Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Ingekuwa vizuri kama kuna mtu anayo video clip ya hotuba hiyo ya Nyerere... Inasemekana imechakachuliwa.
kwa hiyo kutokana na hotuba hii kitabu kilichotetewa mpaka Cambridge kinakuwa batili miongoni mwa academics-kina hold grounds kwa vipofu kama wewe
 
hujajua hoja yake,vivo hivyo huwez kumjibia.
Yumkni hukumuelewa,ila yeye kanielewa.
 
Nimeshaiweka pale juu kabisa ya thread husika mkuu hebu isome

Kwa hiyo nilikuwa naijua Tanganyika African Association. Nilipokuwa ninaondoka kwenda Ulaya kusoma, nilikuwa nimeishaonja shughuli za TAA. Sasa niliporudi, baada ya kukaa Pugu siku chache, nikaja mjini Dar es Salaam. Nikauliza nani wanaongoza TAA? Nikaambiwa kuna jamaa mmoja anaitwa Abdul Sykes. Sasa ni marehemu. Abdul ndiye alikuwa katibu wakati huo.
Ndugu zangu nimekata kipande cha hiyo hotuba alipotajwa Abdulwahid Sykes.
Sasa shuhudieni mambo.

Mimi nilisema Nyerere kasahau cheo cha Abdu.
Mwanae kaleta ushahidi kuwa baba yake alikuwa hadhir.

Hakusahau cheo cha Abdu.
Sasa ni kweli Abdu alikuwa ''katibu wakati huo?''

Soma hii hapo chini:

Nyerere mwenyewe kamwe hajazungumzia kuhusu uchaguzi huu au namna alivyokuja kuongoza TAA Dar es Salaam. Kiasi cha karibu sana alichofika kumhusisha Abdulwahid na historia yake kilikuwa katika ile hotuba ya kuwaaga wazee Dar es Salaam, na kwa bahati mbaya Nyerere alipojaribu kumueleza Abdulwahid, alishindwa kwa kuwa kwa kauli yake alisema hakumbuki cheo alichokuwa akishika Abdulwahid katika TAA wakati yeye Nyerere alipojiunga na chama mwaka 1952. Hata hivyo gazeti la serikali, Daily News [1] lilijaribu kurekebisha historia kwa kutaja cheo cha Abdulwahid, ingawa kwa makosa, kwa kusema kuwa Nyerere alipojiunga na TAA makao makuu Abdulwahid alikuwa katibu. Ukweli ni kuwa Nyerere alimkuta Abdulwahid akiwa rais wa TAA.


(Kutoka ''Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes...'')

Sasa Bwana Nyerere hatuna sababu ya kuandikia mate na wino upo. Sasa tupatie hotuba katika sauti tumalize huu ubishi.
 
Mag3,

Mimi sijwahi kumdhalilisha Nyerere kama unvyotaka kuaminisha watu humu JF ninachopinga ni siasa zake zilikwama na hakufanikiwa kwenye uchumi. Tatizo nyie hamtaki Nyerere apingwe kwa chochote. Mitume wa mungu walikuwa wanapingwa sembuse Nyerere.
 
Last edited by a moderator:
anafahamika,,mimi na wewe pia sote twamfaham,au hilo pia hulijui au unaleta kejeli??
Kuziondoa kwenye mfumo huo tuh haitoshi,je athari zake si zimeonekana?
By the way siwez kupuuza mchango wa julius katika vitu vinavoonekana,siwez kuwa na chuki binafsi na julius,nipo hapa kuongea kile chenye tija pasi na kuhofia wala kuwa na nidham ya woga kwa kuonekana nimechagua upande fulani,kwa hali ilipokafikia ilikua haina budi zaid ya kuziondoa kwenye mfumo huo,ni julius aliziondoa kwenye mfumo huo,
thats why nakuambia kipindi mjomba wangu ndugu gallus abeid anabadili dini ili aweze kuipata secular education kumbuka pia waliokumbwa na hali hiyo na kuathiriwa na mfumo ule ni wengi,heko julius kwa kuutoa mfumo ule kandamizi,ila hilo tuh halifuti haya tunayosema sasa,kwani ni kweli yalifanyika.
 
Mag3, katika minakasha yote tumeelezea sana kuhusu hotuba hiyo kuanzia mwaka 2011.
Mohamed anashikilia kuwa Nyerere hakuwataja wazee wake, na alizuia historia isiandikwe au iandikwe kama alivyotaka yeye( ushahidi upo). Sasa leo imewekwa maneno na ikiwezekana tutaweka video uone jinsi mwalimu alivyosema.

