Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Yericko Nyerere,

Bado sana kwenye historia ya Tanganyika nakuuliza swali moja tu.

1) Manowari ya mamluki wa Kijerumani ilitia nanga Pangani mwaka gani?
 
Last edited by a moderator:
Yericko, Unaweza kuwa ni kweli siijjui historia ya machifu na ningependa kujifunza. Inawezekana kweli pia nikahitaji msaada wa haraka. Ila sifahamu kwa nini huo msaada uwe wa haraka. Yericko unapoandika jitulize usimtazame yule unaekabiliananae. Watazame wasikilizaji wale ndiyo muhimu. Hawa ndiyo wapiga kura wako. Huyu ''opponent'' ni mmoja hakushindi. Jaribu kupata masikio ya wale wasikizaji wanaokusikilizeni. Hawa ni wengi na ndiyo muhimu. Jifunze kuandika kwa adabu.
Haya ni maneno ya busara sana. Hakika Mohamed said sio tu mtaalamu wa historia pia ni mtu aliyebobea sana katika somo zima la Adab. Allah akubarik sana Mohamed Said.
 
Yericko Nyerere,

Bado sana kwenye historia ya Tanganyika nakuuliza swali moja tu.

1) Manowari ya mamluki wa Kijerumani ilitia nanga Pangani mwaka gani?

Swali lako bado sijalielewa, unamaanisha MAMLUKI wapi?

Wajerumani hawakuja kama mamluki bali walikuja kama walivyoitwa WAKOLONI

MAMLUKI ina maana moja tu kuu, nayo ni mtu asiyefahamika miongoni mwa watu mwenye kazi ya kijasusi tu!

Je unamaanisha ujio wao wa kwanza walitia nanga pale Pangani Tanga?

Kama ndivyo badi jibu langu ni ndio, na walikuta tayari Muarabu ashaweka himaya zake za kipagazi kwa maeneo ya pwani yote kama Kilwa, Pangani nk lakini hakuwa na udhibiti mkali wa himaya yake na wakatwaa
 
Last edited by a moderator:
Kati ya watu nnaowakubali hapa JF wewe ( Yericko) ni mmojawapo.Lakini sometimes unaegemea sana upande mmoja kaka. Kila mtu ana maoni yake na mtazamo wake.

Wengi wetu tumekwenda shule na wengine bado tupo shule, kuna vitu vingine huitaji elimu ya juu kujua lizungumzwalo ni kweli ama sio kweli. Kama umebahatika kusoma kitabu chake ( M. Said) jaribu kupambanua uone asemayo ni kweli au analeta uchochezi. Hata iweje histori haiwezi futika. Usinielewe vibaya ndgu tunabadikishana mawazo tu


Sent via EyePhone

Hiyo nimeipenda sana, mimi nilikuwa najuwa kuna Iphone tu kumbe na EyePhone zipo.

Ahsante.
 
Yericko Nyerere, Pole sana mdogo wangu. Kila siku jaribu ''to go an extra mile'' ahsante kwa hilo bandiko kwa maana halisi ya neno ''bandiko.'' Najua ulipotoa hiyo historia. Sasa hebu sikiza maneno haya. Mkwawa jina lake ni Abdallah Mkwawa, Mtwa-Mkwavinyika bin Mtwa Muyigumba Mwamuyinga. Alikuwa na rafiki yake akiitwa Muhammad Khalfan Barwani maarufu kwa jina la Rumaliza. Historia ya Mkwawa na hata ya Wajerumani weyewe katika Tanganyika haikamiliki bila ya kumtaja Rumaliza. Nimesoma bandiko lako taarifa hii muhimu sana haipo. Sitaki kuendelea. Nakupa home work hiyo hapo juu. Rudi ulikopata hiyo historia uliotuwekea na fanya tena tafiti uje na majibu ya Mkwawa na Rumaliza au ukipenda Muhammad Khalfan. Nilibahatika kukutana na Muhammad Said Dubai hiki ni kitukuu cha Rumaliza. Kanipa mengi kuhusu babu yake mkuu. Mwisho Yericko nakukanya mdogo wangu kwa nia njema na mapenzi ya kaka kwa mdogo wake. Hata siku moja usithubutu kunipa changamoto katika mambo haya. Hapakuwa na sababu ya wewe kuanza na kitisho: ''Mohamed Said je wamjua mzalendo huyu aliye ukataa ukoloni wa kijerumani?'' Mzee Abdallah Ross alikuwa rafiki ya baba yangu. Mzee Ross ni mtoto wa dada yake Chief Mkwawa. Watoto wa Mzee Ross ni rafiki zangu kwa hiyo naijua historia yao hata bila ya kusomeshwa. Mzee Ross baba yale alikuwa Muingereza.
Kweli wewe ni Bahr ya historia. Allah azidi kukubariki sana kwa darsa hili kwani tunajifunza mengi ambayo tulikuwa hatuyafahamu.
 
