Udalali wa kutisha wa ardhi ya nchi, Profesa Shivji aonya kuwa watawala hawaoni mbali, wanaangalia pafupi sana

Udalali wa kutisha wa ardhi ya nchi, Profesa Shivji aonya kuwa watawala hawaoni mbali, wanaangalia pafupi sana

S
Professa wa sheria Issa Shivji wa Tanzania anayeheshimiwa duniani na aliyefundisha na kutafiti na kuandika vitabu vingi vya masuala ya ardhi anawakumbusha Watanzania: nchi inauzwa kwa kasi na "Wamawakala wapya wa mabeberu." ambao anasema sifa zao ni "Watawala hawaoni mbali. Siasa zao ni za muda mfupi. Maono yao ni finyu." Na anamalizia kwa kuandika jukumu la kulinda ardhi ya nchi ni la nani.

=========

’TULIPO. TUNAKOELEKEA’ 2 TAFAKURI YA KILA WIKI UPORAJI WA MALIASILI MAMA – ARDHI

PROF. ISSASHIVJI

Jul 7, 2024

Tangu wakoloni wavamie nchi yetu mwishoni mwa karne ya 19 na mwanzoni mwa karne ya 20, uporaji wa ardhi umeendelea. Katika miongo takriban saba hivi wakoloni walitwaa ardhi ya wenyeji kwa ajili ya makampuni ya nje na walowezi ingawa Tanganyika haikuwa ukoloni ambako walowezi wa kizungu walipora maeneo makubwa ya ardhi kama Kenya au nchi za Kusini mwa Bara kama Zimbabwe, Namibia na Afrika Kusini.

Katika miaka takriban sitini baada ya uhuru tena wazalishaji wadogo hususan wakulima na wafugaji wakajikuta ardhi yao inachukuliwa kwa visingizio mbalimbali. Hata nyakati ya awamu ya kwanza ardhi ya wazalishaji haikuwa salama. Taasisi za serikali kama jeshi, magereza n.k walivamia na kuchukua ardhi ya wenyeji na kuzaa migogoro ya ardhi isiyoisha. Kila mara mipaka ya hifadhi inapopanuliwa ardhi ya wakulima na hasa wafugaji inamezwa. Taasisi zingine ambazo zilichukua ardhi ya wanakijiji ni mashirika ya umma. Mifano hai ni ya mashamba ya ngano huko Basotu. Wako pia vibwanyenye kutoka mijini na viongozi wa serikali walichukua ardhi ya wazalishaji – mifano mingi ilitolewa katika juzuu ya pili ya Taarifa Ya Tume ya ardhi.

Pamoja na ukweli kwamba katika awamu zote ardhi ya wenyeji haikuwa salama, katika awamu ya sita uporaji wa ardhi unafanyika kwa kasi kubwa kwa visingizio mbalimbali vya kisasa.

Kisingizio kimojawapo ambacho kimezungumziwa sana na kuathiri hasa jamii za Kimaasai ni upanuaji wa hifadhi. Sakata la Ngorongoro na Loliondo bado lipo. Ingawa habari kutoka eneo lile linakandamizwa, bado mara moja moja taarifa za uaji na mateso ya waMaasai zinavuja. Hata hivyo, vyombo vya habari hawatakikuzigusa na wanaharakati wakishachoka kupiga kelele.

***

Inasemekana serikali ya awamu ya sita ina mpango wa kuongeza maeneo ya hifadhi kutoka asilimia 30 ya ardhi yote ya nchi mpaka asilimia 50, yaani nusu ya ardhi yote ya nchi itageuzwa kuwa hifadhi ili watalii-matajiri na makampuni ya uwindaji waje bila kubughudhiwa na wenyeji. Nchi kama Ujerumani, Umoja wa Kifalme wa Kiaarabu (United Arab Emirates), Benki ya Dunia wanawekeza mabilioni ya dola katika miradi hii.

Vijiji vya KiMaasai pamoja na majengo yao ya shule na zahanati zinabomolewa kwa kisingizio cha kuhifadhi mazingira. Papo hapo wawekezaji wanaruhusiwa kujenga mahoteli na viwanja vya ndege ili wanawafalme kutoka Uarabuni waweze kuja na ndege zao kukaa katika mahoteli ya kianasa na kuwinda wanyamapori! Yaani nchini kwetu wanyamapori na wanawafalme kutoka nje wanathaminiwa zaidi kuliko wananchi wetu wenyewe. Kama kweli nusu ya ardhi ya nchi itageuzwa kuwa hifadhi kwa ajili ya uwindaji na utalii basi tunaelekea kuwa Jamhuri ya Hifadhi ( Republic of National Parks).

