THE BIG SHOW
JF-Expert Member
- Feb 28, 2012
- 16,950
- 13,527
yericko vibaya hivoo,mbona mnaanza kuhamaki nyie kizazi cha nyoka?
Tunawapeni kile alichowanyima mohamed said na kuamua kuwapa ngano za masika.
Mwambie awape ukweli, hao wazee wake akina sykes walitengwa au walijitenga kwa minajiri yao ya kiimani?
Mohamed anajua kila kitu lakini kaamua kuwapotosheni kwa laana ileile.
hahaha. Andikeni basi makala kuping historia? Kama nyerere mwenyewe alijificha uso. Mtaweza nyinyi?
kulikuwa na kamati ya usuluhishi ya waislam chini ya mussa kwikima na ilikuwa na makabrasha na nyaraka nyingi sana.
Baada ya mgogoro kwisha na bakwata kuundwa na serikali.
Wakawa sasa wanapitiwa wanakamati na kutishwa makabrasha yote yakakakusanywa.
Waikela hakuweza kutishwa na yeyote.
Yeye akaficha makabrasha yake kwa miaka 20.
Akayaweka hadi yaliponifikia mimi katika miaka ya 1980s.
Nyaraka za bilal rehani waikela ndizo nilizotumia kuandika shemu ya mwisho ya kitabu changu.
Historia ya waislam tanzania ni nzito.
Hakuna nje ya sisi anaeweza kuwa na ujasiri wa kuiandika.
halafu kibaya zaidi anataka kutuaminisha ya kuwa mateso wanayoyapata masheikh leo yana mfanano na wakati ule wa nyerere alivyowafanyia waislam na hasa masheikh. Hoja hafifu kabisa.
Hilo ndilo jibu lako la hayo ya Sawaya na Kayugwa?
yericko vibaya hivoo,
una haribu mnakasha,jazba za nini?
Tushakuwa kizazi cha nyoka mara hii?
Twende pole pole,kidogo kidogoo.
Serekali ipi ya Muungano wa ya KANISA? kama ya MUUNGANO WAMEFANYA KOSA. LKN KAMA YA KANISA hawakufanya kosa. wewe na WAZEE WA TANU NANI ANAJUA HSTORIA? HISTORIA ULUIOSOMA WEWE SI NDIO HII INAYOSOMESHWA KATIKA SHULE ZA ST ZA KUMTAKASA MWALIMU? HONGERA SHEIKH SAIDNdio ni jibu la hoja, unayo fursa ya kupinga au kukubali mkuu!
Waambie ukweli wafuasi waku kuwa wazee wako waliasi serikali.
unajua maana halisi ya kizazi cha nyoka?
Uliza mkuu usikimbilie kulaumu tu!
Kizazi cha nyoka ni binadamu wote wakizazi baada ya eva/hawa kula tunda la mti wa mema na mabaya!
Hivyo mimi, wewe na yule ni kizazi cha nyoka.
ndio ni jibu la hoja, unayo fursa ya kupinga au kukubali mkuu!
Waambie ukweli wafuasi waku kuwa wazee wako waliasi serikali.
Naona neno uchochezi umeshindwa kulitumia tena baada kushindwa kuthibitisha.
Ni vizuri kujifunza hebu tupe hicho kisa kidogo cha wazee waliofanya uasi na kutaka kumpindua Nyerere. Kwa faida ya JF na wasomaji tupe
na majina yao.
si kweli ya kwamba waliasi serikali,si kweli hata kidogo,
lakini pia,,ndio kusema ya kwamba mara baada ya wazee hao kuasi serikali kama ilivokuwa fabricated hiyo ikawa ni justification ya kufutwa kwa historia yao ya ukombozi wa taifa hili moja kwa moja?
Kilichofuata baada ya kupatikana uhuru ilikuwa ni kukamatwa, kuwekwa kizuizini na kuhamishwa kwa masheikh na Waislam wengine waliodhaniwa kuwa wanapinga utawala wa Wakristo serikalini. Mashuhuri miongoni mwao walikuwa:
Sheikh Hassan bin Amir, Abdillah Schneider Plantan, Sheikh Abdulkarim Abdulwahid, Maalim Popo Saleh, Suleiman Masudi Mnonji, Ali Migeyo, Mufti Sheikh Hassan bin Amir, Sharff Hussein Badawiy, Shariff Mwinyibaba, Shariff Adnan, Bilali Rehani Waikela, Sheikh Jumanne Bias, Maalim Matar, Abdalah Mwamba, Sheikh Hashim Haji Abdallah, Sheikh Nurdin Hussein, Salum Abdallah, Sheikh Mzee Ali Comoriam, Sheikh Al Amin Maftah, Rajab Kiguu cha Mbuzi na wengine wengi.