Kituko,

Alichofanya Mohamed Said ni kuandika.

"Historia iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza katika Tanganyika."

Pitia vizuri hiyo hotuba ya Nyerere anakuambia mwenyewe baada ya kumsomea dua wanamfanyia matambiko hao hao Wazee wa Dar es Salaam.

Matambiko ni mila za makabila wala siyo kitu kigeni.

Mkuu matambiko ni mila za Makabila, kama ulivyo Uislam mila ya Ibrahim, ni mila tofauti ambazo haziwezi changamana, huwezi fanya matambiko ya kikabila na hapohapo ukasema wewe ni Muislam

Point ni kuwa Moh Said ana Wazee wake

Msome vizuri Mohamedi Said, na mwisho utakuja kugundua anatetea nini na kwa Maslahi ya nani, maana kama unafunika uso unaweza kudhani tuko kundi moja na Mzee Moh Said, nadhani FFox tongotongo lilimtoka na kujua Moh Said anatafuta nini kwa maslahi ya nani
hope na wewe soon utaelewa tu
 
Swali lako bado sijalielewa, unamaanisha MAMLUKI wapi?

Wajerumani hawakuja kama mamluki bali walikuja kama walivyoitwa WAKOLONI

MAMLUKI ina maana moja tu kuu, nayo ni mtu asiyefahamika miongoni mwa watu mwenye kazi ya kijasusi tu!

Je unamaanisha ujio wao wa kwanza walitia nanga pale Pangani Tanga?

Kama ndivyo badi jibu langu ni ndio, na walikuta tayari Muarabu ashaweka himaya zake za kipagazi kwa maeneo ya pwani yote kama Kilwa, Pangani nk lakini hakuwa na udhibiti mkali wa himaya yake na wakatwaa

Mamluki kutoka Msumbiji na sehemu zingine sijakuambia Wajerumani ndiyo mamluki.
 
Umechoka kulizungumzia hili jambo ambalo wewe umelipotosha?

Hapa shida ninayo iona ni kwamba ndugu Yeriko hutaki kukubaliana na Mohamed said kwamba wazee wake hawapo kwenya historia ya nchi hii hivyo historia imepotoshwa!
 
Mkuu matambiko ni mila za Makabila, kama ulivyo Uislam mila ya Ibrahim, ni mila tofauti ambazo haziwezi changamana, huwezi fanya matambiko ya kikabila na hapohapo ukasema wewe ni Muislam

Point ni kuwa Moh Said ana Wazee wake

Msome vizuri Mohamedi Said, na mwisho utakuja kugundua anatetea nini na kwa Maslahi ya nani, maana kama unafunika uso unaweza kudhani tuko kundi moja na Mzee Moh Said, nadhani FFox tongotongo lilimtoka na kujua Moh Said anatafuta nini kwa maslahi ya nani
hope na wewe soon utaelewa tu

Kituko,

Naona unachanganya mambo hebu nipe ufafanuzi unaposema matambiko ni mila za makabila, kama ulivyo Uislam mila ya Ibrahim.

Matambiko yanafanywa na mila za makabila, ndiyo maana unaona watu wana dini zao lakini bado wanafanya matambiko ya mila zao kama Wamanyema walivyokuwa wanamfanyia Nyerere.
 
Last edited by a moderator:
Leo naangalia nyuma nakwenda mbali sana.
Toka utoto nikipenda sana kusoma na kusikiliza.

Wazee wakizungumza niko chini ya miguu yao mpaka
wakati mwingne inakuja, ''Mohamed haya kulala sasa.''