Jambo lingine la kusababisha uporaji wa ardhi ni uwekezaji katika maeneo makubwa ya misitu, eti kuhifadhi misitu na kupanda miti ili kuweza kuingia katika biashara ya kaboni. Mwaka jana Tanzania ilisaini mkataba wa maelewano na kampuni ya Dubai Blue Carbon. Chini ya mkataba huu Blue Carbon imepewa eneo la misitu lenye ukubwa wa hekta milioni 8 kuhifadhi misitu na kupanda miti kwa lengo la kushiriki katika biashara ya kaboni. Kampuni hii ya Dubai itauza carbon credits kwa nchi zinazozalisha mafuta na hewa chafuzi inayosababisha tatizo la mabadiliko ya tabianchi. Nchi mojawapo ambayo ni mchafuzi mkubwa wa hewa ni nchi za UAE zenyewe! Kwa hivyo, kampuni ya Dubai itauzia nchi za Kiaarabu carbon credit kusafisha jina lao kama mchafuzi wakati wakiendelea kuzalisha mafuta sambamba na hewa chafuzi! Na hayo yote kwa gharama ya watu wa Tanzania watakao poteza udhibiti na matumizi ya maliasili yao – misitu.

Kwenye hafla ya utiaji saini na Blue Carbon Mhe Waziri na watendaji wengine wa Serikali walisisitiza kwamba miradi ya hewa ukaa ni uchumi mbadala na inatoa fursa kwa Watanzania kukuza uchumi wao kwa kushiriki katika miradi ya biashara ya kaboni. Kwa maana nyingine, wazalishaji mazao ya chakula na mazao mengine yenye soko la ndani wanashawishiwa kudandia biashara ya hewa ukaa na kuachana na uzalishaji chakula. Ni rudio ya uchumi wa kikoloni unaofungamana na soko la kimataifa na kufanya wananchi kuwa wategemezi badala ya kujenga uchumi wa kitaifa unaosukumwa na mahitaji ya ndani. Tunarudia dhambi zilezile za uchumi tegemezi safari hii tukirubuniwa na mawakala wapya wa mabeberu. Wamawakala wapya wa mabeberu.

Mipango inayosukumwa kwa kisingizio cha hifadhi ya misitu na wanyapori ni mbinu mpya wa uporaji maliasili zetu, msingi wake ukiwa mama ardhi.

Suala la ardhi ni nyeti na lilikuwa nyuma ya mapambano na vita ya ukombozi kusini mwa Afrika. Hata mapambano ya mashuja wa Kenya wakiitwa eti MauMau yalikita kwenye uporaji wa ardhi na walowezi. (Wao wenyewe walijiita Jeshi la Kukomboa Ardhi, The Land Freedom Army). Suala la ardhi bado linaendelea kusumbua nchi za Namibia na Afrika Kusini. Sisi kwa sababu za kihistoria tuliepukana na tatizo la ardhi. Lakini sasa badala ya kujifunza kutoka historia, tuko mbioni kujitumbukiza katika kınaması (quagmire) ya tatizo la ardhi.

Suala la msingi kama ardhi (na rasilimali zinazopatikana chini na juu ya ardhi) hatuwezi kuliachia serikali. Watawala hawaoni mbali. Siasa zao ni za muda mfupi. Maono yao ni finyu. Matakwa yao ni ya kibanafsi. Hiki ni kizazi kipya cha watawala kilichokuzwa na mfumo wa uliberali mamboleo; sio tena kizazi kile cha kitaifa na kizalendo kilichotanguliza mbele maslahi ya nchi.

Ni juu ya wananchi wenyewe; wavujajasho wenyewe kulinda rasilimali zao na kuchukua hatma ya nchi yao mikononi mwao.


****************
Shivji hana utofauti na mwanafunzi wake Lissu,wote ni walalamishi,hawana suluhisho,wakosoaji ndio huwa hivyo.
Amekazania kupinga ubepari wakati hawezi kuishi kijamaa,ni mnafiki sana shivji
 
Huyo mzee Shivji nilimtoa maanani kipindi cha kusaka katiba mpya alipokubali kutumika kupotosha umma. Huenda hata sasa anaongea hivyo ili aitwe apewe chochote.
Sasa maoni si huwa yanatofautiana kulingana na mada au jambo husika.

Yaani kama kwenye katiba halikua sawa na wewe kwenye mambo ya ardhi akiwa sawa na wewe basi hafai, ni mbinafsi.

Hii sio sawa, tujifunze kukubali kutokubaliana.
 
Professa wa sheria Issa Shivji wa Tanzania anayeheshimiwa duniani na aliyefundisha na kutafiti na kuandika vitabu vingi vya masuala ya ardhi anawakumbusha Watanzania: nchi inauzwa kwa kasi na "Wamawakala wapya wa mabeberu." ambao anasema sifa zao ni "Watawala hawaoni mbali. Siasa zao ni za muda mfupi. Maono yao ni finyu." Na anamalizia kwa kuandika jukumu la kulinda ardhi ya nchi ni la nani.

