iliitia Tanzania katika siasa ya ujamaa. Sera hii mpya ya uchumi ilipokelewa vyema na wananchi. Mtu ambae hata alikuwa hajulikani, tena mwalimu wa shule ya msingi akijulikana kwa jina la Adam Nasibu ambae alikuwa katibu wa Bukoba wa EAMWS, alichukua nafasi hii kwa kuongoza maandamano hadi ofisi ya TANU ya Mkoa kumuunga mkono Mwalimu Nyerere na sera yake mpya ya uchumi ya Azimio la Arusha. Adam Nasibu inasemekana kuwa alisema ujamaa ni sawa na mafundisho ya Qur'an Tukufu. Adam Nasibu hakuishia hapo alikwenda mbele zaidi na kutoa 'miongozo kwa viongozi wote wa Kiislamu wa Bukoba akifafanua Azimio la Arusha'. Wasiokuwa Waislam walimuona Adam Nasibu kama Muislam mwenye mwamko mzuri wa kimaendeleo, na kwa kuwa yeye alikuwa ni kiongozi wa EAMWS, kuunga kwake mkono Azimio la Arusha kulionekana kama kitendo rasmi cha jumuiya hiyo kuunga mkono sera hiyo. Lakini kabla ya yeye kufanya haya, hakuna mtu aliyemjua mwalimu huyu wa shule kama mwanasiasa licha ya kuwa msomi mwenye uwezo wa kuchambua mambo.

Katika hali ya kawaida, uongozi wa EAMWS pale makao makuu Dar es Salaam ungelikasirishwa kidogo na kitendo cha Adam Nasibu cha ushabiki wa siasa. Lakini uongozi wa EAMWS haukumuonya kiongozi wake wa Bukoba kuhusu jambo lile ambalo dhahiri halikuwa la kupendeza katika jumuiya. Bila shaka uongozi wa EAMWS ulichelea kuwa kwa kufanya hivyo wangelionekana si uzalendo, hasa ukiichukulia jinsi wananchi walivyohamasika na Azimio la Arusha. Hata hivyo Waislamu siku zote ndiyo waliokuwa mbele katika kuongoza siasa. Makao Makuu walibaki kimya kama vile hakuna kilichotokea.

Tofauti na mwaka wa 1963 wakati Nyerere alipojaribu kufanya mapinduzi dhidi ya uongozi wa EAMWS, mwaka wa 1967 hali ya mambo yalikuwa yamebadilika sana yakimwendea Nyerere vyema. Serikali ilikuwa imedhibiti vyombo vyote vya habari ukiondoa gazeti la The Tanganyika Standard ambalo bado lilikuwa chini ya Lonrho. Nyerere alikuwa amemuweka Martin Kiama kama mkurugenzi wa radio ya taifa, na Benjamin William Mkapa kama mhariri wa magazeti mawili ya TANU, The Nationalist na Uhuru. Adam Nasibu aliandikwa katika magazeti na habari zake kutangazwa katika radio kwa ajili ya kitendo chake, hasa kuhusu yale maneno aliyosema kuwa ujamaa ni sawa na mafundisho ya Qur'an.

Katika hali ya mambo kama yalivyokuwa wakati ule hasa jinsi uhasama ilivyokuwapo baina ya serikali na Waislam, baadhi ya Waislam walimuona Adam Nasibu kama kibaraka anaetafuta umaarufu wa bure kwa kujipendekeza kwa TANU, Nyerere na serikali yake. Juu ya haya yote kile kitendo cha katibu wa Bukoba wa EAMWS kitakuja kuwaathiri vibaya jumuiya hiyo na uongozi wake wote pamoja na Mufti Sheikh Hassan Bin Amir.

