Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Hiyo ndiyo ilikuwa propaganda na uongo uliotengenezwa na akina Rashid Kayugwa
aliyekuwa akiongoza operesheni ile.

Huyu alikuwa mtu wa Usalama wa Taifa.

Iko siku akaisikia Qur' an inasomwa Allah anatoa ahadi zake kwa wale watakaosimama
kuipigania dini yake.

Nini yatakuwa malipo yao.

Na wale watakaompiga vita Allah nini utakuwa mwisho wao.

Kainamisha kichwa chini machozi yanambubujika.

Kakumbuka alowatendea askari wa Allah Sheikh Hassan bin Amir na Waislam walokuwa
pamoja na yeye.

Akajitazama hali yake.

Mfumo umemtumia kuhujumu Uislam kisha ukamtupa.

Kayugwa kabla hajafa akawaeleza Waislam fitna yote ile na wahusika wake.
Kisha akaomba Allah amuwie radhi kwa yale alotenda.

Ndugu yangu tunajua mengi sana.

sadkta sheikh mohammed. waambie hao wanaojifanya waislam huku wakitamani uislam ufe lkn ccm ingare kwa kuwafunga masheikh wetu
 
Ndugu yangu Mohamed Said, bado nakusubiri kujua nyaraka za Nyerere za enzi ya TAA na TANU,
anazo nani hii leo?

Nimekuonjesha hiyo ili wewe na wasikizaji wajue kuwa mimi simo humu
kusema uongo.

Nimesoma mengi, nimehadithiwa mengi,
Ya kufurahisha na ya kusikitisha na kuliza.

Historia hii ya wazee wangu nimeipokea na baraka zao.

Kila nyumba niliyobisha hodi nilifunguliwa mlango na wakati wa kuagana
nilisomewa dua.

Wazee hawa wameingia kaburini na kinyongo.
Waliyotegemea siyo yalivyokujakuwa.

Nyumba moja tu nilikataliwa nako ni Tanga kwa Shababi Silabu huyu alianza siasa
Tabora pamoja na Bilal Rehani Waikela.

Yeye aliniuliza kama nina kibali cha serikali kufanya utafiti.
Nikamjibu sihitaji kibali.

Akanikatalia kuzungumza na mimi.
Tukaagana.

Nilipokuja kutafiti habari zake nikaambiwa ni katika wazee wa CCM.

Shabani Silabu hivi sasa ni marehemu.
 
Ndugu yangu Bubu Msemaovyo,
Mzee wetu Mohamed anataka tuanze upya. Tuweke mfumo ambao angalao utamhakikishia yafuatayo:
-Tugawane madaraka, kazi na vyeo kwa uwiano wa KIDINI kwanza; sifa nyingine zitafuata baadae.

-Tuandike upya HISTORIA ya NCHI yetu ambayo haitamsahau mzee wake hata mmoja; hata aliyepika chai Mwalimu akanywa.

-DINI za wapigania uhuru hawa zizingatiwe sana.

-Mapungufu yote ya Mwalimu yasemwe wazi na kwa herufi kubwa. Mapungufu ya wazee wake hayapo na kama yapo anayajua yeye tu.

-Vitabu vyake vyote, machapisho yake yote, mihadhara yake yote, irejewe kila mahala. Mashuleni, vyuoni, makanisani,...

Mwisho kabisa kanisa,serikali na CCM viwaombe radhi WAISLAM wa Tanganyika na baadae Tanzania
 
Last edited by a moderator:
Kisa cha kuvunjika EAMWS ni kirefu sana kwa hapa sitokitendea haki
Lakini kwenye kitabu changu nimekieleza chote pamoja na wahusika
wakuu nimewataja kwa majina yao.

Kuwa kwa nini huko kwengine nako chama kikafa sababu sijui.
Ila sababu ya hapa kupigwa marufuku ni kuwa EAMWS ilikuwa
inataka kujenga chuo kikuu.

