Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Sijakwazika na chochote unapofanya mjadala wakati umeishachagua upande hata ukitoa hoja zako zinakosa nguvu.
OK. Nakupongeza kama umeelewa kuwa nimechagua upande unaosimamia 'hoja za ukweli'. Kama unanifikiria nipo upande mwingine mbali na huo, basi pole sana. Tuendelee.
 

basi julius angeonekana ana busara zaid kama angeamua kuwafungulia mashitaka ya uhaini ili kuujuza ummah wa watanzania juu ya hila kuu iliyokawa inafanywa na wazee wale kuliko kuwaweka kizuizini,ni wazi kabisa kwa kufanya vile alikuwa anahofia ukweli kudhihiri pindi pale wananchi wataamua kuhoji,na leo tumehoji kisha ukweli unadhihiri namna hii..!
 
sasa naamini kwamba mwanakijiji anampinga kikwete kwa sababu ni muislam tu. Mbona nyerere anampamba sana huku akisahau kwamba ndie alietufikisha hapa kwa umaskini?

Sijaona mantiki yako
 

tunashukuru sana,nasi tumeipokea,tumeitathmin kwa kina,tumeidadis kisha nasi tutawarithisha watoto na wajukuu zetu pasi na kificho..!
Siku zote kwenye haki na batili,batili hukaa kando,leo hii imedhihirika.
 

Wewe unaonekana mvivu kusoma vitabu na historia kubwa unayoijua ni ile ya kupita darasani, tena ile ya tuliyosoma shule ya msingi, umekuwa muumini wa vitu vipya kwa sababu huvijui na huna uhakika navyo...unameza tu...soma ndugu
a
 

Unaifahamu sheria ya tanzania inayompa mamlaka rais kumuweka mtu kizuizi?

Kaisome mkuu
 
Ikiwa una maana ya Dentation Act ya 1962 ndiyo naifahamu vyema.

Siyo kuijua tu naifahamu hata historia yake na ilichukuliwa kutoka wapi
na nani aliitilia bidii itumike.

Lakini haya tuyaache majibu ya kifedhuli yana shida zake Waswahili tunasema
itakuwa nipe nikupe mpate mpatae.

Heshima na taadhima zitaondoka.

Hii si nzuri kwa afya ya mnakasha.

Lakini kuna kisa cha Chief Kidaha Makwaia aliyefungwa Tunduru.
Taarifa zake vipi na yeye alikuwa ana mpango wa kupindua serikali?
 
Wewe unaonekana mvivu kusoma vitabu na historia kubwa unayoijua ni ile ya kupita darasani, tena ile ya tuliyosoma shule ya msingi, umekuwa muumini wa vitu vipya kwa sababu huvijui na huna uhakika navyo...unameza tu...soma ndugu
a

Amedandia hoja bila kusoma chanzo cha hoja hiyo!
 
twashukuru sana tena sana Mzee wetu Mohamed Said kwa historia hii.
Umefanya jambo kubwa sana kuikusanya historia iliyofichwa.Mungu atakulipa kwa ihsani hii uliyotufanyia
 
Last edited by a moderator:

mzee Mohamed Said,

hii mitego unaweza kumpasua kichwa huyu kijana

Kaka Do santos upo?
 
Last edited by a moderator:
teh teh teh! nimecheka sana.kwamuda niliamua niwe nasoma tu kuliko kuchangia.
Ila 'kisa' hiki alichokiandika bwana Yericko Nyerere kimenifanya niandike kidogo.
Amekisoma kitabu cha Mohamed Said,kwa bahati mbaya hakukielewa.Amekihisi zaidi kuliko kukitambua.
Ni kitabu kilichofanyiwa utafiti makini tena wa muda mrefu.
Kimemuudhi,kimemkera pia kimemshawishi naye eti ajaribu kuandika historia ya 'baba' yake.
Wazo limekuja ameshachelewa.Ataanzia wapi na kwa nani?
Ni bora achukue maelezo ya Mohamed Said,ayabadilishe kulingana na mahitaji yake.
Ndipo hapo kinapotoka kisa cha kuchekesha.
Ni kazi kuthibitisha.ni kazi kupotosha ukweli.
cc kichwakigumu Ritz Barubaru mv butiama THE BIG SHOW
 
Last edited by a moderator:
1974 Kinshasa.
Muhammad Ali yuko ulingoni na George Foreman.

Foreman alikuwa na record.
Mpinzani havuki duru ya tatu.

Anakuwa keshawekwa chini flat.

Ilipofika raundi ya tatu handlers wa Foreman wakawa kwa sauti
wanamwambia Foreman.

George finish him off.

Ali anasikia.

Daktari wa Ali Dr Pacheco akamgeukia Ali anamuuliza vipi unasikia
maneno hayo?

Ali akamjibu Dr Pacheco akamwambia mimi huyu nampiga.

Pacheco akasema fanya haraka basi.
Ali akamwambia sitaki kumfanyia haraka nataka nistarehe na yeye kwanza.