Hakuuma maneno alisema wakati yanafanyika alikuwa mkristo peke yake. Maana ya haya ni kubwa sana.
Mtu wa kaliba ya Nyerere haongei hovyo kuvuruga taifa anaongea kwa diplomasia. Leo ingekuwaje kama angesema ''wakristo hawakuwepo wakati naombewa dua''.

Ramia, Sykes na Tambaza kawataja, sasa sijui kipi kimebaki hadi anaambiwa hakuwaenzi.
Mwanakijiji aliwahi kuandika mahali kuwa historia ya Mohamed inaweza kusimama na kuanguka hapo hapo.
Kila siku linakuja jambo na kuchujua uzito wa hoja za hisia na kitabu,
 
kwa hiyo kutokana na hotuba hii kitabu kilichotetewa mpaka Cambridge kinakuwa batili miongoni mwa academics-kina hold grounds kwa vipofu kama wewe

Wewe bora ungekaa kimya tu hujui chochote.
 

wacha tuuh mimi niitwe mfuasi wako,wacha tuh wanikejeli na kunitusi,lakini ukweli huu unaoutoa kwa kweli una mantiki kubwa sana kwa jamii ya watu waliokuwa gizani,
thanks a lot.
 

Ndugu zangu mnakasha huu unakwenda vizuri tu lakini naona kidogo hamaki
zinapanda.

Tujutulize tujiepushe na lugha za kushambuliana.

Mimi sijapata kumtukana Nyerere kama Mag3 anavyosema.
La kama ana ushahidi wa hilo na auanike hapa jamvini.

Kuhusu hotuba.
Nimeshaweka post yangu Insha Allah wanaukumbi isomeni.
 
Nani kasema imechakachuliwa? lete iliyosalama mkuu

Mimi hapa miaka ya nyuma nimewahi kuisikia hiyo hotuba tofauti na hiyo uliyoweka hapo hebu weka sauti tumsikie Nyerere akiwaaga wazee wa Dar as Salaam.
 
Ingekuwa vizuri kama kuna mtu anayo video clip ya hotuba hiyo ya Nyerere... Inasemekana imechakachuliwa.
Ndiyo maana Mohamed Said anaulizwa...je, anakubali au anapinga hii hotuba kutolewa na Mwalimu Nyerere mbele ya wazee wake wa Dar es Salaam? Akishajibu tutaendelea...mpaka sasa bado anaomba muda, anadai hajaiona! Je kama ilitolewa, imekuwaje afanye utafiti wote huo miaka yote hiyo asiwe nayo? Ritz unataka video clip, sawa, je ngano zote anazomwaga Mohamed Said kama peremende, kwa nini unaziamini? Alitoa video?
 
Last edited by a moderator:
wacha tuuh mimi niitwe mfuasi wako,wacha tuh wanikejeli na kunitusi,lakini ukweli huu unaoutoa kwa kweli una mantiki kubwa sana kwa jamii ya watu waliokuwa gizani,
thanks a lot.

Uzoefu wangu kwa mambo haya ni mkubwa sana.
Alhamdulilah.

Pale mwindaji anapukuja kugundua kuwa mtego
wake umenasa chui.

Ah! Keshachelewa.

Chui keshamjeruhi.

Mimi sishughulishwi na hawa ndugu zangu.
Nasikia wasikizaji wamegonga 20,000.

Hawa wasikizaji ndiyo ninaozungumzanao.
Hawa hawajapatapo kusikia historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika.
 
samahani MODERATORS,kama itakuwa ni kosa,nimempa mtu password yangu hili aingize audio ya ile hotuba ya nyerere-tuvumiliane but within 24 hours itakuwemo humu cause we need to get to the bottom of this-kanidokezea kwamba the omens are not good for MS
 
Mwanakijiji kaishaandika mengi sana ambayo hayajafanikiwa.
 
Niwekeeni hotuba.

Bado sijaiona.
Mkuu Maalim Mohamed Said, hotuba imewekwa kwa maandishi, neno kwa neno!.
"Kwa hiyo nilikuwa naijua Tanganyika African Association. Nilipokuwa ninaondoka kwenda Ulaya kusoma, nilikuwa nimeishaonja shughuli za TAA. Sasa niliporudi, baada ya kukaa Pugu siku chache, nikaja mjini Dar es Salaam. Nikauliza nani wanaongoza TAA? Nikaambiwa kuna jamaa mmoja anaitwa Abdul Sykes. Sasa ni marehemu. Abdul ndiye alikuwa katibu wakati huo.

