gombesugu,
..basi tukubaliane tu kwamba Znz kulikuwa na
"mpasuko."
..vyovyote vile utakavyoamua kuuita
"mpasuko" huo kama ni uarabu vs uafrika, au mabwanyenye vs wanyonge, au mabwana vs watwana, etc etc vyote ni sawa tu.
..mimi ninachosisitiza kwamba kulikuwa na tatizo/
"mpasuko" ndani ya jamii ya wa-Znz, na hicho ndicho kilichopelekea mapinduzi yale kutokea.
..kwa mtizamo wangu, wa-Znz wengi wako ktk denial. wanajaribu kila njia kuonyesha kwamba kulikuwa hakuna tatizo lolote lile
"internal"; kwamba mapinduzi na ukatili ulioyafuatia, umetokana na fitina za watu wa nje.
..ndugu yangu, kuna mambo mengi sana ambayo tunaweza kuyajadili kama wa-Tanzania/wa-Tanganyika ikiwa utapenda. tatizo ni kwamba kuna "
vichwa maji" wameiteka jamii yetu na kila jambo wanataka kutumbukiza masuala ya udini.
..umewataja ndugu zetu Wagogo, Wahehe, etc etc. sasa hawa tukitaka kuzungumza nao, au hata kuwapa "ukweli mchungu," basi tuna watani wao wanaweza kutusaidia.
..Kwa kweli wa-Tanzania/wa-Tanganyika tusipokuwa makini tunaweza kuisambaratisha nchi kwa haya masuala ya udini-udini. mimi nadhani tufike mahali kila mtanzania/Mtanganyika ajisaili kama matendo yake, na matamshi yake, haswa linapokuja suala la dini/imani, yanaijenga, kuilinda, na kuihifadhi, jamii yetu.
cc:
Nguruvi3,
Mag3,
Wickama,
Ritz,
THE BIG SHOW,
Yericko Nyerere,
Jasusi
JokaKuu,
Natanguliza shukran zangu za dhati kwako ndugu yangu.
Nakubaliana na mengi ulonena na pia nakufahamu uzuri mno. Nafikiri unakumbuka tahadhari nilowahi kutoa mimi binafsi kwa kuonyesha mfano wa
Sudan wakti najadiliana na ndugu yangu
Nyambala,I think it was only on my second week here/
Jamvini!?
Nimecheka kiduchu kwa hilo neno ulotumia
"Mpasuko"!ahaha!! Najua unajitahidi usiwakere nduguzo
Wazanzibary wakaja kukuvamia hapa
jamvini bure bileshi!?ahaha!!
Nafikiri ni neno zuri mno hilo
"mpasuko"..."mpasuko wa Zanzibar". Kwa kifupi sisi tulobaki ni wasindikizaji lakini vinara wa kutunyambulia kwa kina ni
ma-Historians,ndo maana ni muhimu kumpata
Sheikh Mohammed hapa
jamvini nasi tukamuuliza maswali ya kina na kiundani katika hali ya uungwana na ustaarabu,ili tujue mbivu na mbichi!?
Kuhusu
Wazanzibary wengi kuwa katika
denial kama unavyodai;yawezekana ni kweli. Lakini hiyo yawezasababishwa kutokana na mambo mengi mno na hata pia udhaifu/udhalili wa
kimwana-Adam yeyote!?
Nafikiri labda hapo
Wazanzibary wanachojaribu kuonyesha ni yakuwa hata kama walikua na mpasuko/matatizo ya ndani ya nchi yao, ambayo kutokana na
History ya Zanzibar,hayo matatizo/mpasuko illikua ni lazim uwepo yasingeweza kuepukika asilan....lakini sio kwamba hiyo ndio iwe
licence ya kuhalalisha mavamizi ya kutoka
"nchi ya kigeni" kijeshi au kusaidia
waasi kuleta zogo na mauaji!?
Nafikiri valid point nyingine ya
Wazanzibary;ni zile
grievances walizonazo kutokana na
Nyerere alivyoiendesha na kuing'ang'ania nchi yao kwa kipindi kirefu mno,tena huku akiwanyima haki zao nyingi na kurudisha nyuma kwa kiasi kikubwa maendeleo ya
WaTanganyika wenzie!?ahaha!!
Takupa mfano kiduchu;embu angalia jinsi
Rais Aboud Jumbe Mwinyi maskini jinsi alivyofanziwa na
Nyerere na kusambaratishwa kama vile alikua ni
Muhaini!?