Kwa wengine Adam Nasibu alionekana kama mzalendo na Muislamu mwenye 'uoni wa mbali'. Kwa ajili hii basi serikali ikamuona kama kiongozi wa baadae ambayo ingeweza kumtegemea wakati wa shida. Uongozi wa EAMWS makao makuu ukaonekana haupo pamoja na wananchi, wala haujali shida zao na uko mbali sana na sera za serikali. Lakini kwa hakika EAMWS kama taasisi ya dini isingeliweza kujitokeza na kuunga mkono Azimio la Arusha kwa kuwa hayo yalikuwa mambo ya siasa. Kwa kufanya hivyo ingelikuwa inakwenda kinyume na msimamo wake wa kutojiingiza katika siasa. Kwa zaidi ya robo karne toka iasisiwe EAMWS ilikuwa imejiweka mbali sana na mambo ya siasa ikishughulika na masuala ya Uislamu tu. Hata hivyo kuwa nje ya Azimio la Arusha kukaonekana kama kitendo cha kukosa uzalendo na kutoa picha kuwa jumuiya hiyo ilikuwa haijali maendeleo na ustawi wa watu wa Tanzania. Mambo yakawa yamevurugika zaidi kwa kuwa rais wa EAMWS, Tewa Said na makamo wake Bibi Titi Mohamed walikuwa katika baraza la mawaziri la Nyerere na wakapoteza nyadhifa zao za ubunge katika uchaguzi mkuu wa mwaka 1965. Kwa ajili hii basi serikali ikawa inaeneza propaganda kuwa kwa kuwa Tewa na Bibi Titi walikuwa katika uongozi wa juu wa EAMWS, walikuwa wanatumia nafasi zao kujijengea himaya mpya kutoka kwa Waislamu dhidi ya Nyerere. Viongozi hawa ikawa lazima washughulikiwe na kuangamizwa. Mtu wa kufanya kazi hii hakuwa mwingine ila Adam Nasibu katibu wa EAMWS Bukoba, mwalimu wa shule ya msingi ambae elimu yake wala haikuwa kubwa. Adam Nasibu alikuwa tayari keshafanikiwa kufanya mapinduzi dhidi ya rais wa EAMWS, Tewa Said Tewa. Kutokana na vitendo vyake alikuwa ameidhihirishia serikali kuwa yeye angeweza kuwa mtumishi bora kwa dola kuliko ule uongozi wa EAMWS uliokuwa pale makao makuu Dar es Salaam ambao ulikuwa ukionekana umechoka.

Sheikh Farid,

Salaam Al Akhiy.

Umefanza jambo jema mno kuurejesha huu mpini hapa jamvini ili watu tujikumbushie japo kiduchu. Najua Sheikh Mohammed aliulezea kwa utuvu kwenye baadhi ya bayana zake za awali.

Kwenye family album ya Mzee wangu hizo pictures za hiyo safari zipo kadhaa. Nafikiri walipofika pale Beirut ndipo walipokutana/walipoungana na Sheikh Yahya Hussein na Bwana Ali Sykes katika harakati na shughuli hizo hizo.

Shukran.

Cc;Ritz,Sheikh Mohammed Said
 
Wewe ndiyo unajichanganya wapi tumesema tunataka upendeleo tutake upendeleo kwa nani hili iweje.

Mohamed Said anaelezea historia ya Wazee wetu nyie roho zinawauma hakuna sehemu yeyote ambayo mmelazimishwa kuikubali.

Ndiyo maana mkashauriwa na nyie andikeni historia ya wazee wenu.
Mkuu Ritz, kwanini tunawagawanya hawa wazee kwenye haya ya "wetu" na "wenu" ? mbona hawa wote walikuwa wazee wa Tanganyika na wao waliheshimiana sana wakapambana na mkoloni "with a common goal"!
 
Too late Mohamed, hoja iliyokuwepo mbele yetu ni kuwa Nyerere kwa ''udhalimu'' wake alimfukuza Sheikh Amir bila sababu. Hakuna maelezo mengine zaidi ya kusema ukataili wa mwalimu dhidi ya wazee wako.

Leo unataka kueleza kisa baada ya kujulikana kuwa Sheikh alikuwa Msaliti.

Mwisho, Sheikh kuitwa mnafiki na msaliti si tusi, kama lingekuwa tusi linalowaumiza basi msingezunguka duniani mkimsema Nyerere kuhusu viarago na pesa za vitoweo.

Kama lingekuwa linaumiza basi msingemvunjia hishma kwa kusema Laanatullah kila anapotajwa, wala asingeitwa habithi, baradhuli, mnafiki n.k.