Hii ikatia hofu Kanisa Katoliki na Nyerere ikabidi afanye kila juhudi
EAMWS ipigwe marufuku.

Source ya hiyo info. ya sensa ni Islam and Politics cha August Nimitz
unaweza kupata thesis yake Maktaba ya Chuo Kikuu.

Nitajaribu Insha Allah kuangalia kitabu nikupe na ukurasa ninacho katika
''archives'' yangu.

Asante kwa source ya info ya sensa. Nitaitafuta hiyo thesis. japo kwa sasa ninaamini kuwa mwandishi (wa thesis) alitoa wrong estimate probably based on urban population count. I was hoping that the source was some government agency's docs.

Tukirudi kwenye suala la EAMWS kuvunjwa na Nyerere kwa Tanzania, lakini kufa kwa sababu zingine huko Kenya na uganda...
Je haiwezekani kuwa hii EAMWS ingeweza kujifia tu hapa Tanzania hata bila Nyerere kuivunja?
Kwa uelewa wangu islamists walijiunga/walijiweka chini ya EAMWS baada ya AMNUT yao kupigwa chini na waislam wenyewe ndani ya TANU. Na inawezekana kuingia kwa hao islamists kwenye EAMWS ndio kulikosababisha jumuiya hiyo kuvunjwa, ukitilia maanani misimamo ya kidini waliyokuwa (ex-AMNUT members) nayo.

Kabla ya hapo, tangia kuanzishwa kwa EAMWS mwaka 1945 uhusiano kati ya waislam wa ismailia (wamiliki wa EAMWS) haukuwa wa karibu kivile na waislam wengine kama wasunni. Na hata sasa, miaka zaidi ya 60 imepita, sidhani kama makundi haya yapo karibu kihivyo. Honestly, Mzee MS, hivi hata Nyerere asingevunja tawi la Tanzania, unafikiri bado EAMWS ingeendelea kuwepo?
 
Mohamed,
Si kweli kwamba EAMWS ilipigwa marufuku Tanzania kwa sababu ilitaka kujenga chuo. Hili umelirudia mara kadhaa kwa dhana kwamba uongo ukirudiwa mara kwa mara watu wataanza kuamini kuwa ni kweli. EAMWS ilipigwa marufuku baada ya kuingilia mambo ya siasa. EAMWS ilitumika kuchanga fedha ili Nyerere aondolewe uongozi wa TANU. Hilo katu hautalisema. Zilichangwa fedha kwa ushawishi wa Tewa Said Tewa. Na pia hujataja mchango wa Adam Nasib. Unamfahamu huyu Muislamu mzalendo? Hujatuambia juu ya Iringa National Islamic Conference ya 1968. Hujataja kauli ya Sheikh Abeid Karume, makamu wa kwanza wa rais wa Tanzania, kwamba EAMWS ilikuwa inafuata siasa zinazopingana na TANU na AFP. na kuonya juu ya "religious pretenders from outside," na kuwataka uongozi wa Waislamu ukabidhiwe mikononi mwa watu wenyewe. Hebu tuambie ni waziri gani aliyetangaza Desemba 20 1968 kupigwa marufuku kwa EAMWS nchini Tanzania. Hakuwa Muislamu huyu?

Jasusi,

I knew right from the outset it is going to be my word against theirs.
(Samahani natumia Kiingereza kurahisisha) na mimi nikajizatiti vilivyo.

Nimejizatitii vipi?

Nimetafiti na kuandika kiasi nimwachie mtu yoyote atumie ''premise'' ya
''the standard of the reasonable man'' kunihukumu.

Angalia hapa chini:

[1]Rashid Kayugwa Afisa wa Usalama Taifa, Dar es Salaam ndiye aliyepewa
kazi ya kudumisha mawasiliano kati ya kundi la Adam Nasibu serekali.