=========

’TULIPO. TUNAKOELEKEA’ 2 TAFAKURI YA KILA WIKI UPORAJI WA MALIASILI MAMA – ARDHI

PROF. ISSASHIVJI

Jul 7, 2024

Tangu wakoloni wavamie nchi yetu mwishoni mwa karne ya 19 na mwanzoni mwa karne ya 20, uporaji wa ardhi umeendelea. Katika miongo takriban saba hivi wakoloni walitwaa ardhi ya wenyeji kwa ajili ya makampuni ya nje na walowezi ingawa Tanganyika haikuwa ukoloni ambako walowezi wa kizungu walipora maeneo makubwa ya ardhi kama Kenya au nchi za Kusini mwa Bara kama Zimbabwe, Namibia na Afrika Kusini.

Katika miaka takriban sitini baada ya uhuru tena wazalishaji wadogo hususan wakulima na wafugaji wakajikuta ardhi yao inachukuliwa kwa visingizio mbalimbali. Hata nyakati ya awamu ya kwanza ardhi ya wazalishaji haikuwa salama. Taasisi za serikali kama jeshi, magereza n.k walivamia na kuchukua ardhi ya wenyeji na kuzaa migogoro ya ardhi isiyoisha. Kila mara mipaka ya hifadhi inapopanuliwa ardhi ya wakulima na hasa wafugaji inamezwa. Taasisi zingine ambazo zilichukua ardhi ya wanakijiji ni mashirika ya umma. Mifano hai ni ya mashamba ya ngano huko Basotu. Wako pia vibwanyenye kutoka mijini na viongozi wa serikali walichukua ardhi ya wazalishaji – mifano mingi ilitolewa katika juzuu ya pili ya Taarifa Ya Tume ya ardhi.

Pamoja na ukweli kwamba katika awamu zote ardhi ya wenyeji haikuwa salama, katika awamu ya sita uporaji wa ardhi unafanyika kwa kasi kubwa kwa visingizio mbalimbali vya kisasa.

Kisingizio kimojawapo ambacho kimezungumziwa sana na kuathiri hasa jamii za Kimaasai ni upanuaji wa hifadhi. Sakata la Ngorongoro na Loliondo bado lipo. Ingawa habari kutoka eneo lile linakandamizwa, bado mara moja moja taarifa za uaji na mateso ya waMaasai zinavuja. Hata hivyo, vyombo vya habari hawatakikuzigusa na wanaharakati wakishachoka kupiga kelele.

***

Inasemekana serikali ya awamu ya sita ina mpango wa kuongeza maeneo ya hifadhi kutoka asilimia 30 ya ardhi yote ya nchi mpaka asilimia 50, yaani nusu ya ardhi yote ya nchi itageuzwa kuwa hifadhi ili watalii-matajiri na makampuni ya uwindaji waje bila kubughudhiwa na wenyeji. Nchi kama Ujerumani, Umoja wa Kifalme wa Kiaarabu (United Arab Emirates), Benki ya Dunia wanawekeza mabilioni ya dola katika miradi hii.

Vijiji vya KiMaasai pamoja na majengo yao ya shule na zahanati zinabomolewa kwa kisingizio cha kuhifadhi mazingira. Papo hapo wawekezaji wanaruhusiwa kujenga mahoteli na viwanja vya ndege ili wanawafalme kutoka Uarabuni waweze kuja na ndege zao kukaa katika mahoteli ya kianasa na kuwinda wanyamapori! Yaani nchini kwetu wanyamapori na wanawafalme kutoka nje wanathaminiwa zaidi kuliko wananchi wetu wenyewe. Kama kweli nusu ya ardhi ya nchi itageuzwa kuwa hifadhi kwa ajili ya uwindaji na utalii basi tunaelekea kuwa Jamhuri ya Hifadhi ( Republic of National Parks).

Jambo lingine la kusababisha uporaji wa ardhi ni uwekezaji katika maeneo makubwa ya misitu, eti kuhifadhi misitu na kupanda miti ili kuweza kuingia katika biashara ya kaboni. Mwaka jana Tanzania ilisaini mkataba wa maelewano na kampuni ya Dubai Blue Carbon. Chini ya mkataba huu Blue Carbon imepewa eneo la misitu lenye ukubwa wa hekta milioni 8 kuhifadhi misitu na kupanda miti kwa lengo la kushiriki katika biashara ya kaboni. Kampuni hii ya Dubai itauza carbon credits kwa nchi zinazozalisha mafuta na hewa chafuzi inayosababisha tatizo la mabadiliko ya tabianchi. Nchi mojawapo ambayo ni mchafuzi mkubwa wa hewa ni nchi za UAE zenyewe! Kwa hivyo, kampuni ya Dubai itauzia nchi za Kiaarabu carbon credit kusafisha jina lao kama mchafuzi wakati wakiendelea kuzalisha mafuta sambamba na hewa chafuzi! Na hayo yote kwa gharama ya watu wa Tanzania watakao poteza udhibiti na matumizi ya maliasili yao – misitu.

