Salaam ndugu yangu Wickama na wengine mnaoshiriki mnakasha huu.Nimekuwanikifuatilia muendelezo wa mnakasha toka ulipo anza mpaka hii leo lengo langu kuu likiwa ni kufyonza ilm tu.
Hakika nimejifunza mengi kwa ukimya wangu lakini kwa hili ulilofafanua ndugu yangu Wickama nimesukumwa name nitoe yangu machache.
Wickama sikumbuki ni lini waislamu wa Tanzania waliachiwa fursa ya kujenga taasisi zao zenye nguvu na mipango thabiti kwa ajili ya kusimamia miradi yao ya maendeleo.kumekuwa na hofu kubwa miongoni mwa watawala kuwaachia huru waislam kupanga na kusimamia mikakati yao ya maendeleo.
Hivi anapokuja mtu na kusema waislamu hawapendi shule anasahau kwamba ni haohao waislamu waliokuwa na wazo la kwanza la kujenga chuo kikuu na shule kila wilaya kupitia EAMWS.Kuna mtu anaikumbuka taasisi ya African Muslim Relief Agency wakati wa Awamu ya tatu walipokuja na mikakati mikubwa ya kujenga mashule yanayoeleweka pamoja na kuajiri walimu waliobobea kutoka sehemu mbalimbali kwa ajili ya kufundisha shule zao,nini kiliwakuta.
Serikali ya Raisi Mkapa ilizuia source of funds zote kwa taasisi hiyo na kumtimua mlezi wake wa IRINGA kwamba ni gaidi.Wakati African Muslim wanapigwa vita upande mwingine mama Rwakatare alipewa all support. Naomba ndugu zangu wa imani nyingine tuelewe kwamba waislam hawaitaji msaada wala kuonewa huruma bali wanachotaka ni kupewa fursa sawa ili waendeshe mambo yao kama ndugu zetu wakristo mlivyo huru. Ahsante na mchana mwema
Ndg Uthman, salaam. Nadhani hutajali kama nikichangia bandiko lako ambalo kiukweli ulimkusudia Wickama.
Kwanza, napenda kukufahamisha kuwa kila atoae hoja basi huchangiwa kwa hoja. Asitokee mtu akakuambia kuwa kwavile wewe umejitambulisha basi utashambuliwa. Hapa hashambuliwi mtu zinashambuliwa hoja kwa mantiki.
Hivyo jisikie huru na wala usighafilike au kutishika na maneno ya wale wanaoamini katika utengano zaidi ya undugu.
Pili, niweke sawa suala la EAMWS. Tumeshaeleza kuwa taasisi hii chimbuko lake ni Pakistan na hapa EA ilianzia Mombasa.
Kwa bahati mbaya taasisi hii ilitumika na masalia ya AMNUT yaliyotoka kuitumia kisiasa zaidi ya kidini.
Ndiyo maana baada ya kufungwa mlezi wake Agakhan amerudi na sasa anajenga vyuo vikuu.
Kitu kimoja unachopaswa kujiuliza ni kuwa kwanini taasisi hii iliazimia kujenga chuo kikuu ili hali kulikuwa hakuna shule za awali, msingi na sekondari kama ilivyo sasa? Kwahiyo hii inatumika kujenga hoja za waislam kutopewa fursa katika mambo yao wakati si kweli.
Si kweli kwasababu taasisi ya Africam relief agency ilikuwepo kabla ya awamu ya Mkapa.
Ilikuwepo wakati wa Mwinyi.Unless unataka kuifungamanisha na Mkapa ukweli unabaki kuwa ilikuwepo kabla yake.
Nadhani unajua kazi zake na jinsi ilivyokuwa ina operate. Nikupe changamoto utueleze nani alikuwa mkuu wa taasisi hii na ilipoondoka iliondolewa kwa sababu zipi.
World Muslim League ya Rukara ilikuwepo. Nadhani umeona jitihada za makusudi za kuua hoja ya WML. Hakuna anayetaka kuizungumzia kwasababu ya madudu yake. Ilifunga virago yenyewe kwasababu za ndani na wala si serikali.
Ikaja taasisi nyingine iliyotaka kujenga chuo cha ufundi kibaha. Nayo ilikumbwa na madhila yale yale ya taasisi zilizotangulia na kuamua kujenga Mbale Uganda. Hata hivyo kuna shule ya WHIPAS pale kibaha ambayo inaendesha shughuli zake bila kikwazo.
Hivi karibuni kuna taasisi imekuja na kujenga misikiti 700 kote nchini. Jambo zuri sana kwani sehemu za ibada ni muhimu kwa waumini. Taasisi hiyo pamoja na misikiti imejenga pia visima na mambo mengine bila kikwazo chochote kile.
Imesimamia miradi yake yenyewe bila kuingiliwa hadi ilipokamilika.