Kayugwa ndiye aliyekuwa akielekeza kundi la Adam Nasibu mbinu za propaganda
na nini kifanyike na kwa wakati gani ili kuvunja umoja wa Waislam.

Kayugwa alikuwa amepata mafunzo yake ya ukachero Israel, Checkoslovakia na
Marekani.

Katika kuhakikisha mafanikio ya mkutqano wa Iringa, Kayugwa ambae ni mzaliwa
wa Iringa alipendekeza mkutano wa Waislam wa Taifa ufanyike Iringa kwa kuhofu
vurugu na upinzani kutoka kwa Waislam wa Dar es Salaam.

Baada ya kusoma kitabu cha Padri John Sivalon kilichoeleza kuwa Kanisa baada ya
uhuru liliendesha hujuma dhidi ya Uislam na Waislam kwa kupitia serikali, ndipo
ilipomdhihirikia ukweli na kuona kuwa alipokuwa akitumiwa kuhujumu EAMWS hakuwa
akitumikia serikali kama alivyokuwa anadhani bali alikuwa akilitumikia Kanisa, kama
kuomba maghufira kwa Mwenyezi Mungu, aliamua kueleza mchango wake katika
kuwahujumu Waislam na Uislam ili iwe fundisho na onyo kwa Waislam watakao
kuwa katika utumishi wa vyombo kama hivyo siku za usoni.

Kabla ya kufa kwake alieleza masikitiko yake kwa kukandamizwa kwa Waislam na
akatoa mfano wake mwenyewe wa kutopandishwa cheo katika Usalama wa Taifa
kwa sababu tu yeye alikuwa Muislam.
 
Asante kwa source ya info ya sensa. Nitaitafuta hiyo thesis. japo kwa sasa ninaamini kuwa mwandishi (wa thesis) alitoa wrong estimate probably based on urban population count. I was hoping that the source was some government agency's docs.

Tukirudi kwenye suala la EAMWS kuvunjwa na Nyerere kwa Tanzania, lakini kufa kwa sababu zingine huko Kenya na uganda...
Je haiwezekani kuwa hii EAMWS ingeweza kujifia tu hapa Tanzania hata bila Nyerere kuivunja?
Kwa uelewa wangu islamists walijiunga/walijiweka chini ya EAMWS baada ya AMNUT yao kupigwa chini na waislam wenyewe ndani ya TANU. Na inawezekana kuingia kwa hao islamists kwenye EAMWS ndio kulikosababisha jumuiya hiyo kuvunjwa, ukitilia maanani misimamo ya kidini waliyokuwa (ex-AMNUT members) nayo.

Kabla ya hapo, tangia kuanzishwa kwa EAMWS mwaka 1945 uhusiano kati ya waislam wa ismailia (wamiliki wa EAMWS) haukuwa wa karibu kivile na waislam wengine kama wasunni. Na hata sasa, miaka zaidi ya 60 imepita, sidhani kama makundi haya yapo karibu kihivyo. Honestly, Mzee MS, hivi hata Nyerere asingevunja tawi la Tanzania, unafikiri bado EAMWS ingeendelea kuwepo?

Wewe unaichukulia ''premise'' hiyo kwa kuwa huna taarifa za kitu gani
kilipitika kati ya Sheikh Hassan bin Amir na Nyerere washirika wakubwa
wakati wa mapambano, maadui wakubwa toka siku uhuru ulipopatikana.

Hujui hotuba ya mwaka wa 1963 ''Moto wa Waislam Ukiwaka" alosomewa
Nyerere katika mkutano wa EAMWS mbele ya Sheikh Hassan bin Amir.

Hujui hongo zilizotembea.

Mimi wakati mwingine hucheka nikasema hawa jamaa wanadhani haya mambo
yalikuwa hivi hivi tu?

Trump card ya Waislam kilikuwa kile chuo na Kanisa walilijua hilo.
Ndugu yangu tunajua mengi.

Mimi hawa walikuwa wazee wangu.
 