Kwenye hafla ya utiaji saini na Blue Carbon Mhe Waziri na watendaji wengine wa Serikali walisisitiza kwamba miradi ya hewa ukaa ni uchumi mbadala na inatoa fursa kwa Watanzania kukuza uchumi wao kwa kushiriki katika miradi ya biashara ya kaboni. Kwa maana nyingine, wazalishaji mazao ya chakula na mazao mengine yenye soko la ndani wanashawishiwa kudandia biashara ya hewa ukaa na kuachana na uzalishaji chakula. Ni rudio ya uchumi wa kikoloni unaofungamana na soko la kimataifa na kufanya wananchi kuwa wategemezi badala ya kujenga uchumi wa kitaifa unaosukumwa na mahitaji ya ndani. Tunarudia dhambi zilezile za uchumi tegemezi safari hii tukirubuniwa na mawakala wapya wa mabeberu. Wamawakala wapya wa mabeberu.

Mipango inayosukumwa kwa kisingizio cha hifadhi ya misitu na wanyapori ni mbinu mpya wa uporaji maliasili zetu, msingi wake ukiwa mama ardhi.

Suala la ardhi ni nyeti na lilikuwa nyuma ya mapambano na vita ya ukombozi kusini mwa Afrika. Hata mapambano ya mashuja wa Kenya wakiitwa eti MauMau yalikita kwenye uporaji wa ardhi na walowezi. (Wao wenyewe walijiita Jeshi la Kukomboa Ardhi, The Land Freedom Army). Suala la ardhi bado linaendelea kusumbua nchi za Namibia na Afrika Kusini. Sisi kwa sababu za kihistoria tuliepukana na tatizo la ardhi. Lakini sasa badala ya kujifunza kutoka historia, tuko mbioni kujitumbukiza katika kınaması (quagmire) ya tatizo la ardhi.

Suala la msingi kama ardhi (na rasilimali zinazopatikana chini na juu ya ardhi) hatuwezi kuliachia serikali. Watawala hawaoni mbali. Siasa zao ni za muda mfupi. Maono yao ni finyu. Matakwa yao ni ya kibanafsi. Hiki ni kizazi kipya cha watawala kilichokuzwa na mfumo wa uliberali mamboleo; sio tena kizazi kile cha kitaifa na kizalendo kilichotanguliza mbele maslahi ya nchi.

Ni juu ya wananchi wenyewe; wavujajasho wenyewe kulinda rasilimali zao na kuchukua hatma ya nchi yao mikononi mwao.


****************
Kichwa kimetoa maoni yake..m
 
Professa wa sheria Issa Shivji wa Tanzania anayeheshimiwa duniani na aliyefundisha na kutafiti na kuandika vitabu vingi vya masuala ya ardhi anawakumbusha Watanzania: nchi inauzwa kwa kasi na "Wamawakala wapya wa mabeberu." ambao anasema sifa zao ni "Watawala hawaoni mbali. Siasa zao ni za muda mfupi. Maono yao ni finyu." Na anamalizia kwa kuandika jukumu la kulinda ardhi ya nchi ni la nani.

=========

’TULIPO. TUNAKOELEKEA’ 2 TAFAKURI YA KILA WIKI UPORAJI WA MALIASILI MAMA – ARDHI

PROF. ISSASHIVJI

Jul 7, 2024

Tangu wakoloni wavamie nchi yetu mwishoni mwa karne ya 19 na mwanzoni mwa karne ya 20, uporaji wa ardhi umeendelea. Katika miongo takriban saba hivi wakoloni walitwaa ardhi ya wenyeji kwa ajili ya makampuni ya nje na walowezi ingawa Tanganyika haikuwa ukoloni ambako walowezi wa kizungu walipora maeneo makubwa ya ardhi kama Kenya au nchi za Kusini mwa Bara kama Zimbabwe, Namibia na Afrika Kusini.

Katika miaka takriban sitini baada ya uhuru tena wazalishaji wadogo hususan wakulima na wafugaji wakajikuta ardhi yao inachukuliwa kwa visingizio mbalimbali. Hata nyakati ya awamu ya kwanza ardhi ya wazalishaji haikuwa salama. Taasisi za serikali kama jeshi, magereza n.k walivamia na kuchukua ardhi ya wenyeji na kuzaa migogoro ya ardhi isiyoisha. Kila mara mipaka ya hifadhi inapopanuliwa ardhi ya wakulima na hasa wafugaji inamezwa. Taasisi zingine ambazo zilichukua ardhi ya wanakijiji ni mashirika ya umma. Mifano hai ni ya mashamba ya ngano huko Basotu. Wako pia vibwanyenye kutoka mijini na viongozi wa serikali walichukua ardhi ya wazalishaji – mifano mingi ilitolewa katika juzuu ya pili ya Taarifa Ya Tume ya ardhi.