Kwanini udhani kuwa sheik Amir anastahili hishma kuliko Nyerere wote wakiwa wanadamu, wazee na familia zao?

Hapa ndipo nasema kila siku lazima watu waangalie nyuma, pembeni na mbele.
Kurushia watu mawe ukiwa katika nyumba ya glasi si jambo jema.

Kila mzee wetu aliyepigania nchi hii na apewe heshima.
Tuache uchochezi usio na maarifa

Hii inaitwa fitna al maarifa kama anavyosema ndugu yangu Gombesugu.
Tuache haya tuangalie jamii inakwenda wapi, inahitaji nini, tufanye nini kwa pamoja na si kwa chuki na kubaguana.

Muheshimiwa Nguruvi3,

Salaam.

Tatizo lako ndugu yangu una maneno mengi mno,najua mwenyewe unapenda kuziita "hoja".

Inawezekana pia una machungu na stress nyingi mno ambazo umeamua kuja kuzimalizia hapa Jf/jamvini. Mimi binafsi nashukuru kwa sasa huo uhuru wa kusema chochote mtu atakacho hapo Tanzania umekua mwingi mno,tafauti na zile "enzi za Mwalimu".

Kwa sababu naamini mtu kama wewe kama ukiachiwa masaa mengi kuwa mitaani utasababisha madhara makubwa kwa Taifa,khasa kutokana na kauli zako zenye chuki na kuhamasisha maovu. Ndo maana nafarijika kila mara nikuonapo hapa online/jamvini.

Kwa sasa sitanena mengi. Unadai kumwita Sheikh Hassan Bin Amir Mnafiki au Msaliti sio tusi!?

Kuna wakti katika baadhi ya majibizano yenu Sheikh Mohammed Said,alikwambia yakuwa "hilo neno usirudie tena". Wewe ulikereka pita kiasi tena kwa hamaki nyingi mpaka ikanilazim niingilie kati.

Pia ulijaribu kusema yakuwa kwenu Tanga/Makorora hilo ni tusi kubwa mno!? Nilikwambia sio kweli na tukamalizana.

Sasa iweje unarejea tena hapa hapa jamvini,kuhalalisha matusi mengine tena kwa Kiongozi wa kidini,tena huku ukidai na kusisitiza kuwa hilo sio tusi!? Je unajua tafauti ya sifa na kashfa!?

Kwa kifupi kama wewe binafsi umeamua kuendelea kutukana,haina neno. Lakini mtu yeyote mwenye maarifa na akili zake timamu anajua kuwa hilo ni tusi kubwa mno.

Tuendelee na mnakasha ndugu yangu.

Shukran.

Cc;Ritz
 
Shukran kwa tathmini JokaKuu!

Nilivyoelewa mimi ni kuwa namba mbili mpaka nne zinarudi kwenye tatizo uliloliweka namba moja.
Tatizo ni lilelile tu halafu kutokea hapo mtu anaweza kutiririka.

Ninakubali kusahihishwa.
Sideeq,

..je, tumeelewana kwamba Znz ndiyo inainyonya Tgk??

..zaidi, tumekubaliana kwamba kutokana na dhuluma ya muungano dhidi yetu, wa-Tgk ndio tunaopaswa kumlaani Mwalimu Nyerere na siyo nyinyi wa-Zenj??

cc: Nguruvi3, Wickama
 
Last edited by a moderator:
Muheshimiwa Nguruvi3,

Hakikisha safari hii, unapokuja na hii "khabari yako mpya" unaleta na vielelezo vya kutosha(sources zako,links,vitabu,barua ama chochote cha kusadikika kitaaluma). Maana tumechoka maneno matupu.

Au pia kama utaweza kututajia majina ya hao walokutuma kuleta uchafuzi na ufataani huo hapa jamvini.

Fuatisha mfano wa mwenzio Sheikh Mohammed said,japo mnamfanyia kebehi na tashtit,lakini mwenzenu atleast ana kitabu chake mkononi,kwa hiyo tunajua wapi pa kumuanzia.

Natumai utanifahamu ndugu yangu.
Heee ! wenzangu yamekuwa hayo.