Naam.
Ali ulipofika wakati akampiga Foreman kwa nockout.

Katika kitabu cha maisha yake The Greatest Ali anasema.

Kuanzia pale round ya tatu alimchukua Foreman katika njia ambayo kabla yeye
Foreman hakuwahi kutia mguu.

Mimi hawa sina papara nao mimi ni mtoto na mjukuu wa watu walioanzisha TANU.
Ndiyo maana unaona humu natamba.

Mawanda haya yote wazee wangu wamepita na mimi wakanipitisha.
Siyo kwenye mbeleko.

Wamenipitisha mtu mzima na akili zangu natembea mwenyewe kwa miguu yangu.

Niliwawekea tuvuti ya Baba wa Taifa inasema TANU kaasisi Nyerere Pugu.
Wameikataa.

Nimewawekea bandiko zima Sivalon anasema Kanisa Katoliki linautizama Uislam kama
adui.

Wamemkana Sivalon.

Nimeweka taarifa kadhaa.
Wanataka ushahidi wa kimahakama...

Lakini hapa kwa nyakanga.
Nyimbo hazishi.

Insha Allah kuanzia hapa nataka nimchukue Bwana Nyerere katika safari ya masafa marefu
hajapatapo kwenda.

Hajui njia.
 
Kama hata babu yake Mzee Mohamed alikumbana na Mwalimu wakati anahangaika kuiweka NCHI pamoja, sitashangaa tena kumwona mzee huyu akiendeleza chuki zake kali kwa Mwalimu. Huu ni ubinadamu wa kawaida sana. Tatizo ni pale anapojitahidi kisomi na kijanja sana kuwaingiza WAISLAM wote kwenye chuki hii mbaya ya kurithi.

Mzee Mohamed utaona unafanikiwa lakini ni kwa muda tu. Haya yatapita kwa kuwa sasa umeyaanika hadharani. Mungu kama ni wetu sote atakupatiliza tu.
 

Mkuu ndio napambana kwanza na jet lag, halafu ujamaa bado umenikaa - scanner mpaka nikaifuate ya bure maktaba!
 
Mzee Said, babu yako si alikuwa miiongoni mwa wale "radical Muslims" wa mwaka 1957 ambao walitaka kumuondoa Nyerere kama kiongozi wa TANU kwa sababu ya Ukristu wake? na ilikuwa ni mara ya pili kujaribu kufanya hivyo?
 
nipo kaka Mohamed Said 'atamuua' huyu kijana
Anampa ngumi za KO

Hatupo kwenye mnakasha huu ili mtu ashinde, la hasha,

Lau ingekuwa madhumuni ni hayo basi ningeshakabdhiwa kombe mda mrefu sana tangu ukurasa wa kwanza tu!

Hapa tunakosoana kwa hoja na kupeana fikra mpya huku nikimunya Shekhe wenu aache uchochezi usio na tija kwa taifa!

Nimekupeni kisa hicho cha uasi wa washarika waukombozi chini ya TANU, na jnsi mkono wa dola halali ulivyowaangukia kiasi cha kilio chao leo kuakisi hadi kwa mjukuu wao Mohamed Said!

Mkitulia kimuhemuhe nitakupeni kisa hiki kwa upana na kazi nzuri sana waliyoifanya usalama wa taifa kuwazima waasi hawa
 
Last edited by a moderator:
Mzee Said, babu yako si alikuwa miiongoni mwa wale "radical Muslims" wa mwaka 1957 ambao walitaka kumuondoa Nyerere kama kiongozi wa TANU kwa sababu ya Ukristu wake? na ilikuwa ni mara ya pili kujaribu kufanya hivyo?

Nimemkumbusha kisa hicho na kile cha baada ya uchaguzi wa TAA kisha kile kisa mujarabu kilichozaa sheria ya kumuweka mtu kizuizini ya mwaka 1962 baada ya uhuru, amebaki kuhamaki tu na kusema ninauhamisha mjadala,

Nimemwambia atulie tuliii apewe asiyoyajua au anayoyajua lakini anayaficha kwa mlango wa propaganda za udini alionao.
 
Mzee Said, babu yako si alikuwa miiongoni mwa wale "radical Muslims" wa mwaka 1957 ambao walitaka kumuondoa Nyerere kama kiongozi wa TANU kwa sababu ya Ukristu wake? na ilikuwa ni mara ya pili kujaribu kufanya hivyo?

wewe ndio mwanakijiji wa meremeta? kutoka mapambano ya UFISADI Hadi koti la UDINI? kwishnei
 
Siwezi kuweka chuki.
Hatujapata kuwa na chuki.

Wazee wangu walipofukuzwa TANU Office 1963.

Walirejea majumbani kwao wakakaa hadi umauti
ulipowafika.

Wakamwacha Nyerere kama alivyokuwa akitaka awe.
Wamekufa na wakawa wakizikana wenyewe kwa wenyewe.

Nyerere hana habari wala shughuli na wao.

Kama kueleza haya wewe unaona chuki hiyo ni bahati mbaya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…