Pamoja na ukweli kwamba katika awamu zote ardhi ya wenyeji haikuwa salama, katika awamu ya sita uporaji wa ardhi unafanyika kwa kasi kubwa kwa visingizio mbalimbali vya kisasa.

Kisingizio kimojawapo ambacho kimezungumziwa sana na kuathiri hasa jamii za Kimaasai ni upanuaji wa hifadhi. Sakata la Ngorongoro na Loliondo bado lipo. Ingawa habari kutoka eneo lile linakandamizwa, bado mara moja moja taarifa za uaji na mateso ya waMaasai zinavuja. Hata hivyo, vyombo vya habari hawatakikuzigusa na wanaharakati wakishachoka kupiga kelele.

***

Inasemekana serikali ya awamu ya sita ina mpango wa kuongeza maeneo ya hifadhi kutoka asilimia 30 ya ardhi yote ya nchi mpaka asilimia 50, yaani nusu ya ardhi yote ya nchi itageuzwa kuwa hifadhi ili watalii-matajiri na makampuni ya uwindaji waje bila kubughudhiwa na wenyeji. Nchi kama Ujerumani, Umoja wa Kifalme wa Kiaarabu (United Arab Emirates), Benki ya Dunia wanawekeza mabilioni ya dola katika miradi hii.

Vijiji vya KiMaasai pamoja na majengo yao ya shule na zahanati zinabomolewa kwa kisingizio cha kuhifadhi mazingira. Papo hapo wawekezaji wanaruhusiwa kujenga mahoteli na viwanja vya ndege ili wanawafalme kutoka Uarabuni waweze kuja na ndege zao kukaa katika mahoteli ya kianasa na kuwinda wanyamapori! Yaani nchini kwetu wanyamapori na wanawafalme kutoka nje wanathaminiwa zaidi kuliko wananchi wetu wenyewe. Kama kweli nusu ya ardhi ya nchi itageuzwa kuwa hifadhi kwa ajili ya uwindaji na utalii basi tunaelekea kuwa Jamhuri ya Hifadhi ( Republic of National Parks).

Jambo lingine la kusababisha uporaji wa ardhi ni uwekezaji katika maeneo makubwa ya misitu, eti kuhifadhi misitu na kupanda miti ili kuweza kuingia katika biashara ya kaboni. Mwaka jana Tanzania ilisaini mkataba wa maelewano na kampuni ya Dubai Blue Carbon. Chini ya mkataba huu Blue Carbon imepewa eneo la misitu lenye ukubwa wa hekta milioni 8 kuhifadhi misitu na kupanda miti kwa lengo la kushiriki katika biashara ya kaboni. Kampuni hii ya Dubai itauza carbon credits kwa nchi zinazozalisha mafuta na hewa chafuzi inayosababisha tatizo la mabadiliko ya tabianchi. Nchi mojawapo ambayo ni mchafuzi mkubwa wa hewa ni nchi za UAE zenyewe! Kwa hivyo, kampuni ya Dubai itauzia nchi za Kiaarabu carbon credit kusafisha jina lao kama mchafuzi wakati wakiendelea kuzalisha mafuta sambamba na hewa chafuzi! Na hayo yote kwa gharama ya watu wa Tanzania watakao poteza udhibiti na matumizi ya maliasili yao – misitu.

Kwenye hafla ya utiaji saini na Blue Carbon Mhe Waziri na watendaji wengine wa Serikali walisisitiza kwamba miradi ya hewa ukaa ni uchumi mbadala na inatoa fursa kwa Watanzania kukuza uchumi wao kwa kushiriki katika miradi ya biashara ya kaboni. Kwa maana nyingine, wazalishaji mazao ya chakula na mazao mengine yenye soko la ndani wanashawishiwa kudandia biashara ya hewa ukaa na kuachana na uzalishaji chakula. Ni rudio ya uchumi wa kikoloni unaofungamana na soko la kimataifa na kufanya wananchi kuwa wategemezi badala ya kujenga uchumi wa kitaifa unaosukumwa na mahitaji ya ndani. Tunarudia dhambi zilezile za uchumi tegemezi safari hii tukirubuniwa na mawakala wapya wa mabeberu. Wamawakala wapya wa mabeberu.