Umeongelea suala la Lwakatare kupewa misaada na kujenga shule. Nadhani pia ungeangalia upande wa pili kuwa pamoja na kujenga misikiti 700 ambalo ni jambo jema, je taasisi hiyo ilizuiwa kujenga shule, hospitali au chuo? Jibu ni hapana.
Ningelikuwa mshauri wa taasisi hii ningewaambiwa kuwa kila msikiti waliojenga pengine ungekuwa na shule jirani au nursery school. Huenda misikiti 700 isingetimia pengine kungekuwa na misikiti 200 na shule 80. Hadi hapo shule hizo zingekuwa nyingi kuliko za Lwakatare tena zikiwa na vumba vya ibada pembeni. Kwa maneno mengine kungekuwa na huduma za jamii pamoja na za kidihi all together.
Hapa ni suala la priority, quality na quantity na inategemea wewe au mimi tunaangaliaje jambo hili kwa kila mmoja kuwa na maoni yake.
Kitu kimoja ninachotaka kukuhakikishia ni kuwa hakuna hujuma katika taasisi hizo bali kuna hujuma ndani ya taasisi. Nimetoa mfano wa WML ambao kwa muda waliokaa nchini hakuna alama ''mark'' unayoweza kusema taasisi ya kimataifa imeacha kwa uhakika.
Uthaman, lazima pia twende mbele na nyuma. Maandeleo ya watu yanatokana na watu wenyewe. Sidhani fikra za kusubiri taasisi za kigeni ni jambo jema. Hivi kwanini waislam ambao wengi wana uwezo katika biashara wawekeze zaidi katika michezo lakini suala la elimu na afya lisubiri taasisi kama African relief agency? Nadhani unafahamu hili vema.
Hapo Tanga ukienda Pangani kuna pori la maekari ambalo ni mali ya waislam. Je, kuna jitihada gani za kuendeleza kwa waislam wenyewe bila kusubiri taasisi ambazo nyingi zinaweza kuwa na masuala mengine?
Nadhani umesema vizuri kuwa waislam hawahitaji msaada bali uwezo wa kujiamulia mambo yao.
Uwezo huo upo sasa wanahitaji uamuzi wa kujitafutia maendeleo. Pale ubungo, kuna shule ni nani amefunga shule hiyo? hakuna! Sasa kwanini watu wasifikiri kuchukua maeneo na kuyaendeleza eti ni mpaka kuje taasisi kutoka nje!
Kuna suala lingine umeligusia la walimu na tuhuma za ugaidi. Ningependa kukukumbusha kuwa Prof Maliki likuja nchi kama mhadhiri wa hesabu. Wakati anatimuliwa alisema serikali ilishachelewa kwasababu amemaliza kazi ya kupanda mbegu.
Mbegu zake ni hizi za akina Mohamed wanaoamini katika chuki hata kama uislam hausemi hivyo.
Wanaoamini katika kutafuta sababu za kufarakanisha umma hata kama ni kinyume cha mafunzo ya uislam.
Kwahiyo si suala la kusema kila atakaye aje tu kufanya anachotaka. Tutakuwa katika wakati mgumu.
Miaka ya nyuma kuna watu kutoka nje walianzisha kanisa la watchtower. Hili lilizuia watu wake kwenda hospitali au shule. Serikali ikalipiga marufuku mara moja. Na hadi sasa tuna watu wanashikiliwa walioingia nchini kama makasisi na mapadre huku wakiwa wauza dawa.
Suala la usalama wetu ni muhimu sana. Hakuna ibada itakayofanyika wala dini itakyoweza kuwa katika utulivu nchi ikiwa matatani. Nadhani uliona Rwanda, sijui nani alikuwa na muda wa kusali wakati risasi zinarindima mgongoni.
Ndivyo ilivyokuwa Bosnia na ndivyo ilivyo Nigeria.
Na mwsiho, naomba sana wakati ukidhani kuwa EAMWS ingekuwa mkombozi, jiulize zile nafasi za IDB kwa waislam peke yao zinatolewa kwa utaratibu gani na je utaratibu huo umelenga kumwendeleza mwislam au baadhi ya waislam.
Sijui kama unajua kuwa zile nafasi zimekuwa na malalmiko sana. Ndivyo zilivyokuwa kazi za ARMA na WML.
Unaweza usione hilo au kuliona kama ni uzushi, muhimu fanya tafiti kidogo utaweza kunielewa.
Na jiulize kwanini Shia, Bohora, Ismailia wanaendelea na shughuli zao kwa ufanisi lakini nje yao kuna matatizo?
Nikushukuru tena kwa kueleza maoni yako na kila mmoja anaheshimu maoni ya mwenzake.
cc. Gombesugu, Mag3, JokaKuu, Jasusi, Mwanakijiji, Ritz, Wickama, Wimana.