Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Nadhani sasa ni muda muafaka wa kufanya mathalani tathmini kidogo ya yaliyojiri na ikiwezekana kuwawezesha wengi wanaofuatillia huu mjadala kutafakari yaliyojitokeza na kujiuliza maswali kadhaa. Mengi ya haya maswali ni yale ambayo ninaamini majibu yake hayapatikani kirahisi ndani ya vitabu alivyoviandika Mohamed Said kuhusiana na harakati za kudai uhuru wa Tanganyika. Hata hivyo nina ombi moja tu kwamba kuanzia sasa kama kuna hoja ama ufafanuzi unatakiwa kutolewa, utolewe kwa njia inayokubalika kwa lengo la kuelimishana lakini kama mtu hana hoja au jibu sahihi ingefaa sana akibakia msomaji tu.

Wanajamvi naomba kwanza tujaribu kujizuia na majibu ya dhihaka na kejeli tuweze angalau kudumisha amani, upendo, undugu na utanzania ambao tumejivunia kwa miaka mingi bila kubaguana kwa misingi aliyotuwekea Baba wa Taifa. Na pili naomba mimi niwe wa kwanza kumuuliza Mohamed Said maswali mawili matatu ambayo yanaleta utata katika maandiko yake ambayo, kama anavyodai ameyafanyia utafiti wa muda mrefu, sidhani kama atashindwa kuyajibu kwa ufasaha.. Mohamed Said, maswali yangu kwako ni haya;

  1. Baada ya TANU kuasisiwa, viongozi wake wengine wa juu, pasi Mwalimu Nyerere aliyechaguliwa kwa kishindo kuwa Raisi wake wa Kwanza, walikuwa ni akina nani, walipatikanaje (kuteuliwa au kupigiwa kura?) na kwa sifa zipi? Hapa nina maana ya Makamu Raisi, Katibu na msaidizi wake, Katibu Mwenezi kama alikuwapo, Mweka Hazina n.k Hapo naongelea iliyokuwa kama kamati kuu ya TANU baada ya kuzinduliwa kama iliwahi kuwepo.
  2. Kama viongozi hawa waliteuliwa, ni nani aliyewateua na kwa kuzingatia nini. Je, katiba ya TANU ilikuwa inasemaje na je ilifuatwa katika kuwateua?
  3. Kama viongozi hawa walichaguliwa, walipendekezwa na nani waweze kupigiwa kura? Je hawa wajumbe waliowachagua walipatikanaje? Je majina yao yanaweza kuwekwa wazi kwa wanaofuatilia mjadala huu?
  4. Imedaiwa na Mohamed Said kuwa TANU ilivyozidi kupanuka na kuenea sehemu mbali mbali, idadi ya viongozi Wakristo uliongezeka na kuanza kuwatia shaka wenzao wa Kiislaam...je hawa viongozi walipatikanaje? Je waliteuliwa au walichaguliwa kwa kupigiwa kura?... vyovyote vile je katiba ya TANU ilifuatwa?
Wanajamvi naamini haya maswali ya mwanzo ni muhimu sana katika kuangalia, kutafakari na kujiridhisha na timeline kuhusu baadhi ya Watanganyika walioshiriki karika harakati za kudai uhuru kutokuwa na imani na uongozi wa Mwalimu kabla ya uhuru. Baadaye tutaingia kwenye awamu ya pili nayo ni baada ya uhuru...kitu gani kilileta kutokuaminiana?

Asante sana mkuu, wazo zuri na maswali hayo ni mazuri sana.
 
Last edited by a moderator:
Kwamara nyingine ninakwambia kuwa wewe historia unaifahamu ya kuanzia 1950 tu,

Juu ya historia za machifu Tanganyika na afrika unahitaji msaada tena waharaka.

Wewe umesimuliwa na marafiki wa vituku wasiojua undani wa Mkwawa na wahehe.

Tafuta kitabu cha lugha ya kihehe kiitwacho "Ukoo wa Mkwawa na himaya zake"

Kimeandikwa na Wilium Malangalila mpwa wa Mkwawa.

Veve pe wimpefu yono, kong'omale ndikuwunge nyoko gunio ve.

Yericko,

Unaweza kuwa ni kweli siijjui historia ya machifu na ningependa kujifunza.
Inawezekana kweli pia nikahitaji msaada wa haraka.

Ila sifahamu kwa nini huo msaada uwe wa haraka.

Yericko unapoandika jitulize usimtazame yule unaekabiliananae.
Watazame wasikilizaji wale ndiyo muhimu.

Hawa ndiyo wapiga kura wako.

Huyu ''opponent'' ni mmoja hakushindi.
Jaribu kupata masikio ya wale wasikizaji wanaokusikilizeni.

Hawa ni wengi na ndiyo muhimu.

Jifunze kuandika kwa adabu.
 
Kwamara nyingine ninakwambia kuwa wewe historia unaifahamu ya kuanzia 1950 tu,

Juu ya historia za machifu Tanganyika na afrika unahitaji msaada tena waharaka.

Wewe umesimuliwa na marafiki wa vituku wasiojua undani wa Mkwawa na wahehe.

Tafuta kitabu cha lugha ya kihehe kiitwacho "Ukoo wa Mkwawa na himaya zake"

Kimeandikwa na Wilium Malangalila mpwa wa Mkwawa.

Veve pe wimpefu yono, kong'omale ndikuwunge nyoko gunio ve.

Umepewa vitu vidogo tu vya Mkwawa unaanza matusi? Jee, ukianza kushushiwa nondo zenyewe utakuwaje?

Leo utatafuta pakutokea, hung'oki. Umemeza vyote; chambo, ndoano, chubwi na mshipi, pana pakuchomokea hapo?
 
Mag3,

Maswali yako ni ya msingi umeyaandika kiungwana yanaitaji majibu, mie binafsi na swali kwako kabla ya Nyerere kuitawala Tanzania. Tanganyika watu walikuwa hawaishi kwa upendo na amani.
 
Last edited by a moderator:
Yericko,

Unaweza kuwa ni kweli siijjui historia ya machifu na ningependa kujifunza.
Inawezekana kweli pia nikahitaji msaada wa haraka.

Ila sifahamu kwa nini huo msaada uwe wa haraka.

Yericko unapoandika jitulize usimtazame yule unaekabiliananae.
Watazame wasikilizaji wale ndiyo muhimu.

Hawa ndiyo wapiga kura wako.

Huyu ''opponent'' ni mmoja hakushindi.
Jaribu kupata masikio ya wale wasikizaji wanaokusikilizeni.

Hawa ni wengi na ndiyo muhimu.

Jifunze kuandika kwa adabu.
Hehee moja ya makosa unayoyafanya nikuamini na kutaka kila unaejadiliana hapa jf na wingine basi umtawale, jambo hilo hujajua uwa linakuondolea haiba sekunde hadi sekunde.

Kulazimisha adabu ilihali ipo nihukizo mbele za Mungu, hebu itangulizeweye kisha dai.

