Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

GG,

Mwanakijiji kapwelewa.

Nyambala kanishushia Hansard na akafuatisha na maneno makali
ya kebehi kwa wazee wetu kuwa Tanganyika ilikuwa chini ya udhamini
kwa hiyo hakuna cha Abdu Sykes wala bastola yake nk.nk.

Mimi nikamwekea TAA HQ 1950 Political Subcommittee ya akina Sheikh
Hassan bin Amir na kutiwa Earle Seaton katika TAA kama mwanasheria
asaidie katika masuala ya udhamini wa Tanganyika.

Jamaa kanihamakia.
Soma post yake.

Dullah kawaambia hamtuwezi.

Kinachowauma ni kuwa wazee wetu haya wameyafanya 1950 ndani ya TAA
na Nyerere hayupo.

Unajua wanashindwa kukubali ukweli kuwa ni baada ya Nyerere kutoka UNO
ndipo akaanza kuwika Tanganyika nzima.

Kusema hivi si kumvunjia staha yake bali ni ukweli wa historia ya uhuru na
ukweli wa maisha yake.

MS, nimemsoma pia amesema hakuna cha Kiatu wala nani.
 

Hapa ndio mara nyingi unaonesha jinsi usivyo makini katika kujenga hoja. Hakuna mtu anayetatizika na "Muslim symbols". Unafikiri kuwa sisi ni kama Wamarekani au watu wengi wa magharibi ambao kwao Uislamu ni "dini nyingine".

Unavyozungumza ni kana kwamba sisi wengine wote tunauona Uislamu kama adui au Waislamu kama siyo wenzetu. Hili ni kosa kubwa la kimantiki. HIvi umemuuliza nani humu kujua kuwa anakwaza na alama za Uislamu?

Nyerere kwenda kuombewa na wazee wa Kiislamu iwe Bagamoyo au Mnyamani Tanga yeye akiwa ni Mkatoliki je iwakwaze Wakatoliki? Kwanini? Kinyume chake inawafanya watu wamuone Nyerere kama the most tolerant, inclusive leader we have ever had.

Kwamba kwenye mikutano ya Nyerere wanasoma Qurani na kumuombea dua wazee wa Kiislamu iwe kikwazo? why? Labda useme inakukwaza wewe kuwa Mkristu tena Mkatoliki Nyerere alikubalika hivyo, kupendwa, kulindwa na kuheshimiwa na wazee wako wa Kiislamu kiasi kwamba inakushangaza.

Kitu ambacho hujaweza kukisema yumkini ni kuwa wazee wako hawakupaswa kumkirimu na kumpa heshima na uongozi huyu Mkristu Mkatoliki. Kwa sababu ni "mwingine"!

Wengi wetu hapa unapotusimulia jinsi Waislamu na Wakristu walivyoshirikiana katika kupigania uhuru na kulinda umoja wa kitaifa, udugu na heshima ya Mtanzania tunaona fahari.

Tunawaona wazee wetu wa Kiislamu kutoka Tanga wakisimama dhidi ya baadhi ya wazee wako waliotaka kuleta udini kwenye siasa; tunawaona wazee wa Kiislamu wakisimama na Nyerere kumheshimu na kumpenda. Wengi wao hawakudai lolote zaidi ya kusema na wao wametoa mchango wao.

Hizi unazoiita "alama za Waislamu" ukweli ni kuwa ni alama zetu pia. Hivi leo tukifanya shughuli yoyote siyo kwamba tunawaita watu wa dini mbalimbali wakatoa dua zao kwa mujibu wa imani zao? Tumefanya hivyo toka zamani kwanini tukwaze?

Hivi unajua kama kuna kitu ambacho Watanzania tunaporudi nyumbani kama tukiwa nje (hasa hizi nchi za Magharibi) hakuna kitu kinakufanya ujisikie uko Bongo kama kusikia Muazin anaitisha Swala!

Lakini hizi alama za Uislamu ni nini basi? Kama Wakristu hawakwazi na alama hizi za UIslamu na hakuna Mkristu ninayemjua ambaye amewahi kulalama kwanini watu kama wewe ukwaze na alama za Wakristu katika nchi yako?

Prof. Mazrui alisema vizuri sana na labda ujifunze kwake - huu ni urithi wetu wa pande tatu. Uafrika, Uislamu na Ukristu ni urithi wetu sisi watu wa Afrika ya Mashariki. Mimi binafsi kwa mfano, hadi leo hii kutokana na mazoea yangu ya kukulia na kusoma miongoni mwa Waislamu nyama zote ninazonunua nanunua kwenye duka la Waislamu.

Siyo kwa sababu za kidini bali najua naweza kufikiwa na wageni marafiki zangu Waislamu hivyo sitaki kuwalisha haramu. Na siyo mimi tu wapo Wakristu wengi tu ambao toka zamani wamewaheshimu ndugu zao Waislamu, wamesaidiana, wameoloeana na kuuguzana na kuzikana; wameshirikiana katika furaha na machungu. YOte wameyafanya bila kujali dini zao.