Nilipokujajua kusoma na kujua nini kimo katika vitabu
nikawa ''book worm.''

Nasoma vitabu vya Spaniards naingia nao melini
tunang'oa nanga tunaingia Atlantic.

Mawimbi yanapiga meli nami nimo tunaingia Amerika, nimo.
Nikinyanyua kichwa jua limezama.

Maghrib.

Library ilikuwa pale Mtaa wa Mkwepu.
Narudi nyumbani nimeazima kitabu naja kusoma nyumbani.
Hizo ndio ngano wanazozifurahia sana mashabiki wako !!
 
1) Usisahu kutuwekea na majina ya wale waasi walipewa msamaha na Nyerere na wengine wengi kupewa vyeo na mabalozi kama ulivyosema mwenyewe. 2) tuwekee na gari la kwanza la Nyerere uliosema kapewa na Mariale. 3) Utuwekee na kiasi cha pesa alichopewa Nyerere na Mariale kwenda UNO kama ulivyotuambia hapo mwanzo.
Ritz, Sijui kama utaweza kupata majibu ya haya masuala yako. OK Tuvute subra
 
Imekua kosa kubwa kwa Mzee Mohamed Said kuandika historia ya wazee wake! Ajabu ya Rahmaan. Alafu ndo watu wanajiita wasomi na "Great Thinkers".


Yericko Nyerere, TBC wanasemaje? "Kesho haijafika tu" au ndo ilee "Tomorrow never comes"
 
Last edited by a moderator:
Mag3,

Ni muhimu ikatambulika kwamba TAA ilizaliwa miaka zaidi ya 20 kabla ya TANU, wakatu huo Mwalimu akiwa hata hajabalee. Ni baadae sana ndio Mwalimu akaanza mahusiano na TAA, hasa baada ya viongozi wa TAA kumwona Nyerere kama ni mtu makini na mwenye ushawishi mkubwa katika suala zima la kudai uhuru wa Tanganyika. Hivyo viongozi wa TAA na Mwalimu wakaona kwamba wakishirikiana, kila upande utapata kile walichokuwa wanakitafuta.

Ikumbukwe pia kwamba TAA hakikuwa chama cha Siasa bali a Social Movement iliyokuwa ikipigania haki mbalimbali za watanganyika wakati wa Ukoloni.
Umakini wa Mwalimu, hasa uliotokana na uwezo wake mkubwa wa kuunganisha watanganyika bila kujali dini, makabila na jinsia zao, uliwavutia sana viongozi wa TAA na ndipo wakakubali kufanya kazi na Mwalimu. Kila upande ukaleta assets zake muhimu mezani – kwa upande mmoja, Mwalimu akaleta his leadership abilities, Vision, Upeo wa kidunia kutokana na elimu yake Uingereza, Uwezo wa kujieleza, na uwezo wa kuunganisha watanganyika wa dini na makabila mbalimbali. Kwa upande mwingine, TAA nayo ikaleta uzoefu wake wa miaka zaidi ya 20 ya harakati za kudai haki na maslahi ya watu weusi na pia its large territorial base within Tanganyika chini ya wale viongozi kumi na sita ambao walikuwa ni wawakilishi wa TAA katika majimbo mbalimbali Tanganyika. Nyereer alikuja kuongezeka na kuwa mjumbe wa 17 katika mkutano mkuu wa TAA wa mwaka 1954 ambao ndio uliozaa TANU, lakini bado kama a political movement, sio chama cha Siasa.

Kuna mambo makuu matatu ya kuzingatia hapa: Kwanza ni muhimu tufahamu kwamba Nyerere alichaguliwa kuwa Rais wa kwanza wa TANU – TANU ikiwa as a Political Movement, sio Chama cha Siasa kwani ingawa TANU ilizaliwa mwaka 1954, bado hakikuwa Chama cha Siasa. TANU ilisajiliwa rasmi kama Chama Cha Siasa muda mfupi kabla ya Uhuru. Kwahiyo kuhoji jinsi gani Mwalimu alichaguliwa kuwa Rais wa kwanza wa TANU ni kuhoji mchakato jinsi gani VUGUVUGU LA KISIASA linajipatia viongozi wake, hivyo mjadala wa namna hiyo hauna manufaa yoyote kwetu.

