DOKEZO Uchunguzi: 'Makanisa ya Kiroho' na shuhuda FEKI kuwahadaa watanzania

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Dini zimevamiwa na matapeli...
 
Kuna Jamaa kaanzisha...kanisa la mbogamboga...alianza na kupata sadaka laki 2...3....Sasa hivi kila jpili anakusanya si chini ya m10......
Ameanza na kubadili namna ya kuongea...maringo..madoido....kwa kifupi...kiburi..
Anataka watu wamtukuzee🙄🙄🙄
 
Kule kwa Papa, waamini wameambiwa wapeleke shuhuda zao kwa kulipa zaka, halafu eti hizo shuhuda zinapitiwa/ hakikiwa kwanza na kamati ya zaka!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
mleta hoja huko hapaoni, kakazana na makanisa ya kiroho. Nimuombe akayajue kwanza makanisa ya kiroho yakoje na mafundisho ni nini ndio alete utafiti wake tuuchambue tumpe ukweli wa mambo, naona kama anachanganya matango pori , magugu na ngano. Hawa watunga shuhuda za uongo ni wale waganga wa kienyeji walio advance kufuata wateja wao wanakokimbilia kwenye dini baada ya kuwagundua uongo wao. Wanawafuatilia wateja wao kulekule wanakoamini watatuliwa shida zao. Wateja wanapenda dini na waganga wao ikabidi wajibadili kuwa wa dini, matokeo yake ndio hayo maji na mafuta ya upako, keki ya upako na upuuzi mwingine mwingi ukishadidiwa na shuhuda za uongo. Watu wanabebwa na upepo wa kila aina mradi tu watatuliwe shida zao. Wakubwa kwa wadogo walinyweshwa kikombe cha dawa feki za mitishamba kwa ujinga
 
Nyie ambao mnajiona mko sahihi katika dini na madhehebu yenu kaeni na waumini vizuri, wafundisheni kweli ya Mungu wenu. Kama nanyi ni wapuuzi ni lazima mkimbiwe na waumini wenu, wanaenda kwa wapuuzi wengine zaidi yenu halafu mnakuja kulialia humu kuwa mnanyang'anywa waumini kwa shuhuda za uongo wakati nanyi ni wapuuzi walewale tu ila mmezidiana upuuzi wenu. Mnawafanya binadamu wenzenu kuwa watumwa wa fikra zenu kwa kuwabebesha mizigo mizito ya ujinga, maradhi na umasikini. Hubirini kweli iwaweke huru waumini wenu. Tokeni gizani mje kwenye nuru muone mwanga wa matumaini ya kweli
 
Hawa jamaa wanakera sana. Pamoja na hayo yote, bado Bwana Yesu anatenda miujiza ya kweli kupitia watumishi wake wa kweli wanaomtafuta Bwana na nguvu zake. LAKINI muujiza mkuu kwa mwanadamu ni ile hali ya kutubu na kuokoka. Yaani kuishi maisha matakatifu mbali na dhambi huo ndio muujiza mkuu kuacha dhambi. Mithali 28:13. Afichaye dhambi zake hatafanikiwa. Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.
 
Kibaya zaidi kajianika ye ni wa wapi
 
Hizi dini hizi zikiendelea mpaka 2030 tutakuwa maskini sana
 
Yesu Kristo ( Masihi ), katika enzi zake alipingwa pia, ikiwamo yeye kama yeye na hata miujiza aliyokuwa anafanya wakamuambia anafanya kwa nguvu za belzababu.. Hata manabii walio kuwa kabla yake walipigwa sana pia na wengine hata kuuwawa... Ije kwa nyakati hizi ? ambapo Paul Apostle anasema .....

Neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu. Mungu alipenda kuwaokoa waaminio kwa upuzi wa lile neno linalohubiriwa. Kwa sababu upumbavu wa Mungu una hekima zaidi ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…