Hadi ulipotokea wewe na siasa zako za utengano, chuki, kisirani na kisasi. Usipoangalia mzee wangu historia itakukumbuka vibaya kweli kwa kushindwa kutumia yale unayojua kuponya taifa lako na badala yake unajitahidi kila kukicha kueneza propaganda za chuki na itikadi ya mfarakano.

Mzee Said simama uhesabiwa katika kujenga taifa letu; tumia historia uijuayo kuwaleta Watanzania pamoja. Usifanye dhulma ile ile kwa Wakristu ambayo unadai Wakristu wameifanya kwa Waislamu. Si msamaha ni bora zaidi kuliko kisasi Quran inafundisha? Mzee Said tafuta upendo zaidi kuliko chuki, umoja kuliko utengano, uponyaji kuliko kujeruhi.

Imeandikwa: ...Wa Bil-Wālidayni 'Iĥsānāan Wa Bidhī Al-Qurbá Wa Al-Yatāmá Wa Al-Masākīni Wa Al-Jāri Dhī Al-Qurbá Wa Al-Jāri Al-Junubi...Surat Al Nisa (Mwanamke) 4:36

Mzee Said watendee wema (hisan) wote hao na majirani zako walio karibu na waliombali. NI mapenzi ya Mungu hayo. Sijui kama una ndugu Wakristu lakini ungekuwa nao ungeelewa hisia zao kutokana na unachokifanya. Umeambiwa uwafanyie wema ndugu zako pia. Haikusema ndugu zako wa dini moja tu.

MM,

Uislam umekamilika.
Nikiwa na chuki nitakuwa nimekwenda kinyume na mafunzo ya Allah.

Isome historia ya uhuru wa Tanganyika ndipo utathamini wema wa
wazee wetu.

Kisha watazame Waislam walilipwa nini?

Allah anawaeleza Waislam katika Qur'an kuwa, ''Msidhulumu na wala
msikubali kudhulumiwa.''

Mimi napigania dhulma iondoke na haki itawale na haya nisemayo humu
nina ushahidi na ndiyo unaona sijapata kujificha nimeingia hapa na jina
langu kamili na haya Insha Allah nitayasema popote bila hofu.
 
MS, nimemsoma pia amesema hakuna cha Kiatu wala nani.

GG,

Hakika lipo tatizo.
Leo Mshume Kiyate mtu karim na muungwana.

Mshume aliyemvisha kilemba Nyerere baada ya
maasi ya jeshi kumtia moyo leo anatukanwa bila
hofu.

Hakika Allah amesema kweli.
 
mmh kweli wee mbaguzi.

yaani hujui kabisa hio ndio miamba na majabai makubwa sana katika kuijenga TANU?

Ama kweli umekosa fadhwila.

Baru,

Mimi msimamo wangu ni kuwa na dhana nzuri na watu ambao wanatoa jeuri.

Moja kwa moja nakwenda mbali katika makuzi kisha naja sasa nasema huenda
anasema asemayo kwa kuwa haijui historiya wa watu hawa.

Nikifika hapa najipa jukumu la kumuelewesha.

Huyu kijana inaelekea hajui kuwa Mshume Kiyate alikuwa mmoja wa wafadhili
wakubwa wa Nyerere na TANU.

Laiti labda historia ya waze hawa ingethaminiwa na ikafahamika huyu asingekuja
na kibri hiki.

Kwa ufupi ni kumuwia radhi na kumueleza.
 
Alhamdulillah kwa Ilmu unayotupatia katika historia hii,,

Mnamo tarehe 9 september 2000,gazeti la majira lilitoa taarifa kuwa halmashauri kuu ya maaskofu ya baraza la kanisa la pentekoste la tanzania(PCT),Walitoa kitabu chao walichokiita "AMANI KATIKA TANZANIA ITALINDWA KWA KUTENGANISHA DINI NA MAMLAKA YA NCHI",
Walitoa tamko rasmi kuwa kwa tanzania kujiunga na shirika la OIC sharti kuwepo na kura za maoni,tamko hili la maaskofu wa kipentekoste lilitanguliwa na lile la maaskofu wa kanisa la KKKT,lililotolewa kitambo kidogo,lenyewe lilikataa kabisa wazo la tanzania kuijunga na OIC,

lile la maaskofu wa KKKT.LILIFUATIWA NA tamko la KADINALI PENGO wa kanisa katoliki,yeye alipendekeza kuwa wazo hili lazima lipelekwe bungeni,kwenye barua yake aliyomuandikia katibu mkuu wa halmashauri ya waislam tarehe 17.12.1999 mh RAIS MKAPA,KUHUSU suala hilo alisema ya kwamba ni serikali ni lazima iwasikilize wasiokuwa waislam wana maoni gani kuhusu hilo..


