Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Mchambuzi ! Nyerere hakuwa unique,bali alikuwa dhaifu kama ulivyoonyesha!

Waingereza walilijua hili na yeye mwenyewe alilijua ndio maana walimpatia "personal assistant" kabla ya uhuru ambaye nyerere alidumu naye mpaka kufa kwake.

Kama watafiti watajikita katika hili la nyerere na personal assistant wake,connection il iyotumika kumfanya nyerere akubali kupokeam msaidizi aliyepewa na Waingereza hao hao aliokuwa akisuguana nao basi nafikiri kuna vitu "vipya"
vitakavyogundulika.
 
Mjadala wa kujibu swali lako ni dhahiri utakuwa ni wa kisiasa zaidi; nafahamu kwanini africanization ilikuwa ni kipaumbele cha mwalimu, lakini kwanini usitoe mawazo yako juu ya hili kwanza kisha tujadili, kwani kwa jinsi ulivyowasilisha hoja hii, una mengi ya kujadili, vinginevyo ingekuwa kama swali ambalo ritz aliniuliza kwenye bandiko lake huko juu, ningeanza mimi kujibu; Tafadhali nipe mawazo yako katika hili ili tujenge mjadala mzuri;
Mchambuzi. Unajua suala hili nimelitoa kutokana na maandiko yako pale ulipobainisha TAA na TANU na kusema bayana kuwa Nyerere ndie aliyabadilisha mwelekeo wa TANU. Kuna mengi ya kujifunza kutokana na historia ya Tanganyika lakin kikubwa ni vipaumbele tu. Lakin wengi tunapenda kujifunza mengi mengi yaliyosahaulika na kuachwa kiasi cha kufundishwa vitu potovu kama waarabu ndio walioleta biashara ya Utumwa wakti uarabuni hakuna watumwa kutoka Africa bali wengi wapo huko kwa wazungu. Nafikiri nawe una nafasi kubwa ya kuelimisha jamii yote msingi mkubwa uweke reference zako ili wasomi tuchambue ukweli na usahihi wako. Ninalokuhasa kama utaingia USHABIKI wa kumtetea au vingine kuhusu Nyerere bila ushahidi hautafika mbali kwani wasomi tunaamini UTAFITI unajibiwa kwa UTAFITI na sio porojo.
 
kichwakigumu said:
Wapi umepata orodha hii ya wanachama wa mwanzo wa TANU ili nasisi tukaitafute na kujua zaidi kuhusu TANU?

Kuna vitabu vingi sana vimeandika historia ya TANU, kwa mfano the critical phase in Tanzania 1945 - 1968 by cranford Pratt; Lakini vingi ni vya zamani sana, ni ngumu kuvipata mpaka ubahatike kuvikuta kwenye bookshops za old books ambazo zipo in many european countries; tembelea any used book store utakutana na vitabu vingi sana vya historia ya Tanganyika na Afrika, na vitabu hivi vya zamani ni vizuri zaidi kwani viliandika historia as it happened, sio vya sasa vya kupindishwa pindishwa kwa malengo ya kisiasa au kukidhi matakwa ya AID community;
 
Ritz,
swali lako kuhusu majina ya waasisi wa TANU na pia wanachama 20 wa kwanza wa TANU per post number 2971, majibu yangu ni kama ifuatavyo:


  1. J.K Nyerere  territorial president
  2. Germano Pacha  kanda ya magharibi
  3. Kirilo Japhet  Kanda ya Kaskazini
  4. Joseph Kimalando  Kanda ya Kaskazini
  5. C. Milinga  Kanda ya mashariki
  6. A . Iranga  Kanda ya Ziwa
  7. L. Bagohe  Kanda ya Ziwa
  8. S. Kandoro  Kanda ya Ziwa
  9. Kisungutwa Gabara  Kanda ya Ziwa
  10. S. Kitwana  Kanda ya Ziwa
  11. Tewa Said Tewa  Kanda ya Mashariki
  12. D. Azizi  Kanda ya Mashariki
  13. A. W Sykes  Kanda ya Mashariki
  14. A. K. Sykes  Kanda ya mashariki
  15. G Kunambi  Kanda ya Mashariki
  16. J Kasessa  Kanda ya Mashariki
  17. John Rupia  Kanda ya Mashariki.