Mipango inayosukumwa kwa kisingizio cha hifadhi ya misitu na wanyapori ni mbinu mpya wa uporaji maliasili zetu, msingi wake ukiwa mama ardhi.

Suala la ardhi ni nyeti na lilikuwa nyuma ya mapambano na vita ya ukombozi kusini mwa Afrika. Hata mapambano ya mashuja wa Kenya wakiitwa eti MauMau yalikita kwenye uporaji wa ardhi na walowezi. (Wao wenyewe walijiita Jeshi la Kukomboa Ardhi, The Land Freedom Army). Suala la ardhi bado linaendelea kusumbua nchi za Namibia na Afrika Kusini. Sisi kwa sababu za kihistoria tuliepukana na tatizo la ardhi. Lakini sasa badala ya kujifunza kutoka historia, tuko mbioni kujitumbukiza katika kınaması (quagmire) ya tatizo la ardhi.

Suala la msingi kama ardhi (na rasilimali zinazopatikana chini na juu ya ardhi) hatuwezi kuliachia serikali. Watawala hawaoni mbali. Siasa zao ni za muda mfupi. Maono yao ni finyu. Matakwa yao ni ya kibanafsi. Hiki ni kizazi kipya cha watawala kilichokuzwa na mfumo wa uliberali mamboleo; sio tena kizazi kile cha kitaifa na kizalendo kilichotanguliza mbele maslahi ya nchi.

Ni juu ya wananchi wenyewe; wavujajasho wenyewe kulinda rasilimali zao na kuchukua hatma ya nchi yao mikononi mwao.


****************
Na vile visiwa vya znz, vinavyo kodishwa navyo vime kwenye hili dokezo au ndio hivyo hela wapate Sirikali ya mapinduzi, raia wahamie Bara
 
Sasa maoni si huwa yanatofautiana kulingana na mada au jambo husika.

Yaani kama kwenye katiba halikua sawa na wewe kwenye mambo ya ardhi akiwa sawa na wewe basi hafai, ni mbinafsi.

Hii sio sawa, tujifunze kukubali kutokubaliana.
Sina tatizo na alichokisema sasa, bali hata wakati wa nyuma kwenye katiba alikuwa anaongea hivihivi, cha ajabu akapewa kidogo kitu, akaanza kuongea kinyume na alichokuwa anatuaminisha huko nyuma kuhusiana na katiba. Inshort huwa siwachukulii serious watu vigeugeu.
 
Professa wa sheria Issa Shivji wa Tanzania anayeheshimiwa duniani na aliyefundisha na kutafiti na kuandika vitabu vingi vya masuala ya ardhi anawakumbusha Watanzania: nchi inauzwa kwa kasi na "Wamawakala wapya wa mabeberu." ambao anasema sifa zao ni "Watawala hawaoni mbali. Siasa zao ni za muda mfupi. Maono yao ni finyu." Na anamalizia kwa kuandika jukumu la kulinda ardhi ya nchi ni la nani.

=========

’TULIPO. TUNAKOELEKEA’ 2 TAFAKURI YA KILA WIKI UPORAJI WA MALIASILI MAMA – ARDHI

PROF. ISSASHIVJI

Jul 7, 2024

Tangu wakoloni wavamie nchi yetu mwishoni mwa karne ya 19 na mwanzoni mwa karne ya 20, uporaji wa ardhi umeendelea. Katika miongo takriban saba hivi wakoloni walitwaa ardhi ya wenyeji kwa ajili ya makampuni ya nje na walowezi ingawa Tanganyika haikuwa ukoloni ambako walowezi wa kizungu walipora maeneo makubwa ya ardhi kama Kenya au nchi za Kusini mwa Bara kama Zimbabwe, Namibia na Afrika Kusini.

Katika miaka takriban sitini baada ya uhuru tena wazalishaji wadogo hususan wakulima na wafugaji wakajikuta ardhi yao inachukuliwa kwa visingizio mbalimbali. Hata nyakati ya awamu ya kwanza ardhi ya wazalishaji haikuwa salama. Taasisi za serikali kama jeshi, magereza n.k walivamia na kuchukua ardhi ya wenyeji na kuzaa migogoro ya ardhi isiyoisha. Kila mara mipaka ya hifadhi inapopanuliwa ardhi ya wakulima na hasa wafugaji inamezwa. Taasisi zingine ambazo zilichukua ardhi ya wanakijiji ni mashirika ya umma. Mifano hai ni ya mashamba ya ngano huko Basotu. Wako pia vibwanyenye kutoka mijini na viongozi wa serikali walichukua ardhi ya wazalishaji – mifano mingi ilitolewa katika juzuu ya pili ya Taarifa Ya Tume ya ardhi.

Pamoja na ukweli kwamba katika awamu zote ardhi ya wenyeji haikuwa salama, katika awamu ya sita uporaji wa ardhi unafanyika kwa kasi kubwa kwa visingizio mbalimbali vya kisasa.