Jasusi,

I knew right from the outset it is going to be my word against theirs.
(Samahani natumia Kiingereza kurahisisha) na mimi nikajizatiti vilivyo.

Nimejizatitii vipi?

Nimetafiti na kuandika kiasi nimwachie mtu yoyote atumie ''premise'' ya
''the standard of the reasonable man'' kunihukumu.

Angalia hapa chini:

[1]Rashid Kayugwa Afisa wa Usalama Taifa, Dar es Salaam ndiye aliyepewa
kazi ya kudumisha mawasiliano kati ya kundi la Adam Nasibu serekali.

Kayugwa ndiye aliyekuwa akielekeza kundi la Adam Nasibu mbinu za propaganda
na nini kifanyike na kwa wakati gani ili kuvunja umoja wa Waislam.

Kayugwa alikuwa amepata mafunzo yake ya ukachero Israel, Checkoslovakia na
Marekani.

Katika kuhakikisha mafanikio ya mkutqano wa Iringa, Kayugwa ambae ni mzaliwa
wa Iringa alipendekeza mkutano wa Waislam wa Taifa ufanyike Iringa kwa kuhofu
vurugu na upinzani kutoka kwa Waislam wa Dar es Salaam.

Baada ya kusoma kitabu cha Padri John Sivalon kilichoeleza kuwa Kanisa baada ya
uhuru liliendesha hujuma dhidi ya Uislam na Waislam kwa kupitia serikali, ndipo
ilipomdhihirikia ukweli na kuona kuwa alipokuwa akitumiwa kuhujumu EAMWS hakuwa
akitumikia serikali kama alivyokuwa anadhani bali alikuwa akilitumikia Kanisa, kama
kuomba maghufira kwa Mwenyezi Mungu, aliamua kueleza mchango wake katika
kuwahujumu Waislam na Uislam ili iwe fundisho na onyo kwa Waislam watakao
kuwa katika utumishi wa vyombo kama hivyo siku za usoni.

Kabla ya kufa kwake alieleza masikitiko yake kwa kukandamizwa kwa Waislam na
akatoa mfano wake mwenyewe wa kutopandishwa cheo katika Usalama wa Taifa
kwa sababu tu yeye alikuwa Muislam.
Kama ni hivi, Mwalimu anastahili pongezi sana tu. Aliyazima majaribio yote ya UDINI kwa umahiri mkubwa sana. UDINI unarudi tena. Mtu kama Mwalimu hatunae tena. Tutafanyaje.
 
Wewe unaichukulia ''premise'' hiyo kwa kuwa huna taarifa za kitu gani
kilipitika kati ya Sheikh Hassan bin Amir na Nyerere washirika wakubwa
wakati wa mapambano, maadui wakubwa toka siku uhuru ulipopatikana.

Hujui hotuba ya mwaka wa 1963 ''Moto wa Waislam Ukiwaka" alosomewa
Nyerere katika mkutano wa EAMWS mbele ya Sheikh Hassan bin Amir.

Hujui hongo zilizotembea.

Mimi wakati mwingine hucheka nikasema hawa jamaa wanadhani haya mambo
yalikuwa hivi hivi tu?

Trump card ya Waislam kilikuwa kile chuo na Kanisa walilijua hilo.
Ndugu yangu tunajua mengi.

Mimi hawa walikuwa wazee wangu.

But, with all due respect, Sir, It sounds funny.
Kwamba EAMWS Tanzania ilikufa kwa kuvunjwa na Nyerere eti tu kwa sababu ilitaka kuanzisha chuo cha kiislam (Na bila shaka chuo chenyewe kingekuwa kinafundisha dini ya ismailiya) lakini EAMWS kwenye maeneo mengine ya East Africa, ikajifia tu kwa sababu zingine... Doesn't it sound strange to you, or it is just me?
 
