Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Waliwezaje kuamua kwamba Kikwete ndiye mwislamu mwenzao na Prof. Lipumba sio?

Second, au the point here is waislamu ni wengi,ni zaidi ya 60% ya dini nyingine zote, na kwamba, waktristo walimpigia Dr. slaa na kura hazikutosha kwasababu hao wakrusto ni wachache sana.

Huyo ndo Mr. Researcher.

Hahaa huyo ndiye Mohamed Said, wanamtumia sana BBSwahiliTv, na Cambridge University wakimtaja kama mtaalamu wa historia ya siasa za afrika mashariki
 
@Mohamed Said, Jasusi, Mzee Mwanakijiji, THE BIG SHOW,

..nimepata kipande cha hotuba ya Mwalimu wakati akiwaaga wazee wa D'Salaam.

..bahati mbaya sijapata hotuba nzima. sijui kama miongoni mwenu yuko aliye na hotuba nzima.

..ile mjadala uwe mzuri basi tuwe na utaratibu wa ku-quote the original source.

Jokakuu, kipande hicho tu kinajibu kila tuhuma dhidi ya Nyerere. Kawataja akina Sykes hata kusema wao ndio walibuni jina la TANU kabla. Kawataja akina Tambaza na Ramia ambao Mohamed anadai Nyerere aliwatupa.
Sijui atakuja na utetezi gani. Kila jambo amelieleza vizuri tena bila kuuma uma maneno.
 
Jokakuu, kipande hicho tu kinajibu kila tuhuma dhidi ya Nyerere. Kawataja akina Sykes hata kusema wao ndio walibuni jina la TANU kabla. Kawataja akina Tambaza na Ramia ambao Mohamed anadai Nyerere aliwatupa.
Sijui atakuja na utetezi gani. Kila jambo amelieleza vizuri tena bila kuuma uma maneno.

Tarehe 27 Aprili, 1985 Julius Kambarage Nyerere, sasa akijulikana kama Baba wa Taifa,[1] katika sherehe kubwa katika viwanja vya Ikulu, alitoa jumla ya medali 3979 kwa Watanzania waliochangia katika maendeleo ya taifa. Kati ya wale ambao walipewa medali hizo alikuwa Sheikh abdallah Chaurembo. Wazalendo waliotajwa ndani ya kitabu hiki ambao walipigania uhuru wa Tanganyika, hakuna hata mmoja wao aliyekuwa katika orodha ile ya heshima. Baada ya siku chache kupita, Nyerere kama mtu aliyegutuka alimualika Dossa Aziz Ikulu. Dossa Aziz, wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika alikuwa mtu maarufu, mwenye nafasi, na kujiweza sana. Sasa Dossa baada ya miaka kupita hakuwa akifahamika tena na ule umaarufu na utajiri wake ulikuwa umetoweka. Alikuwa akiishi maisha ya kawaida kijijini Mlandege, maili chache nje ya Dar es Salaam. Katika sherehe ya faragha Nyerere alimtunukia medali Dossa Aziz, rafiki yake wa zamani. [1]
 
Mzee Wangu MOHAMED SAID SALAAM WALEIKUM, PILI SHIKAMOO.
MZEE WANGU NIMEFUATILIA KWA MUDA HII MADA, USIKU NA MCHANA, NDANI NA OFISINI.

NAOKUOMBA TU TUOMBE RADHI WATANZANIA, HII HOTUBA KAMA KWELI NI NDIO ALIYOISEMA MWALIMU WAKATI ANANG'ATUKA NI KWELI, BASI IMEJIBU TUHUMA NYINGI SANA AMBAZO ULIZITOA KUUSU YEYE, MFANO TU, KUWA MWALIMU HAKUKUMBUKA HATA CHEO CHA MAREHEMU ABDUL, IKIWA HILI LIKO WAZI, JE HIZO HOJA NYINGINE ULIZOJENGA KWA VIGEZO VYA KUADITHIWA NA WAZEE WAKO NI MANGAPI YAKUAMINIKA,
TUOMBE RADHI, WATANZANIA, SASA HIVI TUNAMPSUKO MKUBWA SANA, HOJA ZAKO NDIO ZIMEJENGA MSINGI WA MPASUKO. KAMA UNAWATOTO NA WAJUKUU BASI WAONEE HAYA HAO NA TANZANIA UNAYOWAACHIA.
 
Kama unamchukulia kama binadamu basi ana mapungufu yake usimpe sifa ya mitume.
 