Hawa ndio walikuwa ni waasisi wa TANU kwa mujibu wa historia ya taifa letu, wajumbe wa mkutano mkuu wa TAA 1954 uliozaa TANU, na wanachama kumi na saba wa kwanza wa TANU; Wengine waliofuatia katika kundi hili ni pamoja na Paul Bomani na wengine ambao wengi wao waliunda baraza la kwanza la mawaziri la serikali ya TANU;

Wanachama wengine wengi walifuatia baadae lakini wa mwanzo walitokea Dar-es-salaam, Tabora, Tarime, Singida na Mara Kaskazini. Sina majina yao.

Mchambuzi,

Hapa ndiyd watu wanapoachana kwenye hii historia nimekuuliza makusudi ili swali kwenye wanachama 20 mwanzo unawatoa hawa.

1) Bibi Titi

2) Suleiman Takadir

3) Idd Faiz Mafongo

4) Idd Tosiri

4) Rashid Heri Baghdelleh

5) Zuberi Mtemvu

6) Rashid Kawawa

7) Dustan Omar

8) Mzee Bin Sudi

9) Jumbe Tambaza

10) Rajabu Diwani

11) Makisi Mbwana

12) Haidari Mwinyimvua

13) Mshando Planan

Na wengine wengi kati ya hawa wote hakuna hata muasisi mmoja wa TANU.
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi. Unajua suala hili nimelitoa kutokana na maandiko yako pale ulipobainisha TAA na TANU na kusema bayana kuwa Nyerere ndie aliyabadilisha mwelekeo wa TANU. Kuna mengi ya kujifunza kutokana na historia ya Tanganyika lakin kikubwa ni vipaumbele tu. Lakin wengi tunapenda kujifunza mengi mengi yaliyosahaulika na kuachwa kiasi cha kufundishwa vitu potovu kama waarabu ndio walioleta biashara ya Utumwa wakti uarabuni hakuna watumwa kutoka Africa bali wengi wapo huko kwa wazungu.

Hii kauli ndugu barubaru haipendezi, sana sana itazaa malumbano ambayo hayana tija kwa taifa letu; ni vizuri ukawa unatumia busara japo kidogo tu kuachana na maneno kama haya kwani hayatujengi, bali yanatubomoa, unless wewe sio mwenzetu;

Nafikiri nawe una nafasi kubwa ya kuelimisha jamii yote msingi mkubwa uweke reference zako ili wasomi tuchambue ukweli na usahihi wako. Ninalokuhasa kama utaingia USHABIKI wa kumtetea au vingine kuhusu Nyerere bila ushahidi hautafika mbali kwani wasomi tunaamini UTAFITI unajibiwa kwa UTAFITI na sio porojo.
nashukuru kwa mtazamo wako juu yangu katika hili; mimi sio mwalimu au msomi bali ni mtu anayependa kujisomea, kitu ambacho watanzanai wengi ni wavivu kukifanya, yet ni mahodari wa kurukia mijadala na kutaka hoja zao zisikilizwe; vinginevyo ninazo reference katika masuala ninayojadili, siamki tu asubuhi na kuja kwenye mijadala humu;

Nikirejea kwenye swali lako kuhusu africanization - unalenga kufahamu nini hasa, na so far, ufahamu wako juu ya hili ni upi?
 
