Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Ritz

Hawa wote akina Mohamed Said, Dr Ghassany, Ahmed Rajabu na wengine wengi, ni aina ile ile, yani unaweza kuita ni mtu mmoja linapokuja suala la Nyerere, uislamu na ukristu!

Kama nimsomaji mzuri wa machapisho yao wala hutapata kuumiza kichwa,

Wao wanamakovu ya Okello na wengine wanamakovu ya Nyerere!

Hivyo kamwe hawezi kuwa 1 mbele ya haya!

Kama wewe ulivyo kuwa sawa na Nguruvi,Mag3 wote kitu kimoja munachuki na mzee MS na uislamu!
 
gombesugu,

..Casimiro Montero, jasusi wa Kireno, ndiye anayenyooshewa kidole kuhusika na mauaji ya Mondlane.

..sasa kama una taarifa mpya kwamba Mwalimu Nyerere ndiye mhusika basi JF kuna watu wengi very open minded tunaweza kuziangalia kama zina ukweli au la.

..lakini wakati utakapozileta naomba nikuulize: movite ya Nyerere kumuua Mondlane ilikuwa ni nini haswa?

..zaidi, what r u trying to prove here, ukizingatia hoja yako ni Mwalimu kumuua Mondlane, na badala yake kushiriki kumsimika ktk uongozi Samora Machel ambaye alikuwa Maxist??

cc: Jasusi, Nguruvi3, Kudi Shauri, Wickama, Mag3
 
Last edited by a moderator:
Vema sana, inawezekana ulipitiwa lakini hii nilishaileta hapa!

Shushia birauli ya maji mkuu!

Ndani ya Zanzibar Okello alipata umaarufu kwa vijana majabari, ambao wengi katika wao walikuwa ni makuli na wachukuzi w meli zilizoingia na kutoka bandarini Zanzibar, kundi lake hili John Okello lilikutana kwa siri. Okello aliwapa matumaini ya mabadiliko watu wake hawa, wafuasi, ambao wakifanya kazi pamoja kwa muda mrefu, mara nyingine katika mazingira ya hatari, na tayari kufuata amri za kiongozi yeyote ambaye ataweza kuwalipa. Wao walikuwa waasi wanaotafuta makaazi.

Usiku wa tarehe 12 Januari 1964 kundi la watu 300 walikitwaa kisiwa cha Unguja wakiongozwa na mtu asiyekuwa maarufu kipindi hicho, aliyekuwa akiitwa John Okello, John Okello alikuwa akiishi Pemba ambako alitokea Uganda miaka michache tu.

Mchafuko wa kisiasa ulikuwa ukiongezeka ndani ya Zanzibar na Pemba tangu kifo cha Sultani Khalifa katika mwaka 1960. Sultani Khalifa alitawala Zanzibar kwa karibu ya miaka 50, tangu mwaka 1911. Baada ya udanganyifu mkubwa kwa majimbo ya uchaguzi na mseto katika chaguzi kuu mbili za mwaka 1961 vyama vikuu vilishindwa kujipatia wingi wa kura kwa kila kimoja.

Waingereza waliondosha majeshi yao kikiwemo kikosi maalumu cha Kiarishi ambacho kilikuwa kimewekwa karibu na uwanja wa gofu na mpaka wa mji mkongwe mapema mwaka 1963. Wakati mfalme mpya, Jemshid akipandisha bendera ya Taifa huru la Zanzibar tarehe 12 Disemba 1963, aliadhimisha uondokaji wa Gavana wa kiingereza Zanzibar na mwisho wa ukoloni Zanzibar.
Uchaguzi mwingine uliofanyika mwishoni mwa mwaka 1963 ukiipa ushindi mdogo wa kura Muungano wa vyama viwili ZNP na (chama cha kizalendo Zanzibar) na ZPPP (Chama cha watu wa Pemba na Unguja). A.S.P (Chama cha Afro shirazi) kilikuwa kiwe kipo katika Serikali iliyo na chini ya nusu ya wabunge kwa mtindo wa bunge la Kiingereza na Sultani, akiwa kama ni mtawala tu lakini sio mtawala mwenye maamuzi ya mwisho.

Taifa hili la Zanzibar ambalo lilikuwa mwanchana kamili wa Jumuia ya madola na mwanachana mpya wa Umoja wa Mataifa lilidumu kwa siku 33 tu.

Majadiliano makali ya kisiasa na maandamano yalikuwa ni matukio ya kawaida siku hizo. Makundi ya watu yaliyokuwa yakiimba na kusifu majina mbalimbali ya viongozi wa kisiasa, huku yakivuka vizuizi vya barabara vilivyokuwa vikilindwa na askari wa kiingereza. Vikundi mbali mbali vilijadiliana juu ya mambo mbali mbali; mfano Haki dhini ya fursa, Wageni dhidi ya wenyeji wa zamani, Ubepari dhidi ya Ujamaa, Wafanyabiashara dhidi ya wamiliki ardhi, Waunguja dhidi ya Wapemba, Waasia dhidi ya pazia la nyuma la vita baridi na harakati za utaifa na kuondosha ukoloni ambazo zilikuwepo kipindi hiki ndani ya Afrika.

John Okello hakuwa na jawabu ya mambo haya nyeti, lakini alikuwa na kipawa cha kutambua kwamba vikundi hivi vinavyoshindana vinatoa nafasi nzuri kwa mtu wa harakati kama yeye Okello.
Hata hivyo, watu kama mia waliojizatiti wangaliwez kutwaa vituo muhimu vya kienyeji vya habari na kambi za Polisi. Mara tu baada ya vituo vya habari na Kambi za polisi pamoja na silaha kudhibitiwa na John Okelo, Ni nani katika visiwa angeweza kumshinda? Jee, wanasiasa wangeliungana na kumshutumu na kumpinga kwa vitendo vyake visivyo halali? Au kama alivyotaraji, wangeendelea kutoaminiana na kutuhumu kwamba kati yao ndio wanaomuunga mkono? Jee, wasingelitaka kukubaliana na yeye, haraka kabla mwengineo hajafanya hivyo? John Okello alichezesha dadu usiku huo wa mwezi wa Januari.

Viongozi wa A.S.P walifadhaishwa na matendo ya Okello (wengi wao, walikuwa hata hawapo visiwani wakati huo). Walikimbilia haraka kuwaunga mkono waasi. Mamia ya wafuasi wa vyama walipigwa na butwaa juu ya wale ambao walikuwa na shuku ya kukata fundo hilo gumu la majadaliano ya kidemokrasia na kukimbilia moja kwa moja kwenye utawala. Hawawalitafuta njia ya kuiandaa jamii kwenda sambamba na kanuni zao. Kanuni siku hizo zilikuwa ni ghali sana kama sarafu ya Marekani. Ubinadamu ulikuwa ni kitu adimu sana.

Baadhi ya viongozi wa ASP baada kuona kwamba serikali itakuwa haina udhibiti na uwezo kujilinda na kutokuwa na imani matokeo ya chaguzi huria zilizofanyika, viongozi hawalitafuta njia za haraka za kuhalalisha udhibiti yale ambayo yaliitwa sasa "Mapinduzi". Makundi ya watu wenye fujo yalikuwa huru. Sheria na amani zilikuwa hazipo katika mitaa ya Zanzibar.
Walimiliki ardhi na wafanya biashara waliburutwa kutoka majumbani na madukani mwao, uporaji na mauaji yalienea mji mkongwe mzima. Kwa kweli mji wenyewe uliporwa.

Waarabu na Waasia , waliokuwa wakiunga mkono vyama vyengine waliuliwa kwa makundi. Kwa usiku mmoja maisha ya watu yasiyovika yalipotea na siku nyengine baadae maelfu ya watu waliikimbia nchi pamoja na kila walichoweza kubeba.