Jokakuu, kipande hicho tu kinajibu kila tuhuma dhidi ya Nyerere. Kawataja akina Sykes hata kusema wao ndio walibuni jina la TANU kabla. Kawataja akina Tambaza na Ramia ambao Mohamed anadai Nyerere aliwatupa.
Sijui atakuja na utetezi gani. Kila jambo amelieleza vizuri tena bila kuuma uma maneno.

Ugomvi si huo.

Ugomvi hiyo historia siyo.
Historia ya Kivukoni si historia ya TANU.
 
Wengine tulizaliwa tulianza kujua au kuwa na ufahamu wakati wa awamu ya pili ila hii thread imetufundisha mengi ambayo tulikua hatuyajui.
 
Mzee Wangu MOHAMED SAID SALAAM WALEIKUM, PILI SHIKAMOO.
MZEE WANGU NIMEFUATILIA KWA MUDA HII MADA, USIKU NA MCHANA, NDANI NA OFISINI.

NAOKUOMBA TU TUOMBE RADHI WATANZANIA, HII HOTUBA KAMA KWELI NI NDIO ALIYOISEMA MWALIMU WAKATI ANANG'ATUKA NI KWELI, BASI IMEJIBU TUHUMA NYINGI SANA AMBAZO ULIZITOA KUUSU YEYE, MFANO TU, KUWA MWALIMU HAKUKUMBUKA HATA CHEO CHA MAREHEMU ABDUL, IKIWA HILI LIKO WAZI, JE HIZO HOJA NYINGINE ULIZOJENGA KWA VIGEZO VYA KUADITHIWA NA WAZEE WAKO NI MANGAPI YAKUAMINIKA,
TUOMBE RADHI, WATANZANIA, SASA HIVI TUNAMPSUKO MKUBWA SANA, HOJA ZAKO NDIO ZIMEJENGA MSINGI WA MPASUKO. KAMA UNAWATOTO NA WAJUKUU BASI WAONEE HAYA HAO NA TANZANIA UNAYOWAACHIA.

Usikimbilie kuombwa radhi.

Tusikize kwanza hotuba sote kile kipande alichosema
hakumbuki cheo cha Abdu kipo?

Kama kataja cheo chake hayo yatakuwa maajabu makubwa.
Kama kipande kimenyofolewa...

Sintoshangaa

Waarabu wanasema sababu huondoa ajabu.

Kuwa na subra tusikize hatoba kwanza.

Ogopa kusema sana kwenye jambo usokuwa na ithibati nalo.
Mie humu sifanyi maskhara.

Nimetafiti na kuandika kitabu tena sasa kina miaka 15.
Ni kitabu rejea katika African Studies duniani.

Hasomi mtu political history ya Tanzania sharti atakipitia kitabu changu.

Iwe niseme Nyerere kasahau cheo cha Abdu katika hotuba yake kisha
iwekwe tape anasikika Nyerere anasema, ''Abdu alikuwa rais wa TAA.''

Kila nilichosema katika kitabu kitabomoka.
Usomi hauna stamala na mtu muongo.

Katika hotuba yake ya kuaga Nyerere aliwasifu wazee wa Kiislamu waliomuunga mkono wakati wa kudai uhuru bila ya kumbagua kwa dini yake, katika hotuba hii alisema kuwa TAA ilikuwa haina nguvu yeye alipochukua uongozi. Nyerere hakutoa hadhi iliyostahili kwa TAA wala kwa Abdulwahid. Alipojaribu kumueleza Abdulwahid alisema kuwa yeye hakumbuki Abdulwahid alikuwa na cheo gani katika TAA wakati yeye anajiunga. Gazeti la serikali Daily News siku ya pili yake, ilisahihisha hotuba ya Nyerere na kusema kuwa Nyerere alipojiunga na na TAA Abdulwahid Sykes alikuwa katibu. Ukweli hasa ni kuwa Abdulwahid alikuwa rais wa TAA. Mkanda wa kunasa sauti wa hotuba hii unapatikana maktaba ya Radio Tanzania, Dar es Salaam.
 
hiyo DAR es salaam ya M Said
27301_320735818037167_482266515_n.jpg
 
Jokakuu, kipande hicho tu kinajibu kila tuhuma dhidi ya Nyerere. Kawataja akina Sykes hata kusema wao ndio walibuni jina la TANU kabla. Kawataja akina Tambaza na Ramia ambao Mohamed anadai Nyerere aliwatupa.
Sijui atakuja na utetezi gani. Kila jambo amelieleza vizuri tena bila kuuma uma maneno.

Hotuba hiyo imebandikwa humu?
 
wengine tulizaliwa tulianza kujua au kuwa na ufahamu wakati wa awamu ya pili ila hii thread imetufundisha mengi ambayo tulikua hatuyajui.

mengi sana,tena yale yaliyokafichikana na kufichwa kwa makusudi.
Na bado tunaendelea kuyapata mengine,kwa ufupi haki na batili zinajipambanua zenyewe.
Lait julius angekuwa ni mtu mwenye kuthamini kweli mchango wa wenzake basi angeuthamin japo kwa vitendo,katika hizo tuzo alizokazitoa ikulu kama ishara ya kutambua mchango wa wale waliojitoa kisawa sawa ambao anakiri na kuwataja baadhi kwenye hotuba yake,kwanin hakuwapa kipaomble katika tuzo hizo??
 
Mohamed,
Ukinukuu uwongo kuthibitisha hoja zako na wewe unakuwa muwongo. Nimekwambia, na narudia tena, baba wa taifa amefariki bila kuwacha tovuti yake. Hiyo tovuti unayoisema na kuinukuu hakuianzisha Nyerere. In fact nitakaporudi Dar-es-Salaam nina mpango wa kuonana na wakuu wa Nyerere Foundation niwashauri waanzishe tovuti authentic ya Nyerere siyo hii bandia unayotuzungumzia hapa. Kwa hiyo ukiendelea kuinukuu tovuti hiyo ambayo unajua, na mimi najua, hyaijaanzishwa na Nyerere na haina baraka ya Nyerere Foundation au familia ya Nyerere unazidi kuendeleza uwongo.

Niwie radhi ndugu yangu sitainukuu tena hiyo tovuti.
 
Mohamed Said,

Allah akupe maisha marefu watu wanakusoma na kujifunza historia kupitia mabandiko yako, watu zaidi ya 20,000 wanafuatilia huu munakasha jikite kuwasomesha hii historia.
 
Last edited by a moderator:
Unaona hapa anavyosutwa Mohamed? Ametuambia katika hotuba hii Nyerere alisema hajui au hakujua Abdul alikuwa na cheo gani. And sometimes it makes me wonder, why didn't Mohamed attempt to get a word from Nyerere when he started writing his book? Was it bias, was it hatred? Angetuwekea quote kama hii kitabu chake kingekuwa more authentic and balanced. But no.
What a shame!

Ndugu zanguni hebu tutulie kwanza.

Tusisikize hotuba sote tusikie kile kipande alichosema
hakumbuki cheo cha Abdu kipo?

Kama kataja cheo chake hayo yatakuwa maajabu makubwa.
Kama kipande kimenyofolewa....

Kuwa na subra tusikize hatoba kwanza.

Ogopa kusema sana kwenye jambo usokuwa na ithibati nalo.
Mie humu sifanyi maskhara.

Nimetafiti na kuandika kitabu tena sasa kina miaka 15.
Ni kitabu rejea katika African Studies duniani.

Hasomi mtu political history ya Tanzania sharti atakipitia kitabu changu.
Iwe niseme Nyerere kasahau cheo cha Abdu kisha iwekwe tape anasikika
Nyerere anasema, ''Abdu alikuwa rais wa TAA.''

Kila nilichosema katika kitabu kitabomoka.
Usomi hauna stamala na mtu muongo.

Katika hotuba yake ya kuaga Nyerere aliwasifu wazee wa Kiislamu waliomuunga mkono wakati wa kudai uhuru bila ya kumbagua kwa dini yake, katika hotuba hii alisema kuwa TAA ilikuwa haina nguvu yeye alipochukua uongozi. Nyerere hakutoa hadhi iliyostahili kwa TAA wala kwa Abdulwahid. Alipojaribu kumueleza Abdulwahid alisema kuwa yeye hakumbuki Abdulwahid alikuwa na cheo gani katika TAA wakati yeye anajiunga. Gazeti la serikali Daily News siku ya pili yake, ilisahihisha hotuba ya Nyerere na kusema kuwa Nyerere alipojiunga na na TAA Abdulwahid Sykes alikuwa katibu. Ukweli hasa ni kuwa Abdulwahid alikuwa rais wa TAA. Mkanda wa kunasa sauti wa hotuba hii unapatikana maktaba ya Radio Tanzania, Dar es Salaam.
 
Back
Top Bottom