Lakini ukweli ulikuwa kwamba si wote katika wale waliokamatwa na kuwekwa kizuizini walijihusisha na siasa.
Baadhi yao walikamatwa kwa sababu tu walikuwa wakishirikiana na wale waliodhaniwa ni wapinzani wa Nyerere.
Maalim Matar na Shariff Adnan walifungwa jela kwa sababu tu walihusika na msikiti wa Badawiy mjini Dar es Salaam ambako Sheikh Hassan bin Amir, wakati huo akichukuliwa kuwa ndiyo roho ya waumini wa Tanganyika, alikuwa ikiendesha madrasa yake kila magharibi pale msikitini.
Shariff Hussein na nduguye Mwinyibaba walihamishiwa Kenya, walikotoka si kwa sababu walikuwa wamejishughulisha katika harakati za kuipinga serikali, ila lakini kwa sababu walikuwa waangalizi wa msikiti wa Badawiy.
Sheikh Mzee Ali Comorian alitiwa kizuizini kwa sababu kila mara alikuwa akifuatana na Sheikh Hassan bin Amir kama vile alikuwa kivuli cha sheikh.
Hakuna katika orodha hii ya masheikh hata mmoja aliyefikishwa mahakamani kwa kesi ya uhaini.
Jina lenye mstari Salum Abdallah ni babu yangu.
Salum Abdallah aliongoza mgomo (General Strike) wa 1947.
Salum Abdallah alikuwa mfadhili wa AA hadi TAA Tabora.
Salum Abdallah alikuwa katika kamati ya siri ya kuibuka na TANU 1954
akihudhuria mikutano yote ya ''uchochezi'' dhidi ya Waingereza.
Salum Abdallah alitoa fedha nyingi kupita wote kumpa Germano Pacha
kuja Dar es Salaam kuwakilisha Western Province katika kuasisi TANU.
Salum Abdallah ni mmoja wa wanachama wa mwanzo wa TANU
Salum Abdallah 1955 alikuwa rais muaisisi wa Tanganyika Railway African
Union (TRAU) chama hiki kilipigana bega kwa bega na TANU katika kupigania
uhuru.
Salum Abdallah aliongoza mgomo wa Railway wa 1960 uliodumui siku 82 mgomo
kama huu wa miezi 3 haujapata kutokea.
Salum Abdallah katika mkutano wa Moshi 1962 alimpinga Nyerere katika suala la
kuweka vyama vya wafanyakazi chini ya TANU.
Hii ndiyo sababu ya yeye kuwekwa kuzuizini.
Babu yangu hakuwa haini.
Babu yangu alikuwa mzalendo mpigania uhuru kwa vitendo toka enzi za African
Association akiwa akiwa Dar es Salaam.
Nyerere alipata hofu ya wazalendo kama hawa waliokuwa na uwezo wa kuwakusanya
wananchi pamoja kudai haki zao.
Mgomo ule wa 1960 ndiyo uliomfanya Nyerere apate hofu na Salum Abdallah.
Alipokufa 1974 TANU walifika mazikoni na walisoma taazia ya kumsifia babu yangu
na kumwita mzalendo aliyejitolea kwa hali na mali yake kuipigania nchi yake.
Huyu alikuwa Mmnanyema kizazi cha kwanza kuzaliwa Tanganyika baba yake Samitungo
aliingia nchini kama askari katika jeshi la Wajerumani.
Bwana Nyerere,
Ahsante sana kwa michango yako lakini naona kama
mnakasha unaanza kupoteza ladha yake kama chai
iliyopoa au mchuzi usio ndimu.
Sijui kama hii ni dalili ya uchovu au kitu gani.
Mimi kwa sababu ambazo nadhani ziko wazi huwa sina
kawaida ya kumuuliza mtu swali lolote labda kama
nataka ufafanuzi.
