Mzee Saidi hili la hansard najua limekuchoma vilivyo and I know why, ulikuwa hujawahi kuiona miaka yote hii ya kitabu chako ukijiita mtafifiti na mwanahistoria ya Tanganyika ulikuwa hujui kuhusu hii document ambayo ilikuwa ndiyo centre ya huo uhuru. What a joke???????? Kama nilivyosema mwanzo unasumbuliwa na ushindani ("trophy collecting mentallity"). Ni aibu kwa mtu wa nafasi yako badala ya kuleta hoja unaleta viroja nimekushauri hiyo waachie vijana wako.
Ngoja nikukumbushe kidogo tulikotokea ile asubuhi!!!!!!
Nikakujibu, na hoja ikiwa hansard si sawa na kujinukuu!!!!!! Lakini pia nikajibu hoja yako kwa kutoa maandiko yafuatayo nikitegemea utakuwa mtulivu upate darsa, maana wewe umeelezea uwepo wa tukio mimi nimetoa baadhi ya contents
Ukajibu kama ifuatavyo:
Kumbuka nilikuaga mida ile kuwa naelekea kwa kazi jambo ambalo si la kawaida humu maana it's easy unalog ou tu,
ukanijibu:
.
Sasa nashangaa hata sijarudi tambo zilishaanza kwa vijana wako, ni ustaarabu wa wapi huuu mzee Saidi, lakini huu ni uthibitisho mwingine kwamba una nia ovu na hivyo basi muda wowote anapotokea mtu kuweka records straight inakughafirisha sana.
Mzee Saidi unatakiwa ufahamu haya nayowakilisha wala si kwa juhudi ni mambo yapo kwa mtu yeyote if you want to know.
Kwa kusaidia tu hayo maandiko yenye ushahidi ni jinsi gani hao jamaa wa TAA wakiongozwa na Abdu Sykes walikuwa hawakujiandaa na hawana umoja zinapatikana kuanzia pg 177 ndani ya kitabu " Voices from Tanganyika: Great Britian, the United Nations and the Decolonization of a Trust Territory, 1946-1961" by Ulrich Lohrmann. Tafuta hiki kitabu kitakusaidia sana kabla hujaendelea kujiumbua.
The last one kwa faida ya Mkanasha, wanajamvi na vijana wako "Unaweza kututajia wazee waliokuwa na Nyerere kwenye negotiating team na waingereza kuhusu upatikanaji uhuru wa Tanganyika??" Please. Maana hiyo ndiyo hasa ilikuwa nguzo ya kupatikana uhuru Dec 09, 1961. If not basi usipepese sema sijui utapewa darasa. Inshalah tutaonana panapo majaliwa .
Nyambala,
Ahsante kwa majibu.
Kinyume unavyodhani ile document uloweka hapa ya Hansard na ya TAA
mimi nimekushukuru.
Nimekushukuru kwa sababu umenisomesha.
Mie sikujua kuwa katika mawasilisho palitokea mgongano wa fikra katika
TAA.
Mimi kichwa changu kiko wazi naichukua elimu popote na ndiyo maana
husema siku zote siko humu kushinda mjadala ila kueleza lile nilijualo.
Hivyo ducument haikuniumiza hata kidogo.
Yote ulosema ya Nyerere na timu yake waloweka tarehe ya uhuru yote
sawa kabisa.
Hakuna anaeweza kubisha haya yote kwa kuwa ni ukweli wa kihistoria.
Mimi nilichofanya na ndiyo kilichotukutanisha hapa JF nimeandika historia ya
wazee wangu waliompokea Nyerere, wakaishinae majumbani mwao.
Wakamkabidhi chama na wakawanae bega kwa bega hadi wakampeleka UNO.
Siku ya kurudi wakampa mapokezi hakuwahi hata kuota au kufikiria kwa mbali
yanawezekana.
Wakatembeanae nchi nzima kuitangaza TANU nk. nk. hadi uhuru ukapatikana.
Katika hawa wazee wengine nikawafahamu vizuri kwa kuwa nafumbua macho
nawaona mtaani wakipita wengine wakija mpaka nyumbani kwetu.
Kwangu mie ni faraja kubwa sana kuwa leo wazee hawa wameingia JF wasikizaji
wakiwa 90,000 and counting wanawazungumza mashujaa hawa wa uhuru wetu
ambao walifutwa kwa makusudi kwa kuhofu kuwa waliokuwa mstari wa mbele na
kusimama kidete dhidi ya ukoloni walikuwa Waislam.
Kwangu mimi huu ni ushindi mkubwa sana.
Yaliyobaki ni matayassar.