Sasa tukirud kwenye MEMORANDUM OF UNDERSTANDING YA 1992 BAINA YA SERIKALI NA MAKANISA ya TEC NA CCT NA MASHIRIKA YA DINI ZA NJE PAMOJA NA SERIKALI ZAO,

Kwanini serikali haikuona umuhimu wa kuwauliza wasiokua wakristo kuhus mambo nyeti kama hayo?na badala yale wakachukua tuh jukum lakufanya maamuz ambayo wanayajua wao tena bila hata bunge kuhusishwa??

Pia kama hizo kura za maoni kuhusu OIC zilikuwa na umuhimu,lini serikali iliitisha kura za maoni kuwahoji wasiokuwa wakristo kuhusu uwepo wa UBALOZI WA VATIKAN AMBAYO NI KAMA TAASISI TUH YA KIDINI NA SI NCHI YENYE MAMLAKA NA RAIA WAKE?

Yaliyofichikana na yanayoleta ukakasi ni mengi sana..

Kwa mara nyingine tena, Vatican si taasisi ya kidini. Ni sovereign. Kama ni kuvunja uhusiano na Vatican basi tuvunje uhusiano na Iran na Saudi Arabia ambazo zinatawaliwa kwa misingi ya kidini.
 
Mimi napigania dhulma iondoke na haki itawale na haya nisemayo humu
nina ushahidi na ndiyo unaona sijapata kujificha nimeingia hapa na jina
langu kamili na haya Insha Allah nitayasema popote bila hofu.

Mzee Said, hupiganii dhulma iondoke; unatengeneza dhulma nyingine. Qurani inaenda mbali zaidi kwani haiishi kusema hivyo unadai. Inasema pia: Wa Jazā'u Sayyi'atin Sayyi'atun Mithluhā ۖ Faman `Afā Wa 'Aşlaĥa Fa'ajruhu `Alá Al-Lahi ۚ 'Innahu Lā Yuĥibbu Až-Žālimīna (42:40). Ni bora kupatanisha (suluhu) kuliko kulipiza kisasi. Mzee Said umefanya nini ili kuziletea jumuiya zetu hizi mbili pamoja katika kupatanisha? Ni lini umejaribu kukaa na viongozi wa Kikristu au kuwashawisi mashehe kukaa na viongozi wa Kikristu kuyaangalia madai yako? Ni lini umejaribu kutumia majukwaa unayopata kuzungumza lugha ya suluhu na upatano badala ya lugha ya utengano, kisasi na kupasha moto hisia za watu?

Mzee Said iheshimu dini yako na uwe mkweli kwa taifa lako. Usijitahidi kubomoa jaribu kujenga. Wazee wetu walifanya mema kwa pamoja, walishirikiana kwa umoja, na katika changamoto nyingi wametupatia taifa hili tulilonalo. Kwanini leo mwenzetu unajitahidi kututenganisha kwa kupotosha historia? Kwanini leo mwenzetu unaandika historia ya "Wazalendo Waislamu waliosahaulika" badala ya kuandika juu ya "Wazalendo waliosahaulika"? Of course najua jibu lako - hao wakristu siyo wazee wako! Wewe ulitaka kuandika wazee wako - Waislamu tu.

Mola akusaidie kuona dhulma unayoifanya kwa jina la kupinga dhulma. Mzee Said uondoa uovu kwa wema Qurani inasema: Adfa` Bi-Atī Hiya 'Aĥsanu As-Sayyi'ata ۚ Naĥnu 'A`lamu Bimā Yaşifūna (23:96). Ulipe uovu kwa wema; umeona dhulma mzee Said tuoneshhe katika kutenda mema. Qurani haisemi upinge tu dhulma lakini vile vile utende hisani na wema; kwa ndugu, wazazi, jirani, n.k

Mzee Said ukiona watu wanatumia Uislamu kuchoma makanisa uwe wa kwanza kulaani siyo kutafuta udhuru wa kwanini wamefanya hivyo; ukiona watu wanafanya ubaya kwa jina la Uislamu dhidi ya ndugu zao uwe wa kwanza kukataa uovu uovu huo. Vinginevyo, wewe mwenyewe unaonekana ni sehemu ya kutetea uovu huo na kuuchochea kwa jina la kupinga dhulma. HIyo siyo dini.
 
Kwa mara nyingine tena, Vatican si taasisi ya kidini. Ni sovereign. Kama ni kuvunja uhusiano na Vatican basi tuvunje uhusiano na Iran na Saudi Arabia ambazo zinatawaliwa kwa misingi ya kidini.

Jasusi,

Tanzania ndipo ilipo hapo hivi sasa.
Hakuna anaemtakia kheri mwenzake.

Tunatazamana kwa jicho baya sana.
Inatisha na inasikitisha.
 