Nimeweka vitu vingi ambavyo nilidhani ukumbi watavichangamkia.
Kuna mtu alisema EAMWS ilikuwa inamchimba Nyerere.
Mimi nikasema hiyo ilikuwa propaganda ya serikali na nikamueleza
na hata kuweka jina la bingwa wa propaganda wa zama zile.
Rashid Kayugwa.
Nilitegemea hapa pangenogesha barza.
Wapi mmetishika.
Mmetishika kwa kuwa mmepata mshtuko kuwa Mohamed hakika
haya mambo anayajua.
Nilitegemea mtaunganisha na jina la mgawaji hongo kwa wanafiki
waunge mkono BAKWATA.
Mgawaji hongo yaani rushwa aliyekuwa akizunguka na mikoba iliyojaa
fedha alikuwa...
Geoffrey Sawaya.
Mkurugenzi wa Mashtaka ya Jinai.
Hii ndiyo serikali yenyewe na vyombo vyake vya ukandamizaji vikiwa
kazini.
Waislam walikuwa yatima.
Walichokipigania kimeporwa na kanisa.
Nilitegemea angalau mniite muongo mpiga soga nk. nk.
Lakini hadi sasa kama vile nimekumwagieni maji ya baridi ya kuzizima.
Turudishe mnakasha katika reli tuache hii kutupiana madongo kama vijana
mnavyopenda kusema.
Huu ni mjadala mzuri sana.
Si muda mrefu viongozi wa dini zetu kuu hizi watakaa mezani kuzungumza.
Itakuwa vyema sisi wafuasi tujue chanzo cha chokochoko na fitna hii inayogawa
taifa letu.
Kubwa zaidi tuwajue walosababisha hii fitna.
Nashukuru sana ndugu yangu Mohamed Said kwakuamua sasa kuwapa ukweli halisi wanajamvi wanaotufuatlia hapa!
Ndugu zangu wanajamvi, Mashehe aliowataja hapo juu na baadhi ya makasisi wa kikristu, ndio wali ASI serikali ya TANU iliyokuwa chini ya Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere,
Tuipongeze serikali ya TANU kwakuzima maasi yale ya chini kwa chini na kufanikiwa kuwatia nguvuni viongozi na waambata wao wote wa maasi dhidi ya ukombozi wa nchi yetu takatifu.
Mohamed Said, mimi ninajua mengi huenda kuliko hata kukuzidi wewe, kinachonishangaza, mbona hukutaka kuwaambia ukweli kwenye Kitabu chako mashabiki wako hasa waislamu wenzio wanaokuunga mkono?
Waambie tu usiogope, waambie kuwa "wazee wetu akina Sheikh Hassan bin Amir waliasi, na wakakumbana na mkono wa sheria ya nchi"!
Hongera kwa vijana wa wakizalendo wa usalama wa taifa Sawaya na Kayugwa waliojitolea nafti zao kupambana na mashehe hawa walioasi, kwakuwa walifanya kazi nzito katika mazingira magumu na wakafanikiwa.
Darwin,Soma haya machache kutoka paper yangu ''Christian Hegemony and the Rise of Muslim Militancy in Tanzania'' (Zentrum Moderner Orient (ZMO), Berlin. Paper hii niliiwasilisha Ujerumani 2011:''It took a decade to bring the Muslim movement back on track and the irony for that was, it was not CCM the old enemy which was responsible for that but an opposition party, Chama Cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA) seemingly under the tutelage of Catholic Church out to oust a Muslim president, Mrisho Jakaya Kikwete, which broke the camels back. The Catholic Church prior to election issued an Election Manifesto and a document of guidance on how Christians should vote. The presidential candidate for CHADEMA was a former Roman Catholic priest. That said it all. Muslims mobilised for the general election in a manner never seen before to oppose CHADEMA and the Church. Muslims irrespective of their political affiliations campaigned for the return to office of a Muslim president Jakaya Mrisho Kikwete.''Siasa zetu ndipo zilipotufikisha hapa. Wakati umefika wa kujiuliza vipi tumefikia hali hii ilhali wakati wa kupigani uhuru wa nchi hii tulikuwa wamoja?
Moh' Said na vijana wako akina Boko Haram!Sometimes huwa tunajiuliza weledi wenu nyie kama wasomi hasa mnaposhabikia vitu mnavyojua kabisa kuwa ni propaganda.Moh' Said, unasema habari za EAMWS kuhusishwa na radical islamists miaka hiyo mpaka kupigwa marufuku kwake, ilikuwa ni propaganda tu.Yes, ilikuwa ni propaganda kwa sababu unataka kuhusisha kanisa na Nyerere kwamba ndio wali-collude.Lakini kuhusu Chadema kuwa chama cha kikatoliki kwa vile tu mgombea wake aliwahi kuwa Padre- hizi sio propaganda, si ndio?Kwa mtaji huo mtaendelea kutumiwa na wanasiasa mpaka mchanganyikiwe (kama bado hamjachanganyikiwa).Mzee Mohamed Said kama kuna siku umepiga msumari mzito ni leo yani hapa ndio ni likuwa nataka nadhani YERICKO NYERERE yuko hoi mimi nilikuwa nataka ajibu hii point yako hapa
Bora umekuja kwa mtindo mwingine kuja njia nyingi za kujifunza.
Ndio ni jibu la hoja, unayo fursa ya kupinga au kukubali mkuu!
Waambie ukweli wafuasi waku kuwa wazee wako waliasi serikali.
Ndugu yangu Ritz, mnakasha huu tutakufunza mengi ambayo naamini toka moyoni mwangu tena upande wa kushoto ulipo moyo, haungeyapata popote mpaka safari yako duniani inaisha na unaingia kaburini, si wewe tu bali ni wengi tu hapa wanazidi kufunguliwa!
Hawakufutwa kama unavyodai/mnavyodai,(SASA WAKO WAPI??MBONA NIMEJITAHID KUSOMA VITABU VINGI SANA VYA HISTORIA LAKINI SIJAKUTANA NA HAWA NDUGU ZANGU KAMA WALIVOAINISHWA NA MKWASI WA HISTORIA NDUGU MOH' SAID??
Historia inawafahamu wote, ni wewe tu na wengine ndio mnaoamini kuwa wazee wenu walifutwa.(KAMA INAWAFAHAM WOTE,KWANINI SASA JULIUS PEKEE NDIE AWE KINARA NA WENZAKE WALIOMKARIBISHA MJINI NA KUMUUNGANISHA KWENYE HARAKATI WAKAPUUZWA NA KUACHWA NJE YA ULINGO HUO MOJA KWA MOJA??
Hakuna tamko mahala popote lililotamkwa na kiongozi wa nchi hii kuwa amefuta rasmi historia ya wazee hao, ila Uchochezi na propaganda za akina Mohamed Said tu ndizo mnazoozisikia na kuamini.(KWANI YAHITAJI TAMKO ILI TUWEZE FAHAM KUWA HISTORIA YAO WALE WAZEE IMEFIFISHWA??MADHARA YA KUKAA KUSUBIRI TAMKO NDIO HAYA YALIYOPELEKEA HADI JULIUS KUVESHWA UBABA WA TAIFA HILI,YERICKO UPO??BILA SHAKA TUNAENDA SAWA SASA,
UBARIKIWE SANA YERICKO NDUGU YANGU,UZI WAKO HUU UMEWAFUNGUA MACHO WENGI,USHUKURIWE YERICKOO..
Haya maneno yananikumbusha uzalilishwaji wa masheikh wetu kama Sheikh Nurdin Hussein na Sheikh Mohamed Nasoro wa Zanzibar.Sheikh Nurdin Hussein na familia yake walitolewa Lindi na kuhamishiwa Muheza,Tanga kwa mabavu chini ya maagizo ya Nyerere.Katika maeneo yaliyokuwa na uislam au kuonyesha ustawi wa maendeleo yenye kuwagusa waislamu Nyerere aliyavuruga na kigezo cha vijiji vya ujamaa na kuyaacha huku upande wa pili kuyapa fursa za maendeleo maeneo yanayokaliwa kwa wingi ma wakristu.Halafu kibaya zaidi anataka kutuaminisha ya kuwa mateso wanayoyapata Masheikh leo yana mfanano na wakati ule wa Nyerere alivyowafanyia Waislam na hasa Masheikh. Hoja hafifu kabisa.