John Okello mwenyewe alijipachika cheo cha Jemedari Mkuu akishirikiana na bataliani zake zenye fujo walianzisha utawala wa vitisho ndani ya visiwa vya Unguja na Pemba. John Okello alitangaza vitisho visivyo vya kawaida na ahadi ya kifo kwa wote watakaojaribu kumpinga yeye. John Okello aliamini alikuwa akipokea maelekezo /dokezo kutoka kwa Mungu na akionyesha uwezo usiokuwa wa kawaida kwa kutumia nambari, kwa mfano tarehe 13 Januari, 1964, alitangaza ujumbe ufuatao." Serikali sasa inaendeshwa na sisi ikiwa mtakuwa wakaidi na kukataa kutii amri, Nitachukua hatua kali mara 88 zaidi ya hatua ninazozichukua hivi sasa" na "Na ikiwa yeyote atashidnwa kutii amri ya kutotoka nje ya nyumba kama walivyofanya wengine.sitokuwa na njia nyengine lakini kutumia silaha nzito. Sisi, ni jeshi lenye nguvu ya 99,099,000".

Vitisho vyake na uwezo wake wa kuvitekeleza viliwatia hofu raia, hasa makundi mbali mbali ya jamii zilizo ndogo. Tarehe 14 Januari, 1964 alitangaza maneno haya ya kufadhaisha" Huyu hapa ni Jemedari Mkuu wa Unguja na PembaNafikiria kuelekea kijiji cha Mtendeni kukiangamiza ikiwa watu wa hapo hawatafuata amri. Baada ya dakika 40 nitawamaliza nyote hasa Wangazija", " na kwa vijana wote wa kiarabu wanaoishi Malindi; Nitapita Malindi nikiwa nimesheheni silaha ambazo mimi mwenyewe ndie nizijuazo. Nataka kuona kila mmoja abakie na chupi na kulala chini. Nataka kuwaona wao wanaimba... Baba wa Waafrika. Mungu Mbariki yeye na malengo yake na yale ya Jemedari Mkuu"

Wakati unyanyasaji uliposima jamii za tamaduni tofauti za Zanzibar zilikuwa zimeparaganyika. Taifa la chama kimoja lilitangazwa. Lakini bado jTaifa hili likihofia uwezekano wa kufufuka upinzani kutoka kwa wapinzani waliokimbia nchi. Wanamapinduzi hawa baadae walijihakikishia udhibiti zaidi baada ya kusaini mkataba wa muungano wa Tanganyika. Hii ingeruhusu maelfu ya marafiki wa kisiasa wa Tanganyika kuingilia kati upinzani wowote wa baadae katika visiwa hivi. Askari polisi wa Zanzibar walibadilishwa kwa askari polisi kutoka Tanganyika ambao ni watiifu kwa chama na pazia la siasa za utengano ziliwakumba wazanzibari ambazo zilitakiwa kudumu kwa zaidi ya miaka 20.

Leo hii siasa hizi za utengano hazipo tena, kumalizika kwa vita vya baridi na kuelekea kwa uchumi wa kisasa umeweza kuifungulia Zanzibar milango kwa ulimwengu wa nje. Uchaguzi wa vyama vingi ulifanyika mwaka 1995, 2000, 2005,2010 na mwingine unatarajiwa 2015.

Viongozi wa kweli na wenye kujali hali za watu wameibuka Tanzania na hii imewafanya wakimbizi waliokimbia wakati wa mapinduzi kurejea visiwani. Uvumilivu na amani wa watu wa aina tofauti, ambayo ni tabia ya maisha ya wazanzibari, sasa hivi unajitahidi kurejea katika mitaa ya mji mkongwe.

Yericko Nyerere,

Usipende kusafiria nyota za watu unatumia maandishi ya watu bila kumtaja muhusika jina huu ni ujinga na upuuzi wa hali ya juu.

Watu wanaumiza vichwa kufanya utafiti kuandika makala za historia, hili bandiko siyo lako ukibisha tawaonyesha wanaukumbi ulipo liiba.

Unajifanya mwandishi kumbe una lolote unaiba kazi za watu.

Angalia mimi naleta bandiko humu na nimtaja mwandishi.

Mohamed Said, Barubaru, Kadogoo, gombesugu, THE BIG SHOW,
 
Last edited by a moderator:
gombesugu,

..Casimiro Montero, jasusi wa Kireno, ndiye anayenyooshewa kidole kuhusika na mauaji ya Mondlane.

..sasa kama una taarifa mpya kwamba Mwalimu Nyerere ndiye mhusika basi JF kuna watu wengi very open minded tunaweza kuziangalia kama zina ukweli au la.

..lakini wakati utakapozileta naomba nikuulize: movite ya Nyerere kumuua Mondlane ilikuwa ni nini haswa?

..zaidi, what r u trying to prove here, ukizingatia hoja yako ni Mwalimu kumuua Mondlane, na badala yake kushiriki kumsimika ktk uongozi Samora Machel ambaye alikuwa Maxist??

cc: Jasusi, Nguruvi3, Kudi Shauri, Wickama, Mag3
jokaKuu,
How can you take anybody seriously who claims that Nyerere conspired with Kennedy to kill Lumumba. Now he must have also conspired with PIDE, the secret Portuguese police to kill Mondlane. And for what reason? Really?
 
Hongera sana mkuu, jambo jema sana!

Nilipomsoma John Iliffe katika A Modern History of Tanganyika sikuwa na hofu na mtu ninaejadiliana nae huyu Mohamed Said, niliona wazi kuwa sio mwandishi bali muokoteza maneno na muongo wakutupwa!

Sasa kaungana na vijana wake kwakubadili mada na kunigeukia mimi,

Haahaa hawana tofauti na wanawake wa saluni tu!


...huna tofauti na wanawake wa vilabuni....! maana wale kwa maneno machafu....sion tofauti yao na yako
 
Huu mpini mwingine kutoka kwa Ahmed Rajabu.
Siku John Okelo alipotimuliwa Zanzibar
Ahmed Rajab

...Usiku wa manane wa Januari 11, makada wapatao 200 wa Umoja wa Vijana wa Afro-Shirazi (Afro-Shirazi Youth League) walielekea kwenye kambi ya polisi ya Ziwani, nje kidogo ya mji huko Unguja. Wakiongozwa na Yusuf Himid wapinduzi hao hawakukabiliwa na upinzani walipofika Ziwani ila waliikuta ghala ya silaha iko wazi na wakazinyakua silaha na kukimbia nazo hadi kwenye uwanja ulio nje ya jengo la Raha Leo.

Hapo ndipo palipokuwa makao makuu ya Mapinduzi kwa siku chache na ndipo wapinduzi walikokuwa wakipewa silaha. Studio za redio ya Serikali pia zilikuwa hapo. Moja ya sababu zilizoyafanya Mapinduzi yafanikiwe haraka ni uamuzi wa viongozi wa Serikali iliyopinduliwa - Sheikh Muhammed Shamte na Sheikh Ali Muhsin Barwani - kuwataka wafuasi wao wasitumie nguvu kuyapinga.

Hivyo, mbali na mapigano yaliyozuka saa za asubuhi ya Jumapili Januari 12, mbele ya Steshini ya Polisi Malindi, hapajazuka mapigano Unguja kati ya waliopindua na waliopinduliwa. Pemba nako pia hakukuwa na upinzani ijapokuwa kisiwa hicho kilikuwa ngome ya vyama vya ZNP na ZPPP.

Wengi wa wapiganaji waliokuwa kwenye Stesheni ya Polisi ya Malindi walikuwa wakuu wa polisi Wakiingereza. Wakipigana na makada wa Umma Party ambao ndio pia waliouteka uwanja wa ndege, bandari pamoja na kituo cha mawasiliano ya nje cha Cable & Wireless, kilichokuwa kwenye jengo ambalo sasa ni Hoteli ya Serena Mji Mkongwe.

Kwa hakika, kinyume cha baadhi ya watu walivyoandika hapakutokea mauaji ya kimbari. Aliyeanzisha uvumi huo alikuwa John Okello aliyeandika kwenye kitabu chake kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar kwamba watu zaidi ya elfu kumi waliuliwa. Okello aliongeza kwamba aliamrishwa na Yesu Kristo kuwakomboa ‘Waafrika' wa Zanzibar kutoka kwa ‘wageni'.