Mzee Said, hupiganii dhulma iondoke; unatengeneza dhulma nyingine. Qurani inaenda mbali zaidi kwani haiishi kusema hivyo unadai. Inasema pia: Wa Jazā'u Sayyi'atin Sayyi'atun Mithluhā ۖ Faman `Afā Wa 'Aşlaĥa Fa'ajruhu `Alá Al-Lahi ۚ 'Innahu Lā Yuĥibbu Až-Žālimīna (42:40). Ni bora kupatanisha (suluhu) kuliko kulipiza kisasi. Mzee Said umefanya nini ili kuziletea jumuiya zetu hizi mbili pamoja katika kupatanisha? Ni lini umejaribu kukaa na viongozi wa Kikristu au kuwashawisi mashehe kukaa na viongozi wa Kikristu kuyaangalia madai yako? Ni lini umejaribu kutumia majukwaa unayopata kuzungumza lugha ya suluhu na upatano badala ya lugha ya utengano, kisasi na kupasha moto hisia za watu?

Mzee Said iheshimu dini yako na uwe mkweli kwa taifa lako. Usijitahidi kubomoa jaribu kujenga. Wazee wetu walifanya mema kwa pamoja, walishirikiana kwa umoja, na katika changamoto nyingi wametupatia taifa hili tulilonalo. Kwanini leo mwenzetu unajitahidi kututenganisha kwa kupotosha historia? Kwanini leo mwenzetu unaandika historia ya "Wazalendo Waislamu waliosahaulika" badala ya kuandika juu ya "Wazalendo waliosahaulika"? Of course najua jibu lako - hao wakristu siyo wazee wako! Wewe ulitaka kuandika wazee wako - Waislamu tu.

Mola akusaidie kuona dhulma unayoifanya kwa jina la kupinga dhulma. Mzee Said uondoa uovu kwa wema Qurani inasema: Adfa` Bi-Atī Hiya 'Aĥsanu As-Sayyi'ata ۚ Naĥnu 'A`lamu Bimā Yaşifūna (23:96). Ulipe uovu kwa wema; umeona dhulma mzee Said tuoneshhe katika kutenda mema. Qurani haisemi upinge tu dhulma lakini vile vile utende hisani na wema; kwa ndugu, wazazi, jirani, n.k

Mzee Said ukiona watu wanatumia Uislamu kuchoma makanisa uwe wa kwanza kulaani siyo kutafuta udhuru wa kwanini wamefanya hivyo; ukiona watu wanafanya ubaya kwa jina la Uislamu dhidi ya ndugu zao uwe wa kwanza kukataa uovu uovu huo. Vinginevyo, wewe mwenyewe unaonekana ni sehemu ya kutetea uovu huo na kuuchochea kwa jina la kupinga dhulma. HIyo siyo dini.

MM,

Nitakujibu moja tu.

Muislam akitoka kwenda kuchoma kanisa
huo ni wazimu wake.

Hayo si mafunzo ya Allah wala Mtume wake
SAW.
 
GG,

Mwanakijiji kapwelewa.

Nyambala kanishushia Hansard na akafuatisha na maneno makali ya kebehi kwa wazee wetu kuwa Tanganyika ilikuwa chini ya udhamini kwa hiyo hakuna cha Abdu Sykes wala bastola yake nk.nk.

Mimi nikamwekea TAA HQ 1950 Political Subcommittee ya akina Sheikh Hassan bin Amir na kutiwa Earle Seaton katika TAA kama mwanasheria asaidie katika masuala ya udhamini wa Tanganyika.

Jamaa kanihamakia. Soma post yake.

Dullah kawaambia hamtuwezi. Kinachowauma ni kuwa wazee wetu haya wameyafanya 1950 ndani ya TAA
na Nyerere hayupo.

Unajua wanashindwa kukubali ukweli kuwa ni baada ya Nyerere kutoka UNO ndipo akaanza kuwika Tanganyika nzima.

Kusema hivi si kumvunjia staha yake bali ni ukweli wa historia ya uhuru na ukweli wa maisha yake.

Mzee Saidi hili la hansard najua limekuchoma vilivyo and I know why, ulikuwa hujawahi kuiona miaka yote hii ya kitabu chako ukijiita mtafifiti na mwanahistoria ya Tanganyika ulikuwa hujui kuhusu hii document ambayo ilikuwa ndiyo centre ya huo uhuru. What a joke???????? Kama nilivyosema mwanzo unasumbuliwa na ushindani ("trophy collecting mentallity"). Ni aibu kwa mtu wa nafasi yako badala ya kuleta hoja unaleta viroja nimekushauri hiyo waachie vijana wako.

Ngoja nikukumbushe kidogo tulikotokea ile asubuhi!!!!!!

Nyambala,

Watu kama wewe ni lulu katika JF.

Ila mimi kwa utu uzima wangu nakupa ushauri mdogo na mfupi sana.

Unapokuja na vitu kama hivi (nyaraka za Hansard) usivichafue kwa lugha mbaya.
Sasa nami nakuwekea hali ya mambo yalikuwaje pale TAA Office, New Street, Dar es Salaam:

TAA HQ, Dar es Salaam 1950

''Baada ya kuunda kamati hii (TAA Political Subcommittee), Abdulwahid alianza kuyaandikia matawi ya TAA ili kuyahuisha.

