kmbwembwe
JF-Expert Member
- Aug 16, 2012
- 10,892
- 7,780
Ubeberu wa kimataifa umejiundia tangu kale mahusiano ya kiuchumi ambayo wao ni kama bahari. Mito yote kutoka nchi kavu na maziwa lazima yaishie kwao baharini.
Kuna mito huingia kwenye maziwa halafu kuna mito inatoka kwenye maziwa kwenda baharini. Kenya ni kama ziwa kwa uchumi wa tanzania. Wanatunyonya kutokana na uchumi wao mkubwa wa viwanda tangu ukoloni. Kila tanzania ikijaribu kuelekeza baadhi ya bidhaa zake moja kwa moja kwenye masoko ya nje kwa kuziongeza thamani wenyewe bila kuzipitisha Kenya hapo kunatokea kutoelewana. Kenya watatumia kila njia na hila kutukwamisha. Kama ni mifugo kama ni mazao au madini mambo kwa tanzania yanakua magumu kufunga mto wa kiuchumi unaopita kenya kuelekea baharini.
Suala hili la madini ya tanzanite linahitaji ujasiri mkubwa kuwazuia wakenya wasiendelee kunyonya na kuidhulumu tanzania. Tumejenga ukuta lakini unatobolewa tanzanite inafika kenya kwa kiasi kilekile au zaidi. Tumeweka EPZ mererani ubeberu wameweka upofu wa kusudi kwa baadhi ya viongozi kama sendeka alivyomueleza waziri mkuu. Dealers wakubwa wahindi na wakenya wameazimia hatufanikiwi lazima tanzanite iende kua processed kenya na india. Wao ndio wapate faida na watu wao wapate kazi. Sisi tupate makombo na serikali yetu isipate kodi.
Kuna mapambano makali kutoka jirani zetu kuhakikisha licha resources tulizo nazo hatuwi uchumi mkubwa kuliko wao. Yaani sisi tusiwe ziwa kama wao au mto mojakwa moja kuelekea baharini kiuchumi. Lazima tuongeze ujasiri tusiwe wa kuibiwa kwa nguvu uchumi na jirani na huku kimataifa kwenye biashara ubeberu unatukandamiza.
Mahusiano mazuri na Kenya isiwe sisi kukaa kimya huku kila mbinu ya kukuza uchumi wetu uchumi wao unatuhujumu kwa kupitisha madini na bidhaa zetu njia za panya bila wao kutoa ushirikiano kuzuia kwa kua wao ni wanufaika.
Kuna mito huingia kwenye maziwa halafu kuna mito inatoka kwenye maziwa kwenda baharini. Kenya ni kama ziwa kwa uchumi wa tanzania. Wanatunyonya kutokana na uchumi wao mkubwa wa viwanda tangu ukoloni. Kila tanzania ikijaribu kuelekeza baadhi ya bidhaa zake moja kwa moja kwenye masoko ya nje kwa kuziongeza thamani wenyewe bila kuzipitisha Kenya hapo kunatokea kutoelewana. Kenya watatumia kila njia na hila kutukwamisha. Kama ni mifugo kama ni mazao au madini mambo kwa tanzania yanakua magumu kufunga mto wa kiuchumi unaopita kenya kuelekea baharini.
Suala hili la madini ya tanzanite linahitaji ujasiri mkubwa kuwazuia wakenya wasiendelee kunyonya na kuidhulumu tanzania. Tumejenga ukuta lakini unatobolewa tanzanite inafika kenya kwa kiasi kilekile au zaidi. Tumeweka EPZ mererani ubeberu wameweka upofu wa kusudi kwa baadhi ya viongozi kama sendeka alivyomueleza waziri mkuu. Dealers wakubwa wahindi na wakenya wameazimia hatufanikiwi lazima tanzanite iende kua processed kenya na india. Wao ndio wapate faida na watu wao wapate kazi. Sisi tupate makombo na serikali yetu isipate kodi.
Kuna mapambano makali kutoka jirani zetu kuhakikisha licha resources tulizo nazo hatuwi uchumi mkubwa kuliko wao. Yaani sisi tusiwe ziwa kama wao au mto mojakwa moja kuelekea baharini kiuchumi. Lazima tuongeze ujasiri tusiwe wa kuibiwa kwa nguvu uchumi na jirani na huku kimataifa kwenye biashara ubeberu unatukandamiza.
Mahusiano mazuri na Kenya isiwe sisi kukaa kimya huku kila mbinu ya kukuza uchumi wetu uchumi wao unatuhujumu kwa kupitisha madini na bidhaa zetu njia za panya bila wao kutoa ushirikiano kuzuia kwa kua wao ni wanufaika.