But, with all due respect, Sir, It sounds funny.
Kwamba EAMWS Tanzania ilikufa kwa kuvunjwa na Nyerere eti tu kwa sababu ilitaka kuanzisha chuo cha kiislam (Na bila shaka chuo chenyewe kingekuwa kinafundisha dini ya ismailiya) lakini EAMWS kwenye maeneo mengine ya East Africa, ikajifia tu kwa sababu zingine... Doesn't it sound strange to you, or it is just me?
Moja kati ya mambo mazuri kabisa ya Mzee Mohamed ni msimamo wake usioyumba kwa lile analoamini ndivyo lilivyo. Hautombadili sio tu kwa hilo la EAMWS bali na mengine yote anayoyasimamia humu hata ataujua ukweli. Mimi namwelewa kwa kuwa haya ameyaandika na kuyahubiri sana. Anabadilikaje na hadhi yake iko juu namna hii kwa uongo huu?
 
Moja kati ya mambo mazuri kabisa ya Mzee Mohamed ni msimamo wake usioyumba kwa lile analoamini ndivyo lilivyo. Hautombadili sio tu kwa hilo la EAMWS bali na mengine yote anayoyasimamia humu hata ataujua ukweli. Mimi namwelewa kwa kuwa haya ameyaandika na kuyahubiri sana. Anabadilikaje na hadhi yake iko juu namna hii kwa uongo huu?

Nafikiri huu msimamo wake umemsaidia sana kukubalika katika jamii ya watu wa pwani kama mswahili mwenzao. Bila hivyo labda wangeendelea kumwona 'mlugaluga' mwenye asili ya bara. Si unajua huwa kuna dharau fulani hivi ya watu wa pwani kwa watu wa bara? Lakini aah, mzee wa watu anawapigisha stories zenye hisia, akichanganyia na lafudhi ya kiarabu, Anawasimulia jinsi alivyofika uskochi, marekani, ujerumani...,kwanini wasimkubali bwana. Si unaona yule mmanyema mwingine aliyesweka ndani, naye aliamua aonekane ana msimamo mkali na kwamba anajua dini sana, ili akubalike?
 
Moja kati ya mambo mazuri kabisa ya Mzee Mohamed ni msimamo wake usioyumba kwa lile analoamini ndivyo lilivyo. Hautombadili sio tu kwa hilo la EAMWS bali na mengine yote anayoyasimamia humu hata ataujua ukweli. Mimi namwelewa kwa kuwa haya ameyaandika na kuyahubiri sana. Anabadilikaje na hadhi yake iko juu namna hii kwa uongo huu?

Hilo ni moja ya tatiz kuu alilonalo mzee Mohamed Said,

Haamini katika kweli halisi ya kadamnasi bali kile alicholishwa na awaitao wazee wake!

Kichekesho ni kuwa kila mzee wakiislamu anaemtaja hapa anadai ni babu, baba, bibi, nk,

Sasa sijui yupi ni ndugu yake wa damu na ni yupi ndugu tu?
 
Nafikiri huu msimamo wake umemsaidia sana kukubalika katika jamii ya watu wa pwani kama mswahili mwenzao. Bila hivyo labda wangeendelea kumwona 'mlugaluga' mwenye asili ya bara. Si unajua huwa kuna dharau fulani hivi ya watu wa pwani kwa watu wa bara? Lakini aah, mzee wa watu anawapigisha stories zenye hisia, akichanganyia na lafudhi ya kiarabu, Anawasimulia jinsi alivyofika uskochi, marekani, ujerumani...,kwanini wasimkubali bwana. Si unaona yule mmanyema mwingine aliyesweka ndani, naye aliamua aonekane ana msimamo mkali na kwamba anajua dini sana, ili akubalike?

Two words, Utter Rubbish!
 
Mohamed anaanza kufunguka.
Kadri anavyoongea ndivyo anavyozidi kushindwa kutetea hoja zake na kujichanganya.

Kwanza amemtuhumu Mzee Silabu kuwa alikuwa mzee wa CCM ndio maana hakutoa ushirikiano katika utafiti wake.