Wazanzibary woote hawakuhusishwa kwa chochote wala lolote,mimi nilikuwapo
Zanzibar ule mwaka. Nakumbuka jioni inatangazwa kwenye Tv yakuwa
Rais Jumbe ati "amejiuzulu" na atarejea
Zanzibar akiwa sio
Rais tena bali kuja tu kufungasha virago vyake na kwenda kupumzika pale
Mjimwema!?ahaha!!
Kisiwa chote kilikua chini ya
standby ya Kijeshi,safari zoote za maji na anga zilizoonekana sio muhimu zilisitishwa kwa siku kadhaa. Kwa kifupi ilikua kama vile kumefanzika
Mapinduzi baridi.
Seif Shariff,tunajua alifurahika mno...na ndo alifikiri plan na ndoto zake za kuwa
Rais wa Zanzibar wakti huo zingetimia. Kumbe alikua kaghafilika kiduchu yakuwa
Nyerere alikua ni
political mastermind! "Machele punga" maskini Seif mpaka kesho!ahaha!!
Hata hiyo changamoto ya kudai hiyo
Tanganyika iliyopo leo na hata wale
G55 waliokua wakiongozwa na
Philip Marmo nafikiri wakti ule,hizo zoote ni mojawapao ya matunda na fikra za
Rais Jumbe.
Nafikiri unakumbuka jinsi gani
Nyerere alivyotumia ubabe na maguvu mengi mno kupingana na madai ya wale
G55 ya kutaka iwepo
Serikali Tatu ikiwemo ya
Tanganyika!?
Kama
WaTanzania kweli tungekua wastaarabu na kukumbuka mema basi ilitakiwa
Rais Kikwete au
Serikali itoe tamko Rasmi la
kumtaka radhi Rais Jumbe kwa jinsi alivyodhalilishwa kipindi choote kile huku akionekana kama Muhaini maskini.
kumbe yale yoote aliokua akishauri au alotaka yafanzike ndo leo yamekua ati yanashikiwa mabango na wazandiki wengine wakiongozwa na yule Mzandiki na fitna mkubwa
Seif Shariff Hamad na huko
Bara/Tanganyika ati nako kuna "Tume ya Katiba" ikiongozwa na
Sinde Warioba!?
Kwa kifupi
Seif ni mroho tu wa madaraka,kama si hivyo aachie ile ngazi ampe na pia amsaidie kumtangaza mwenzie
Juma Ali Duni kule
Pemba tena kwa nguvu zoote sio kinafiki...
Msomi mkali kushinda yeye na
good orator na pia ni Mwanasiasa Nguli azijuaye na kuzimudu fitna zilizomo kwenye siasa za
Kizanzibary!?
Nakumbuka kuna wakti niliweka mjadala mkali mno na ndugu zangu tena wa karibu toka
Unguja waliponitembelea;basi katikati ya majadiliano akatokea ndugu yangu mmoja mstaarabu tena msomi mzuri...ati akaniomba tutoke nje ya nyumba kiduchu tukapigane/akanipige!?ahaha!! Ati kisa niliwaambia
"ukweli mchungu", nakukopa neno lako hapa kiduchu.
Colonel Seif Bakari a.k.a "Kiwavi"...alisimama kwenye kikao cha CC ya NEC ya
CCM na kutaka kumzaba
Rais Jumbe kibao mbele ya
Nyerere na almost full Cabinet ilikuwapo. Seif Bakar,alimwambia Jumbe yakwamba si tulikuambia na kukukataza yakuwa usivunje
ASP na wala usikubali kuunganisha vyama asilan,nawe hukutaka kutusikia!? Leo kiko wapi,sisi tunamjua huyo
Nyerere fitna na ghilba zake!?
Kumbuka
Seif Bakar,na takriban Members woote wa
BMZ walimshauri
Rais Jumbe yakuwa asikubali asilan kuvunja hata ule
Usalama wa Taifa wa
Zanzibar na kuunganishwa uwe jambo la
Muungano. Lakini nafikiri baada ya kifo cha
Karume,ile confidence ya
Rais Jumbe ilkua kiduchu mno,ndipo pale
Nyerere alichukua
advantage na kuanza kumtisha na kumlazimisha na kumsainisha mikataba na mambo kadhaa kinguvu,bila hata ya kufuata
sharia za nchi. Vitu ambavyo Nyerere
asingethubutu/hakuthubutu kumfanzia au kumlazimisha yule
mbabe Baharia Karume!?
Nafikiri sisi soote tunajua yeyote aliekua akihoji chochote au lolote khasa kuhusu Muungano wakti huo ilikua
Nyerere anamtia ndani bila hata ya kwenda Mahakamani au kufuata sharia!?ahaha!!