Kisingizio kimojawapo ambacho kimezungumziwa sana na kuathiri hasa jamii za Kimaasai ni upanuaji wa hifadhi. Sakata la Ngorongoro na Loliondo bado lipo. Ingawa habari kutoka eneo lile linakandamizwa, bado mara moja moja taarifa za uaji na mateso ya waMaasai zinavuja. Hata hivyo, vyombo vya habari hawatakikuzigusa na wanaharakati wakishachoka kupiga kelele.

***

Inasemekana serikali ya awamu ya sita ina mpango wa kuongeza maeneo ya hifadhi kutoka asilimia 30 ya ardhi yote ya nchi mpaka asilimia 50, yaani nusu ya ardhi yote ya nchi itageuzwa kuwa hifadhi ili watalii-matajiri na makampuni ya uwindaji waje bila kubughudhiwa na wenyeji. Nchi kama Ujerumani, Umoja wa Kifalme wa Kiaarabu (United Arab Emirates), Benki ya Dunia wanawekeza mabilioni ya dola katika miradi hii.

Vijiji vya KiMaasai pamoja na majengo yao ya shule na zahanati zinabomolewa kwa kisingizio cha kuhifadhi mazingira. Papo hapo wawekezaji wanaruhusiwa kujenga mahoteli na viwanja vya ndege ili wanawafalme kutoka Uarabuni waweze kuja na ndege zao kukaa katika mahoteli ya kianasa na kuwinda wanyamapori! Yaani nchini kwetu wanyamapori na wanawafalme kutoka nje wanathaminiwa zaidi kuliko wananchi wetu wenyewe. Kama kweli nusu ya ardhi ya nchi itageuzwa kuwa hifadhi kwa ajili ya uwindaji na utalii basi tunaelekea kuwa Jamhuri ya Hifadhi ( Republic of National Parks).

Jambo lingine la kusababisha uporaji wa ardhi ni uwekezaji katika maeneo makubwa ya misitu, eti kuhifadhi misitu na kupanda miti ili kuweza kuingia katika biashara ya kaboni. Mwaka jana Tanzania ilisaini mkataba wa maelewano na kampuni ya Dubai Blue Carbon. Chini ya mkataba huu Blue Carbon imepewa eneo la misitu lenye ukubwa wa hekta milioni 8 kuhifadhi misitu na kupanda miti kwa lengo la kushiriki katika biashara ya kaboni. Kampuni hii ya Dubai itauza carbon credits kwa nchi zinazozalisha mafuta na hewa chafuzi inayosababisha tatizo la mabadiliko ya tabianchi. Nchi mojawapo ambayo ni mchafuzi mkubwa wa hewa ni nchi za UAE zenyewe! Kwa hivyo, kampuni ya Dubai itauzia nchi za Kiaarabu carbon credit kusafisha jina lao kama mchafuzi wakati wakiendelea kuzalisha mafuta sambamba na hewa chafuzi! Na hayo yote kwa gharama ya watu wa Tanzania watakao poteza udhibiti na matumizi ya maliasili yao – misitu.

Kwenye hafla ya utiaji saini na Blue Carbon Mhe Waziri na watendaji wengine wa Serikali walisisitiza kwamba miradi ya hewa ukaa ni uchumi mbadala na inatoa fursa kwa Watanzania kukuza uchumi wao kwa kushiriki katika miradi ya biashara ya kaboni. Kwa maana nyingine, wazalishaji mazao ya chakula na mazao mengine yenye soko la ndani wanashawishiwa kudandia biashara ya hewa ukaa na kuachana na uzalishaji chakula. Ni rudio ya uchumi wa kikoloni unaofungamana na soko la kimataifa na kufanya wananchi kuwa wategemezi badala ya kujenga uchumi wa kitaifa unaosukumwa na mahitaji ya ndani. Tunarudia dhambi zilezile za uchumi tegemezi safari hii tukirubuniwa na mawakala wapya wa mabeberu. Wamawakala wapya wa mabeberu.

Mipango inayosukumwa kwa kisingizio cha hifadhi ya misitu na wanyapori ni mbinu mpya wa uporaji maliasili zetu, msingi wake ukiwa mama ardhi.

Suala la ardhi ni nyeti na lilikuwa nyuma ya mapambano na vita ya ukombozi kusini mwa Afrika. Hata mapambano ya mashuja wa Kenya wakiitwa eti MauMau yalikita kwenye uporaji wa ardhi na walowezi. (Wao wenyewe walijiita Jeshi la Kukomboa Ardhi, The Land Freedom Army). Suala la ardhi bado linaendelea kusumbua nchi za Namibia na Afrika Kusini. Sisi kwa sababu za kihistoria tuliepukana na tatizo la ardhi. Lakini sasa badala ya kujifunza kutoka historia, tuko mbioni kujitumbukiza katika kınaması (quagmire) ya tatizo la ardhi.