Nilipelekwa na Kasela Bantu - ambaye naye aliteleza-teleza na hatunaye hapa (kwenye mkutano). Kasela Bantu alikuwa mwalimu mwenzangu. Tulifundisha pamoja Milambo. Nilipokuja Dar es Salaam, nikakuta anafanya kazi Redio (Tanganyika Broadcasting Corporation). Ni Kasela Bantu aliyenipeleka kwa Sykes.

Wakati huo mambo yalikuwa yanasinzia kidogo. Kwa muda mfupi mwaka ule, tukafufua-fufua, hasa kutoka Januari. Kufika Aprili, TAA ikafufuka. Tukafanya mkutano hapo Anautouglou. Kwenye mkutano huu wakanichagua kuwa Rais wao – wa TAA.

Ninasema yote haya kwa shukrani kwa wazee. Jamaa hawa walikuwa watu wazima wa Dar es Salaam, na mimi kijana mdogo Mzanaki, na Kiswahili changu si kizuri sana – cha matatizo.

Sasa kama yalioandikwa yote ni kweli ndiyo yaliyotamkwa, then wewe kuitwa mchochezi sio kutukanwa bali huo ndio ukweli halisi wa "the motive behind" kitabu chako!.

Ila pia kwa sisi Waafrika tunaoamini imani za mizimu, kumsingizia marehemu kunaleta laana ya aina fulani, nakushauri utubu ungali hai ili kuiepushia "bad karma" familia yako utakayoiacha nyuma baada ya wewe kutangulia mbele ya haki, isije kuadhibiwa kwa makosa yako!. Huu ni ushauri tuu na only if you belive the universal law of "cause and effects", "karma" haina mswalie Mtume wala haina huruma kwa wasio na hatia!.
Pasco.
 
samahani MODERATORS,kama itakuwa ni kosa,nimempa mtu password yangu hili aingize audio ya ile hotuba ya nyerere-tuvumiliane but within 24 hours itakuwemo humu cause we need to get to the bottom of this-kanidokezea kwamba the omens are not good for MS
Asante sana Son of Alaska lakini kama uonavyo, wapo watakaodai hata video...hawajui hata mwaka kituo cha kwanza cha Television kilipofunguliwa nchini! Ritz tayari anadai aliwahi kuisikia lakini...hatuamini hata sisi tuliokuwapo na kuipata "live".
 

kwa hiyo nilikuwa naijua tanganyika african association. Nilipokuwa ninaondoka kwenda ulaya kusoma, nilikuwa nimeishaonja shughuli za taa. Sasa niliporudi, baada ya kukaa pugu siku chache, nikaja mjini dar es salaam. Nikauliza nani wanaongoza taa? nikaambiwa kuna jamaa mmoja anaitwa abdul sykes. Sasa ni marehemu. Abdul ndiye alikuwa katibu wakati huo.

Ndugu zangu nimekata kipande cha hiyo hotuba alipotajwa Abdulwahid Sykes.
Sasa shuhudieni mambo.

Mimi nilisema Nyerere kasahau cheo cha Abdu.
Mwanae kaleta ushahidi kuwa baba yake alikuwa hadhir.

Hakusahau cheo cha Abdu.
Sasa ni kweli abdu alikuwa ''katibu wakati huo?''

Soma hii hapo chini:

Nyerere mwenyewe kamwe hajazungumzia kuhusu uchaguzi huu au namna alivyokuja kuongoza taa dar es salaam. Kiasi cha karibu sana alichofika kumhusisha abdulwahid na historia yake kilikuwa katika ile hotuba ya kuwaaga wazee Dar es Salaam, na kwa bahati mbaya nyerere alipojaribu kumueleza Abdulwahid, alishindwa kwa kuwa kwa kauli yake alisema hakumbuki cheo alichokuwa akishika abdulwahid katika taa wakati yeye Nyerere alipojiunga na chama mwaka 1952. Hata hivyo gazeti la serikali, Daily News (6 Desemba 1985) [1] lilijaribu kurekebisha historia kwa kutaja cheo cha Abdulwahid, ingawa kwa makosa, kwa kusema kuwa nyerere alipojiunga na taa makao makuu abdulwahid alikuwa katibu. Ukweli ni kuwa Nyerere alimkuta Abdulwahid akiwa rais wa TAA.

(kutoka ''Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes...'')

Sasa bwana Nyerere hatuna sababu ya kuandikia mate na wino upo. Sasa tupatie hotuba katika sauti tumalize huu ubishi.
 

Unaposema gazeti la serikali, Daily News lilirekebisha cheo cha Abdul, na katika hotuba ya Mwalimu ya kuaga mbele ya Wazee wa Dar Mwalimu alisema wazi kuwa Abdul alikuwa Katibu wa TAA, Je unataka tukuamini wewe kwa uthibitisho upi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…