Mkuu Maalim Mohamed Said, hotuba imewekwa kwa maandishi, neno kwa neno!.
"Kwa hiyo nilikuwa naijua Tanganyika African Association. Nilipokuwa ninaondoka kwenda Ulaya kusoma, nilikuwa nimeishaonja shughuli za TAA. Sasa niliporudi, baada ya kukaa Pugu siku chache, nikaja mjini Dar es Salaam. Nikauliza nani wanaongoza TAA? Nikaambiwa kuna jamaa mmoja anaitwa Abdul Sykes. Sasa ni marehemu. Abdul ndiye alikuwa katibu wakati huo.
Nilipelekwa na Kasela Bantu - ambaye naye aliteleza-teleza na hatunaye hapa (kwenye mkutano). Kasela Bantu alikuwa mwalimu mwenzangu. Tulifundisha pamoja Milambo. Nilipokuja Dar es Salaam, nikakuta anafanya kazi Redio (Tanganyika Broadcasting Corporation). Ni Kasela Bantu aliyenipeleka kwa Sykes.
Wakati huo mambo yalikuwa yanasinzia kidogo. Kwa muda mfupi mwaka ule, tukafufua-fufua, hasa kutoka Januari. Kufika Aprili, TAA ikafufuka. Tukafanya mkutano hapo Anautouglou. Kwenye mkutano huu wakanichagua kuwa Rais wao – wa TAA.
Ninasema yote haya kwa shukrani kwa wazee. Jamaa hawa walikuwa watu wazima wa Dar es Salaam, na mimi kijana mdogo Mzanaki, na Kiswahili changu si kizuri sana – cha matatizo.
Sasa kama yalioandikwa yote ni kweli ndiyo yaliyotamkwa, then wewe kuitwa mchochezi sio kutukanwa bali huo ndio ukweli halisi wa "the motive behind" kitabu chako!.
Ila pia kwa sisi Waafrika tunaoamini imani za mizimu, kumsingizia marehemu kunaleta laana ya aina fulani, nakushauri utubu ungali hai ili kuiepushia "bad karma" familia yako utakayoiacha nyuma baada ya wewe kutangulia mbele ya haki, isije kuadhibiwa kwa makosa yako!. Huu ni ushauri tuu na only if you belive the universal law of "cause and effects", "karma" haina mswalie Mtume wala haina huruma kwa wasio na hatia!.
Pasco.