Jambo kubwa lililomkabili Abdulwahid na ile kamati ya siasa ilikuwani hadhi ya Tanganyika kama nchi ya udhamini chini ya Umoja wa Mataifa.

Abdulwahid alimuingiza katika kamati ya siasa Earle Seaton, mwanasheria kutoka Bermuda aliyekuwa akikaa Moshi ili aishauri kamati kuhusu mambo ya sheria ya katiba.

Aidha alitakiwa kuwashauri jinsi ya kuliendea shauri la kutaka Uingereza itoe uhuru ili Tanganyika ijitawale yenyewe kwa kuwa nchi hiyo haikuwa koloni, bali nchi chini ya udhanini wa Umoja wa Mataifa.

Mwaka wa 1948 Baraza la Udhamini la Umoja wa Mataifa tayari lilikuwa limetuma ujumbe wake wa kwanza kuzuru Tanganyika.

Lakini hakuna jambololote la manufaa lilipatikana kutoka kwa ujumbe huo.''

Nyambala mimi nimeona nikuwekee kwanza haya machache tu kukupa hali ilikuwaje katika fikra ya uongozi
wa TAA pale New Street, 1950.

Nitakuongeza pia kuwa Baraza la Udhamini lilipokuja Tanganyika mwaka 1950 aliyetoa maelezo ya TAA alikuwa
Said Chamwenyewe.

Ukipenda nikuwekee vitu zaidi tafadhali usisite kusema.

Nikakujibu, na hoja ikiwa hansard si sawa na kujinukuu!!!!!! Lakini pia nikajibu hoja yako kwa kutoa maandiko yafuatayo nikitegemea utakuwa mtulivu upate darsa, maana wewe umeelezea uwepo wa tukio mimi nimetoa baadhi ya contents

Unayafahamu haya hapa chini????
2mes6za.jpg



30ness1.jpg






Ukajibu kama ifuatavyo:

Nyambala,

Sijapata kuiona hiyo document.

Nitashukuru kama utaiweka yote.

Nakushukuru kwa juhudi hizi zako.

Kumbuka nilikuaga mida ile kuwa naelekea kwa kazi jambo ambalo si la kawaida humu maana it's easy unalog ou tu,

Naenda kwa kazi tuonane bidae.

ukanijibu:

Insha Allah ndugu yangu.
.

Sasa nashangaa hata sijarudi tambo zilishaanza kwa vijana wako, ni ustaarabu wa wapi huuu mzee Saidi, lakini huu ni uthibitisho mwingine kwamba una nia ovu na hivyo basi muda wowote anapotokea mtu kuweka records straight inakughafirisha sana.

Mzee Saidi unatakiwa ufahamu haya nayowakilisha wala si kwa juhudi ni mambo yapo kwa mtu yeyote if you want to know.

Kwa kusaidia tu hayo maandiko yenye ushahidi ni jinsi gani hao jamaa wa TAA wakiongozwa na Abdu Sykes walikuwa hawakujiandaa na hawana umoja zinapatikana kuanzia pg 177 ndani ya kitabu "
Voices from Tanganyika: Great Britian, the United Nations and the Decolonization of a Trust Territory, 1946-1961" by Ulrich Lohrmann. Tafuta hiki kitabu kitakusaidia sana kabla hujaendelea kujiumbua.

The last one kwa faida ya Mkanasha, wanajamvi na vijana wako "Unaweza kututajia wazee waliokuwa na Nyerere kwenye negotiating team na waingereza kuhusu upatikanaji uhuru wa Tanganyika??" Please. Maana hiyo ndiyo hasa ilikuwa nguzo ya kupatikana uhuru Dec 09, 1961. If not basi usipepese sema sijui utapewa darasa.
Inshalah tutaonana panapo majaliwa .


 
Mzee Saidi hili la hansard najua limekuchoma vilivyo and I know why, ulikuwa hujawahi kuiona miaka yote hii ya kitabu chako ukijiita mtafifiti na mwanahistoria ya Tanganyika ulikuwa hujui kuhusu hii document ambayo ilikuwa ndiyo centre ya huo uhuru. What a joke???????? Kama nilivyosema mwanzo unasumbuliwa na ushindani ("trophy collecting mentallity"). Ni aibu kwa mtu wa nafasi yako badala ya kuleta hoja unaleta viroja nimekushauri hiyo waachie vijana wako.

Ngoja nikukumbushe kidogo tulikotokea ile asubuhi!!!!!!



Nikakujibu, na hoja ikiwa hansard si sawa na kujinukuu!!!!!! Lakini pia nikajibu hoja yako kwa kutoa maandiko yafuatayo nikitegemea utakuwa mtulivu upate darsa, maana wewe umeelezea uwepo wa tukio mimi nimetoa baadhi ya contents



Ukajibu kama ifuatavyo:



Kumbuka nilikuaga mida ile kuwa naelekea kwa kazi jambo ambalo si la kawaida humu maana its easy unalog ou tu,



ukanijibu:

.