Jambo la pili la kuzingatia ni kwamba – TAA kama a social movement kwa miaka zaidi ya 20 kabla ya kubadilika kuwa TANU, kilikuwa ni chombo chenye organizational culture yake, Siasa zake, makundi yake n.k, ambayo TANU ilikuja kuyarithi yote mwaka 1954. Katika hali hii, watu makini wanatakiwa kujikita zaidi katika kujadili jinsi gani Mwalimu Nyerere katika umri wa wakw mdogo na bila uzoefu wowote wa kisiasa na uongozi, aliweza kumudu misukosuko yote iliyotokana na sera ya mkoloni ya divide and rule, sera ya mkoloni to suppress dini moja dhidi ya nyingine au makabila Fulani Fulani dhidi ya mengine, na pia disruption zilizokuja baada ya mkoloni kuanzisha chama chake cha Siasa kama njia ya kuidhibiti TANU – Chama Cha UTP (United Tanganyika Party), ambacho kilifanya kila jitihada kuhakikisha kwamba TANU as a political movement hakigeuki kuwa chama cha Siasa;

Kwa kufanya haya, tutakuwa tunatendea haki historia ya nchi yetu na pia kuimarisha mshikamano wetu kama taifa, hasa kwa kutazama tunapoenda kuliko kujikita katika siasa za kujadili dini zetu, makabila yetu, na Ikulu yetu.

Contradictions kibao.
 
Nadhani sasa ni muda muafaka wa kufanya mathalani tathmini kidogo ya yaliyojiri na ikiwezekana kuwawezesha wengi wanaofuatillia huu mjadala kutafakari yaliyojitokeza na kujiuliza maswali kadhaa. Mengi ya haya maswali ni yale ambayo ninaamini majibu yake hayapatikani kirahisi ndani ya vitabu alivyoviandika Mohamed Said kuhusiana na harakati za kudai uhuru wa Tanganyika. Hata hivyo nina ombi moja tu kwamba kuanzia sasa kama kuna hoja ama ufafanuzi unatakiwa kutolewa, utolewe kwa njia inayokubalika kwa lengo la kuelimishana lakini kama mtu hana hoja au jibu sahihi ingefaa sana akibakia msomaji tu.

Wanajamvi naomba kwanza tujaribu kujizuia na majibu ya dhihaka na kejeli tuweze angalau kudumisha amani, upendo, undugu na utanzania ambao tumejivunia kwa miaka mingi bila kubaguana kwa misingi aliyotuwekea Baba wa Taifa. Na pili naomba mimi niwe wa kwanza kumuuliza Mohamed Said maswali mawili matatu ambayo yanaleta utata katika maandiko yake ambayo, kama anavyodai ameyafanyia utafiti wa muda mrefu, sidhani kama atashindwa kuyajibu kwa ufasaha.. Mohamed Said, maswali yangu kwako ni haya;

  1. Baada ya TANU kuasisiwa, viongozi wake wengine wa juu, pasi Mwalimu Nyerere aliyechaguliwa kwa kishindo kuwa Raisi wake wa Kwanza, walikuwa ni akina nani, walipatikanaje (kuteuliwa au kupigiwa kura?) na kwa sifa zipi? Hapa nina maana ya Makamu Raisi, Katibu na msaidizi wake, Katibu Mwenezi kama alikuwapo, Mweka Hazina n.k Hapo naongelea iliyokuwa kama kamati kuu ya TANU baada ya kuzinduliwa kama iliwahi kuwepo.
  2. Kama viongozi hawa waliteuliwa, ni nani aliyewateua na kwa kuzingatia nini. Je, katiba ya TANU ilikuwa inasemaje na je ilifuatwa katika kuwateua?
  3. Kama viongozi hawa walichaguliwa, walipendekezwa na nani waweze kupigiwa kura? Je hawa wajumbe waliowachagua walipatikanaje? Je majina yao yanaweza kuwekwa wazi kwa wanaofuatilia mjadala huu?
  4. Imedaiwa na Mohamed Said kuwa TANU ilivyozidi kupanuka na kuenea sehemu mbali mbali, idadi ya viongozi Wakristo iliongezeka kwa kasi na kuanza kuwatia shaka wenzao wa Kiislaam...je hawa viongozi walipatikanaje? Je waliteuliwa au walichaguliwa kwa kupigiwa kura?... vyovyote vile je katiba ya TANU ilifuatwa?
Wanajamvi naamini haya maswali ya mwanzo ni muhimu sana katika kuangalia, kutafakari na kujiridhisha na timeline kuhusu baadhi ya Watanganyika walioshiriki karika harakati za kudai uhuru kutokuwa na imani na uongozi wa Mwalimu kabla ya uhuru. Baadaye tutaingia kwenye awamu ya pili nayo ni baada ya uhuru...kitu gani kilileta kutokuaminiana?