Kwa maneno mengine wazee wa CCM siyo miongoni mwake. Lau kana ingekuwa hivyo basi Dar es Salaam isingekuwa ilivyo.Wanaoiweka CCM Dar ni nani kama si wazee wake?

Pili, MS amesema mwaka 1963 Nyerere ''alisomewa maneno makali'' mbele ya Mufti Amir. Kwa mara ya kwanza katika mnakasha huu MS ameonyesha kuwa Nyerere hakuwa mwendawazimu kuamka asubuhi na kumtimua.

Asichowaambia wana ukumbi ni kuwa waziri wa mambo ya ndani alikuwa Ali Maswanya, makamu wa Rais Kawawa n.k. na wakati huo wazee wengine kama akina Fundikira, Tewa Said walikuwepo! Hakuna hata mmoja aliyejiuzulu kupinga hatua ya Nyerere.

Kumbe basi Mufti alikuwa na harakati zingine.
Nyerere alimtimua kama Mwinyi alivyomfanya Sheikh Kassim Juma ,
Kikwete alivyomweka ndani Ponda au Dr Shein alivyomweka ndani Farid.
Vipi Nyerere aonekana mhalifu wakati play book anaitumia kila mmoja wetu?

Tatu, Mohamed anasema chuo kikuu cha EAMWS iliuawa na Kanisa kwa kushirikiana na Nyerere. Tumemwambia atupe uthibitisho wa ushiriki wa kanisa hajaweza kutoa zaidi ya hisia zake binafsi anazotaka kuzisokomeza kwenye akili za watu wenye akili.

Tumemuuliza kama Chuo kikuu kilikuwa ukombozi, basi atuambie nchi mmoja tu ya kiafrika iliyowahi kujenga chuo cha kiislam kati ya 60-70 ambayo inaweza kuwa mfano, Mohamed hakuwa na jibu.

Tumemuuliza chuo kikuu angesoma nani ikiwa sasa hivi kuna shule zinafungwa kule Kilwa n.k. kwasababu wanafunzi hawaendei shule, seuse mwaka 1968.

Mohamed hana jibu amebaki kuaminisha kuwa wasomi wangepatika kwa kutengenezwa maabara.

Wanajamvi kisomo cha Ngumbaru kilianzishwa mwaka 1970 ili kupunguza illiterate level. Mohamed anataka umma uamini kuwa waislam hawakuwa sehemu ya tatizo la illiteracy kiasi kwamba walikuwa na uwezo wa kujenga chuo na kuwa na wanafunzi.
Hisia ni kama maradhi, sijui tiba yake ni nini, ninachojua ni maradhi.
 
Hilo ni moja ya tatiz kuu alilonalo mzee Mohamed Said,

Haamini katika kweli halisi ya kadamnasi bali kile alicholishwa na awaitao wazee wake!

Kichekesho ni kuwa kila mzee wakiislamu anaemtaja hapa anadai ni babu, baba, bibi, nk,

Sasa sijui yupi ni ndugu yake wa damu na ni yupi ndugu tu?

Wewe elimu haijakugomboa. Mzee Mohamed Said kafanya research, published his book, his book being reviewed in the best universities in the world, bado yote hukubali.

Embu tujaalie wewe umefanya research, umeandika kitabu, kikawa published, kikawa-reviewed to the best universities in the world, alafu anakuja mtu anasema "research yako ni ngano, uongo mtupu". Unadhani atakua amekutendea haki huyo mtu?


nina doubt sana uwezo wako
 
Jasusi,

I knew right from the outset it is going to be my word against theirs.
(Samahani natumia Kiingereza kurahisisha) na mimi nikajizatiti vilivyo.

Nimejizatitii vipi?

Nimetafiti na kuandika kiasi nimwachie mtu yoyote atumie ''premise'' ya
''the standard of the reasonable man'' kunihukumu.