Sasa nashangaa hata sijarudi tambo zilishaanza kwa vijana wako, ni ustaarabu wa wapi huuu mzee Saidi, lakini huu ni uthibitisho mwingine kwamba una nia ovu na hivyo basi muda wowote anapotokea mtu kuweka records straight inakughafirisha sana.

Mzee Saidi unatakiwa ufahamu haya nayowakilisha wala si kwa juhudi ni mambo yapo kwa mtu yeyote if you want to know.

Kwa kusaidia tu hayo maandiko yenye ushahidi ni jinsi gani hao jamaa wa TAA wakiongozwa na Abdu Sykes walikuwa hawakujiandaa na hawana umoja zinapatikana kuanzia pg 177 ndani ya kitabu "
Voices from Tanganyika: Great Britian, the United Nations and the Decolonization of a Trust Territory, 1946-1961" by Ulrich Lohrmann. Tafuta hiki kitabu kitakusaidia sana kabla hujaendelea kujiumbua.

The last one kwa faida ya Mkanasha, wanajamvi na vijana wako "Unaweza kututajia wazee waliokuwa na Nyerere kwenye negotiating team na waingereza kuhusu upatikanaji uhuru wa Tanganyika??" Please. Maana hiyo ndiyo hasa ilikuwa nguzo ya kupatikana uhuru Dec 09, 1961. If not basi usipepese sema sijui utapewa darasa.
Inshalah tutaonana panapo majaliwa .



Wewe ungekuwa unajua ustaraabu na umefunzwa adabu na wazazi wako wala usingethubutu na kujaribu kumuita Marehemu Mzee Mshume Kiyate, KIATU.
 
Mkuu wangu zumbemkuu unamshangaa Mohamed Said kumlinganisha zomba mzee wa kucopy na kupesti aliyetolewa kamasi na Matola .

Ukweli ni kwamba ukitafuta vichwa vitano vya ukweli hapa JF Mkuu nguruvi yumo.Ngoja niandae list yangu Nguruvi3 Mchambuzi Mzee Mwanakijiji Jasusi Mag3 ....Mpaka hapo Ustadhi Moh na mpiga tarumbeta wake hawajaingia.Nikiandaa list nyingine ya 10 bora bado jina la zomba halitii pua kabisa labda 1000 a itategemea mnajadili nini.

Ukianzishwa mjadala wa kuisifu CCM ya Kikwete zomba anaweka akili kando anakimbilia madata ya kuchongo hata kama hayana uhalisia.Ukiijadili CCM ya Mkapa zomba atamponda ukiijadili CCM ya Mzee Ruksa zomba huyo huyo ataisifu bila kujali kipindi cha Mzee Ruksa MoU iliasisiwa na vurugu za Mwembechai atatupiwa Mrema Mwinyi hausiki kabisa ha ha ha.
Mzee wangu Mo ukifika mahali ukasifu hata visivyosifiwa unapunguza heshima yako ingawa tayari sioni kabisa.



dah!
hii kali ya mwaka. zomba ni zaidi ya Nguruvi3 ????????????????????
 
Last edited by a moderator:

Hapa ndio mara nyingi unaonesha jinsi usivyo makini katika kujenga hoja. Hakuna mtu anayetatizika na "Muslim symbols". Unafikiri kuwa sisi ni kama Wamarekani au watu wengi wa magharibi ambao kwao Uislamu ni "dini nyingine".

Unavyozungumza ni kana kwamba sisi wengine wote tunauona Uislamu kama adui au Waislamu kama siyo wenzetu. Hili ni kosa kubwa la kimantiki. HIvi umemuuliza nani humu kujua kuwa anakwaza na alama za Uislamu?

Nyerere kwenda kuombewa na wazee wa Kiislamu iwe Bagamoyo au Mnyamani Tanga yeye akiwa ni Mkatoliki je iwakwaze Wakatoliki? Kwanini? Kinyume chake inawafanya watu wamuone Nyerere kama the most tolerant, inclusive leader we have ever had.

Kwamba kwenye mikutano ya Nyerere wanasoma Qurani na kumuombea dua wazee wa Kiislamu iwe kikwazo? why? Labda useme inakukwaza wewe kuwa Mkristu tena Mkatoliki Nyerere alikubalika hivyo, kupendwa, kulindwa na kuheshimiwa na wazee wako wa Kiislamu kiasi kwamba inakushangaza.

Kitu ambacho hujaweza kukisema yumkini ni kuwa wazee wako hawakupaswa kumkirimu na kumpa heshima na uongozi huyu Mkristu Mkatoliki. Kwa sababu ni "mwingine"!

Wengi wetu hapa unapotusimulia jinsi Waislamu na Wakristu walivyoshirikiana katika kupigania uhuru na kulinda umoja wa kitaifa, udugu na heshima ya Mtanzania tunaona fahari.