Kuna vitabu vingi sana vimeandika historia ya TANU, kwa mfano the critical phase in Tanzania 1945 - 1968 by cranford Pratt; Lakini vingi ni vya zamani sana, ni ngumu kuvipata mpaka ubahatike kuvikuta kwenye bookshops za old books ambazo zipo in many european countries; tembelea any used book store utakutana na vitabu vingi sana vya historia ya Tanganyika na Afrika, na vitabu hivi vya zamani ni vizuri zaidi kwani viliandika historia as it happened, sio vya sasa vya kupindishwa pindishwa kwa malengo ya kisiasa au kukidhi matakwa ya AID community;

Shukran kaka kwa jibu lako

Naomba niulize tena,

Katika hao uliowataja, unaweza kutupa nyadhifa zao katika chama cha TANU? Meaning who had what responsibilities within the party

Natanguliza shukran zangu
 
Sasa jamani, Ngongo katoa wazo tuchunge kauli zetu, anakuja mtu anasema maneno kama haya

Ngongo, au huyu anautendea haki jamvi hili?
Mkuu,njoo tu kwa ID yako original....lakini nakuhakikishia hii misheni yako utashinda nje ya Jf lakini huwezi shinda ndani ya JF kwani JF kuna vichwa makini
 
Ritz,
swali lako kuhusu majina ya waasisi wa TANU na pia wanachama 20 wa kwanza wa TANU per post number 2971, majibu yangu ni kama ifuatavyo:


  1. J.K Nyerere – territorial president
  2. Germano Pacha – kanda ya magharibi
  3. Kirilo Japhet – Kanda ya Kaskazini
  4. Joseph Kimalando – Kanda ya Kaskazini
  5. C. Milinga – Kanda ya mashariki
  6. A . Iranga – Kanda ya Ziwa
  7. L. Bagohe – Kanda ya Ziwa
  8. S. Kandoro – Kanda ya Ziwa
  9. Kisungutwa Gabara – Kanda ya Ziwa
  10. S. Kitwana – Kanda ya Ziwa
  11. Tewa Said Tewa – Kanda ya Mashariki
  12. D. Azizi – Kanda ya Mashariki
  13. A. W Sykes – Kanda ya Mashariki
  14. A. K. Sykes – Kanda ya mashariki
  15. G Kunambi – Kanda ya Mashariki
  16. J Kasessa – Kanda ya Mashariki
  17. John Rupia – Kanda ya Mashariki.

Hawa ndio walikuwa ni waasisi wa TANU kwa mujibu wa historia ya taifa letu, wajumbe wa mkutano mkuu wa TAA 1954 uliozaa TANU, na wanachama kumi na saba wa kwanza wa TANU; Wengine waliofuatia katika kundi hili ni pamoja na Paul Bomani na wengine ambao wengi wao waliunda baraza la kwanza la mawaziri la serikali ya TANU;

Wanachama wengine wengi walifuatia baadae lakini wa mwanzo walitokea Dar-es-salaam, Tabora, Tarime, Singida na Mara Kaskazini. Sina majina yao.

Nilisema, anatuletea historia ya kivukoni.

Bado u mdogo hujakomaa lakini tutakufunda majina yao taratibu taratibu, wenzako walikuja hivyohivyo. Anza na huyu:

Naam kumekucha.

Sheikh Suleiman Takadir (Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU Makao Makuu, New Street Dar es Salaam) alikuwa akipanda jukwaani pale Mnazi Mmoja siku za mwanzo za TANU alikuwa anaanza na kibwagizo hiki: "Kwaaaacha!" (yaani kumekucha) na wananchi wana TANU wakijibu kwa pamoja: "Kweupeeee." Kisha anasoma dua halafu anamkaribisha Mwalimu Nyerere kuhutubia.

Yote haya utayapata katika kitabu hicho.

Hakika kumekucha.
 
Mchambuzi,

Hapo ndipo watu tunapoachana kwenye hii historia nimekuuliza makusudi ilo swali kwenye wanachama 20 mwanzo unawato hawa.

