Wanabodi tunasubiri darsa la historia ya Tanganyika.
Ritz, historia ya Tanganyika ilijengwa katika misingi ya lengo fulani kufuatana na Mohamed.
Ni historia hiyo ndiyo inasemwa imeendelezwa hadi kuwa na mfumo Kristo ambao Mohamed hajaweza kusimama kuutetea au kuuleza ni kitu gani.
Wametokea watu na kuuleza mfumo kristo unaotokana na historia na tunajibu vipengele kimoja baada ya kingine.
Nadhani umeona na tutaendelea.
Kama unataraji historia ya Tanganyika ni ile ya majina ya vinyozi nadhani huko utakuwa umekosea.
Historia ya Tanganyika ni zaidi ya Narung'ombe na kipata, ni zaidi ya wacheza mpira na vinyozi.
Tunaendelea kuiangalia historia katika mfumo kristo,hadi sasa vipengele viwili vimejibiwa na kusimama bila kujibiwa.
Kama unadhani watu hawajui historia ya Tanganyika basi Mo asingeambiwa AA si ya Sykes ni ya Matola.
Asingeambiwa ah ah! Nyerere kabla ya kukutana na Sykes alishafika Dar
Kaambiwa Sykes walifisadi nyumba ya chama.
Kaambiwa hadi ticket alizoficha kuzieleza
Na mambo chungu nzima ambayo si rahisi mtu kuyajua kama hana background ya historia.
Labda kama una maanisha wapi vipande vya vitabu vilivyonukuliwa na kuwekwa hapa! Do you mean that?
Tunaiangalia historia kwa ujumla wake na yatokanyo na wala si kwa jicho moja la udini, ugerezani au Unarung'ombe.
Tutaenedlea kufumua vipengele alivyoshangilia Mohamed kama definition ya watoto ilivyoletwa.
Tunamjibu Mo na si vijana wanaojua copy and paste. Tunaendelea na hilo na mwisho utaona linakufa kifo cha sensa 1967.
By the way Mo baada ya kubanwa sawa sawa wiki hii amekimbia na aliporudi kwa dharura alikumbana na hoja ya kumtaka alete source za sensa ya mwaka 1957. Kama hatarudi atakuwa amesalimika akirudi atakutana na hoja.
''Mwacheni mzee wa watu apunzike-JK''