Tunawaona wazee wetu wa Kiislamu kutoka Tanga wakisimama dhidi ya baadhi ya wazee wako waliotaka kuleta udini kwenye siasa; tunawaona wazee wa Kiislamu wakisimama na Nyerere kumheshimu na kumpenda. Wengi wao hawakudai lolote zaidi ya kusema na wao wametoa mchango wao.

Hizi unazoiita "alama za Waislamu" ukweli ni kuwa ni alama zetu pia. Hivi leo tukifanya shughuli yoyote siyo kwamba tunawaita watu wa dini mbalimbali wakatoa dua zao kwa mujibu wa imani zao? Tumefanya hivyo toka zamani kwanini tukwaze?

Hivi unajua kama kuna kitu ambacho Watanzania tunaporudi nyumbani kama tukiwa nje (hasa hizi nchi za Magharibi) hakuna kitu kinakufanya ujisikie uko Bongo kama kusikia Muazin anaitisha Swala!

Lakini hizi alama za Uislamu ni nini basi? Kama Wakristu hawakwazi na alama hizi za UIslamu na hakuna Mkristu ninayemjua ambaye amewahi kulalama kwanini watu kama wewe ukwaze na alama za Wakristu katika nchi yako?

Prof. Mazrui alisema vizuri sana na labda ujifunze kwake - huu ni urithi wetu wa pande tatu. Uafrika, Uislamu na Ukristu ni urithi wetu sisi watu wa Afrika ya Mashariki. Mimi binafsi kwa mfano, hadi leo hii kutokana na mazoea yangu ya kukulia na kusoma miongoni mwa Waislamu nyama zote ninazonunua nanunua kwenye duka la Waislamu.

Siyo kwa sababu za kidini bali najua naweza kufikiwa na wageni marafiki zangu Waislamu hivyo sitaki kuwalisha haramu. Na siyo mimi tu wapo Wakristu wengi tu ambao toka zamani wamewaheshimu ndugu zao Waislamu, wamesaidiana, wameoloeana na kuuguzana na kuzikana; wameshirikiana katika furaha na machungu. YOte wameyafanya bila kujali dini zao.

Hadi ulipotokea wewe na siasa zako za utengano, chuki, kisirani na kisasi. Usipoangalia mzee wangu historia itakukumbuka vibaya kweli kwa kushindwa kutumia yale unayojua kuponya taifa lako na badala yake unajitahidi kila kukicha kueneza propaganda za chuki na itikadi ya mfarakano.

Mzee Said simama uhesabiwa katika kujenga taifa letu; tumia historia uijuayo kuwaleta Watanzania pamoja. Usifanye dhulma ile ile kwa Wakristu ambayo unadai Wakristu wameifanya kwa Waislamu. Si msamaha ni bora zaidi kuliko kisasi Quran inafundisha? Mzee Said tafuta upendo zaidi kuliko chuki, umoja kuliko utengano, uponyaji kuliko kujeruhi.

Imeandikwa: ...Wa Bil-Wālidayni 'Iĥsānāan Wa Bidhī Al-Qurbá Wa Al-Yatāmá Wa Al-Masākīni Wa Al-Jāri Dhī Al-Qurbá Wa Al-Jāri Al-Junubi...Surat Al Nisa (Mwanamke) 4:36

Mzee Said watendee wema (hisan) wote hao na majirani zako walio karibu na waliombali. NI mapenzi ya Mungu hayo. Sijui kama una ndugu Wakristu lakini ungekuwa nao ungeelewa hisia zao kutokana na unachokifanya. Umeambiwa uwafanyie wema ndugu zako pia. Haikusema ndugu zako wa dini moja tu.
Ewe Mwenyezi Mungu uzidi kumjaza Mzee huyu roho ya hekima na maarifa kama ya Nabii Suleimani.Umtembelee Mzee Mohamedi kama ulivyomgusa Sauli.Ninakuomba Baba yetu uliye mbinguni uzidi kuimarisha upendo,mshikamano na amani miongoni mwetu Watanzania.Amina.
 
Kwa mara nyingine tena, Vatican si taasisi ya kidini. Ni sovereign. Kama ni kuvunja uhusiano na Vatican basi tuvunje uhusiano na Iran na Saudi Arabia ambazo zinatawaliwa kwa misingi ya kidini.

Jasusi,

Nipe hoja za kisheria zinazosema kuwa vatican ni nchi? Nimebishana nanyie katika Memorandum of Understanding mmeshindwa kuniletea hoja za msingi nikiwauliza ni hoja gani za msingi zinazoifanya Vatican ambayo hakuna wazawa iitwe nchi? Vile vile ni hoja gani za msingi mnaweza kutuambia tofauti ya Holy See na Vatican ni ipi? Vilevile tuambiwe ni mtoto gani alizaliwa Vatican akakulia vatican akafa vatican. Vyenginevyo tuambieni huo uhusiano wa nchi mmueutoa wapi?
 
Jasusi,

Nipe hoja za kisheria zinazosema kuwa vatican ni nchi?