1) Bibi Titi

2) Suleiman Takadir

3) Idd Faiz Mafongo

4) Idd Tosiri

4) Rashid Heri Baghdelleh

5) Zuberi Mtemvu

6) Rashid Kawawa

7) Dustan Omar

8) Mzee Bin Sudi

9) Jumbe Tambaza

10) Rajabu Diwani

11) Makisi Mbwana

12) Haidari Mwinyimvua

13) Mshando Planan

Na wengine wengi hawa wote hakuna hata muasisi mmoja wa TANU.

kwani kuwa muasisi maana yake nini? Waasisi wa CCM 1977 ni kina nani? au Waasisi wa Chadema 1995 ni kina nani? Sio kila mwanachama lazima awe ni muasisi; Katika siasa za vyama, kuna Founding Members and Early Recruits;
 
Unamaana gani unaposema "kila kiumbe anazaliwa Muislam". Hata nguruwe anazaliwa hivyo?

Hata nguruwe ni kiumbe hata wewe ni kiumbe ambae pia nimeharamishiwa kukula au wewe ni halali kuliwa?

Umeshajiuiza kabla ya kubatizwa ulikuwa dini gani? au na nguruwe umeshambatiza?
 
Nimesoma kwa umakini sana kuhusu hoja za Yericko Nyerere na Mohamed said nimegundua huyu Mohamed anasukumwa na Udini na hata mashabiki wake wameshindwa kuja na ushahidi wa wanayoyasimamia. Kuna maswali ameulizwa hapo nyuma ameshindwa kuyajibu kabisa na hata hoja za kisomi zaidi toka kwa Mchambuzi ameshindwa kuzijibu. kwa hiyo naona ni mchochezi tu wa makusudi katika kitabu chake.
Ahsante kama na wewe umeliona hilo...lakini leo hapa atoki' mimi kuna watu wangu humu nawaaminia kwa nondo zenye hoja mzito hakika watamkimbiza tu.
 
kwani kuwa muasisi maana yake nini? Waasisi wa CCM 1977 ni kina nani? au Waasisi wa Chadema 1995 ni kina nani? Sio kila mwanachama lazima awe ni muasisi; Katika siasa za vyama, kuna Founding Members and Early Recruits;

Tatizo hujui maana ya kuasisi, na hujui maana ya founding members, Jee, unajuwa kuwa TANU iliasisiwa Burma?
 
Nilisema, anatuletea historia ya kivukoni.

Bado u mdogo hujakomaa lakini tutakufunda majina yao taratibu taratibu, wenzako walikuja hivyohivyo. Anza na huyu:
Bora mimi ambae kama sijui kitu naweka wazi kuliko wewe kujifanya mjuaji, na hivyo ndivyo mna angamiza taifa letu kiuongozi; Vinginevyo nashukuru kufahamu majina husika, kwani pamoja na wewe kuyafahamu na mimi kutoyafahamu, kuna mengine mengi kuhusiana na majina hayo ambayo wewe huyajui na kuna mwingine humu au kwenye jamii anajua;

Baada ya kuyajua majina hayo, nini kinafuata sasa - hoja yako katika ujenzi wa taifa letu ni nini sasa;

Pia natumaini nimekupa elimu tosha kuhusu tofauti ya vyama vya siasa na vuguvugu la kisiasa kwani majina hayo ni kitu unaweza kuhadithiwa hata kibarazani na babu au bibi mkiwa mmeketi kwenye mkeka, lakini masuala mengine bila ya uchambuzi unaoendana na bidii ya kujielimisha, utatoka mtupu;
 