cc. sweke 34, Ritz, Nguruvi3, zomba, Mwanakijiji, Boko haram, Saint Ivuga, Ngekewa, Sideeq, Barubaru, Mohamed Said, Abdulhalim, Ngongo, Tuko, Pasco, AshaDii, Kibunango, Tume ya Katiba, masopakyindi, Dingswayo, BAK, matumbo, jmushi1, Son of Alaska, mdizi, Joka Kuu, Campanero, Yericko Nyerere, Spike Lee, Jasusi, warioba E.W., Remote, Nanren, Do santos, Raia Fulani, Wimana, Birigita, THE BIG SHOW, WildCard, njiwa, Mwita Maranya, Rutashobolwa, Mchambuzi, kichwakigumu, adolay, Kituko, deadteja, Fundi Mchundo, Bukyanagandi, Mungi, Mingoi

Mag3,

Ni muhimu ikatambulika kwamba TAA ilizaliwa miaka zaidi ya 20 kabla ya TANU, wakatu huo Mwalimu akiwa hata hajabalee. Ni baadae sana ndio Mwalimu akaanza mahusiano na TAA, hasa baada ya viongozi wa TAA kumwona Nyerere kama ni mtu makini na mwenye ushawishi mkubwa katika suala zima la kudai uhuru wa Tanganyika. Hivyo viongozi wa TAA na Mwalimu wakaona kwamba wakishirikiana, kila upande utapata kile walichokuwa wanakitafuta.

Ikumbukwe pia kwamba TAA hakikuwa chama cha Siasa bali a Social Movement iliyokuwa ikipigania haki mbalimbali za watanganyika wakati wa Ukoloni. Umakini wa Mwalimu, hasa uliotokana na uwezo wake mkubwa wa kuunganisha watanganyika bila kujali dini, makabila na jinsia zao, uliwavutia sana viongozi wa TAA na ndipo wakakubali kufanya kazi na Mwalimu. Kila upande ukaleta assets zake muhimu mezani – kwa upande mmoja, Mwalimu akaleta his leadership abilities, Vision, Upeo wa kidunia kutokana na elimu yake Uingereza, Uwezo wa kujieleza, na uwezo wa kuunganisha watanganyika wa dini na makabila mbalimbali. Kwa upande mwingine, TAA nayo ikaleta uzoefu wake wa miaka zaidi ya 20 ya harakati za kudai haki na maslahi ya watu weusi na pia its large territorial base within Tanganyika chini ya wale viongozi kumi na sita ambao walikuwa ni wawakilishi wa TAA katika majimbo mbalimbali Tanganyika. Nyereer alikuja kuongezeka na kuwa mjumbe wa 17 katika mkutano mkuu wa TAA wa mwaka 1954 ambao ndio uliozaa TANU, lakini bado kama a political movement, sio chama cha Siasa.

Kuna mambo makuu matatu ya kuzingatia hapa: Kwanza ni muhimu tufahamu kwamba Nyerere alichaguliwa kuwa Rais wa kwanza wa TANU – TANU ikiwa as a Political Movement, sio Chama cha Siasa kwani ingawa TANU ilizaliwa mwaka 1954, bado hakikuwa Chama cha Siasa. TANU ilisajiliwa rasmi kama Chama Cha Siasa muda mfupi kabla ya Uhuru. Kwahiyo kuhoji jinsi gani Mwalimu alichaguliwa kuwa Rais wa kwanza wa TANU ni kuhoji mchakato jinsi gani VUGUVUGU LA KISIASA linajipatia viongozi wake, hivyo mjadala wa namna hiyo hauna manufaa yoyote kwetu.