Tutamrejelea Okello na wengine waliokuwa Raha Leo baadaye. Kwanza tukumbushe kwamba mkesha wa Januari 12, mwaka 1964, Zanzibar haikuwa na jeshi. Kulikuwa polisi waliokuwa wakiongozwa na Waingereza. Wengi wa askari polisi walikuwa raia wa Tanganyika. Serikali iliyopinduliwa ilikataa kuandikiana mkataba wa kijeshi na Uingereza kwa sababu ikihisi mkataba kama huo utaonekana kuwa wa kikoloni.

Hatuwezi kusema ni nani hasa aliyepiga risasi ya mwanzo au ya mwisho katika Mapinduzi. Naitoshe tusemapo kwamba kwa vile hakukuwa na upinzani, Serikali iliyokuwa madarakani iliporomoka kama ‘nyumba ya karata'.
Tuwarejelee sasa waliokuwa Raha Leo, makao makuu ya Mapinduzi kwa siku chache. Kwanza tumuangalie Okello ambaye sauti yake ndiyo iliyokuwa ikivuma kwenye Redio Zanzibar.

Hatuna uhakika nani alimpeleka Okello Raha Leo. Wengine wanasema ni Yusuf Himidi. Wengine wanasema ni Seif Bakari aliyetoa rai atumiwe kutoa matangazo kwenye redio kwa vile sauti yake ilikuwa na lafudhi ngeni ya kutisha.
Uhakika tulio nao ni kwamba Okello alipotokea Raha Leo na mabastola yake, Aboud Jumbe alishtuka na akauliza: "Nani huyu? Katokea wapi?"

Kijana huyo aliyekuwa na umri wa miaka 27 hakujulikana kabla ya Mapinduzi. Alikuwa mtu asiyejua kuandika wala kusoma na akili zake zikimtosha mwenyewe. Hakuwa na sifa za uongozi na wala hakushiriki katika vuguvugu lolote la kisiasa. Akijibandika cheo cha kijeshi cha Field Marshall ni yeye aliyetangaza kwamba serikali ya ZNP/ZPPP imepinduliwa.

Kwa hakika, kazi hiyo ya kutangaza kufanikiwa kwa Mapinduzi kwanza alipewa Ramadhan Haji, mmoja wa wapinduzi. Lakini alikataa. Jina la Okello lisingelisikika lau Ramadhan Haji angekubali kutangaza kwamba Serikali imepinduliwa na kwamba wapinduzi waliidhibiti nchi.

Waliokuwa wakiongoza mambo Raha Leo tangu Mapinduzi yaanze, hadi Jumatatu Januari 13, walikuwa Aboud Jumbe, mmoja wa viongozi wa chama cha Afro-Shirazi (ASP), Thabit Kombo (Katibu Mkuu wa ASP) na Badawi Qullatein wa Umma Party. Muda wote huo, Sheikh Abeid Amani Karume (kiongozi wa ASP), Abdulrahman Babu (mwenyekiti wa Umma Party) na Abdalla Kassim Hanga (ASP) walikuwa Dar es Salaam.

Mnamo siku hizo hizo liliundwa Baraza la Mapinduzi na Baraza la Mawaziri lililokuwa na mamlaka kamili ya kuiendesha Zanzibar. Mabaraza hayo mawili yalikuwa taasisi kuu za Serikali ya kimapinduzi ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar. Na sio ile iitwayo ‘Kamati ya Watu Kumi na Nne' ambayo baadhi ya watu wanasema kuwa ndiyo iliyoandaa Mapinduzi.

Okello akipenda kujigamba kwamba ndiye aliyeyapanga na kuyaongoza Mapinduzi. Alikuwa akitoa matamshi ya kushtusha na ya ajabu-ajabu kwenye Redio Zanzibar. Kwa mfano, siku moja alidai kwamba alipwe mshahara mkubwa zaidi ya aliokuwa akilipwa Rais Karume. Siku nyingine akasema kwamba kasri zote alizokuwa akitumia sultani kupumzikia apewe yeye.

Kuna siku aliyotoa hukumu kwamba mzee mmoja wa zaidi ya miaka 60 afungwe kwa miaka 99. Alisema kama huyo bwana atakufa gerezani basi mwanawe afungwe ili kuendeleza kifungo na mwanawe akifa basi mjukuu wake afungwe mpaka itimie miaka 99.

Nyakati nyingine aliwaonya watu wazitie moto familia zao na wao wenyewe mpaka wafe ‘kabla ya majeshi yangu kuja.' Alikuwa akitoa vitisho visivyowahi kamwe kusikika Zanzibar. Kuna siku alitangaza kwamba wakazi wa eneo moja ambako alikuwa apite, wajipange foleni barabarani wakiwa wamevaa chupi tu.

Okello alikuwa ni adha, kitisho, kichekesho na fedheha kwa Zanzibar. Viongozi wapya wa nchi walichoka naye na wakaamua kumchukulia hatua. Salim Rashid, mmoja wa viongozi wa Umma Party aliyekuwa katibu wa Baraza la Mapinduzi anasema kwamba, kwanza alilizungumza suala la Okello na Sheikh Karume. Halafu akalizungumza na Brigadia Yusuf Himid na mwisho yeye, Yusuf Himid na Kanali Ali Mahfoudh wakalitafutia dawa.

Ilisadifu kuwa siku moja Okello alisafiri kwenda Dar es Salaam akifuatana na Jaha Ubwa, aliyekuwa katibu wake. Walipokuwa wanatarajiwa kurudi Zanzibar, Karume, Yusuf Himid, Salim Rashid na Ali Mahfoudh walikwenda uwanja wa ndege kumsubiri.

Siku hiyo anaikumbuka vizuri Luteni Hashil Seif aliyekuwa ofisa wa zamu kwenye kambi ya jeshi huko Migombani karibu na uwanja wa ndege. Alipigiwa simu akitakiwa aende kwa haraka uwanja wa ndege. Hakuambiwa anaitiwa nini.

Alipofika ndipo alipoambiwa kwamba kuna ndege ya Shirika la Ndege la Afrika ya Mashariki iliyokuwa inakuja kutoka Dar es Salaam ndani yake wakiwemo pia Okello na Jaha Ubwa. Akaelezwa kwamba awaruhusu abiria wote pamoja na Ubwa washuke, lakini amzuie Okello asishuke. Halafu amwambie rubani ampeleke Okello Kenya.

Hashil naye akampigia simu komredi mwenzake Luteni Amour Dugheshina kumwita aende uwanja wa ndege amsaidie. Maluteni wote wawili walikuwa na bunduki za aina ya ‘machine gun'. Ndege ilipotua walipanda ndani ya ndege, wakampokonya silaha Okello na kutekeleza amri waliopewa. Rubani wa ndege alikasirika sana. ‘Uso wake ulighadhibika, utafikiri mnyama aliyekosewa risasi,' alieleza Hashil.

Lakini rubani hakuwa na la kufanya ila kuiwasha ndege na kuelekea Kenya. Huku nyuma Salim Rashid akampigia simu Oginga Odinga, Makamu wa Rais wa Kenya, kumuarifu kwamba wamemfukuza Okello na ‘wanamrejesha' Kenya. Alifanya hivyo kwa makosa kwa sababu kutokana na jina lake akifikiri kuwa Okello ni Mjaluo kutoka Kenya.

Kumbe alikuwa mtu wa kabila la Acholi aliyezaliwa Uganda na alikwenda Unguja kabla ya kuhamia Pemba ambako alikuwa mwashi, mtiaji rangi nyumba na mpasuaji mawe. Swali la kujiuliza hapa ni; je, iwapo kweli Okello alikuwa ‘kiongozi mpendwa wa Mapinduzi' ilikuwaje wafuasi wake na wanamapinduzi wenzake wasimtetee alipoadhiriwa uwanja wa ndege na kufukuzwa nchini? Ilikuwaje akafukuzwa kwa urahisi hivyo?

Kuna uzushi mwingi kuhusu kipindi hiki kifupi cha historia ya Zanzibar. Kwa mfano, kuna filamu ya kubuni ya Wataliana inayoonyesha maiti chungu nzima za watu waliopigwa risasi. Filamu hiyo ilikuwa na lengo moja tu; kuonyesha ‘ukatili na unyama wa Waafrika.'