Mimi nimeuliza maswali mbona nashambuliwa kiasi hiki.
Tena imefikia mahali naitwa fataani, nimetumwa n.k. Hivi kwanini watu wanaghadhabu nami.
Yaani hata mahali nisipoingia mtu atatafuta upenyo apitishe jina langu ilimradi tu.

Gombesugu, Mohamed ndiye mwandishi na msomi pekee ninaye mfahamu anayefanya ''self quotation'' au reference.
Huko mimi sipo.

Haya tunayoongea hapa tuna ufahamu nayo. Kama tungekuwa hatujui tusingemvua Mohamed nguo, tukamfunga mikono na miguu kwa nguo hizo na hata kumchapa usoni na mtambara yake.

Wewe ulijua kuwa balozi hakuhutubia Bunge! Tulimuuliza akaingia na tarehe tukamchapa nazo usoni.
Sasa hivi amebaki na Mkoba wa Ibadan! FYI we have strong and wide background! Ninaiangalia dunia kwa mtazamo mpana siyo wa kipata au mfenesini! Gombesugu!

Kama unataka link n.k. tutoa, kwani si unataka link za jinsi gani Rukara alipata passport ya Tz.
Unataka tutaje hata ufuska na majina ya wahusika! ndivyo unataka?
Mimi nasitiri watu na kujisitiri, sipiti nikizungumzia vyumba vya watu na vitoweo hovyo barabarani, nina weledi.

Najua kinachowatia hasira ni sheikh Amir kuitwa Mnafiki na mfitini mkubwa.
Mimi nasema Amir ni mnafiki mkubwa sana nimeeleza sababu kwa kufanya quotation ya maneno ya Mohamed ili muamini zaidi. Nasema Bibi Titi alikuwa na uadilifu kuliko huyu mnafiki mkubwa anayeitwa sheikh.
Mnafiki huyu habri zake za kinafiki zinajulikana.

Nafahamu pia hasira ni kutokana na miba ya muungano, hasa kwa wznz! nawe unajua hilo kwahiyo sitegemei kusikia neno zuri kutoka kwako linalonihusu. Guess what, mimi spade naita spade sisemi ni big spoon!

Kama hakuna majibu ya maswali nitaleta link, subra yavuta heri
 
Heee ! wenzangu yamekuwa hayo.

Mimi nimeuliza maswali mbona nashambuliwa kiasi hiki.
Tena imefikia mahali naitwa fataani, nimetumwa n.k. Hivi kwanini watu wanaghadhabu nami.
Yaani hata mahali nisipoingia mtu atatafuta upenyo apitishe jina langu ilimradi tu.

Gombesugu, Mohamed ndiye mwandishi na msomi pekee ninaye mfahamu anayefanya ''self quotation'' au reference.
Huko mimi sipo.

Haya tunayoongea hapa tuna ufahamu nayo. Kama tungekuwa hatujui tusingemvua Mohamed nguo, tukamfunga mikono na miguu kwa nguo hizo na hata kumchapa usoni na mtambara yake.

Wewe ulijua kuwa balozi hakuhutubia Bunge! Tulimuuliza akaingia na tarehe tukamchapa nazo usoni.
Sasa hivi amebaki na Mkoba wa Ibadan! FYI we have strong and wide background! Ninaiangalia dunia kwa mtazamo mpana siyo wa kipata au mfenesini! Gombesugu!

Kama unataka link n.k. tutoa, kwani si unataka link za jinsi gani Rukara alipata passport ya Tz.
Unataka tutaje hata ufuska na majina ya wahusika! ndivyo unataka?
Mimi nasitiri watu na kujisitiri, sipiti nikizungumzia vyumba vya watu na vitoweo hovyo barabarani, nina weledi.

Najua kinachowatia hasira ni sheikh Amir kuitwa Mnafiki na mfitini mkubwa.
Mimi nasema Amir ni mnafiki mkubwa sana nimeeleza sababu kwa kufanya quotation ya maneno ya Mohamed ili muamini zaidi. Nasema Bibi Titi alikuwa na uadilifu kuliko huyu mnafiki mkubwa anayeitwa sheikh.
Mnafiki huyu habri zake za kinafiki zinajulikana.

Nafahamu pia hasira ni kutokana na miba ya muungano, hasa kwa wznz! nawe unajua hilo kwahiyo sitegemei kusikia neno zuri kutoka kwako linalonihusu. Guess what, mimi spade naita spade sisemi ni big spoon!

Kama hakuna majibu ya maswali nitaleta link, subra yavuta heri

Muheshimiwa Nguruvi3,

Nakupenda mno ndugu yangu.

Lakini kutokana na hizo kauli zako, hivi sasa nahisi umepandwa na Shamrani. Kwa hiyo nakwacha kiduchu utuame/upumzike,halafu nitaendelea kukubana tena mbavu mpaka ucheue leo.

Leo nafanyia shughuli zangu hapa hapa nyumbani,kwa hiyo nina muda mzuri wa kuchungulia baadhi ya vitu hapa jamvini na huku nikipambana na wewe.

Shukran.
 
Mkuu Nguruvi3 hii habari nikiwahi kuisikia sikia bahati mbaya Mzee wangu wa Gerezani Mohamed Said hakuitia kwenye kitabu chake sijui kwani wakti suala la EAMWS kalizungumzia kwa undani sana ingawa pia kakwepa kuzungumzia sababu za kutimuliwa Kenya.

Mkuu wangu nasubiri darsa,usisahau kunimention nisijepitwa na uhondo.

Nakala Ritz gombesugu JokaKuu Mag3 zumbemkuu kwa taarifa...


Wanajamvi,
kuna habari za kufuja mali za EAMWS, mnajua zilisababisha nini na zilifanywa na nani?

Abdul Wahid na Sheikh Amir kuna mahali wanakutana katika chama nje ya TAA na TANU.
Mnajua ni wapi na ni nani kiongozi wa taasisi hiyo?

CC Zumbemkuu, Mag3, JokaKuu, Shariff Ritz, al maarufu Gombesugu, Jasusi, Wickama
 
Last edited by a moderator:
Tanzania bara ni Tanganyika na Zanzibar visiwani ndio zanzibar ama vipi sasa mbona katika ushahidi ulowekwa katika links ambazo nilitakiwa kusoma hamna maelezo hayo sasa aidha unalazimisha kitu ambacho hakipo ama wao wamefanya mistake soma hapa ili uelewe zaidi labda sisi wengine akili za madrasa nyinyi wasomi.

MUHTASARI WA RIPOTI YA MASUALA YA FEDHA
YANAYOHUSU MAMBO YA MUUNGANO

Utangulizi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ina Muundo wa
Serikali
mbili; Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania (SMT)
ambayo imepewa majukumu ya
kusimamia Mambo ya Muungano na yasiyo ya Muungano
kwa Upande wa Tanzania Bara na
Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar (SMZ)
imepewa majukumu ya kusimamia
Mambo yasiyo ya Muungano kwa Zanzibar.

Mkuu umeifahamu hiyo paragraph hapo Jamhuri ya muungano imejengeka kwa serikali mbili 1:Serikali ya jamhuri ya muungano sisi hatujaungana na serikali ya jamhuri ya muungano
muungano unatokana na serikali mbili Tanganyika ilokufa na zanzibar ambayo inakuja kama hivi Tanganyika+Zanzibar=Tanzania ndo maana tunasema Tanzania ndo Tanganyika kipi ulichokua hufahamu hapo mkuu.




Nambokola,

Salaam.

Mimi binafsi nakufahamu na nakuelewa kwa utuvu na nafuatilia hizi hoja za ndugu zangu JokaKuu na Nguruvi3, khasa kuhusu haya "madeni ya Muungano".

Siku chache zilizopita niliwahi kumwambia Nguruvi3 yakuwa kuna significant evidences ya kuonyesha huo Muungano wenyewe kwanza tangia awali haukuwa halali!

Na ukichungulia japo kiduchu kwenye legality of additional matters outside the Articles of Union....tayari utaona yakuwa kuna practical problems. Hapo peke yake utaona yakuwa hayo "madeni" tayari yashajifuta!

Haina neno tuendelee na mnakasha.

Shukran.


Cc; Ritz,JokaKuu,Nguruvi3
 
Back
Top Bottom