Nafikri unajua baada ya kile kikao kilichomkuta
Seif Bakar!? Ilikua katika utawala wa
Rais Mwinyi maskini,ndo alokuja kumtoa kizuizini nduguye na kumpa
Mkuu wa Wilaya nafikiri.
Hapo sasa ndo tupo hapa jamvini kusikiza kwa utuvu toka kwa
Sheikh Mohammed.
Nafikiri tuyaache kwa hapo,na huo pia ni mtazamo wangu kiduchu tu ndugu yangu. Kama kuna yeyote mwenye kutaka
source ya hizo khabar tafadhali anijuze!ahaha!!
Kuhusu hao watu ulowaita
"Vichwa Maji wafia udini";ni kweli hao watu ni khatar wanapokuwepo popote pale dunia nzima.
Leo tunaona wale wapumbavu kule
Syria wanauana wenyewe kwa wenyewe huku
mwa-Amerika na Kibaraka wao
Saud Royal Family wakiwapeleka kwa remote control!?ahaha!!
Tunaona leo yule mwanaharamu
Joseph Kony unyama wake...anabaka,kuuwa,kuchoma na kutesa viumbe vyoote tuvijuavyo tena ana-justify hayo kwa kutumia
dini,khalaf ati anafikiri ndio atakwenda kukutana na
Bwana Yesu kesho peponi!?ahaha!! Kuna viumbe wapumbavu saana hapa duniani!
Pana mifano na vichekesho vingi mno kila pembe ya dunia. Lakini tuangalie na hapo kwetu japo kiduchu.
Embu angalia ati nimesikia imefikia mpaka watu kufa/kuuana na kufanziana hasama na farka zisizo mipaka hapo
Tanganyika...ati kisa wanagombania kuchinja majogoo na ngo'mbe!?ahaha!!
Yaani
wa-Afrika sisi ni watu wa ajabu mno,wenzetu wanataka na kuharakisha kuhamia kwenye sayari nyinginezo,sisi ndo kwanza tunauana ati kwa kugombania
kuchinja majogooo!?ahaha!!
Nastaajabu,tena kuna mpaka
Viongozi kadhaa wa kidini wenye kuheshimika na wenye influence kubwa hapo nchini,ati nao wameamua kujikita kwenye masuala hayo tena huku wakimtaka/wakimtishia na
Rais wa nchi aingilie kati kwa haraka,na huku wakimpa
ultimatum!?
Takupa mfano kiduchu,wakti nipo mduchu tukikaa pale
Mlimani UDSM. Wakti ule takriban majirani zetu woote walikua
Wakristo,wenye mapenzi hishma na ustaarabu wa hali ya juu mno.
Rafiki yangu mmojawapo alikua ni Gilbert,mtoto wa
Prof. Mbwiliza...Gil alikua kila wakitaka kuchinja kuku anakuja kunitafuta,anakua ametumwa na Mama yao au Baba yao ili nikawachinjie.
Pia walikua wakihakikisha lazim wanikaribishe dinner siku hiyo ili tule na kufurahika pamoja siku hiyo...japo takriban mara zoote nilikua natoa excuse zangu.
Halikadhalika,tulipohama pale pia tulikua na jirani yetu mwingine Mzee mstaarabu mno wa Kihaya,msomi mzuri na Mkristo mtiifu mno akiitwa
Mzee Mutakyahwa....nae halikadhalika tuliishi nao vyema na Family zetu zilikua zina mapenzi makubwa mno. Hii khabar ya kuchinja pia niliendelea nayo kwa hawa Mutakyahwa's.
Najua kuna
"wasomi wa hali ya juu" hapa
jamvini,wanaweza kuona hivi vitu havina maana yeyote na pia waka-over look point fulani. Lakini binafsi naamini yakuwa uhusiano mwema au mbaya siku zoote huanzia baina ya watu au family fulani,majirani au kwenye kijiji/Tarafa kabla yakuwa/haujawa aidha janga au mafao
kwaTaifa!
Kwa hiyo binafsi nakhis, kabla ya
kulaumiana Ki-Taifa,yatakiwa pia tujikumbushe ule wajibu wetu wa kila siku kwa majirani zetu bila ya kujali viwango vyao vya Ilm,dini zao,matabaka/makabila yao,urangi wao na mengineyo mengi mno.
Niwie radhi kwa nilonena kwenye huo uchechefu wangu,na kama unakhis kuna lolote hukupendezwa nalo tusameheane ndugu yangu.
Ahsanta sana.
Cc;Ritz