Hakuna ithibati yoyote kwamba watu waliouawa katika siku za mwanzo za Mapinduzi walifika elfu kumi. Ukweli ni kwamba jumla ya watu waliouawa siku hizo haipindukii 200, katika sehemu za mjini hawazidi 25. Uzushi mwingine ni kwamba walipelekwa Watanganyika, Zanzibar wakiwa na silaha kwenda kupindua. Na si kweli kwamba Mapinduzi yalikuwa na msisitizo wa kikabila. Katika kipindi cha mwanzo cha Mapinduzi msisitizo ulikuwa wa kitabaka. Nyimbo zilizokuwa zikiimbwa kwenye Redio Zanzibar zikiwazungumzia ‘wakwezi na wakulima' na wafanyakazi kwa jumla na si makabila.

Mapinduzi ya Zanzibar yalianzisha taasisi mpya za utawala zikiwa pamoja na Baraza la Mapinduzi, Baraza la Mawaziri na ofisi ya Rais. Taasisi hizo zilikuwa zifanye kazi kwa muda wa mwaka mmoja tu kwa vile ilikwishaamuliwa kwamba Januari 1965 pafanywe uchaguzi wa kulichagua Bunge la Katiba, lililokuwa litunge Katiba ya kudumu ya Zanzibar.

Baraza la Mapinduzi la Zanzibar pamoja na Serikali mpya zilianza kwa ubia baina ya chama cha ASP na Umma Party. Ingawa wanachama wa ASP ndio waliofanya Mapinduzi waliutambua mchango wa wafuasi wa Umma Party na hasa mchango wa makada wao waliopata mafunzo ya kijeshi nchini Cuba.

Vijana hao wa Umma walizitia wasiwasi serikali za Marekani na Uingereza na kuzifanya ziamini kuwa utawala mpya wa Zanzibar ulikuwa wa ‘kikomunisti'. Dhana hiyo ndiyo iliyosababisha kuchukuliwa hatua ya kuyachimba na kuyagandamiza Mapinduzi ya Zanzibar yaliyodumu kutoka Januari 12, hadi 26 Aprili, mwaka 1964.
Nimeamua kuuweka huu unaoitwa mpini na Ritz kwa namna rahisi kidogo ili wanajamvi wausome tena taratibu na kwa umakini mkubwa. Sina hakika na huu mpini wa Ritz kama na wenyewe unaelezwa kama historia ya kweli ya Mapinduzi Zanzibar. Baadaye nafasi ikipatikana huu mpini nao utachambuliwa taratibu kama mpini wa Mohamed Said kuhusu alichodai ni historia ya kweli ya harakati za uhuru wa Tanganyika ulivyochambuliwa na unazidi kuchambuliwa.

Hata hivyo kabla ya uchambuzi huo kufanyika natoa tahadhari kwa wana JF; ni vizuri kufahamu malengo na nia za watu kama hawa ambao wako tayari kuita mchana usiku, mwanga giza na cheupe cheusi. Mohamed Said anadai BAKWATA haiwawakilishi Waislaam Tanzania bali ipo inautumikia mfumo Kristo; kwa maana nyingine kama unakubaliana na BAKWATA, kama ni kiongozi wa BAKWATA au kama wewe ni mwanachama wa BAKWATA basi Uislaam wako una walakini.

Hoja hii ya nguvu imetumika kuwadanganya, kuwasuta na kuwatisha Waislaam wasiokubaliana na mahubiri yake ya chuki. Kwa nini nasema hivi? Labda tuanze na NATIONAL MUSLIM COUNCIL OF TANZANIA (BAKWATA) ni nini, hapa naona nianze kwa kunukuu maelezo yaliyotolewa na jumuiya yenyewe miaka ya nyuma kidogo;

BAKWATA said:
The National Muslim Council of Tanzania (BAKWATA) is a well established faith based Islamic organisation registered since 1968. The Council has branch offices all over Tanzania with a network from the national to grassroots level with 22 regional and 113 district offices served by over 700 sheikhs.

Around 2,800 mosques run under its co ordination. It owns around 40 acres of land in each of its 22 regions and it has 20 secondary schools, two teachers' colleges, two theological colleges, and a radio station and supports numerous madras schools.
Swali kwa wanajamvi; tumweleweje mtu ambaye anao ujasiri wa kudai kuwa BAKWATA si chombo cha Waislaam wala kinachowawakilisha Waislaam bali ni chombo kinachoongozwa kwa maelekezo ya Kanisa? Je mtu huyu analitakia mema taifa hili? Kwamba Sheikh Mkuu wa Tanzania anatekeleza majukumu yake kwa maelekezo ya Kanisa! Kwamba kiongozi Mkuu wa serikali na jemadari Mkuu wa taifa, Al Haj Dr. Jakaya Mrisho Kikwete anatekeleza wajibu wake kwa matakwa ya Kanisa! Huyo ndiye Mohamed Said.

Baada ya hiyo tahadhari, naendelea kuutafakari mpini ulioletwa na Ritz akiwanukuu Dr. Ghassany na mwandishi anayeitwa Ahmed Rajabu. Kama isingekuwa kuwa madai yaliyotolewa hayatoi mwanya wa kutafsiriwa vibaya na watu wenye uelewa mdogo na hivyo kuweza kutumika kichochezi, wala hata nisingehangaika kuyajibu, ningebaki tu nacheka kwani simulizi utadhani ni hekaya za Abunwasi...hadithi njoo, uongo njoo, utamu kolea!
 
...huna tofauti na wanawake wa vilabuni....! maana wale kwa maneno machafu....sion tofauti yao na yako

kumbe mkuu wewe ni mtu wa vilabuni sana, Sasa jitahidi mida hii ukiwa unatoka kilabuni usiwe unapost maana unaharibu mjadala.

Mwalimu wangu wa jamvini alinifundisha mtu akikutukana ulevini na wewe mrudishie hapo hapo, kesho asije akasema alikuwa amelewa.
 
Aaah wapi...ndugu yangu ktk IMAAN...huyu mleta hoja amechoka kifikra...hana hoja anaishia kutoa matusi...Nna wasiwasi na akili yake! Mzee Mwanakikijiji ndio kabisa amejichimbia kwenye kutengeneza ngano mpya za huba.....muda mwingi anatumia hisia zake zake zaid katika kuumba hoja kuliko tafakuri

MAY ALLAH REWARD YOU....MOHAMED SAID

Dilikeni,
Amin, Amin, Amin.
 
Pole sana ndugu yangu, tena pole sana kwa masaibu yalokukumba katika harakati za ukombozi wa Mzanzibar!

Pamoja na madhila yoooote hayo bado yatabaki kuitwa ni mapinduzi ya Okello yaliyozaa Zanzibar hii ya leo, na wazanzibar wote watabaki kuyaheshimu na kuyatukuza kama wafanyavyo sasa!

Huo ndio ukweli mchungu lakini ni dawa!

Yericko,
Stizai ndiyo mwenza kwa yule ambae hakufikwa.

Tumekusomeni hapa mkikejeli, mkikebehi na mwisho
mkitukana.

Waswahili tuna msemo.
Mdomo haumkatai bwana wake.

Hakuna wa kukuzuia kumpa sifa Okello.

Lakini historia ya Zanzibar tunaijua siyo kwa kuwasoma
Wazungu bali kwa kuishi ndani yake.

Rejea mabandiko yangu niloweka kuhusu historia ya mapinduzi
kisha fananisha na usemayo kuna jambo utaliona dhahir shahir.
 
Ndugu yangu,

Kumchumchukia na kutopenda kumzungumzia hakuondoi ukweli,

Ukweli husimama wima na huwa hauwi tenge hata nyuzi moja!

Kwa nusu muongo sasa wazanzibar wanayaadhimisha mapinduzi haya tena kwa furaha yapekee!

Labda ujue kuwa katika ukombozi wa taifa kwa mtutu wa bunduki, damu ni sehemu ya chagizo la ukombozi huo!

