The Big Show,
Salaam Al Akhiy.
Ndo nachungulia kwa utuvu asubuhi hii ile mipini yenu na bayana zenu adimu na Shariff Ritz, mloziteremsha jana baada ya Salat Al Ishai.
Nimecheka kiduchu ulipomwambia ndugu yetu Maika nafikiri,yakuwa huo ufumbuzi toka kwa Sheikh Mohammed kwani yeye anafanza mradi/utafiti wa Malaria!?ahaha!!
Nakhis ukiangalia kwa utuvu haya majambo,ni kinyume cha matarajio ya wengi mno khasa huyo Yericko&Co. Yaani huu mnakasha/mjadala pia umesaidia mno kuondosha kabisa ile Credibility(kama iliwahi kuwapo) ilokua inapewa ile Historia ya Kivukoni.
Nafikiri kwa Sheikh Mohammed,yeye amepata jukwaa zuri na jingine zaidi la kutambulika nchini na kuzidi kusomesha.
Wanajamvi wengi mno hapa ambao pamoja na kukiri kwao yakuwa hawakubaliani na baadhi ya vitu/maandiko ya Sheikh Mohammed...lakini nafikiri kwa mara ya kwanza wamejikuta wanakumbana na vitu adimu toka kwa Sheikh Mohammed,na wao wenyewe kukiri kwa mapana bila ya kulazimishwa/kuhimizwa na yeyote,yakuwa Historia ya Kivukoni ni utumbo na uozo mtupu...na sio tu yakuwa ina matundu mengi mno, bali ile ina mashimo na mahandaki mengi mno!
Nastaajabu,huyo Yericko hiyo kesi yake ya "Uchochezi,Uhaini na Ugaidi" dhidi ya Sheikh Mohammed alitakiwa ende akawafungulie wale mazumbukuku na Wachochezi wa amani ya nchi waloandika ule utumbo wa Kivukoni!?
Ahsanta.
Cc;Ritz