Mchambuzi, Hapa ndiyd watu wanapoachana kwenye hii historia nimekuuliza makusudi ili swali kwenye wanachama 20 mwanzo unawatoa hawa. 1) Bibi Titi 2) Suleiman Takadir 3) Idd Faiz Mafongo 4) Idd Tosiri 4) Rashid Heri Baghdelleh 5) Zuberi Mtemvu 6) Rashid Kawawa 7) Dustan Omar 8) Mzee Bin Sudi 9) Jumbe Tambaza 10) Rajabu Diwani 11) Makisi Mbwana 12) Haidari Mwinyimvua 13) Mshando Planan Na wengine wengi kati ya hawa wote hakuna hata muasisi mmoja wa TANU.
Ritz, Hapa ndio siku zote ninapoona kuwa tanganyika kuna historia mbili za Uhuru wake. Kwani watu maarufu kama Bibi TITI ambaye amepewaa mpaka mtaa mkubwa katikati ya Dar hayumo kabisa katika waasisi wa TANU, Achilia mbali akina KAwawa, Sheikh takadir, Jumbe tambaza na wengineo. Sijui Mchambuzi unaweza kutueleza nini kuhusu hawa. J e walipandika Train la TANU njiani na hawakuanzia mwanzo?
 
Last edited by a moderator:
Hoja yangu ya msingi katika hili ni kwamba TAA ilizaliwa katika kipindi ambacho Mwalimu alikuwa na umri chini ya miaka kumi; Ni baada ya Mwalimu kusoma vizuri, kwenda nje kupata exposure n.k ndio akaanza interest na siasa; Awali Mwalimu hakuwa ana operate kitaasisi, bali as an individual hasa kwa kushirikiana na young elites wa wakati ule katika vikao vyao vya kahawa na kashata; Baadae ilipohitajika nguvu zaidi and more organized efforts, wazo la TAA ndio likazaliwa, na consensus ikafikiwa kwamba there was no need to reinvent the wheel kwani tayari TAA ilikuwa na experience as an organization (ingawa informally) na pia ilikuwa na a huge base throughout the territory; Majadiliano baina ya viongozi wa TAA na mwalimu ikawa kwamba TAA hiyo hiyo itumike lakini igeuzwe kuwa na political orientation; Wakakubaliana kwamba Mwalimu would work on the new constitution which would completely reorient the association's objectives and policy; Walipokubaliana juu ya hilo, ndio Mkutano Mkuu wa TAA Taifa ukaitishwa in early 1954 na ni hapo ndio TANU ikazaliwa to replace TAA, huku orientation ya awali ya TAA ambayo ilikuwa ni mchanganyiko wa social-political-cultural, ikageuzwa kuwa a fully fledged political organization yenye lengo kuu moja - kudai full political independence kutoka kwa mkoloni;
Lakini tunaona katika hotuba ya kuaga nyerere anasema kuwa alitaka kuanzisha chama cha siasa akaambiwa kuwa tayari kuna chama cha (siasa) vipi leo wewe utuambie kuwa TAA hakikuwa chama cha kisiasa?

nyerere asingekubali kuacha kuendelea na uundaji wa chama chake cha kisiasa na kuja kujiunga na chama cha "kitamaduni"
 
Jadili contradictions zangu kwa hoja kwa jinsi ulivyo highlight kwenye bandiko husika hoja moja baada ya nyingine - huku ukitoa mawazo yako mbadala, sijaona bado, sana sana unajichanganya tu;

Hujaona? nilikwamba hutaona kwa sababu hukijui ukisemacho? hata hints nilizokupa umeshindwa kuziona.

Na swali nililokuuliza pia umeshindwa kuliona? ndio wale wale, usiogope, jibu, hapa tutakupa darsa bila papara, taratiiibu, mpaka tutakuonesha hizo "contradictions" , unanikumbuka. Pokea hivi vipande viwili ambavyo unajifanya hujaviona:

Pia nnakuhakikishia nnaijuwa ni nini maana ya "political movement" na nnaijuwa ni nini maana ya "chama cha siasa" vitu ambavyo wewe vimekushinda kuvielezea kwa lugha moja. Kung'ang'ania kuyaongelea hayo mawili kwa lugha tofauti kunaonesha ni jinsi usivyojuwa unachotaka kukisema, kipi cha ajabu hapo hata moja liwe kwa Kiswahili "chama cha siasa" na lingine liwe kwa Kiingereza "political movement"? hakuna ila ni upeo wako tu ulipoishia.

Historia ya nchi yangu ilinifundisha kuwa Waarabu wanakuja kuchukuwa watumwa hapa, lakini leo naona kuwa Mohamed Said ameandika kuna meli ilikuwa ikipeleka watumwa huko Atlantic inaitwa "Jesus", hilo wewe ulifundishwa shuleni kwenu?

Bado huoni?
 
Kaka Mchambuzi,

Wapi umepata orodha hii ya wanachama wa mwanzo wa TANU ili nasisi tukaitafute na kujua zaidi kuhusu TANU?
Mwanzo mliomba orodha...sasa mmepewa orodha na nasasa mnataka ushahidi wa alipoitoa. Na mkionyeshwa hiyo sehemu mtasema tunataka ushahidi mwingine. Kaazi kwelikweeeli
 
Tatizo hujui maana ya kuasisi, na hujui maana ya founding members, Jee, unajuwa kuwa TANU iliasisiwa Burma?

Mwasisi ni mwanzilishi, chama hakiwezi kuwa na waanzilisha elfu kumi, chama kinatokana na juhudi za watu wachache ambao wanakaa pamoja na kuamua kuunda organization husika, kisha baadae kuanza kufanya recruitment; Kwa mujibu wa historia ya nchi yetu, waasisi wa TANU ni hao kumi na saba na mengine nimeshajadili huko juu;

Kuhusu TANU kuasisiwa Burma, huu ni mwendelezo tu wa ujuaji - SO WHAT? Wewe unajua ANC ya Afrika ya kusini iliasisiwa wapi? Au what matters ni mafanikio yake...
 
Bora mimi ambae kama sijui kitu naweka wazi kuliko wewe kujifanya mjuaji, na hivyo ndivyo mna angamiza taifa letu kiuongozi; Vinginevyo nashukuru kufahamu majina husika, kwani pamoja na wewe kuyafahamu na mimi kutoyafahamu, kuna mengine mengi kuhusiana na majina hayo ambayo wewe huyajui na kuna mwingine humu au kwenye jamii anajua; Baada ya kuyajua majina hayo, nini kinafuata sasa - hoja yako katika ujenzi wa taifa letu ni nini sasa; Pia natumaini nimekupa elimu tosha kuhusu tofauti ya vyama vya siasa na vuguvugu la kisiasa kwani majina hayo ni kitu unaweza kuhadithiwa hata kibarazani na babu au bibi mkiwa mmeketi kwenye mkeka, lakini masuala mengine bila ya uchambuzi unaoendana na bidii ya kujielimisha, utatoka mtupu;
Mchambuzi. Mimi nafikiri wa Tanganyika inabidi mkae kitako kuandika historia sahihi kabisa ya vuguvugu la uhuru wenu bila kufanya upendeleo. kama alivyobainisha RITZ ni vizuri kuchukua Historia ya TANU ya kivukoni na ile iliyoandikwa na ambayo sasa inafanyiwa kazi na vyuo vingi ulaya na America iliyoandikwa na Mohamed Said na kuunda jopo la kufanya utafiti kwa kurejea vitabu hivyo viwili na kisha kuandika historia ya kweli kwa faida ya kizazi chenu. Kwani kwa aina yoyote utaona kuna mengi yameachwa na wengi wamesahaulika katika historia zenu.
 
Hata nguruwe ni kiumbe hata wewe ni kiumbe ambae pia nimeharamishiwa kukula au wewe ni halali kuliwa?

Umeshajiuiza kabla ya kubatizwa ulikuwa dini gani? au na nguruwe umeshambatiza?
Wazee tukae kwenye mada husika hayo mengine si mahala pake.
 
Back
Top Bottom