Nimebishana nanyie katika Memorandum of Understanding mmeshindwa kuniletea hoja za msingi nikiwauliza ni hoja gani za msingi zinazoifanya Vatican ambayo hakuna wazawa iitwe nchi?

Vile vile ni hoja gani za msingi mnaweza kutuambia tofauti ya Holy See na Vatican ni ipi? Vilevile tuambiwe ni mtoto gani alizaliwa Vatican akakulia vatican akafa vatican.

Vyenginevyo tuambieni huo uhusiano wa nchi mmueutoa wapi?


......

Hoja mfu kama hizi unapaswa kupeleka kwenye mihadhara na vijiwe vya kahawa. if you don't mind be friend of Google he will educate you enough than wasting our time.
 
Sio wote, angalau a considerable number, especially wale ambao hawana bagagge ya kulipiza kisasi cha wazee wao kuwekwa dentetion na kufukuzwa na Nyerere kutoka nchini. I take it Mohamed and Njozi represents an extreme element of muslims. I also take that we have moderate muslims in Tanzania. Kwa sababu hii njozi ya Kigoma Malima kuanzisha namba za mitihani imeshakuwa discredited kwa hiyo hii taarifa ya Dear brothers and sisters in Islam si credible.

Nini tofauti kati ya moderat and extreme muslims?
 
Mzee ms,

Kwa story za namna hii mnaweza mkakesha, hakuna anae kuweza.
Sasa tatizo linakuja ukigongwa swali weeeee!!!???....
Unaluka kimanga..... Utasikia mala oooo hiyo ni historia ya wazee wangu, mala na nyie andikeni.
Jalibu uwe unajibu kila swali midhali upo hapa.
Tofauti na hivyo basi tujue tu kuwa una ajenda yako ya sili.

Unajua sisi watani wetu ni wasambaa! bila shaka wewe ni Msambaa bisha nikupe ushahidi!
 
Mkuu Jasusi asante sana kwa kisa hiki cha kusisimua sasa pata picha kama Aikael Mbowe angekuwa mzee wa Gerezani nakwambia Mzee wetu Mohamed Said angemwandika page 20 kuelezea kisa hiki kwa mbwembwe na mashamshamu ya kufa mtu.

.......
Mohamed,

Umemtaja mzee Aikaeli Mbowe. Ngoja nikupe kisa kimoja kumhusu huyu mzee na ulinganishe na malalamiko yako ya Nyerere kuwasahau akina Dosa Aziz wakati alipokuwa Ikulu.

Mzee Mbowe alikuwa na shida sana kukutana na Nyerere kila alipokwenda Dar-es- Salaam. Alitumia kila mbinu, akipiga simu Ikulu kuomba appointment lakini wale wasaidizi wa Mwalimu ambao hawakumjua, walimzuia.

Mzee Mbowe aliamua siku moja kusubiri pale nje ya gate wakati Nyerere anakwenda Ikulu. Nyerere akamwona pale nje, akashuka kwenye gari lake na kumuuliza mbona anasubiri nje.

Akamwelezea shida aliyokuwa nayo kukutana naye. Basi akamshika mkono akaenda naye Ikulu. Akawaambia wale maafisa wake kuwa kuanzia siku hiyo, kama huyo mzee anataka kuonana naye asiwekewe pingamizi.
 
Hoja mfu kama hizi unapaswa kupeleka kwenye mihadhara na vijiwe vya kahawa. if you don't mind be friend of Google he will educate you enough than wasting our time.

If you say Google is your reference my friend you are one of shallowest thinker in JF I have came across with. Google really !!!!! Tell me which act of law? Which ruling? Which international law that states the characteristics that vatican has constitute a sovereign nation!!!! Otherwise mnaishushia hadhi JF ndugu.
 
  • Thanks
Reactions: Ami


Siyo kwa sababu za kidini bali najua naweza kufikiwa na wageni marafiki zangu Waislamu hivyo sitaki kuwalisha haramu.


Ndugu, Mzee M,

Jee, ukiwa hauko ktk maeneo yenye rafiki zako Waislamu huwa unakula haramu?


MM,

Huo ni muhali mkubwa sana.
Siwezi hata kidogo kula haram kwa kuwa nayajua madhara yake.

Haram inaathir hadi fikra na hulka za mlaji.
Kwahiyo kamwe siwezi kuigusa.

Achilia mbali hayo makubwa.

Mathalan nina chakula halal kabisa mfano wa kamba, pweza na majongoo ya pwani.
Kwangu mimi hivi vitoweo na delicacy na ukienda Kempisky bei yake ni kali.

Kuna makabila vyakula vya pwani vinawapa shida na mimi najua leo nimemkaribisha
chakuka sahib wangu ambae vyakula hivi haviwezi basi sitavileta mezani ingawa ni halal.
na yeye anaweza akavikwepa akala kitoweo kingine.

Huu ndiyo ustaarabu waliotufunza wazee wetu na ndiyo Uislam khasa.
Sembuse iwe chakula ni haram vipi nitakula hata nikiwa peke yangu?
 
Back
Top Bottom