Angalia hapa chini:

[1]Rashid Kayugwa Afisa wa Usalama Taifa, Dar es Salaam ndiye aliyepewa
kazi ya kudumisha mawasiliano kati ya kundi la Adam Nasibu serekali.

Kayugwa ndiye aliyekuwa akielekeza kundi la Adam Nasibu mbinu za propaganda
na nini kifanyike na kwa wakati gani ili kuvunja umoja wa Waislam.

Kayugwa alikuwa amepata mafunzo yake ya ukachero Israel, Checkoslovakia na
Marekani.

Katika kuhakikisha mafanikio ya mkutqano wa Iringa, Kayugwa ambae ni mzaliwa
wa Iringa alipendekeza mkutano wa Waislam wa Taifa ufanyike Iringa kwa kuhofu
vurugu na upinzani kutoka kwa Waislam wa Dar es Salaam.

Baada ya kusoma kitabu cha Padri John Sivalon kilichoeleza kuwa Kanisa baada ya
uhuru liliendesha hujuma dhidi ya Uislam na Waislam kwa kupitia serikali, ndipo
ilipomdhihirikia ukweli na kuona kuwa alipokuwa akitumiwa kuhujumu EAMWS hakuwa
akitumikia serikali kama alivyokuwa anadhani bali alikuwa akilitumikia Kanisa, kama
kuomba maghufira kwa Mwenyezi Mungu, aliamua kueleza mchango wake katika
kuwahujumu Waislam na Uislam ili iwe fundisho na onyo kwa Waislam watakao
kuwa katika utumishi wa vyombo kama hivyo siku za usoni.

Kabla ya kufa kwake alieleza masikitiko yake kwa kukandamizwa kwa Waislam na
akatoa mfano wake mwenyewe wa kutopandishwa cheo katika Usalama wa Taifa
kwa sababu tu yeye alikuwa Muislam.

Na Karume je? Unamweka kundi gani? Naye alitumiwa kuhujumu Waislamu?
 
Nafikiri huu msimamo wake umemsaidia sana kukubalika katika jamii ya watu wa pwani kama mswahili mwenzao. Bila hivyo labda wangeendelea kumwona 'mlugaluga' mwenye asili ya bara. Si unajua huwa kuna dharau fulani hivi ya watu wa pwani kwa watu wa bara? Lakini aah, mzee wa watu anawapigisha stories zenye hisia, akichanganyia na lafudhi ya kiarabu, Anawasimulia jinsi alivyofika uskochi, marekani, ujerumani...,kwanini wasimkubali bwana. Si unaona yule mmanyema mwingine aliyesweka ndani, naye aliamua aonekane ana msimamo mkali na kwamba anajua dini sana, ili akubalike?

Siyo kukubalika tu. Sheikh Mohamed is on a crusade. He is galvanizing the Moslems in Tanzania so they realize that Christianity is an enemy. Christianity has taken over the government and is the reason the Muslims are lagging behind.
Hujamsikia anasema wameshapeleka malalamiko yao serikalini? Wanasikilizwa? What is to come out of this? An insurrection?
 
Mohamed anaanza kufunguka.
Kadri anavyoongea ndivyo anavyozidi kushindwa kutetea hoja zake na kujichanganya.

Kwanza amemtuhumu Mzee Silabu kuwa alikuwa mzee wa CCM ndio maana hakutoa ushirikiano katika utafiti wake.

Kwa maneno mengine wazee wa CCM siyo miongoni mwake. Lau kana ingekuwa hivyo basi Dar es Salaam isingekuwa ilivyo.Wanaoiweka CCM Dar ni nani kama si wazee wake?

Pili, MS amesema mwaka 1963 Nyerere ‘’alisomewa maneno makali’’ mbele ya Mufti Amir. Kwa mara ya kwanza katika mnakasha huu MS ameonyesha kuwa Nyerere hakuwa mwendawazimu kuamka asubuhi na kumtimua.