Jambo la pili la kuzingatia ni kwamba – TAA kama a social movement kwa miaka zaidi ya 20 kabla ya kubadilika kuwa TANU, kilikuwa ni chombo chenye organizational culture yake, Siasa zake, makundi yake n.k, ambayo TANU ilikuja kuyarithi yote mwaka 1954. Katika hali hii, watu makini wanatakiwa kujikita zaidi katika kujadili jinsi gani Mwalimu Nyerere katika umri wa wakw mdogo na bila uzoefu wowote wa kisiasa na uongozi, aliweza kumudu misukosuko yote iliyotokana na sera ya mkoloni ya divide and rule, sera ya mkoloni to suppress dini moja dhidi ya nyingine au makabila Fulani Fulani dhidi ya mengine, na pia disruption zilizokuja baada ya mkoloni kuanzisha chama chake cha Siasa kama njia ya kuidhibiti TANU – Chama Cha UTP (United Tanganyika Party), ambacho kilifanya kila jitihada kuhakikisha kwamba TANU as a political movement hakigeuki kuwa chama cha Siasa;

Kwa kufanya haya, tutakuwa tunatendea haki historia ya nchi yetu na pia kuimarisha mshikamano wetu kama taifa, hasa kwa kutazama tunapoenda kuliko kujikita katika siasa za kujadili dini zetu, makabila yetu, na Ikulu yetu.
 
Kama hayo yatafanywa kwa uadilifu mkubwa basi mtapata historia iliyojitosheleza. Tuombe heir
 
Funga domo lako we mjinga, kwanini humuulizi Ritz aliyelileta hilo!

Kama Ritz kaja kusema ovyo kuhusu Madrasa upo sahihi. La kama si hivyo msome Confucius. Anasema "A fool despises good counsel, but a wise man takes it to heart."
 
Last edited by a moderator:
Contradictions kibao.

Haujui historia ya nchi yako, bali utawala wenye maslahi yako, hilo ndio tatizo; ni aibu kwamba hauelewi TANU na TAA vyote havikuanza kama vyama vya siasa bali social movement (TAA), Political Movement (TANU); vinginevyo kuhusu jinsi gani na kwanini Mwalimu na TAA walikuja anza ushirikiano, hata kwa mtoto wa darasa la kwanza lazima atagundua kwamba hii ilitokana na ukweli kwamba Nyerere was a unique character katika mazingira ya wakati ule,

na baadae ilikuja bainika hivyo kwamba he was unique sio kwa Tanganyika tu bali dunia ya tatu kwa ujumla; vinginevyo uliyo highlight hapo juu kwamba ni contradictions, ni dhahiri kwamba hauna uthubutu wa kupambana na mimi kwa hoja, hauwezi jadiliana na mimi, wewe sio kiwango changu, kiwango chako ni cha kutetea madudu ya CCM ya awamu ya nne;
 
Wewe kinakushinda nini kuandika hayo ya waze wako wa kipagani aliyoyawacha Mohamed Said? mbona hukuuliza kwanini kitabu cha kivukoni kiliwaacha wote? mwenzako aliona wazee wake wapigania Uhuru hawakutajwa na kitabu cha kivukoni akaanza kuandika chake, wewe jee? hebu tueleze mzee wako yupi wakipagani alimweka nyerere nyumbani kwake? mzee wako yupi wa kipagani alimpelekea resheni nyerere nyumbani kwake? mzee wako yupi wa kipagani alikuwa akimpa lifti nyerere kumpeleka pugu? mzee wako yupi wa kipagani alikwenda kuchukuwa michango tanga ya kuchangia safari ya nyerere? mzee wako yupi wa kipagani alikuwa kwenye AA, TAA, TANU ambae kivukoni walimtaja na Mohamed Said hakumtaja?

Au hilo kundi la wazee wako walikuwa wakitambika tu?
Historia kiboko sana hii. Mzee Mohamed hakuandika ni wapi Mwalimu alikuwa anajisaidia akibanwa na haja kubwa au ndogo!
 
Back
Top Bottom