Juu ya kujifunza kuandika, nijambo linalo nifurahisha sana,ninaamini hata upewe na muumba miaka mingine 60 hutakuja kunifukia kwa uwezo wakuandika kwa nidhamu ya kimalenga
 
KUMBUKUMBU YA MIAKA 8 YA KIFO CHA KOMREDI LAWI NANGWANDA SIJAONA: MZALENDO, MWADILIFU NA MTUMISHI MCHAPAKAZI ALIYEWAACHA WANAMTWARA MAYATIMA KATIKA MSARAGAMBO WAO.

Jana (Januari 28) imetimia miaka 8 tokea Taifa letu likumbwe na Msiba Mzito wa kumpoteza Shujaa wetu, Mzalendo wa Kupigiwa Mfano, Mwananchi Mwadilifu na mwenye kujali Utu, Kindakindaki wa Tanzania aliyeipenda Nchi yake kwa dhati, Mchapakazi na Mtumishi asiyechoka, Komredi Lawi Nangwanda Sijaona aliyetutoka Duniani Tarehe 28, Januari Mwaka 2005.

Sitashangaa kama Msomaji wa Maandishi haya hutaweza kumtambua Mtumishi huyu wa Kutukuka kwa kuwa Miundo na Mifumo ya Elimu ya Taifa hili haiwezeshi Watu wema na waliolitumikia Taifa hili kwa Uzalendo wa hali ya Juu kama Komredi Lawi kukumbukwa, kuenziwa na mema yao kurithishwa kizazi hadi Kizazi.

Kumbukumbu hii ya kifo chake imeonekana kusahauliwa na wengi (ukiacha watu wa Familia yake) hasa katika wakati huu ambao Taifa letu linapitia katika kipindi kigumu cha Mapambano ya Wananchi wanyonge dhidi ya Serikali yao kwa Upande Mmoja pamoja na Kampuni za Kibeberu zinazonyonya Rasilimali za Nchi hii kwa Jina la Uwekazaji ambao hauwanufaishi Wananchi hao. Bahati Mbaya ama nzuri Mapambano hayo ya Wanyonge yakianzia Mtwara Nyumbani kwao Shujaa huyu.

Kwa Heshima ya Kumbukumbu hii nimeona niwaletee Wasifu wa Maisha ya Mzalendo huyu ulioandikwa na Mwandishi Andrew Chale na kuchapishwa Katika Gazeti la Tanzania Daima siku chache zilizopita.

LAWI NANGWANDA SIJAONA: USHUJAA WAKE UMESAHAULIKA.

NI mmoja wa wapigania uhuru wa Tanganyika, akifanya kazi kubwa ya kuasisi vyama vya siasa vya ukombozi, tangu TAA, TANU na hatimaye CCM. Alikuwa kiongozi na mzalendo wa mfano wa aina yake, Akifanya mambo mengi makubwa na ya kukumbukwa hapa nchini.

Hakuwa "Fisadi", "Mwizi" wala "Mla Rushwa", alikuwa Mwadilifu na mtu aliyelinda kwa nguvu kubwa Rasilimali za Nchi hii. Kumbe, mwisho wake akafa, akazikwa na mema yote, Akasahaulika!.

Huyu ni Lawi Nangwanda Sijaona, aliyezaliwa Novemba 24, 1928, Chiyanga katika eneo la sasa la Kijiji cha Mnyambe kilichopo Tarafa ya Chilangala, Wilaya ya Newala mkoani Mtwara na kufariki Januari 28, mwaka 2005.

Ni mmoja wa vijana wa Tanganyika waliong’ara katika elimu na kujaliwa kipaji cha uongozi. Akiwa amezaliwa katika familia ya mkulima, Nangwanda alipatia elimu ya msingi Utende kuanzia mwaka 1937 na kumaliza darasa la nne mwaka 1942. Alijiunga na Chuo cha Mtakatifu Joseph Chidya, kilichopo wilayani Masasi mwaka 1943.

Mwaka 1948 alijiunga na Chuo cha Mtakatifu Andrea, Minaki alikopata elimu ya kidato cha tatu hadi cha sita na kuhitimu mwaka 1951. Baadae alijiunga na Chuo Kikuu cha Makerere, nchini Uganda kwa masomo ya juu.

HARAKATI ZA UONGOZI.

Nyota ya uongozi ilianza kujichomoza alipokuwa akisoma Minaki. Kutokana na Nidhamu yake na Umaridadi wake, aliteuliwa kuwa Msaidizi wa Kiranja Mkuu, na pia kusimamia suala la chakula.

Alianza kuandika makala na barua nyingi katika majarida na magazeti mbalimbali kuhusu mambo ya siasa, pamoja na kupigwa marufuku na serikali ya kikoloni.

UANDISHI WA HABARI.

Kutokana na harakati zake, haikuwa ajabu kwa Nangwanda kuanza kazi ya uandishi wa habari mwaka 1952 katika Ofisi ya Sekretari Mkuu, Idara ya Mahusiano kwa Umma na akawa mhariri wa gazeti la kila wiki lililojulikana kama “Habari za Leo”.

Alifanya kazi hiyo kwa miaka miwili hadi mwaka 1954 alipoacha na kisha akaombwa na Halmashauri ya Wilaya ya Newala kuwa mtendaji mkuu wa kwanza katika halmashahuri. Hata hivyo alishika nafasi hiyo kwa mwaka mmoja tu.

SHUGHULI ZA KISIASA.

Kutokana na mapenzi yake kwa taifa, Nangwanda licha ya kuwa mfanyakazi wa serikali, Novemba 5, 1953, alijiunga na Chama cha Tanganyika African Association (TAA), na kupewa kadi namba 204. Novemba 1955, Rais wa TANU, Mwalimu Julius Nyerere alitembelea Jimbo la Kusini na kufika hadi nyumbani kwa Nangwanda Newala.

Kutokana na kuzuiwa kwake kujiingiza katika siasa, Nangwanda aliweza kufanya shughuli za kisiasa kwa siri kubwa ikiwemo kumkaribisha nyumbani kwake, Mwalimu Nyerere aliyekuwa akianza harakaati za kuikomboa Tanganyika. Mwalimu Nyerere alilala nyumbani kwa Nangwanda pamoja na kushiriki kupanga mipango mbalimbali ya kuikomboa Tanganyika.

Akiwa amedhamiria kuunga mkono kazi ya kupigania uhuru wa Tanganyika, Nangwanda alifanya uamuzi mgumu wa kuacha kazi nzuri serikalini na kujiunga na TANU wakati wote. Mwaka 1955, Nangwanda alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa kwanza wa TANU, Wilaya ya Newala na mwaka mmoja baadae, alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa TANU Jimbo la Kusini na kuhamia Lindi, yalikokuwa makao makuu ya jimbo.

Nangwanda aliishi Lindi akifanya kazi za TANU wakati wote bila malipo, na wakati huo huo akiwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya TANU. Katika harakati za TANU, Nangwanda alienda India kikazi, na wakati wa kurejea nchini, ndege ilitua kwenye uwanja wa Nairobi, ambako alishikiliwa kwa saa tatu na askari kanzu wa wakoloni.