Ni jambo lakujivunia na kumshukuru Mungu kuwa uhuru wa Tanganyika hatukubeba mtutu kuupata na hilo ni sehemu ya linalochagiza sifa kuu za kiongozi wetu wa harakati za uhuru huo mzee Nyerere!

Pamoja na utawala wa mkono wa chuma wa mwanamapinduzi Field Marshal John Okello katika ardhi ya Zanzibar, bado ukweli unasimama kuwa yeye ndie baba wa taifa la Zanzibar!

Yeye ndie kawatoa toka minyororo ya utumwa wa sultani, bila yeye nani muweza?

Katika kipindi cha miezi sita ya utawala wake hakuna kiongozi barani afrika na ulaya aliyethubutu kukenua kinywa juu yake!

Paka walichinjwa kwaajili yakulishana yamini na jeshi lake tiifu!

Ni Nyerere tu ndie aliyefanikiwa kuzungumza nae nakupunguza mbinyo hadi kuchukua madaraka ASP


Sasa ukichukia kuzungumza ukweli huo huko ni kujipunja mwenyewe kama mzanzibar na mtanzania

Tatizo lako hii historia huijui bali unajikita kwa USHABIKI tu kuwa katika taifa la Znz ambao wengi waislam UHURU wao uliletwa na Mkristo tena mmoja ambaye ni mgeni asiye na hata konde hapo Unguja.

Vile vile unatakiwa kujua kuwa Uhuru wa Tanganyika wamepewa ofisini kwani nchi hiyo iliwekwa chini tu ya uangalizi wa wAingereza. sasa inapotokea mtu kujiita baba wa Taifa kwa sababu ya kusafirishwa na kwenda kupewa uhuru ofisini je ni Ubaba gani huo. hebu niambie baba wa Taifa lolote unalolijua wewe ambaye Uhuru alipewa ofisini.

lakin na la kujiuliza Je ni kikao gani halali cha Bunge kilichopitisha kuitwa Nyerere baba wa Taifa. nafikiri hizo ni baadhwi tu ya wanafunzi wake ambao aliowaangalia kwa jicho la huruma na kuwapa madaraka ndio hao vinara wa kumpa kila cheo.

je una taarifa na sasa baada ya Kufariki anataka kupewa cheo kingine cha Mwenye kheir?

Ushauri wangu kama utaondoa USHABIKI na Pupa nafikiri utafunzwa mengi hapa kwani unachoandika wengine kimetutokea na tumekishuhudia mchana kweupeeee si wewe wa kuhadithiwa na kuwekewa chumvi.

Jitulize usomeshwe.

 
Yericko,
Stizai ndiyo mwenza kwa yule ambae hakufikwa.

Tumekusomeni hapa mkikejeli, mkikebehi na mwisho
mkitukana.

Waswahili tuna msemo.
Mdomo haumkatai bwana wake.

Hakuna wa kukuzuia kumpa sifa Okello.

Lakini historia ya Zanzibar tunaijua siyo kwa kuwasoma
Wazungu bali kwa kuishi ndani yake.

Rejea mabandiko yangu niloweka kuhusu historia ya mapinduzi
kisha fananisha na usemayo kuna jambo utaliona dhahir shahir.

Swadakta Al Akhiy Mohamed said.

Mimi nimemnasihi Atulie kitako tumpe darsa hapa kwani yeye amehadithiwa lakin wengine tumeyashuhudia kwa macho yetu.

lakin siku zote ukikumbwa na USHABIKI na pupa basi ilmu itakupita pembeni kwani siku zote ilmu bora ni ile unayotulia na kuipokea tartibu kwa mpangilio na mtiririko wake.

Tumpe pole na kumnasihi aache jazba ili adarsishwe hapa. na akiondoa Ushabiki basi ataelewa zaidi.

Ahsantum Al Akhiy .

 
Nimeamua kuuweka huu unaoitwa mpini na Ritz kwa namna rahisi kidogo ili wanajamvi wausome tena taratibu na kwa umakini mkubwa. Sina hakika na huu mpini wa Ritz kama na wenyewe unaelezwa kama historia ya kweli ya Mapinduzi Zanzibar. Baadaye nafasi ikipatikana huu mpini nao utachambuliwa taratibu kama mpini wa Mohamed Said kuhusu alichodai ni historia ya kweli ya harakati za uhuru wa Tanganyika ulivyochambuliwa na unazidi kuchambuliwa.

Hata hivyo kabla ya uchambuzi huo kufanyika natoa tahadhari kwa wana JF; ni vizuri kufahamu malengo na nia za watu kama hawa ambao wako tayari kuita mchana usiku, mwanga giza na cheupe cheusi. Mohamed Said anadai BAKWATA haiwawakilishi Waislaam Tanzania bali ipo inautumikia mfumo Kristo; kwa maana nyingine kama unakubaliana na BAKWATA, kama ni kiongozi wa BAKWATA au kama wewe ni mwanachama wa BAKWATA basi Uislaam wako una walakini.

Hoja hii ya nguvu imetumika kuwadanganya, kuwasuta na kuwatisha Waislaam wasiokubaliana na mahubiri yake ya chuki. Kwa nini nasema hivi? Labda tuanze na NATIONAL MUSLIM COUNCIL OF TANZANIA (BAKWATA) ni nini, hapa naona nianze kwa kunukuu maelezo yaliyotolewa na jumuiya yenyewe miaka ya nyuma kidogo;


Swali kwa wanajamvi; tumweleweje mtu ambaye anao ujasiri wa kudai kuwa BAKWATA si chombo cha Waislaam wala kinachowawakilisha Waislaam bali ni chombo kinachoongozwa kwa maelekezo ya Kanisa? Je mtu huyu analitakia mema taifa hili? Kwamba Sheikh Mkuu wa Tanzania anatekeleza majukumu yake kwa maelekezo ya Kanisa! Kwamba kiongozi Mkuu wa serikali na jemadari Mkuu wa taifa, Al Haj Dr. Jakaya Mrisho Kikwete anatekeleza wajibu wake kwa matakwa ya Kanisa! Huyo ndiye Mohamed Said.

Baada ya hiyo tahadhari, naendelea kuutafakari mpini ulioletwa na Ritz akiwanukuu Dr. Ghassany na mwandishi anayeitwa Ahmed Rajabu. Kama isingekuwa kuwa madai yaliyotolewa hayatoi mwanya wa kutafsiriwa vibaya na watu wenye uelewa mdogo na hivyo kuweza kutumika kichochezi, wala hata nisingehangaika kuyajibu, ningebaki tu nacheka kwani simulizi utadhani ni hekaya za Abunwasi...hadithi njoo, uongo njoo, utamu kolea!

Naona huu "Mpini" umekuchanganya kabisa mpaka hujitambui unajifanya unacheka wakati nafsi inalia.

Naona unakunywa sumu kwa maziwa...ha haa ha.

Cc.. gombesugu,
 
Last edited by a moderator:
Yericko Nyerere,

Usipende kusafiria nyota za watu unatumia maandishi ya watu bila kumtaja muhusika jina huu ni ujinga na upuuzi wa hali ya juu.

Watu wanaumiza vichwa kufanya utafiti kuandika makala za historia, hili bandiko siyo lako ukibisha tawaonyesha wanaukumbi ulipo liiba.

Unajifanya mwandishi kumbe una lolote unaiba kazi za watu.

Angalia mimi naleta bandiko humu na nimtaja mwandishi.

Mohamed Said, Barubaru, Kadogoo, gombesugu, THE BIG SHOW,

Mbona unaropoka kwa hamaki hivyo?

Wapi nimesema mimi ndie mwandishi?

Hukuona makala zingine zote nilizoleta hapa nilikuwa naweka jina langu mwisho?

Usiwe na papara kijana, tulia soma na ujue mantiki!

