Nanren
JF-Expert Member
- May 11, 2009
- 3,135
- 3,392
Labda nikuulize kwa nini unataka maswali hayo yote nijbu mimi peke yangu ilhal humu ukumbini
ni jamajamala?
Huu ukumbi hauna ubaguzi kila mtu yuko huru kuchangia na ndiyo maana unaona mijadala inastawi.
Huu mjadala ukishakuwa baina ya watu wawili, mie na wewe utapoteza maana.
Mkuu Mohamed Said, ningependa unijibu wewe kwa vile, tofauti zetu kwenye mijadala ya nyuma, ilikuwa ni kati ya wewe na waliokuwa "wanakuelewa" kwa upande mmoja na sisi ambao tulikuwa "hatukuelewi" kwa upande mwingine. Masimulizi yako ndio yalikuwa yakitenganisha hizi pande mbili.
Lakini pia, ni kwamba, ninapendelea uungwana wako katika kujibu, ukilinganisha na wengine wa upande huo.
Hivyo, basi, naomba urejee tena post yangu ya awali, ambapo nimekuuliza kama bado unaamini ile misingi ya "kutofautiana kwetu". Post yenyewe ni hii hapa chini
Swali kwa @[Mohamed said]
Siku za nyuma, kwenye threads zako tulitofautiana katika mambo kadhaa, wewe ukiwa unasaidiwa na barubaru, mdondoaji, faizafoxy na topical just to mention a few. Katika mambo ambayo tulitofautiana ni pamoja na misingi ya "historia" yako kwamba:
1. Vita ya maji maji ilikuwa ni baina ya Waislam na Wakristo.
2. Hapa nchini kuna waislam na wakristo tu, hamna wapagani.
3. Majina yanaashiria dini fulani, kwa mfano Ally Songea lazima alikuwa muislam, na John Smith lazima alikuwa mkristo.
4. Kwamba kwa ujumla, waislam Tanzania ni wengi kuliko wakristo, ila kwasabau ya kukandamizwa/uonevu kwa waislam, ndio maana waislam wanakuwa wachache katika elimu ya juu, makazini na serikalini
5. Kwamba kanisa katoliki (Tanzania) lilikuwa na bado lina uadui na uislam na lina mpango mkakati wa kudhoofisha uislam afrika mashariki.
6. Mkatoliki Nyerere alikuwa anatimiza maagizo ya kanisa kuutokomeza uislam na ndio maana hata wizara ya elimu iliwahi kuongozwa na padre, na kwamba hata kupendekezwa kwake na kanisa kwenye sainthood kunatokana na kazi aliyofanya ya kudhibiti uislam.
Je bado unaamini kama nilivyoeleza hapo juu? Kama bado unaamini nitaomba ufafanuzi japo kidogo, sababu ya kuamini kwako.
Naomba swali hili lijibiwe na Mohamed Said na si mwingine wa "upande" huo.