Mzee Said, swali hilo hapo vipi?
Huwa sijibu swali kama anavyotaka muulizaji.
Najibu swali kwa ufahamu wangu.
Hilo swali nimelijibu.
Nimesema wanafunzi wa Masters wakija kwangu kwa msaada huwa
sioni kitabu changu kwenye literature review yao.
Nikiwauliza kulikoni?
Wanasema kitabu chako kinatisha walimu wetu.
Hawataki hata kitiwe katika bibliography.
Kama hukuridhika na jibu hili langu basi sina la kufanya.
Lakini hebu na wewe jishughulishe kidogo.
Pitia ''dissertations'' za miaka 10 nyuma zilizofanya utafiti unaohusu historia
ya Tanganyika uangalie kama kitabu changu kipo katika bibliography.
Fika hapa Idara ya Historia uangalie na Insha Allah utujuvye.
Majina ya walimu Idara ya Historia si siri.
Lakini tujaalie nimesema fulani na fulani.
Ndiyo iwe nini.
Na wao wakasema nimewasingizia.
Ndiyo itakuwa nini.
Hakuna tija.
Sana sana nitakuwa nimewafedhehesha na watu ''source'' zote zitaniogopa.
Sijui kuweka siri.