Musimulizi wa hayo ni Barghash:
 
Last edited by a moderator:
Hii shule tunayopata kwenye huu mjadala ni kali,kumbe Field Marshall OKELLO ndio baba wa taifa wa zanzibar-asanteni wachangiaji
 
Kwa niaba ya Alyh Bab, gombesugu, basi chukuwa huu mpini walaahai...kutoka kwa Harith Ghassany.
Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru: Zanzibar na Mapinduzi ya Afrabia

HATA kama hupendi kusoma vitabu; hiki si cha kukosa. Kwanza kimeandikwa kwa Kiswahili fasaha; lugha yetu mama inayoanza kufifishwa na kuchujwa na kizazi kisichosoma vitabu siku hizi. Pili, kimepikwa na mtaalamu halisi. Dk Harith Ghassany alizaliwa Zanzibar akapata shahada ya udaktari wa Falsafa Chuo Kikuu cha Harvard, Massachussets, Marekani. Harvard ni chuo cha kale sana; kilianzishwa mwaka 1636 na kwa muda mrefu kimeorodheshwa na magazeti, watalaamu na chama cha vyuo vikuu duniani kuwa cha kwanza duniani.
Fani yake kuu ni utafiti. Dk Ghassany ambaye anasema alitafiti kitabu hiki muhimu kuanzia 2004 hadi 2009 alikuwa awali Profesa Msaidizi Chuo cha Udaktari na Sayansi za Afya , Chuo Kikuu cha Sultani Qaboos, kilichoko Muscat, Oman, Uarabuni. Nilipomhoji kutokea Marekani anakoishi, Dk Ghassany alifafanua lengo la kuandika kigongo hiki chenye kurasa 500: Nia yangu ni kuziondoa fitina za upotoshaji wa historia ili uhusiano mkongwe baina ya Wazanzibari, baina ya Wazanzibari na Watanganyika (Watanzania) na baina ya Waafrika na Waarabu, upate kuendelea kutiririka na kuimarika kwa maslahi ya kujenga amani na neema kwa faida ya walio wengi na vizazi vya baadaye vya pande zote. Sijawahi kusoma kitabu kinachomhusu kila Mtanzania kama hiki.
Licha ya kuhadithia, kinatafakari maswali mengi. Je, neno Afrika asilia yake nini? Vipi tukaitwa Tanzania? Vipi Wazanzibari wengine hawautaki Muungano? Mapinduzi ya Unguja yalianzia wapi? Nani hasa alihusika? Je, viongozi waliopindua ndiyo waliotawala? Ndani ya sura ya pili, inayohusu Mirengo ya Kizalendo na Mapinduzi, ukurasa 23, mwandishi anatueleza bila kupepesa macho: Msomaji anatakiwa awe makini kabisa na hata kabla hajaendelea kusoma inampasa afahamu kuwa viongozi wakubwa wa Chama cha Afro Shirazi kama marehemu, Mzee Abeid Amani Karume, marehemu Mzee Thabiti Kombo Jecha au Sheikh Aboud Jumbe hawakushiriki katika mipango halisi ya mapinduzi ya Zanzibar. Si kitabu cha kisasi chenye azma ya kusakama wakuu wa nchi na mashujaa wetu wa zamani kibwege; au kuwachafua. Dk Ghassany anakiri hana kabisa mshawasha wa kutaka kuja kuwa mwanasiasa au mgombea kiti cha urais. Zamani Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alipenda kutuambia wasomi tusisahau tulikotoka. Kambarage alimlinganisha msomi na kijana aliyetumwa na kijiji chenye njaa kukitafutia ahueni kisha arudi kuwasaidia wanavijiji wenzake.
Dk Ghassany ni msomi wa kabila hilo. Katimiza wajibu wake. Anasema kitabu kilikuwa kigumu kukiandika na pia kigumu kukisoma. Moja ya msingi mahsusi wa kazi za historia ni kutukumbusha watu tuliowasahau na mafunzo yake.
Tunamkumbuka John Okello? Je, Oscar Kambona, mpinzani mkuu wa hayati Nyerere na ujamaa aliyeishia uhamishoni hapa London, alihusikaje katika mapinduzi ya visiwani? Je, nini kilitokea wakati wa maasi ya wanajeshi wa Tanganyika mwaka huo huo wa 1964? Je, silaha za mapinduzi ya Zanzibar zilitoka wapi? Je, vyama vingine kama Umma Party cha hayati Abdulrahaman Babu vilifanya nini? Kassim Hanga ni nani? Je, kwanini Kassim Hanga akanyongwa miaka michache baada ya mapinduzi ya Unguja, 1964? Je, aliyekuwa zamani kiongozi wa Algeria, Ahmed Ben Bella (ambaye yu hai) alihusikaje? Je, wanamapinduzi maarufu wa Cuba Fidel Castro na Che Guevara walihusika? Kwanini shirika la Upelelezi la Marekani, CIA lilikuwa likiogopa sana Unguja? Je, vipi maelfu ya Wazanzibari wamezagaa ulimwenguni wakiishi Ulaya, Marekani na Uarabuni, baada ya kuikimbia nchi yao? Je, mwanajeshi maarufu Kanali Ali Mahfoudh alifanya nini? Maswali mengi yamejibiwa si tu kwa utafiti maridadi alioufanya mtaalamu huyu bali pia kupitia midomo ya waliohusika.
Kitabu kimejazana hati za siri, za kiserikali na pia mahojiano na wazee hai walioshika mapanga enzi hizo. Wengine wao kama Victor Mkello (aliyekuwa zamani mmoja wa viongozi wakubwa wa Chama cha Wafanyakazi na TANU wanahadithia kinauga ubaga ama walivyotiwa ndani, walivyosakamwa na nani alifanya nini katika ngazi za juu. Hiki si kitabu cha mchezo. Kuna pia mchango wa mzalendo na mwanahistoria mwingine Mohamed Said (aliyeandika vitabu viwili vinavyohusika na historia ya TANU, kimojawapo Uchaguzi wa mwaka 1958 katika kutafiti habari kibao.
Alivyokuwa mkweli, mbali ya utafiti na picha lukuki; Dk Ghassany aliwaonyesha viongozi wa sasa Unguja na bara muswaada wa kitabu kabla ya kuutoa. Anasema : Mustakbali utakuwa mzuri iwapo utajiri wake mkubwa wa kihistoria wa kijiografia wa Zanzibar na Tanzania utatumika kuuimarisha Muungano wake na Tanganyika baada ya Baraza adhimu la wawakilishi kuipitia na kuifanyia marekebisho katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuyalinda maslahi ya Zanzibar na kuonyesha njia mpya ya Muungano wa Jamhuri ya Tanzania. Unguja na Pwani kijumla ndiko lilipo chimbuko la lugha ya Kiswahili. Kama kazi ya fasihi ya lugha hii tukufu, kitabu kitakusaidia msomaji (hata uwe si mpenzi wa mambo mazito ya kihistoria na kisiasa) kuboresha ujuzi wako wa Kiswahili fasaha, hasa vijana. Kwa watu wa makamo na wazee, wataalamu na wapenda nchi yetu watapata changamoto na jopo la kufanya majadiliano, kupitia mambo ambayo tuliyasikia tu mitaani miaka 40 iliyopita.


Huu mpini mwingine kutoka kwa Ahmed Rajabu.
Siku John Okelo alipotimuliwa Zanzibar