Asichowaambia wana ukumbi ni kuwa waziri wa mambo ya ndani alikuwa Ali Maswanya, makamu wa Rais Kawawa n.k. na wakati huo wazee wengine kama akina Fundikira, Tewa Said walikuwepo! Hakuna hata mmoja aliyejiuzulu kupinga hatua ya Nyerere.

Kumbe basi Mufti alikuwa na harakati zingine.
Nyerere alimtimua kama Mwinyi alivyomfanya Sheikh Kassim Juma ,
Kikwete alivyomweka ndani Ponda au Dr Shein alivyomweka ndani Farid.
Vipi Nyerere aonekana mhalifu wakati play book anaitumia kila mmoja wetu?

Tatu, Mohamed anasema chuo kikuu cha EAMWS iliuawa na Kanisa kwa kushirikiana na Nyerere. Tumemwambia atupe uthibitisho wa ushiriki wa kanisa hajaweza kutoa zaidi ya hisia zake binafsi anazotaka kuzisokomeza kwenye akili za watu wenye akili.

Tumemuuliza kama Chuo kikuu kilikuwa ukombozi, basi atuambie nchi mmoja tu ya kiafrika iliyowahi kujenga chuo cha kiislam kati ya 60-70 ambayo inaweza kuwa mfano, Mohamed hakuwa na jibu.

Tumemuuliza chuo kikuu angesoma nani ikiwa sasa hivi kuna shule zinafungwa kule Kilwa n.k. kwasababu wanafunzi hawaendei shule, seuse mwaka 1968.

Mohamed hana jibu amebaki kuaminisha kuwa wasomi wangepatika kwa kutengenezwa maabara.

Wanajamvi kisomo cha Ngumbaru kilianzishwa mwaka 1970 ili kupunguza illiterate level. Mohamed anataka umma uamini kuwa waislam hawakuwa sehemu ya tatizo la illiteracy kiasi kwamba walikuwa na uwezo wa kujenga chuo na kuwa na wanafunzi.
Hisia ni kama maradhi, sijui tiba yake ni nini, ninachojua ni maradhi.

Usichokijua kuhusu mimi ndicho wewe kinakushangaza na unatumia neno ''nafunguka.''

Ngoja nikufahamishe kukuweka sawa.
Mimi si CCM sijapata kuwa.

Sina anijuaye CCM kwa bahati mbaya sana.

Achana na lugha ''kumtimua.''
Unapoteza ladha na ''seriousness'' ya huu mnakasha.

Hiyo hotuba ya ''Moto wa Kiislam Ukiwaka'' ni milestone katika
historia ya Waislam.

Hotuba hiyo ilisomwa na Bilal Rehani Waikela na taarifa ya habari ya
Tanganyika Broadcasting Corporation (TBC) waliirusha.

Kutokana na hotuba ile Bilal Waikela alipokelewa kwa zafa na Waislam Tabora
akasindikizwa hadi nyumbani kwake.

(Hebu nifafanulie kuhusu kujiuzulu kwa Tewa na Fundikira sijaelewa mantiki).

Sheikh Hassan bin Amir harakati zake ilikuwa elimu kwa vijana wa Kiislam na ndiyo
kisa cha chuo kikuu.

Mimi ukiniuliza habari za nchi nyingine unanikwamisha sizijui.
Hizo za Kilwa na nyingine za akina Farid tuzitafutie wakati wake.

Hapa tuwe na mpaka wa majadiliano ''keep your eye on the ball.''

Uthibitisho wa kuuliwa kwa EAMWS kama mahakama inavyotaka ni tabu kupata katika
''social research.''

Hili nishalisema humu ndani mara nyingi tu.
 
Mohamed Said,

Naomba kujua hawa wazee Stephen Mhando, Dr Wilbard B. K, Dr Michael Lungazia, Rashid Sisso, walikuwa na mchango gani kwenye TANU.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom