Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Hii shule tunayopata kwenye huu mjadala ni kali,kumbe Field Marshall OKELLO ndio baba wa taifa wa zanzibar-asanteni wachangiaji

Karibu sana dada jackline1,

Huo ndio ukweli mchungu kwa baadhi ya wahafidhina wa Zanzibar!

Wanalijua hilo lakini kwao wanaona ni aibu,

Wacuba leo hii baba wa taifa lao ni mgeni kabisa Ernest Che Guevara,

Imewalazimu kwa heshima ya kutambua mchango wake wamesafiri mpaka Argentina kufukua kaburi la Che-Guevara nakuja kulizika kitaifa nchini Cuba!

Sasa leo wazalendo hawa wa Zanzibar wakiamua kumuenzi mkombozi wao dhidi ya minyororo ya utumwa kuna ubaya gani kwao?
 
Karibu sana dada jackline1,

Huo ndio ukweli mchungu kwa baadhi ya wahafidhina wa Zanzibar!

Wanalijua hilo lakini kwao wanaona ni aibu,

Wacuba leo hii baba wa taifa lao ni mgeni kabisa Ernest Che Guevara,

Imewalazimu kwa heshima ya kutambua mchango wake wamesafiri mpaka Argentina kufukua kaburi la Che-Guevara nakuja kulizika kitaifa nchini Cuba!

Sasa leo wazalendo hawa wa Zanzibar wakiamua kumuenzi mkombozi wao dhidi ya minyororo ya utumwa kuna ubaya gani kwao?

Wewe dogo mbona muongo muongo sana, hujui historia ya Guevara.

Kwanza siyo Ernest ni Ernesto Guevara wala hakufia Argentina alifia Bolivia.

Nifunguke zaidi nikupe darsa?

Hivi unajua historia ya taifa la Cuba au unaropoka tu.

Baba wa Taifa wa Cuba ni Carlos Manuel De Cespedes.

Umeipata wapi kuwa Che Guevara ni raia wa Cuba?
 
Field Marshal John Okello yawezekana wapo watu wakajidanganya kuwa wanaweza kufuta historia yake lakini dunia itaendelea kumkumbuka kama huyu mbunge wa Uganda alivyoandika Jumapili Octoba 7, 2012 wakati wa kusherehekea siku ya uhuru wa Uganda.

Field Marshal John Okello, the forgotten hero
The writer is MP for Ajure County

As Uganda celebrates independence, let me bring into perspective the sacrifices made by Field Marshal John Okello in the liberation of the present day Zanzibar.

On January 12, 1964, with popular support from the Island’s oppressed native African majority, Okello and his men fought their way to the capital of Zanzibar, Stone Town, where the Sultan lived. Even though they were poorly armed, Okello and his men surprised the police force of Zanzibar and they took over power.

A Ugandan peasant turned revolutionary, Okello does not deserve to be forgotten by both his home country Uganda and the country he freed; current day Zanzibar.

My recent visit to Zanzibar reawakened my historical recollection and memory about the patriotic role played and legacy left by a Ugandan born revolutionary Field Marshal John Okello in the 1964 Zanzibar Revolution.

In major historical sites in Zanzibar, the name of Field Marshal John Okello is inscripted amongst the 31 members of the Revolutionary Committee/Council that staged the successful, historical and remarkable revolution of Zanzibar. In African history, Zanzibar is viewed as the fountain of civilization in East and Central Africa with her great mercantile past and a literate and Islamic Swahili culture that existed for centuries.

According to Zanzibari historical sources, during a speech on radio after the takeover, Okello dubbed himself the “Field Marshal of Zanzibar and Pemba”. In fact, some political analysts consider/considered him as the first President of the new Revolutionary Government of Zanzibar.

The self proclaimed Field Marshal there after created the Revolutionary Council and named the leader of the Afro-Shirazi Party, Abeid Karume as President. Karume was residing in Tanganyika, but returned to Zanzibar, where he was welcomed by Okello.

Afterwards, Okello appeared to be too unstable to play any role in government of the new country and was quietly sidelined from the political scene by President Karume, who only allowed him to retain his title of Field Marshal.

But after two months, he was captured and declared a prohibited immigrant while he was in Tanganyika, then later sent to Kenya. He was incarcerated multiple times and was allegedly last seen with the Ugandan President Idi Amin in 1971 and vanished afterwards.

In the book “Revolution of Zanzibar”, written by Don Petterson, it is more or less assumed and believed that Idi Amin saw him as a threat. It is further alleged in that book that after President Amin promoted himself, Okello reportedly joked that “now Uganda has two Field Marshals”, and had arranged his assassination. This remains speculative, however.

In April 1964, three months after the Revolution, the then Tanganyika and Zanzibar decided to make a hasty Constitutional merger of their two countries. The new state was named Tanzania, Nyerere as the Union President, Karume and Rashid Kawawa became the two Vice Presidents of Tanzania.

Okello is a born of Iyama village, Alebtong Parish, Aloi Sub-county, Moroto county, Alebtong District (Formerly part of Lira District), Lango Sub-region. He is survived by two wives and children. According to family sources, he left his home village at 15 and set out on his own and found work in several places within East Africa. Okello left for Pemba and Zanzibar in 1959 and 1963 respectively where he lived and worked as a clerk, manservant, gardener and later on a police officer.


More importantly, the dependants of the late Field Marshal Okello live in chronic and abject poverty. I therefore appeal to the Government of Uganda in conjunction with the Revolutionary Government of Zanzibar to honestly come in and extend a hand of help aimed at salvaging the plight of Field Marshal John Okello’s dependants.
 
Alichoeleza Ahmad Rajab ni sahihi kabisa kwani ndio kwani yeye mwenyewe ni mmoja walioshuhudia mapinduzi hayo akiwa na Rafiki yake Salem Saleh mitaa ya shanghani.

Kwani mambo haya yanataka umakini sana katika mapokeo yake lakin utapata machungu sana kama utaingiza ushabiki.

Kumbuka kuwa Brig Yusuf Himid ndie aliyakuwa Mkuu wa kwanza wa majeshi upand ewa Znz na akina Seif Bakari ( nilizowea kumwita mndengereko wa jang'ombe) alikuwa msaidizi wake.

Ahsantum Ritz kumwekea historia toka kwa mtafiti ambaye alishuhudia tukio hilo.

Hahaa mkuu, wanajamvi wanakusoma wazi!

Kumbuka maelezo yako ya mwanzo ulisema hutaki kabisa kuzungumzia mapinduzi yale chini ya Okello ukisema wazi yalipoteza watu wengi sana wakiwemo ndugu zako wa damu,

Lakini baada yakumsoma mpotoshaji mwingine Ahamed Rajab umegeuka na kuwa upande wake,

Unanishangaza kwa hilo mkuu, kumbuka wewe uliyashuhudia mapinduzi yale
 
Field Marshal John Okello yawezekana wapo watu wakajidanganya kuwa wanaweza kufuta historia yake lakini dunia itaendelea kumkumbuka kama huyu mbunge wa Uganda alivyoandika Jumapili Octoba 7, 2012 wakati wa kusherehekea siku ya uhuru wa Uganda.

Mkuu kwakweli inachekesha hasa ukiwaona hawa ndugu zangu wanapopika data za uongo na ngano kibao ilimradi kupotosha umma na kumuondoa Okello katika historia ya Zanzibar!

Ukweli histori hujiandika, na huwa haibadilishwi bali hujibadilisha yenyewe!

Kamwe huwa haifuti ama kujifuta!
 
Hahaa mkuu, wanajamvi wanakusoma wazi!

Kumbuka maelezo yako ya mwanzo ulisema hutaki kabisa kuzungumzia mapinduzi yale chini ya Okello ukisema wazi yalipoteza watu wengi sana wakiwemo ndugu zako wa damu,

Lakini baada yakumsoma mpotoshaji mwingine Ahamed Rajab umegeuka na kuwa upande wake,

Unanishangaza kwa hilo mkuu, kumbuka wewe uliyashuhudia mapinduzi yale
Sayyid Jamshid bin Abdullah Al Said hawezi kumsahau Field Marshal John Okello, Dunia haiwezi kumsahau Field Marshal John Okello, Afrika Mashariki haiwezi kumsahau Field Marshal John Okello na Zanzibar ndiyo kabisa haitaweza kumsahau Field Marshal John Okello. Kama si hekima na juhudi za Mwalimu Nyerere ya kumshawishi Okello aje Dar es Salaam na kumpa nafasi Karume apumue, mambo yangekuwa mengine kabisaaa.
 
Sayyid Jamshid bin Abdullah Al Said hawezi kumsahau Field Marshal John Okello, Dunia haiwezi kumsahau Field Marshal John Okello, Afrika Mashariki haiwezi kumsahau Field Marshal John Okello na Zanzibar ndiyo kabisa haitaweza kumsahau Field Marshal John Okello. Kama si hekima na juhudi za Mwalimu Nyerere ya kumshawishi Okello aje Dar es Salaam na kumpa nafasi Karume apumue, mambo yangekuwa mengine kabisaaa.

Hili darasa linanizidi kimo- kwa hiyo wa kulaumiwa ni nyerere????? kwa kumuondoa okello katika historia kama inavyodaiwa alivyowaondoa wazee wa gerezani?????????
 
Hili darasa linanizidi kimo- kwa hiyo wa kulaumiwa ni nyerere????? kwa kumuondoa okello katika historia kama inavyodaiwa alivyowaondoa wazee wa gerezani?????????

Hehee dada mada hii ni nzuri na chungu kwa wabora sisi,


Ukipekua ukura wa pili ama wa tatu nyuma hapo nimeweka makala inayoeleza wazi utawala wa Okello wa miezi sita ulivyokuwa mgumu kwa watu na sababu za Mwalimu kutumia turufu ileile aliyotumia kumshawishi Gavana Twaining wa kutupa nchi yetu ndipo akamshawishi Okello aje ikulu Dar na maridhiano ya kukabidhi madaraka kwa karume yakatukia!


Karume asingeguza ikulu ya zanzibar na kuwa rais bila mwanadiplomasia mahiri wa afrika Julius Kambarage Nyerere!
 
kwa hiyo kiuhalisia rais wa kwanza wa zanzibar ni Okello???


"According to Zanzibari historical sources, during a speech on radio after the takeover, Okello dubbed himself the "Field Marshal of Zanzibar and Pemba". In fact, some political analysts consider/considered him as the first President of the new Revolutionary Government of Zanzibar"
 
Hili darasa linanizidi kimo- kwa hiyo wa kulaumiwa ni nyerere????? kwa kumuondoa okello katika historia kama inavyodaiwa alivyowaondoa wazee wa gerezani?????????
jackline, kwanza mpe heshima kidogo Baba wa Taifa...ni Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Pili tarehe 9/12/1961 Tanganyika ikijikomboa kutoka mikononi mwa mkoloni mwingereza, aliyeongoza mapambano alikuwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Tatu, tarehe 12/1/1964 Zanzibar ikijikomboa kutoka mikononi mwa mkoloni mwarabu, aliyeongoza mapambano alikuwa Field Marshal John Okello.




Iti is Field Marshal John Okelo who named the leader of the Afro-Shirazi Party, Abeid Karume as President. Karume was residing in Tanganyika, but returned to Zanzibar, where he was welcomed by Okello.
 
Last edited by a moderator:
Hivi kuna swali limenijia;

Abdulwahid Sykes alikuwa upande gani ilipoundwa AMNUT?
Abdulwahid Sykes alikuwa upande gani ilipovunjika EAMWS?

(Alisema nini kuhusiana na yote haya mawili?)
 
Wanajmvi,
Nakumbuka mwaka jana tulikuwa na mjadala huu wa mapinduzi na ushiriki wa Nyerere. Katika mjadala huo swali langu lilikuwa lile lile '' kwanini wznz wanasherehekea na kutukuza mapinduzi'' yaliyokuwa na dhima ya kuua Uislam?

Swali la pili likiwa ''kwanini kuna wznz wanasema mapinduzi daima, na wengine wanasema mapinduzi haram''?
Baada ya kukosa majibu, Ahmed Rajab kwa kutumia gazeti la Raia mwema alitoa majibu.
Ingawa hakusema ni kujibu JF mnakasha, dhahiri ilikuwa na lengo hilo kwa mwenye akili.

Ahmed alisema, inategemea wakati wa mapinduzi nani alikuwa upande gani. Akasema wapo walioona mapinduzi yalikuwa na mnaufaa na wapo waliosema hayana manufaa kwa kuzingatia masilahi ya kila mmoja kwa wakati ule.
Hakuweza kusema ni halali au siyo zaidi ya habari nyingine.

Leo nimemsoma Mohamed Said kurasa chache zilizopita. Yeye anatamba kutaja majina ya waliohusika na punda waliohusika nadhani akimaanisha waislam walioshiriki kama ndivyo.

Ukisoma maelezo ya Ahmed na Mohamed yanatofautiana sana na ni wazi kuwa kwa hili kila mmoja anavutia upande wake ingawa wana common interest ambayo ni mashambulizi dhidi ya Nyerere. Kwa Ahmed si makali kama Mohamed.

Mohamed anasema yeye ni mtafiti na amefanya utafiti. Kitu cha kushangaza ni kuwa utafiti siku zote hueleza pale ambapo utafiti zaidi unahitaji au kama hakuna basi conclusion ya ule uliopo.

Sasa utafiti wa Mohamed ni pamoja na kupata majina ya waliohusika hata kufahamu nani alilala kwa bibi au babu yake.
Yote hayo ni kheri. Kinachosumbua sana katika utafiti wake ni pale ambapo utafiti unashindwa kujibu hoja muhimu sana.

Anadai Nyerere alipeleka wamakonde wa Kipumbwi kwenda kupindua serikali ya Sultan kwa lengo la kuua uislam.
Kwa maneno mengine mapinduzi ni haramu kwasababu hayakutokana na wznz bali Nyerere na ukatoliki wake.

Sasa tunapomuuliza conclusion ya maneno yake hana jibu anakimbia huku na huko akitaja majina ya watu.
Mohamed, Je, unawaambia nini wznz, kwamba mapinduzi ni haramu na waache kuyatukuza?

Haiwezekani iwe haramu kufanya mapinduzi kulikotokana na Nyerere halafu ikawa halali kwa waislam wa znz kutukuza mapinduzi haramu!!!

Wapi haram ilikuwa halali kisa imeshikwa na mwislam?

Contradictions kama hizi zinafanya watu wahoji, nini maana ya utafiti kama hauna answer to the question.
Is it not fabrication?

Bottom line, Je, mzanzibar ana uhalali wa kushangilia na kutukuza mapinduzi? Kama ni ndiyo,je, Nyerere apongezwe au alaumiwe? kama ni hapana mapinduzi ni haram? Jibu likiwa ndiyo, halali ya waislam 99 wa znz kuyashangalia inatoka wapi?
 
kwa hiyo kiuhalisia rais wa kwanza wa zanzibar ni Okello???


"According to Zanzibari historical sources, during a speech on radio after the takeover, Okello dubbed himself the “Field Marshal of Zanzibar and Pemba”. In fact, some political analysts consider/considered him as the first President of the new Revolutionary Government of Zanzibar"

Huo ndio ukweli pekee unaokwepwa bila sababu za msingi!

Field Marshal John Okello au Mungu wa Afrika ndie BABA halisi wa Taifa la Zanzibar,

Ulie, ukatae, unune, ususe huo ndio ukweli!

Na wazanzibar wanayo fursa ya kumuenzi kama mkombozi wao sio kuyaenzi tu mapinduzi yake kwa mgongo wa chupa!
 
Wanaukumbi nafurahi kiasi naoa mjadala unaelekea ukingoni hoja mbali mbali zimejibiwa kiustaharabu na kwa ufundi wa hali ya juu sana.Nimefurahi kuona jambo moja likijitokeza wazi pasipo na shaka yoyote kwamba sumu iliyokuwa ikimwagwa kwa muda mrefu hatimaye imepata majibu stahiki.Ni wajibu wetu sote kuhakikisha masuala ya mazito kama haya yanapojitokeza yasiachwe yakisambaa kwa muda mrefu yakaharibu jamii yetu.

Nawashukuru wote waliojitolea muda wao mwingi na kushughulisha akili kwa faida ya VIZAZI VYA SASA NA VIJAVYO hapa pia napenda angalizo na Wickama lizingatiwe sana hii mitandao ina nafasi kubwa na pana kuliko hata vitabu ambavyo kwa sehemu kubwa havisomwi na vijana wengi ukilinganisha na mitandao.

Sasa wewe unashukuru, mara unasifia, nani kakupa kazi ya kuwa kama mgeni rasmi aliealikwa kufungua na kufunga mijadala? huna lolote unalochangia ktk mnakasha huu wa Yericko juu yakile kinachoitwa uchochezi wa MS! kazi yako wewe ni kudandia na kuteremka! we una tuwekea Conclusion hapa kama nani?
 
Yan Yericko sasa amefikia hatua mbaya sana,anatufananaisha Moh Said na vijana wake sawa na wanawake wa saluni??
Kweli kakosa malezi ya baba,si bure..!
 
Hivi kuna swali limenijia;

Abdulwahid Sykes alikuwa upande gani ilipoundwa AMNUT?
Abdulwahid Sykes alikuwa upande gani ilipovunjika EAMWS?

(Alisema nini kuhusiana na yote haya mawili?)
Mzee Mwanakijiji, Abdulwahid Sykes alipata nafasi tatu za kuonesha alivyo maarufu kisiasa, mahiri kiuongozi na mashuhuri kijamii.

  1. Nafasi ya kwanza ilijitokeza mwaka 1950 alipogombea nafasi ya uongozi wa juu wa TAA katika uchaguzi uliofanyika kumpata kiongozi mwenye sifa zote hizo.
  2. Nafasi ya pili aliipata mwaka 1953 uchaguzi wa TAA ulipofanyika kumpata kiongozi mwenye "vision" ambaye angeweza kuiwezesha TAA kukabiliana na changamoto mpya zilizoikabili
  3. Nafasi ya tatu ilijitokeza mwaka 1954 chama cha TANU kilipozaliwa na kutakiwa kiongozi ambaye angeweza kusimamia imara harakati za kisiasa katika kudai uhuru.
Baada ya hapo? Your guess is as good as mine...a boxful of disappointment. Je kitu gani kilifuatia baada ya hapo? Hizi simulizi za Mohamed Said nadhani zinatupa kwa mbali taswira ya yaliyomsononesha Abdulwahid Sykes. Je kama kungetokea chama pinzani na TANU, angekiunga mkono hata kama si kwa waziwazi? Ni nini chanzo cha machungu yaliyomo ndani ya simulizi alizokuwa akipewa Mohamed Said utotoni? Ni kitu gani kiko nyuma ya malalamiko yale? Mathalani mwaka 1958 tunawaona waliokosa uvumilivu kama Chamwenyewe wakiaasisi AMNUT kwa imani kwamba kitaungwa mkono na waumini wenzake halafu kinakataliwa na hao hao waumini...disappointment on top of disappointment! As I said before, your guess is as good as mine.
 
Shariff Barubaru,

Kuna vitu vingine inabidi ujifunze kutoka kwa wahusika haiwekani mtu anatoka Mwitongo au Magu au Kemendo, anataka kuelezea historia ya mapinduzi ya Zanzibar.

Mimi binafsi kuhusu mapinduzi ya Zanzibar nimejifuza kutoka kwa wahusika wenyewe waliokuwepo.

Nasisi wengine tuna fyonza ILM toka kwa MS na yeyote mkweli!
 
Nyerere alikuwa na nia kubwa ya kupambana na Uislam wa Tanganyika.

Kumbuka kuwa wazungu walitumia devide and Rule katika utawala wao na kwa kuangalia mazingira ya nchu husika.

Tukianzia na Kenya na Uganda huko kulikuwa na makabila machache sana huko waliyumia UKABILA katika kuwatawala na hilo mpaka leo linawasibu kama kovu la ukoloni.

Kwa upande wa Tanganyika ambako kulikuwa na makabila mengi sana alishindwa kutumia mbinu hiyo na hapo walitumia UDINI yaani dini moja kuifanya superior zaidi ya nyingine, wasomi zaidi ya nyingine na walifanikiwa kwalo.

Kwa kuwa Nyerere alikuwa na nia ya kuliendeleza hilo alipenda kuungana na waZnz ili kuwalagha waislam kutoka Bara. na hata alipogawa madaraka hakukuwa na waislam kutoka bara bali walichukua watu kutka Znz.

ndio maana nasema ni vizuri tuweke uzi maalum tusasambue kwani wengine tumeyaona hayo bila kusimuliwa.

Baubau, Sikajiji ameuliza swali rahisi sana. ''Je wewe unadhani Nyerere aliinjinia Mapinduzi''
Hayo maelezo yako hapo juu hayajibu swali.

Katika maelezo yako hapo juu unajaribu sana kuweka fikra zako zaidi ya ukweli licha ya kukimbia swali la msingi.
Nakuomba uzirejee sababu zilizopelekea Karume kukubali muungano. Katika hili lazima uwafikirie akina A.Babu na Uslama wa Karume.

Lakini basi kama Nyerere alitaka kuwalaghai waislam wa Tanganyika, je hiyo ndiyo sababu ya yeye kuinjinia Mapinduzi?

Mzanzibar anaposhindwa kuieleza historia ya nchi yake inashangaza na kusikitisha
 
Mzee Mwanakijiji, Abdulwahid Sykes alipata nafasi tatu za kuonesha alivyo maarufu kisiasa, mahiri kiuongozi na mashuhuri kijamii.

  1. Nafasi ya kwanza ilijitokeza mwaka 1950 alipogombea nafasi ya uongozi wa juu wa TAA katika uchaguzi uliofanyika kumpata kiongozi mwenye sifa zote hizo.
  2. Nafasi ya pili aliipata mwaka 1953 uchaguzi wa TAA ulipofanyika kumpata kiongozi mwenye "vision" ambaye angeweza kuiwezesha TAA kukabiliana na changamoto mpya zilizoikabili
  3. Nafasi ya tatu ilijitokeza mwaka 1954 chama cha TANU kilipozaliwa na kutakiwa kiongozi ambaye angeweza kusimamia imara harakati za kisiasa katika kudai uhuru.
Baada ya hapo? Your guess is as good as mine...a boxful of disappointment. Je kitu gani kilifuatia baada ya hapo? Hizi simulizi za Mohamed Said nadhani zinatupa kwa mbali taswira ya yaliyomsononesha Abdulwahid Sykes. Je kama kungetokea chama pinzani na TANU, angekiunga mkono hata kama si kwa waziwazi? Ni nini chanzo cha machungu yaliyomo ndani ya simulizi alizokuwa akipewa Mohamed Said utotoni? Ni kitu gani kiko nyuma ya malalamiko yale? Mathalani mwaka 1958 tunawaona waliokosa uvumilivu kama Chamwenyewe wakiaasisi AMNUT kwa imani kwamba kitaungwa mkono na waumini wenzake halafu kinakataliwa na hao hao waumini...disappointment on top of disappointment! As I said before, your guess is as good as mine.

Wanajamvi,
Abdu Sykes hakupata kuipa mgongo TANU kwa mapenzi wala ufadhili.

Katika Tatizo la AMNUT yeye alikuwa upande wa Nyerere kama wenzake
wote alioundanao TANU toka enzi za TAA 1950s hadi rasmi walipoiunda
1954.

Kuhusu EAMWS hili alikuwa upande wa Waislam na nimeeleza katika kitabu
mazungumzo yake na Nyerere Ikulu kuhusu kuandamwa Waislam siku chache
kabla hajafa.

Abdu hakuwa mtu aliyechangia kuasisi TANU kwa kukamata nafasi za uongozi.
Abdu yeye sifa yake kubwa ni kile kipaji chake cha kusuka mipango dhidi ya
Waingereza na kufadhili harakat.

Haya yote nimeyaeleza katika kitabu toka alipokuwa Burma hadi alipohusika
na mgomo wa makuli 1947, kuleta mageuzi ya uongozi TAA 1950 na mwisho
kuasisi TANU 1954 kadi yake ikiwa na 3, mdogo wake Ally Sykes kadi na 2 na
Nyerere kadi na 1.

Said Chamwenyewe hakupata kuwa mwanachama wa AMNUT yeye alikuwa Congress
na Zuberi Mtemvu.

Juu ya maelezo haya mtu bado yuko huru kuamini historia aionayo imemkalia vizuri.
 
Back
Top Bottom