Asante sana
JokaKuu, nilikuwa nimeweka kalamu chini, lakini hii hotuba ya Baba wa Taifa ambayo sisi wengine kwa bahati tuliisikiliza "live", ngano za huyu mpuuzi na mchochezi,
Mohamed Said, zilituacha mdomo wazi! Nianze kwanza kwa kutamka wazi wazi, "sitaomba radhi kwa kumuita mpuuzi na mchochezi" na kama JF itanifungia na iwe hivyo. Sijaanza kumuita hivyo leo, nilianza toka nianze kusoma makala yake ambayo ameyatumia kujipatia pesa kwa kueneza uwongo na chuki na kama kawaida hakukosa washabiki, watu wenye fikra finyu ambao kwa bahati mbaya sana idadi yao si ndogo. Ni kweli kama alivyowahi kusema Abraham Lincoln wa Marekani,
"You can fool all the people some of the time, and some of the people all the time, but you cannot fool all the people all the time"
Kama ni kweli kuna mhadhiri/wahadhiri wa UDSM walikataa kitabu cha huyu mchochezi kutumiwa kama reference ya historia ya Tanganyika, waliona mbali kwani walimwona mchochezi kwa rangi yake kamili.
Mohamed Said hana tofauti yoyote na Sheikh Ponda, hana tofauti yoyote na Sheikh Ilunga na kama iko tofauti ni kwamba yeye amejipatia ulaji kupitia makala yake ya uwongo na ya kichochezi. Kabla sijaendelea namwomba
Mohamed Said aseme hapa JF kama anakiri au anapinga hii hotuba iliyoletwa na
JokaKuu kama ni kweli ilitolewa na Baba wa Taifa. Nina hakika ndugu zangu Waislaam wenye mapenzi ya kweli na taifa hili, hawaungi mkono hizi nja:smile:ma za chuki zinazopandikizwa na watu hatari kama huyu, [MENTION=12431]Mohamed Said[/MENTIO
Naomba kabla ya mtu yeyote kutoa mchango wake hapa asome kwa makini hii hotuba ya Baba wa Taifa halafu alinganishe na madai ya
Mohamed Said...tuendelee!