MWENYEKITI WA KWANZA MWAFIKA.

Mwaka 1958, Tanganyika ilifanya uchaguzi wa kwanza wa serikali za mitaa, Mpigania uhuru huyu alijitosa kugombea na kuchaguliwa kuwa Diwani na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Lindi. Ushindi huo, ulimfanya kuweka historia ya pekee kwa kuwa mwenyekiti wa kwanza Mwafrika kwenye halmashauri za miji katika Afrika Mashariki.

UCHAGUZI WA KURA TATU.

Nyota ya Nangwanda iliendelea kung’ara na mwaka 1959, wakati wa uchaguzi wa kura tatu, aliteuliwa na TANU kuwakilisha Jimbo la Kusini na akachaguliwa bila kupingwa. Haikushangaza kwamba mwaka 1960, alichaguliwa kuwa Mbunge wa Wilaya ya Lindi.

Mwaka 1965, Nangwanda alirudi nyumbani kwao Newala kugombea ubunge na kushinda kwa kishindo, Ni mbunge wa pekee aliyechaguliwa bila kupingwa katika Wilaya ya Newala katika uchaguzi wa mwaka 1970.

UWAZIRI, UKUU WA MKOA.

Desemba 1961, wakati wa uhuru wa Tanganyika, Nangwanda aliteuliwa kuwa Waziri mdogo wa Serikali za Mitaa na Tawala za Majimbo na baadae alihamishiwa Wizara ya Fedha. Desemba 1962, aliteuliwa kuwa Waziri wa Mila za Taifa na Uongozi wa Vijana.

Aprili 1964, wakati wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar aliteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu na Makamu wa Pili wa Rais. Utendaji wake bora ulimwezesha kuhamishwa katika wizara mbalimbali zikiwemo za Ardhi, Maji na Makazi. Mambo ya Ndani ya Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu na Makamu wa Pili wa Rais na Afya na Ustawi wa Jamii.

Mwaka 1972, Wakati wa Madaraka Mikoani, Nangwanda aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ziwa Magharibi na baada ya miezi sita, akahamishiwa Mkoa wa Mwanza. Mwaka 1976 aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na mwaka 1980-1983 alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.

KUSTAAFU.

Akiwa na umri wa miaka 55, mnamo Machi 1983, aliomba kustaafu. Tofauti na watendaji wengi wa serikali wanaolazimika kubaki mijini, Nangwanda alirudi kijijini kwake Mnyambe, ambako aliishi kama mkulima hadi alipoaga dunia. Hata hivyo, kutokana na uwezo wake wa kuongoza, Machi 1983, alikuwa mbunge wa kuteuliwa hadi Bunge lilipovunjwa mwaka 1985.

MIKUTANO YA KAMATI MBALIMBALI.

Akiwa kwenye harakati za siasa na uongozi wa nchi, Nangwanda alifanya mambo mbalimbali akiwa mwakilishi, ambapo mwaka 1956, aliweza kuwakilisha TANU kwenye mkutano wa Asian Socialist Conference uliofanyika Bombay, India.

Mwaka 1959 alikuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya TANU na Katibu Mkuu wa kwanza wa Umoja wa Vijana wa TANU.

Pia mwaka huo huo 1959, baada ya kuwa mjumbe wa kuchaguliwa katika Legislative Council (LEGCO) aliteuliwa kuwa mjumbe wa Tume ya Kuangalia Muundo wa Serikali ya Tanganyika baada ya kujitawala iliyoongozwa na Sir Richard Ramage, iliyoitwa Tume ya Ramage.

Mwaka 1961, aliteuliwa kuwa Mjumbe wa Mkutano wa Katiba (Constitutional Conference). Mwaka 1961-1962, alikuwa mjumbe wa East African Lagistlative Assembly.

Mwaka 1962, wakati akiwa Waziri mdogo wa Fedha, Nangwanda alikuwa mwakilishi wa Serikali ya Tanganyika katika kamati ya nchi 11 ya Economic Commision for Africa, iliyoteuliwa kushauriana na serikali za Afrika juu ya kuanzishwa kwa Benki ya Maendeleo ya Afrika ambayo sasa makao makuu yapo Abidjan, Ivory Coast.

Mwaka 1976, Nangwanda alichaguliwa kuwa mjumbe wa tume ya watu 20 iliyoandaa Katiba ya CCM, na baadaye tume hiyo hiyo iliteuliwa na Rais wa Tanzania, kuandaa Katiba ya Kudumu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa upande wa vyama vya hiyari, alikuwa mwanachama wa maisha wa Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania, Mwanachama wa Tanzania Tuberculosis and Leprosy Association na Tanzania Wildlife Conservation Society.

Pamoja na kazi kubwa ya kutukuka, inashangaza kwamba historia yake haijulikani kwa Watanzania wengi. Ni wachache mno ikiwemo familia yake inayoweza kuwa na ukweli wote wa maisha ya mwanasiasa huyu.

Hakuna mfumo wa kutunza na kusambaza historia za viongozi aina ya Nangwanda waliolitumikia taifa kwa uadilifu, uaminifu na uchapakazi wa kutukuka.

Pamoja na kukosa uangalizi wa kutosha mara baada ya kustaafu, pia serikali imeshindwa kuweka wazi rekodi za utumishi wake ili kuwa kumbukumbu kwa vizazi vijavyo.

P.S. Kumbe kuna wengi waliosahauliwa.

Jasusi hakika ni wengi wamesahauliwa na wamekwenda kaburini na kinyongo.
Mmojawapo ni Suleiman Masudi Mnonji.

Huyu Masudi Mnonji ndiye aliyemtia Lawi Sijaona katika siasa.
Nimefahamiana na mtoto wa Sijaona, Sijali kwa miaka mingi.

Kila ninapokutana humkumbusha, ''Sijali vipi mbona huandiki
maisha ya mzee tukamsoma?''

Jibu la Sijali ni lile lile siku zote, ''Nitaandika.''

Hebu kwa uchache kutana na Masudi Mnonji:

[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD] Southern Province, 1955[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]
The TAA in Lindi was under the leadership of Suleiman Masudi Mnonji and Mohamed Waziri, President and Secretary and respectively. Mnonji was a tailor and Waziri was a draughtsman.

The TAA was formed belatedly in Lindi in 1953 at the time when the TAA leadership in Dar es Salaam was not only transforming the association into an open political party but was making arrangements to send a delegate to the United Nations to plead the cause of independence.

Masudi Mnonji had a fair amount of experience in politics. After World War Two, with his friend and fellow tradesman, Bakari Msham, he had tried to organise trade unions in different sisal estates in the Southern Province.

His efforts did not end there; he also organised cooks and washermen in Lindi to form their own organisation to fight for their rights. It was through his personal initiative that TAA came to be formed in Lindi and he offered his house at Makonde Street as its office.
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601"] Realising the importance of having educated leadership, Mnonji contacted Lawi Nangwanda Sijaona who was at that time living in Newala to come to Lindi and advise TAA on how to organize effectively.

Mnonji was a well-to-do African. He was the main supplier of government uniforms in the south.

Through this business he was able to own three houses in Lindi and when TAA was transformed to TANU he donated one of his houses as the first TANU office in Lindi, and probably the first in Southern Province.

Mnonji’s influence did not end there; one of his two wives, Bibi Zaituni Fadhili, was also involved in politics during the struggle.

Bibi Zaituni Fadhili and another woman, Bibi Shariffa bint Mzee, were among early women activists in Lindi.

Bibi Zaituni Fadhili died in 1995 as a serving member of parliament.
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[/TR]
[TR]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD] Masudu Mnonji baada ya uhuru kupatikana aliwekwa Kizuizini pamoja na Waislam wengine.
Ipo barua Mnonji alimwandikia Nyerere akiwa jela. Sijaona alikwenda jela kumtembelea Mnonji na Mzee Mnonji alimwomba Sijaona amwandikie barua kwa Nyerere.

Baadhi ya maneno katika barua hiyo Mnonji alimwambia Nyerere maneno haya:

''Ikiwa Muheshimiwa una ushahidi kuwa mimi nilikuwa napanga njama za kupindua serikali yako basi nakuomba nipeleke mahakamani nikajibu mashtaka. Lakini ikiwa hakuna ushahidi huo, nakuomba Muheshimiwa uniachie nirudi nyumbani kwangu.

Mwisho Muheshimiwa nakuomba utazame nyuma uangalie wewe na mimi tumetoka wapi.''
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Umepewa vitu vidogo tu vya Mkwawa unaanza matusi? Jee, ukianza kushushiwa nondo zenyewe utakuwaje?

Leo utatafuta pakutokea, hung'oki. Umemeza vyote; chambo, ndoano, chubwi na mshipi, pana pakuchomokea hapo?

kacheze chandimu hapa si mahala pako
 
Yericko,

Unaweza kuwa ni kweli siijjui historia ya machifu na ningependa kujifunza.
Inawezekana kweli pia nikahitaji msaada wa haraka.

Ila sifahamu kwa nini huo msaada uwe wa haraka.

Yericko unapoandika jitulize usimtazame yule unaekabiliananae.
Watazame wasikilizaji wale ndiyo muhimu.

Hawa ndiyo wapiga kura wako.

Huyu ''opponent'' ni mmoja hakushindi.
Jaribu kupata masikio ya wale wasikizaji wanaokusikilizeni.

Hawa ni wengi na ndiyo muhimu.

Jifunze kuandika kwa adabu.

mzee said naomba kumfahamu mzee LAWI NANGWANDA SIJAONA wa Mtwara na ushirki wake kwenye historia naamini nae ni mmoja kati ya wale wazee wakiislamu walioachwa na historia ya sasa juu ya uhuru wa Tanganyika.

Lakini kwenye maandishi yako sijapata kumuona!?

N.B
ninayo picha yake ila nashindwa kuiweka natumia simu yenye uwezo mdogo; labda nimuombe Mzee Mwanakijiji aiweke kwani nimeikuta kwenye ukuta wake wafacebook moja ya rafiki zake akiwa ame'tag
 
Last edited by a moderator:
Katika biography ya Muhammad Ali "The Greatest" kuna kisa anahadithia
fujo alizofanya Drew Bundini kwenye kupima uzito pambano na Sony Liston
Miami Beach Florida 1964.

Kweli Ali anasema nilimtuma Bundini tufanye "fujo" ya kupata "publicity"
magazeti na TV zitutoe.

Ali anasema Bundini kafanya vurugu iliyofurtu ada.
Akajuta.

"Kweli tuliandikwa sana lakini tulipigwa faini na boxing board."

Alipomuuliza Bundini akajibu, "Si ulisema tufanye fujo."

Ali anamaliza mkasa huu kwa kusema kuwa toka siku ile alimuogopa Bundini.
Sababu ni kuwa Bundini alikuwa mwehu.

Ali anasema mtu mzima yoyote lazima amuogope mwendawazimu.
 
Yericko Nyerere,Pole sana mdogo wangu.Kila siku jaribu ''to go an extra mile'' ahsante kwa hilo bandiko kwa maana halisi ya neno ''bandiko.''Najua ulipotoa hiyo historia.Sasa hebu sikiza maneno haya.Mkwawa jina lake ni Abdallah Mkwawa, Mtwa-Mkwavinyika bin Mtwa Muyigumba Mwamuyinga.Alikuwa na rafiki yake akiitwa Muhammad Khalfan Barwani maarufu kwa jina la Rumaliza.Nimesoma bandiko lako taarifa hii muhimu sana haipo.Sitaki kuendelea.Nakupa home work hiyo hapo juu.Mzee Abdallah Ross alikuwa rafiki ya baba yangu.Mzee Ross ni mtoto wa dada yake Chief Mkwawa. Watoto wa Mzee Ross ni rafiki zangu kwa hiyo naijua historia yao hata bila ya kusomeshwa. Mzee Ross baba yale alikuwa Muingereza.

Mkuu Moh, nilipo ona anazungumzia historia ya Mkwawa kwa kirefu bila ya kuzungumzia jina lake la ubatizo na alikuwa madhebu gani - ndio nikamwanzia mbali kwamba "nasikia Mkwawa alikuwa anajuwa kuandika na kusoma kiarabu" - amejibu ndio! Hii ina maana alikuwa anaelewa kila kitu, sasa kwa nini akulisema hilo, au ndio yanarudi yale yale ya kupidisha historia kwa kuondoa mambo muhimu ambayo yanaonekana yatawapa umaarufu watu/kudi fulani!!


Hata ili la kuanzisha historia ya Mkwawa kabla atujamaliza tuliyo anza nayo kwanza inashangaza kidogo, kuna jamaa walitaka alete vitu fulani fulani humu lakini naona hilo hakulitekeleza!


Wengi wetu humu tuna kiu ya kutaka kujua kiundani historia ya kweli kuhusu mababa/mababu zetu wanzilishi wa harakati za kupingana na ukoloni wa Kingereza, kuanzia kwenye miaka ya 1920s mpaka late 1950s, watajwe kwa majina yao, mchango wao na madhehebu yao - kama kuna baadhi ya wanaharakati walio shindwa kuelewana na Nyerere kwa sababu mbali mbali baada ya kukaribishwa kwenye kikundi chao, basi zielezwe sababu na ni nani alihusika kuwafuta kwenye historia ya nchi yetu na zitolewe sababu za msingi za kufanya mambo ya kiimla yanayo litia dosari historia ya Taifa letu, niliona juzi juzi hapa ndio JK alitumia uwanadamu kwa kuwakumbuka baadhi ya wanaharakati hawa kwa kuwatunuku nishani walio hai na wengine ambao wamekwisha tangulia mbele ya haki, sina shaka raia wema wataedelea kumpatia JK majina ya wale wote walio sahulika kuhusu harakati hizo.

Mimi nilikuwa nashauri historia kuhusu Mkwawa, Abushiri, Mangi Meli, Milambo, Rumanyika, Songea nk hayo tuachane nayo kwanza.
 
FM,

Hapana hilo neno ''plagiarism'' unalitumia wewe.
Mimi nililikwepa.

Unaandika kwa hasira sijui kwa nini.
Maneno kama ''mmisheni'' yanaondoa utamu wa majibu yako.

Mimi siwezi kuumwa na chochote kwa kuwa hiyo Appendix
ni mimi niliyeandika.

Ilikuwa ni orbituary ya Peter Colmore ambae mimi nikimjua toka
wakati mimi ni kijana mdogo sana.

Ofisi na makao yake akiwa Dar es Salaam yalikuwa jirani na nyumbani
kwetu katika miaka ya mwanzo ya 1960.

Nikaja kukutananae ukubwani wakati naandika ''Under the Shadow of
British Colonialism...''

Nikimfanyia mahojiano nyumbani kwake Muthaiga au Muthaiga Club
Nairobi.

Kilichonisukuma kuandika ile taazia ni pale nilipoona taazia zilizochapwa
na magazeti ya Kenya hayakumtendea haki.

Orbituary hiyo iliyo kwenye Appendix ilichapwa na The East African.
Mhariri wa The East African, James Odindo alinipigia simu kuniuliza vipi
nilimjua Peter Colmore kwa kiasi kile.

Jibu langu nilimwambia alikuwa ni mzee wangu.

Ikiwa unajua staili yangu ya uandishi utanisikia humo nazungumza.

Sasa ukipenda pita ndani ya kitabu hicho cha Mwakikagile utanikuta.
Sina sababu ya kusema uongo.

Kwa kumaliza napenda kukufahamisha hii si mara ya kwanza kwa maandishi
yangu kutumiwa na waandishi wengine ndani ya kitabu.

Lakini kama nilivyosema katika Uislam hilo si kosa.

Hiyo hukumu juu yangu kuwa mimi napenda ''pretensions of grandeur''
hizo ni fikra zako na una haki nazo.

Kama ni wewe uliyeiandika mbona iko katika first person narrative? Au wewe ndie ulianzisha kampuni ya Sykes Sales Promotion? Au wewe ndie uliyeajiriwa na Colmore katika kampuni yake ya real estate? Au haujaisoma ile appendix?

Mwaikakagile kwa kuiweka kwenye appendix na sio kwenye main body ya text kunaashiria wazi kuwa yeye sie author bali ni documents ambazo ameambatanisha kuongezea uzito yale aliyoandika mwenyewe.

Na mwisho amesema wazi kuwa ameitoa kwenye gazeti la The East African la 16 Februari 2004. Kwa hali hiyo hata kama ni wewe ndie uliyeiandika (kitu ninachotia wasiwasi) basi mtu yeyote ambae angetaka kujua nani mwandishi wa hiyo obituary, angekukuta.

Ndio maana nasema una pretensions of grandeur na sense of victimhood. Kila wakati unahisi umeonewa hata pale ambapo sio.

Mimi natumia neno mmisheni kama vile wewe unavyotumia uislamu. Kugawa, kuonyesha tofauti.Kuonyesha kuwa kwa mtazamo wako mkristu bado ni yule wa mishen kota, adui na mbaya wa waislamu. Tofauti yangu na wewe, mimi natumia neno hili kuonyesha upuuzi wa hoja hiyo. Mmisheni katika ujumla wake hajawahi kuwa adui wa muislamu na vice versa.

Amandla......
 
Yericko Nyerere,

Pole sana mdogo wangu.

Kila siku jaribu ''to go an extra mile'' ahsante kwa hilo bandiko kwa maana halisi ya neno ''bandiko.''
Najua ulipotoa hiyo historia.

Sasa hebu sikiza maneno haya.

Mkwawa jina lake ni Abdallah Mkwawa, Mtwa-Mkwavinyika bin Mtwa Muyigumba Mwamuyinga.
Alikuwa na rafiki yake akiitwa Muhammad Khalfan Barwani maarufu kwa jina la Rumaliza.

Historia ya Mkwawa na hata ya Wajerumani weyewe katika Tanganyika haikamiliki bila ya
kumtaja Rumaliza.

Nimesoma bandiko lako taarifa hii muhimu sana haipo.

Sitaki kuendelea.
Nakupa home work hiyo hapo juu.

Rudi ulikopata hiyo historia uliotuwekea na fanya tena tafiti uje na majibu ya Mkwawa na Rumaliza
au ukipenda Muhammad Khalfan.

Nilibahatika kukutana na Muhammad Said Dubai hiki ni kitukuu cha Rumaliza.
Kanipa mengi kuhusu babu yake mkuu.

Mwisho Yericko nakukanya mdogo wangu kwa nia njema na mapenzi ya kaka kwa mdogo wake.
Hata siku moja usithubutu kunipa changamoto katika mambo haya.

Hapakuwa na sababu ya wewe kuanza na kitisho: ''Mohamed Said je wamjua mzalendo huyu aliye
ukataa ukoloni wa kijerumani?''

Mzee Abdallah Ross alikuwa rafiki ya baba yangu.
Mzee Ross ni mtoto wa dada yake Chief Mkwawa.

Watoto wa Mzee Ross ni rafiki zangu kwa hiyo naijua historia yao hata bila ya kusomeshwa.

Mzee Ross baba yale alikuwa Muingereza.

Muhammad b.Khalfan al Barwani alikuwa mfanyabiashara mkubwa wa watumwa. Ni kweli alipigana na wajerumani lakini haikuwa katika kutetea uafrika au waafrika bali biashara yake. Mwaka 1890, shujaa huyu alikuwa tayari kuungana na wajerumani ili mradi wamwachie eneo la kutawala kama mdhalimu mwenzake Tippu Tip. Mwaka 1908 aliandika kitabu kinachoitwa " ndoto za Sheykh Ahmad" ambacho kilitafsiriwa na baadhi ya watu kama wito kwa muangano wa waislamu. Huyu, bila shaka, alikuwa muislamu kwanza na sidhani kama alijiona hata siku moja kama mwafrika. Kwa mtazamo wangu, kama alikuwa rafiki wa "Abdalah" Mkwawa basi ilikuwa marriage of convenience ya "adui wa adui yangu ni rafiki yangu". Unless tuambiwe kuwa "Abdalah" Mkwawa alipokuwa akipigana na wajerumani alikuwa anatetea uislamu wake na sio wahehe wake! Rumaliza akama alivyokuwa Tippu Tip hakuwa shujaa wa Afrika. Kwangu mimi, hakuwa na tofauti na wajerumani aliokuwa akipigana nao.

Amandla.....
 
KUna msemo wa kuwa unaweza kuwa "unatwanga maji kwenye kinu" au ni sawa "na kumpigia mbuzi gitaa". Kama watu wametusoma vya kutosha humu kuna mambo yako wazi kabisa kuhusu maandishi ya Bw. Mohammed Said. NIkiamua kujumlisha tu kwa ufupi ni kwamba:

1: Hakutaka kuandika kazi ya historia

Japo mara kwa mara ndugu yetu anapenda kuelezea maandishi yake kuwa ni kazi ya kihistoria ukweli ni kuwa - na tumefanikiwa kuuonesha mara kadhaa sasa - Bw. Said alitaka kuanzika simulizi (narrative) ya wazazi wake biila kujali USHAHIDI kihistoria. Sote katika utoto tumekaa na wazee wetu ambao wametusimulia mambo mengi - yawe ya uhuru au ya maisha ya kijijini - na yametupa mawazo fulani juu yetu sisi wenyewe. Kwa mfano, kuna watu ambao wanamchukia Nyerere kwa kuendesha kampeni ya Ujamaa Vijijini kwa sababu wazazi wao waliwasimulia jinsi hali ilivyokuwa mbaya. Wapo wengine ambao walijikuta wanamchukia Idi Amin kwa sababu wakati wanakua simulizi kubwa pale nyumbani lilikuwa ni chuki dhidi ya Idi Amin.

Sasa masimulizi hayo ya utotoni hata yakitoka kwa baba, babu, wajomba au shangazi hayawi historia kwa sababu wao wamesema. Yanakuwa historia kama yana ushahidi wa kihistoria. Bahati mbaya sana Bw. Said hajajali ushahidi wa kihistoria kwani ushahidi pekee ambao yeye kautumia ni ule wa kuthibitisha hoja yake. Kwa kufanya hivyo Bw. Said amefanya kosa kubwa sana katika uandishi wa historia - kuonesha historical bias. Sasa historical bias ni rahisi sana kuiona kwenye maandishi ya mtu.

Kitabu cha Bw. Said kinampa msomaji kile kinachojulikana kama revisionist history; yaani ameamua kutoka kwenye historia ilivyo na kuielea kwa misingi ya bias yake.

2. Bias kubwa ya Bw. Said naweza kusema inatokana na kile ambacho yeye anaamini ni nguvu yake - yaani wazee wake. Kwa kujaribu kuandika historia kwa kutumia wazee wake kama "the most reliable sources' na kushindwa kuwa huru kimawazo kusoma mawazo yanayopingana na wazee wake amejikuta anaandika historia kwa kutumia bias without any sense of objectivity. Kwa yeye anaamini hilo ni sawa kwa sababu "ni historia ya wazee wangu". Tatizo ni kuwa historia ya wazee wake haiwi historia kwa vile wamemsimulia yeye inakuwa historia kama inaangaliwa objectively. Hili ndio tatizo kubwa.

3. Kutokana na hayo mawili hapo juu maandishi ya Bw. Said yamejaa hisia zaidi kuliko ushahidi wa kihistoria. Hisia ambazo zinatokana na mapenzi ya mtoto kwa wazee wake, uchungu wa mjukuu kwa babu yake, na hisia ya fungamano la dini. Bw. Said ataamini yale yote anayoambbiwa na wazee wake bila kuyahoji kwani kuhoji ni kuwavunjia heshima, kuuliza ni kutokuwaamini. Mwanahistoria mzuri ni yule ambaye anahoji na kuuliza maswali. Bw. Said amekuwa mpokeaji wa majibu lakinibila kuuliza maswali wala kuwa tayari kutambua contradictions katika maelezo ya watu.

4. HIvyo Bw. Said kaandika kile nilichokipa jina la "histohisia" yaani historia inayoandikwa kutoka kwenye hisia. Bw. Said aliaminishwa toka utotoni kuwa wazee wake walionewa; pale mtaani alipokulia alizungukwa na watu ambao walimuaminisha kuwa Waislamu wameonewa na wazee wa Dar hususan wamefutwa katika historia. Aliambiwa adui aliyefanya hivi ni Julius Nyerere aliyekaribishwa na wazee wake na kufanyiwa kila aina ya ukarimu; akaambiwa kuwa alipoingia madarakani Nyerere aliwageuka Waislamu wa Dar na kuwatenga. Simulizi hili lilimgusa ndugu Said kiasi kwamba alijiapia mwenyewe kuwa akipata nafasi ya kuandika simulizi la wazee "wake" atafanya hivyo.

Maandishi yake basi na yeye mwenyewe ameshasema mara nyingi ni kutimiza ndoto ya kusimulia yaliyowakuta wazazi wake kwa kadiri walivyomwambia. Hakufanya juhudi zozote za kutaka kuhakikisha kama aliyoambiwa na wazee wake ni kweli na kama ni kweli basi kwa kiasi gani na je kuna maelezo mengine yanayoweza kuelezea aliyosimuliwa.

5. Kutokana na hilo la nne kwa makusudi kabisa na pasi ya kufikiria sana Bw. Said akaamua kufanya mambo mawili makubwa sana ambayo yanaharibu kabisa simulizi zake.

a. Kutosimulia wazee wengine ambao walishirikiana na wazee wake katika harakati za Uhuru pamoja na Baba wa Taifa. Na wazee hawa WOTE ni Wakristu. Kimsingi, Bw. Said amefanya exactly kile ambacho anamtuhumu Nyerere. Bw. Said anasema Nyerere aliacha historia iandikwe ikimuweka yeye kama 'peke yake' katika harakati za uhuru na kuwaacha wazee wa Kiislamu (hasemi wazee wengine); na yeye kwa makusudi ameamua kuandika historia ya wazee wa Kiislamu na kuwaacha wazee wengine! Lakini la kwake analihalalisha kuwa ni sawa kuandika 'historia' kwa kuangalia upande mmoja lakini ni makosa kwa waandishi wa historia ya Nyerere kuandika kwa upande mmoja!

b. Kutoka kwenye simulizi la historia aliyosimuliwa Bw. Said akaenda mbali zaidi na kuanza kuelezea kwa misingi ya kuonesha kuwa Wakristu nchini wananufaika na wamenufaika sana na uhuru kuliko Waislamu na hii imetokana na ukwlei kuwa Wakristu wamependelewa na Waislamu wametengwa. Simulizi lake basi limetoka kuwa la kihistoria na kuwa la kiharakati - sasa hili halina tatizo kabisa kama akisema awali kuwa ni suala la harakati.

6. Bw. Said amefanikiwa kupata wasikilizaji wengi na watu wengi wakimuamini kwa sababu wengi wa hawa hawana namna ya kujua mbinu anazotumia kujenga hoja. Ikumbukwe kuwa Bw. Said hajatumia mbinu za uandishi wa kihistoria ambao unaongozwa na historical method. Yeye kaandika kama alivyosmuliwa na alikusanya nyaraka na kuzipa tafsiri ya yeye anachoamini. Ukimsoma sana utaona ni jinsi gani anaandika kama ana uwezo wa kujua nia, hisia, na mawazo ya wahusika.

7. Kitabu chake maarufu kinachomzungumzia Abdul Sykes kwa kweli ni sehemu ndogo sana inahusiana na maisha ya Abdulwahid Sykes. NI kitabu ambacho kinaelezea kwa kirefu uwezo, ushawishi na uongozi wa Mwalimu Nyerere kati ya wazee wake Jijini Dar - Wakristu, Waislamu, Wahindi na Wapagani! Binafsi nilipokisoma kitabu hicho kwa kuangalia 'facts' peke yake nilikipenda mno kwani kinamuonesha Nyerere kwa mwanga mzuri sana. Ni pale tu Bw. Said anapoweka hisia zake ndipo unapoona utamu wa kitabu kufutika kwa sababu kwa kiasi kikubwa hisia zake hazina ushahidi wowote wa kuzithibitisha. Kwa mfano anaposema "ilisemwa" au "iliaminika" au "alidhaniwa" ni wazi kuwa hana namna yoyote ya kujua hisia hizo isipokuwa kwa kukisia - ndio maana naiita 'histohisia'.

Binafsi nashauri watu wote wanaopenda kujifunza tofauti ya historia na histohisia wakitafute kitabu hiki kwani kitawafundisha namna YA KUTOANDIKA HISTORIA.

MMM
 
Hehee moja ya makosa unayoyafanya nikuamini na kutaka kila unaejadiliana hapa jf na wingine basi umtawale, jambo hilo hujajua uwa linakuondolea haiba sekunde hadi sekunde.

Kulazimisha adabu ilihali ipo nihukizo mbele za Mungu, hebu itangulizeweye kisha dai.

Juu ya kujifunza kuandika, nijambo linalo nifurahisha sana,ninaamini hata upewe na muumba miaka mingine 60 hutakuja kunifukia kwa uwezo wakuandika kwa nidhamu ya kimalenga

Hii yote baada ya kusikia kuwa kumbe Mkwawa nae ni Abdallah.

pole kijana, fata nasaha za waliokutangulia, usiwe na kibri utafaidika, nakuasa pitia nyuzi yangu hii, ambayo labda wewe utaielewa, wengi walijidai hawaelewi: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/345499-watanzania-na-ubaguzi-wa-ujinga.html
 
Mag3,

Maswali yako ni ya msingi umeyaandika kiungwana yanaitaji majibu, mie binafsi na swali kwako kabla ya Nyerere kuitawala Tanzania. Tanganyika watu walikuwa hawaishi kwa upendo na amani.

Nyerere mwenyewe alikaribishwa kiuungwana na watu wa dar vijana kwa wazee, hilo anakiri nyerere mwenyewe, na hapo alikuwa hata ndoto ya kuwa atakuwa mtawala hana.

"Ninasema yote haya kwa shukrani kwa wazee. Jamaa hawa walikuwa watu wazima wa Dar es Salaam, na mimi kijana mdogo Mzanaki, na Kiswahili changu si kizuri sana – cha matatizo.

Nimekuja, natoka Ulaya, tena masomoni. Muda mfupi tu jamaa hawa wakaniamini haraka sana"

Hapo ninamnukuu bandiko la Yericko la post namba moja.

 
Muhammad b.Khalfan al Barwani alikuwa mfanyabiashara mkubwa wa watumwa. Ni kweli alipigana na wajerumani lakini haikuwa katika kutetea uafrika au waafrika bali biashara yake. Mwaka 1890, shujaa huyu alikuwa tayari kuungana na wajerumani ili mradi wamwachie eneo la kutawala kama mdhalimu mwenzake Tippu Tip. Mwaka 1908 aliandika kitabu kinachoitwa " ndoto za Sheykh Ahmad" ambacho kilitafsiriwa na baadhi ya watu kama wito kwa muangano wa waislamu. Huyu, bila shaka, alikuwa muislamu kwanza na sidhani kama alijiona hata siku moja kama mwafrika. Kwa mtazamo wangu, kama alikuwa rafiki wa "Abdalah" Mkwawa basi ilikuwa marriage of convenience ya "adui wa adui yangu ni rafiki yangu". Unless tuambiwe kuwa "Abdalah" Mkwawa alipokuwa akipigana na wajerumani alikuwa anatetea uislamu wake na sio wahehe wake! Rumaliza akama alivyokuwa Tippu Tip hakuwa shujaa wa Afrika. Kwangu mimi, hakuwa na tofauti na wajerumani aliokuwa akipigana nao.

Amandla.....

Na huyo huyo "Muhammad b.Khalfan al Barwani alikuwa mfanyabiashara mkubwa wa watumwa" ndiye rafiki yake mkubwa mtawala chifu Abdallah Mkwawa, walikuwa na nini in common?
 
KUna msemo wa kuwa unaweza kuwa "unatwanga maji kwenye kinu" au ni sawa "na kumpigia mbuzi gitaa". Kama watu wametusoma vya kutosha humu kuna mambo yako wazi kabisa kuhusu maandishi ya Bw. Mohammed Said. NIkiamua kujumlisha tu kwa ufupi ni kwamba:

1: Hakutaka kuandika kazi ya historia

Japo mara kwa mara ndugu yetu anapenda kuelezea maandishi yake kuwa ni kazi ya kihistoria ukweli ni kuwa - na tumefanikiwa kuuonesha mara kadhaa sasa - Bw. Said alitaka kuanzika simulizi (narrative) ya wazazi wake biila kujali USHAHIDI kihistoria. Sote katika utoto tumekaa na wazee wetu ambao wametusimulia mambo mengi - yawe ya uhuru au ya maisha ya kijijini - na yametupa mawazo fulani juu yetu sisi wenyewe. Kwa mfano, kuna watu ambao wanamchukia Nyerere kwa kuendesha kampeni ya Ujamaa Vijijini kwa sababu wazazi wao waliwasimulia jinsi hali ilivyokuwa mbaya. Wapo wengine ambao walijikuta wanamchukia Idi Amin kwa sababu wakati wanakua simulizi kubwa pale nyumbani lilikuwa ni chuki dhidi ya Idi Amin.

Sasa masimulizi hayo ya utotoni hata yakitoka kwa baba, babu, wajomba au shangazi hayawi historia kwa sababu wao wamesema. Yanakuwa historia kama yana ushahidi wa kihistoria. Bahati mbaya sana Bw. Said hajajali ushahidi wa kihistoria kwani ushahidi pekee ambao yeye kautumia ni ule wa kuthibitisha hoja yake. Kwa kufanya hivyo Bw. Said amefanya kosa kubwa sana katika uandishi wa historia - kuonesha historical bias. Sasa historical bias ni rahisi sana kuiona kwenye maandishi ya mtu.

Kitabu cha Bw. Said kinampa msomaji kile kinachojulikana kama revisionist history; yaani ameamua kutoka kwenye historia ilivyo na kuielea kwa misingi ya bias yake.

2. Bias kubwa ya Bw. Said naweza kusema inatokana na kile ambacho yeye anaamini ni nguvu yake - yaani wazee wake. Kwa kujaribu kuandika historia kwa kutumia wazee wake kama "the most reliable sources' na kushindwa kuwa huru kimawazo kusoma mawazo yanayopingana na wazee wake amejikuta anaandika historia kwa kutumia bias without any sense of objectivity. Kwa yeye anaamini hilo ni sawa kwa sababu "ni historia ya wazee wangu". Tatizo ni kuwa historia ya wazee wake haiwi historia kwa vile wamemsimulia yeye inakuwa historia kama inaangaliwa objectively. Hili ndio tatizo kubwa.

3. Kutokana na hayo mawili hapo juu maandishi ya Bw. Said yamejaa hisia zaidi kuliko ushahidi wa kihistoria. Hisia ambazo zinatokana na mapenzi ya mtoto kwa wazee wake, uchungu wa mjukuu kwa babu yake, na hisia ya fungamano la dini. Bw. Said ataamini yale yote anayoambbiwa na wazee wake bila kuyahoji kwani kuhoji ni kuwavunjia heshima, kuuliza ni kutokuwaamini. Mwanahistoria mzuri ni yule ambaye anahoji na kuuliza maswali. Bw. Said amekuwa mpokeaji wa majibu lakinibila kuuliza maswali wala kuwa tayari kutambua contradictions katika maelezo ya watu.

4. HIvyo Bw. Said kaandika kile nilichokipa jina la "histohisia" yaani historia inayoandikwa kutoka kwenye hisia. Bw. Said aliaminishwa toka utotoni kuwa wazee wake walionewa; pale mtaani alipokulia alizungukwa na watu ambao walimuaminisha kuwa Waislamu wameonewa na wazee wa Dar hususan wamefutwa katika historia. Aliambiwa adui aliyefanya hivi ni Julius Nyerere aliyekaribishwa na wazee wake na kufanyiwa kila aina ya ukarimu; akaambiwa kuwa alipoingia madarakani Nyerere aliwageuka Waislamu wa Dar na kuwatenga. Simulizi hili lilimgusa ndugu Said kiasi kwamba alijiapia mwenyewe kuwa akipata nafasi ya kuandika simulizi la wazee "wake" atafanya hivyo.

Maandishi yake basi na yeye mwenyewe ameshasema mara nyingi ni kutimiza ndoto ya kusimulia yaliyowakuta wazazi wake kwa kadiri walivyomwambia. Hakufanya juhudi zozote za kutaka kuhakikisha kama aliyoambiwa na wazee wake ni kweli na kama ni kweli basi kwa kiasi gani na je kuna maelezo mengine yanayoweza kuelezea aliyosimuliwa.

5. Kutokana na hilo la nne kwa makusudi kabisa na pasi ya kufikiria sana Bw. Said akaamua kufanya mambo mawili makubwa sana ambayo yanaharibu kabisa simulizi zake.

a. Kutosimulia wazee wengine ambao walishirikiana na wazee wake katika harakati za Uhuru pamoja na Baba wa Taifa. Na wazee hawa WOTE ni Wakristu. Kimsingi, Bw. Said amefanya exactly kile ambacho anamtuhumu Nyerere. Bw. Said anasema Nyerere aliacha historia iandikwe ikimuweka yeye kama 'peke yake' katika harakati za uhuru na kuwaacha wazee wa Kiislamu (hasemi wazee wengine); na yeye kwa makusudi ameamua kuandika historia ya wazee wa Kiislamu na kuwaacha wazee wengine! Lakini la kwake analihalalisha kuwa ni sawa kuandika 'historia' kwa kuangalia upande mmoja lakini ni makosa kwa waandishi wa historia ya Nyerere kuandika kwa upande mmoja!

b. Kutoka kwenye simulizi la historia aliyosimuliwa Bw. Said akaenda mbali zaidi na kuanza kuelezea kwa misingi ya kuonesha kuwa Wakristu nchini wananufaika na wamenufaika sana na uhuru kuliko Waislamu na hii imetokana na ukwlei kuwa Wakristu wamependelewa na Waislamu wametengwa. Simulizi lake basi limetoka kuwa la kihistoria na kuwa la kiharakati - sasa hili halina tatizo kabisa kama akisema awali kuwa ni suala la harakati.

6. Bw. Said amefanikiwa kupata wasikilizaji wengi na watu wengi wakimuamini kwa sababu wengi wa hawa hawana namna ya kujua mbinu anazotumia kujenga hoja. Ikumbukwe kuwa Bw. Said hajatumia mbinu za uandishi wa kihistoria ambao unaongozwa na historical method. Yeye kaandika kama alivyosmuliwa na alikusanya nyaraka na kuzipa tafsiri ya yeye anachoamini. Ukimsoma sana utaona ni jinsi gani anaandika kama ana uwezo wa kujua nia, hisia, na mawazo ya wahusika.

7. Kitabu chake maarufu kinachomzungumzia Abdul Sykes kwa kweli ni sehemu ndogo sana inahusiana na maisha ya Abdulwahid Sykes. NI kitabu ambacho kinaelezea kwa kirefu uwezo, ushawishi na uongozi wa Mwalimu Nyerere kati ya wazee wake Jijini Dar - Wakristu, Waislamu, Wahindi na Wapagani! Binafsi nilipokisoma kitabu hicho kwa kuangalia 'facts' peke yake nilikipenda mno kwani kinamuonesha Nyerere kwa mwanga mzuri sana. Ni pale tu Bw. Said anapoweka hisia zake ndipo unapoona utamu wa kitabu kufutika kwa sababu kwa kiasi kikubwa hisia zake hazina ushahidi wowote wa kuzithibitisha. Kwa mfano anaposema "ilisemwa" au "iliaminika" au "alidhaniwa" ni wazi kuwa hana namna yoyote ya kujua hisia hizo isipokuwa kwa kukisia - ndio maana naiita 'histohisia'.

Binafsi nashauri watu wote wanaopenda kujifunza tofauti ya historia na histohisia wakitafute kitabu hiki kwani kitawafundisha namna YA KUTOANDIKA HISTORIA.

MMM

MM,

Nime nimekusoma.
Lazima sisi kama binadamu tutakhitilafiana.

Wewe unakhitilafiana na mimi kama mimi nilivyokhitilafiana na kitabu
cha ''Historia ya TANU 1954 -1977'' kilichoandikwa na Chuo Cha Kivukoni.

Kitabu hiki hakikuwataja wazee wangu waliopigania uhuru wa Tanganyika.
Kitabu hakikumtaja Abdulwahid Sykes kilitosheka na Nyerere peke yake.

Sikufurahi.

Nikanyanyua kalamu nikawarejesha katika historia kupitia kitabu changu wale
wote waliosahauliwa.

Na wewe hujaridhika na kitabu changu kwa kuwaandika wazee wangu una
haki ya kuandika kitabu chako.

Hivi ndivyo usomi unavyokwenda.
Kila siku ni kutafuta kile ambacho hakikuwa kinafahamika na kukiweka hadharani.

From the known to the unknown.
 
Back
Top Bottom