Ahmed Rajab
YAFUATAYO ni masimulizi mafupi ya kipindi kifupi cha Mapinduzi ya Zanzibar ya Januari, 1964 yaliyoipindua serikali ya ubia ya chama cha Zanzibar Nationalist (maarufu Hizbu) na kile cha Zanzibar and Pemba Peoples Party (ZPPP). Tunaangazia nini hasa kilitokea usiku wa Jumamosi Januari 11, yaliyojiri siku ya pili yake na mwezi mzima wa Januari, mwaka 1964 .
Tumeyakusanya masimulizi haya baada ya kuzungumza na walioshiriki katika Mapinduzi hayo ambao baadaye walisaidia kudhibiti madaraka na kuunda taasisi zilizoziba pengo la Serikali iliyopinduliwa ya Waziri Mkuu, Muhammed Shamte Hamadi.
Usiku wa manane wa Januari 11, makada wapatao 200 wa Umoja wa Vijana wa Afro-Shirazi (Afro-Shirazi Youth League) walielekea kwenye kambi ya polisi ya Ziwani, nje kidogo ya mji huko Unguja.
Wakiongozwa na Yusuf Himid wapinduzi hao hawakukabiliwa na upinzani walipofika Ziwani ila waliikuta ghala ya silaha iko wazi na wakazinyakua silaha na kukimbia nazo hadi kwenye uwanja ulio nje ya jengo la Raha Leo.
Hapo ndipo palipokuwa makao makuu ya Mapinduzi kwa siku chache na ndipo wapinduzi walikokuwa wakipewa silaha. Studio za redio ya Serikali pia zilikuwa hapo.
Moja ya sababu zilizoyafanya Mapinduzi yafanikiwe haraka ni uamuzi wa viongozi wa Serikali iliyopinduliwa Sheikh Muhammed Shamte na Sheikh Ali Muhsin Barwani kuwataka wafuasi wao wasitumie nguvu kuyapinga.
Hivyo, mbali na mapigano yaliyozuka saa za asubuhi ya Jumapili Januari 12, mbele ya Steshini ya Polisi Malindi, hapajazuka mapigano Unguja kati ya waliopindua na waliopinduliwa. Pemba nako pia hakukuwa na upinzani ijapokuwa kisiwa hicho kilikuwa ngome ya vyama vya ZNP na ZPPP.
Wengi wa wapiganaji waliokuwa kwenye Stesheni ya Polisi ya Malindi walikuwa wakuu wa polisi Wakiingereza. Wakipigana na makada wa Umma Party ambao ndio pia waliouteka uwanja wa ndege, bandari pamoja na kituo cha mawasiliano ya nje cha Cable & Wireless, kilichokuwa kwenye jengo ambalo sasa ni Hoteli ya Serena Mji Mkongwe.
Kwa hakika, kinyume cha baadhi ya watu walivyoandika hapakutokea mauaji ya kimbari. Aliyeanzisha uvumi huo alikuwa John Okello aliyeandika kwenye kitabu chake kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar kwamba watu zaidi ya elfu kumi waliuliwa. Okello aliongeza kwamba aliamrishwa na Yesu Kristo kuwakomboa Waafrika wa Zanzibar kutoka kwa wageni.
Tutamrejelea Okello na wengine waliokuwa Raha Leo baadaye. Kwanza tukumbushe kwamba mkesha wa Januari 12, mwaka 1964, Zanzibar haikuwa na jeshi. Kulikuwa polisi waliokuwa wakiongozwa na Waingereza. Wengi wa askari polisi walikuwa raia wa Tanganyika. Serikali iliyopinduliwa ilikataa kuandikiana mkataba wa kijeshi na Uingereza kwa sababu ikihisi mkataba kama huo utaonekana kuwa wa kikoloni.
Hatuwezi kusema ni nani hasa aliyepiga risasi ya mwanzo au ya mwisho katika Mapinduzi. Naitoshe tusemapo kwamba kwa vile hakukuwa na upinzani, Serikali iliyokuwa madarakani iliporomoka kama nyumba ya karata.
Tuwarejelee sasa waliokuwa Raha Leo, makao makuu ya Mapinduzi kwa siku chache. Kwanza tumuangalie Okello ambaye sauti yake ndiyo iliyokuwa ikivuma kwenye Redio Zanzibar.
Hatuna uhakika nani alimpeleka Okello Raha Leo. Wengine wanasema ni Yusuf Himidi. Wengine wanasema ni Seif Bakari aliyetoa rai atumiwe kutoa matangazo kwenye redio kwa vile sauti yake ilikuwa na lafudhi ngeni ya kutisha.
Uhakika tulio nao ni kwamba Okello alipotokea Raha Leo na mabastola yake, Aboud Jumbe alishtuka na akauliza: Nani huyu? Katokea wapi?
Kijana huyo aliyekuwa na umri wa miaka 27 hakujulikana kabla ya Mapinduzi. Alikuwa mtu asiyejua kuandika wala kusoma na akili zake zikimtosha mwenyewe. Hakuwa na sifa za uongozi na wala hakushiriki katika vuguvugu lolote la kisiasa.
Akijibandika cheo cha kijeshi cha Field Marshall ni yeye aliyetangaza kwamba serikali ya ZNP/ZPPP imepinduliwa.
Kwa hakika, kazi hiyo ya kutangaza kufanikiwa kwa Mapinduzi kwanza alipewa Ramadhan Haji, mmoja wa wapinduzi. Lakini alikataa. Jina la Okello lisingelisikika lau Ramadhan Haji angekubali kutangaza kwamba Serikali imepinduliwa na kwamba wapinduzi waliidhibiti nchi.
Waliokuwa wakiongoza mambo Raha Leo tangu Mapinduzi yaanze, hadi Jumatatu Januari 13, walikuwa Aboud Jumbe, mmoja wa viongozi wa chama cha Afro-Shirazi (ASP), Thabit Kombo (Katibu Mkuu wa ASP) na Badawi Qullatein wa Umma Party. Muda wote huo, Sheikh Abeid Amani Karume (kiongozi wa ASP), Abdulrahman Babu (mwenyekiti wa Umma Party) na Abdalla Kassim Hanga (ASP) walikuwa Dar es Salaam.
Mnamo siku hizo hizo liliundwa Baraza la Mapinduzi na Baraza la Mawaziri lililokuwa na mamlaka kamili ya kuiendesha Zanzibar. Mabaraza hayo mawili yalikuwa taasisi kuu za Serikali ya kimapinduzi ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar. Na sio ile iitwayo Kamati ya Watu Kumi na Nne ambayo baadhi ya watu wanasema kuwa ndiyo iliyoandaa Mapinduzi.
Okello akipenda kujigamba kwamba ndiye aliyeyapanga na kuyaongoza Mapinduzi. Alikuwa akitoa matamshi ya kushtusha na ya ajabu-ajabu kwenye Redio Zanzibar. Kwa mfano, siku moja alidai kwamba alipwe mshahara mkubwa zaidi ya aliokuwa akilipwa Rais Karume. Siku nyingine akasema kwamba kasri zote alizokuwa akitumia sultani kupumzikia apewe yeye.
Kuna siku aliyotoa hukumu kwamba mzee mmoja wa zaidi ya miaka 60 afungwe kwa miaka 99. Alisema kama huyo bwana atakufa gerezani basi mwanawe afungwe ili kuendeleza kifungo na mwanawe akifa basi mjukuu wake afungwe mpaka itimie miaka 99.
Nyakati nyingine aliwaonya watu wazitie moto familia zao na wao wenyewe mpaka wafe kabla ya majeshi yangu kuja. Alikuwa akitoa vitisho visivyowahi kamwe kusikika Zanzibar.
Kuna siku alitangaza kwamba wakazi wa eneo moja ambako alikuwa apite, wajipange foleni barabarani wakiwa wamevaa chupi tu.
Okello alikuwa ni adha, kitisho, kichekesho na fedheha kwa Zanzibar. Viongozi wapya wa nchi walichoka naye na wakaamua kumchukulia hatua. Salim Rashid, mmoja wa viongozi wa Umma Party aliyekuwa katibu wa Baraza la Mapinduzi anasema kwamba, kwanza alilizungumza suala la Okello na Sheikh Karume. Halafu akalizungumza na Brigadia Yusuf Himid na mwisho yeye, Yusuf Himid na Kanali Ali Mahfoudh wakalitafutia dawa.
Ilisadifu kuwa siku moja Okello alisafiri kwenda Dar es Salaam akifuatana na Jaha Ubwa, aliyekuwa katibu wake. Walipokuwa wanatarajiwa kurudi Zanzibar, Karume, Yusuf Himid, Salim Rashid na Ali Mahfoudh walikwenda uwanja wa ndege kumsubiri.
Siku hiyo anaikumbuka vizuri Luteni Hashil Seif aliyekuwa ofisa wa zamu kwenye kambi ya jeshi huko Migombani karibu na uwanja wa ndege. Alipigiwa simu akitakiwa aende kwa haraka uwanja wa ndege. Hakuambiwa anaitiwa nini.
Alipofika ndipo alipoambiwa kwamba kuna ndege ya Shirika la Ndege la Afrika ya Mashariki iliyokuwa inakuja kutoka Dar es Salaam ndani yake wakiwemo pia Okello na Jaha Ubwa. Akaelezwa kwamba awaruhusu abiria wote pamoja na Ubwa washuke, lakini amzuie Okello asishuke. Halafu amwambie rubani ampeleke Okello Kenya.
Hashil naye akampigia simu komredi mwenzake Luteni Amour Dugheshina kumwita aende uwanja wa ndege amsaidie. Maluteni wote wawili walikuwa na bunduki za aina ya machine gun.
Ndege ilipotua walipanda ndani ya ndege, wakampokonya silaha Okello na kutekeleza amri waliopewa. Rubani wa ndege alikasirika sana. Uso wake ulighadhibika, utafikiri mnyama aliyekosewa risasi, alieleza Hashil.
Lakini rubani hakuwa na la kufanya ila kuiwasha ndege na kuelekea Kenya.
Huku nyuma Salim Rashid akampigia simu Oginga Odinga, Makamu wa Rais wa Kenya, kumuarifu kwamba wamemfukuza Okello na wanamrejesha Kenya. Alifanya hivyo kwa makosa kwa sababu kutokana na jina lake akifikiri kuwa Okello ni Mjaluo kutoka Kenya.
Kumbe alikuwa mtu wa kabila la Acholi aliyezaliwa Uganda na alikwenda Unguja kabla ya kuhamia Pemba ambako alikuwa mwashi, mtiaji rangi nyumba na mpasuaji mawe.
Swali la kujiuliza hapa ni; je, iwapo kweli Okello alikuwa kiongozi mpendwa wa Mapinduzi ilikuwaje wafuasi wake na wanamapinduzi wenzake wasimtetee alipoadhiriwa uwanja wa ndege na kufukuzwa nchini? Ilikuwaje akafukuzwa kwa urahisi hivyo?
Kuna uzushi mwingi kuhusu kipindi hiki kifupi cha historia ya Zanzibar. Kwa mfano, kuna filamu ya kubuni ya Wataliana inayoonyesha maiti chungu nzima za watu waliopigwa risasi. Filamu hiyo ilikuwa na lengo moja tu; kuonyesha ukatili na unyama wa Waafrika.
Hakuna ithibati yoyote kwamba watu waliouawa katika siku za mwanzo za Mapinduzi walifika elfu kumi. Ukweli ni kwamba jumla ya watu waliouawa siku hizo haipindukii 200, katika sehemu za mjini hawazidi 25.
Uzushi mwingine ni kwamba walipelekwa Watanganyika, Zanzibar wakiwa na silaha kwenda kupindua. Na si kweli kwamba Mapinduzi yalikuwa na msisitizo wa kikabila. Katika kipindi cha mwanzo cha Mapinduzi msisitizo ulikuwa wa kitabaka. Nyimbo zilizokuwa zikiimbwa kwenye Redio Zanzibar zikiwazungumzia wakwezi na wakulima na wafanyakazi kwa jumla na si makabila.
Mapinduzi ya Zanzibar yalianzisha taasisi mpya za utawala zikiwa pamoja na Baraza la Mapinduzi, Baraza la Mawaziri na ofisi ya Rais. Taasisi hizo zilikuwa zifanye kazi kwa muda wa mwaka mmoja tu kwa vile ilikwishaamuliwa kwamba Januari 1965 pafanywe uchaguzi wa kulichagua Bunge la Katiba, lililokuwa litunge Katiba ya kudumu ya Zanzibar.
Baraza la Mapinduzi la Zanzibar pamoja na Serikali mpya zilianza kwa ubia baina ya chama cha ASP na Umma Party. Ingawa wanachama wa ASP ndio waliofanya Mapinduzi waliutambua mchango wa wafuasi wa Umma Party na hasa mchango wa makada wao waliopata mafunzo ya kijeshi nchini Cuba.
Vijana hao wa Umma walizitia wasiwasi serikali za Marekani na Uingereza na kuzifanya ziamini kuwa utawala mpya wa Zanzibar ulikuwa wa kikomunisti. Dhana hiyo ndiyo iliyosababisha kuchukuliwa hatua ya kuyachimba na kuyagandamiza Mapinduzi ya Zanzibar yaliyodumu kutoka Januari 12, hadi 26 Aprili, mwaka 1964.

Cc.. Wickama, Mag3, gombesugu, Barubaru, Nguruvi3, Kadogoo, JokaKuu, WildCard, THE BIG SHOW, Jasusi, zomba, Spike Lee, Pasco, Mzee Mwanakijiji,

Alichoeleza Ahmad Rajab ni sahihi kabisa kwani ndio kwani yeye mwenyewe ni mmoja walioshuhudia mapinduzi hayo akiwa na Rafiki yake Salem Saleh mitaa ya shanghani.

Kwani mambo haya yanataka umakini sana katika mapokeo yake lakin utapata machungu sana kama utaingiza ushabiki.

Kumbuka kuwa Brig Yusuf Himid ndie aliyakuwa Mkuu wa kwanza wa majeshi upand ewa Znz na akina Seif Bakari ( nilizowea kumwita mndengereko wa jang'ombe) alikuwa msaidizi wake.

Ahsantum Ritz kumwekea historia toka kwa mtafiti ambaye alishuhudia tukio hilo.

 
Ritz

Hawa wote akina Mohamed Said, Dr Ghassany, Ahmed Rajabu na wengine wengi, ni aina ile ile, yani unaweza kuita ni mtu mmoja linapokuja suala la Nyerere, uislamu na ukristu!

Kama nimsomaji mzuri wa machapisho yao wala hutapata kuumiza kichwa,

Wao wanamakovu ya Okello na wengine wanamakovu ya Nyerere!

Hivyo kamwe hawezi kuwa 1 mbele ya haya!


Kwani Nyerere ni nani mbele ya watu hao mpaka wamchukie.

kumbuka kuwa matendo yako na tarbia zako ndio zinazokuhukumu. na Nyerere anahukumiwa kwa matendo yake alotenda na si vinginevyo.

tafadhwali usimtukuze mtu kiasi cha kukufuru na kumpa swifa za uungu kama unavyotaka kumpa Nyerere.

Pole sana
 
Mbona unaropoka kwa hamaki hivyo?

Wapi nimesema mimi ndie mwandishi?

Hukuona makala zingine zote nilizoleta hapa nilikuwa naweka jina langu mwisho?

Usiwe na papara kijana, tulia soma na ujue mantiki!

Musimulizi wa hayo ni Barghash:

Sikiliza dogo hapa unaongea na vichwa vya Madrassa usilete ujanja ujanja.

Mohamed Said, kakuuliza kama unajua chochote kuhusu mapinduzi weka ulivyokuwa kauzu umejitapa kisha ukamjibu kwa maandishi ya mtu mwingine kwa kuwa wewe huna unachokijua.

Bila mimi kusema ungemtaja mwenye maandishi wa hiyo makala? Acha utoto.

Cc.. gombesugu, Barubaru,
 
Last edited by a moderator:
Alichoeleza Ahmad Rajab ni sahihi kabisa kwani ndio kwani yeye mwenyewe ni mmoja walioshuhudia mapinduzi hayo akiwa na Rafiki yake Salem Saleh mitaa ya shanghani.

Kwani mambo haya yanataka umakini sana katika mapokeo yake lakin utapata machungu sana kama utaingiza ushabiki.

Kumbuka kuwa Brig Yusuf Himid ndie aliyakuwa Mkuu wa kwanza wa majeshi upand ewa Znz na akina Seif Bakari ( nilizowea kumwita mndengereko wa jang'ombe) alikuwa msaidizi wake.

Ahsantum Ritz kumwekea historia toka kwa mtafiti ambaye alishuhudia tukio hilo.


Shariff Barubaru,

Kuna vitu vingine inabidi ujifunze kutoka kwa wahusika haiwekani mtu anatoka Mwitongo au Magu au Kemendo, anataka kuelezea historia ya mapinduzi ya Zanzibar.

Mimi binafsi kuhusu mapinduzi ya Zanzibar nimejifuza kutoka kwa wahusika wenyewe waliokuwepo.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom