Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 51,303
- 40,190
Ritz inabidi sasa tukusaidie wewe kufikiri vizuri ndugu yangu. Nyerere alikuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mwaka 1988 lakini Rais alikuwa ni Ali Hassan Mwinyi na serikali yake. Ukisoma hapa Mohammed Said anasema kuwa uamuzi wa kuondoa gazeti lililokuwa na makala yake ulifanywa na CCM (agizo la Mwenyekiti). Na anasema lilitekelezwa na mtu wa CCM - Kiwanuka na kuwa licha ya Kiwanuka kukusanya makala hizo na kuzichoma moto Kiwanuka huyo huyo aliandika makala kumjibu Mzee Said, sawa. Stori imenoga kwa wanaopenda stori; lakini kwa mtu ambaye chembe za Ubongo zinafanya kazi maswali kadhaa yako wazi:
a. CCM haijawai kuwa na mamlaka ya kuzuia kitabu au andiko bila serikali; yaani serkali inatekeleza mapendekezo ya chama. Kumbuka kuwa kama ilivyokuwa mwaka 1988 ndivyo ilivyo sasa; sheria ya magazeti ya mwaka 1976 ndiyo iliyokuwa ikitumika. MTu pekee ambaye anaruhusiwa kuondoa gazeti au kufungia gazeti ni Waziri wa Habari na mamlaka yake ni ya mwisho (hata mahakamani huwezi kupinga). Sasa, ni Wazirri gani aliyetoa agizo hilo?
b. Tukiachilia hilo la a tujiulize Kiwanuka alikuwa anatekeleza agizo la nani? Kama alikuwa anatekeleza agizo la Nyerere, itabidi ajieleze alipewa na Nyerere wapi? Kama alitekeleza matakwa yake kama afisa mahusiano wa chama je ni lazima Nyerere awe anajua au aliomba baraka? Mtu pekee wa kujibu hili ni Kiwanuka.
c. Lakini kama Kiwanuka alikuwa anatekeleza jambo lililokubaliwa na serikali basi mtu ambaye anapaswa kujua ni Rais Mwinyi ambaye alikuwa kwenye madaraka. JE Mwinyi alitoa agizo hilo? Mtu wa kujibu hili ni Mwinyi, umemsikia Mohammed kaenda kumuuliza?
d. Lakini cha kushangaza na sijui kama umekiona; Mohammed Said huyu huyu anatuambia toleo linalofuatia Kiwanuka aliandika makala kumjibu. Sasa, kama gazeti limepigwa marufuku Tanzania na hakuna wa kulisoma Kiwanuka alikuwa anamuandikia nani?
Naona unakurupuka kujibu mwenzenu Yericko Nyerere kasema mwaka 1988 Nyerere alikuwa hana cheo chochote zaidi ya kwenye familia yake.
Nadhani ingekuwa vyema kama ungemsaidia Yericko siyo mimi.
Mwanakijiji kila siku anandika habari za kuishambulia CCM kuwa ndiyo imeleta ufisadi uoni kama unakuwa unapoteza muda wako badala ya kuishambulia serikali mnawashambulia kina Kinana, Makamba, Mwigulu.