Suala la msingi kama ardhi (na rasilimali zinazopatikana chini na juu ya ardhi) hatuwezi kuliachia serikali. Watawala hawaoni mbali. Siasa zao ni za muda mfupi. Maono yao ni finyu. Matakwa yao ni ya kibanafsi. Hiki ni kizazi kipya cha watawala kilichokuzwa na mfumo wa uliberali mamboleo; sio tena kizazi kile cha kitaifa na kizalendo kilichotanguliza mbele maslahi ya nchi.

Ni juu ya wananchi wenyewe; wavujajasho wenyewe kulinda rasilimali zao na kuchukua hatma ya nchi yao mikononi mwao.


****************
Ndio hatari ya nchi kuongozwa na kiongozi asiye na maarifa wala maono. Uwekezaji kama hizo ndio vitu rais anaweza kushauriwa na vigogo serikalini wasio na uzalendo na wapenda rushwa. Ule mfano wa mkataba wa bandari uwe mfano kwa mikataba yote nchi hii inaweza kupatiwa na nchi ya dubai na nchi zingine wakala wa ubeberu duniani. Ni jambo muhimu sana 2025 nchi kuzingatia kupata kiongozi mzalendo mwenye uwezo na maono sahihi kwa mustakabali wa nchi.
 
Kila MTU atakufa,kifo ni Haki...lakini kwanini hawa nguchiro wengine kama shivji wasitangulie KWANZA??
 
Duh,
Silaha kubwa ya wananchi wa kawaida ambao ndiyo wengi katika kujikomboa kutoka kwa makucha ya watawala waovu ni kura zao, lakini bahati mbaya kwa Tanzania sanduku la kura halina tija
Nani kakudanganya kura za wananchi ndio silaha zao?
 
Professa wa sheria Issa Shivji wa Tanzania anayeheshimiwa duniani na aliyefundisha na kutafiti na kuandika vitabu vingi vya masuala ya ardhi anawakumbusha Watanzania: nchi inauzwa kwa kasi na "Wamawakala wapya wa mabeberu." ambao anasema sifa zao ni "Watawala hawaoni mbali. Siasa zao ni za muda mfupi. Maono yao ni finyu." Na anamalizia kwa kuandika jukumu la kulinda ardhi ya nchi ni la nani.

=========

’TULIPO. TUNAKOELEKEA’ 2 TAFAKURI YA KILA WIKI UPORAJI WA MALIASILI MAMA – ARDHI

PROF. ISSASHIVJI

Jul 7, 2024

Tangu wakoloni wavamie nchi yetu mwishoni mwa karne ya 19 na mwanzoni mwa karne ya 20, uporaji wa ardhi umeendelea. Katika miongo takriban saba hivi wakoloni walitwaa ardhi ya wenyeji kwa ajili ya makampuni ya nje na walowezi ingawa Tanganyika haikuwa ukoloni ambako walowezi wa kizungu walipora maeneo makubwa ya ardhi kama Kenya au nchi za Kusini mwa Bara kama Zimbabwe, Namibia na Afrika Kusini.

Katika miaka takriban sitini baada ya uhuru tena wazalishaji wadogo hususan wakulima na wafugaji wakajikuta ardhi yao inachukuliwa kwa visingizio mbalimbali. Hata nyakati ya awamu ya kwanza ardhi ya wazalishaji haikuwa salama. Taasisi za serikali kama jeshi, magereza n.k walivamia na kuchukua ardhi ya wenyeji na kuzaa migogoro ya ardhi isiyoisha. Kila mara mipaka ya hifadhi inapopanuliwa ardhi ya wakulima na hasa wafugaji inamezwa. Taasisi zingine ambazo zilichukua ardhi ya wanakijiji ni mashirika ya umma. Mifano hai ni ya mashamba ya ngano huko Basotu. Wako pia vibwanyenye kutoka mijini na viongozi wa serikali walichukua ardhi ya wazalishaji – mifano mingi ilitolewa katika juzuu ya pili ya Taarifa Ya Tume ya ardhi.

Pamoja na ukweli kwamba katika awamu zote ardhi ya wenyeji haikuwa salama, katika awamu ya sita uporaji wa ardhi unafanyika kwa kasi kubwa kwa visingizio mbalimbali vya kisasa.

Kisingizio kimojawapo ambacho kimezungumziwa sana na kuathiri hasa jamii za Kimaasai ni upanuaji wa hifadhi. Sakata la Ngorongoro na Loliondo bado lipo. Ingawa habari kutoka eneo lile linakandamizwa, bado mara moja moja taarifa za uaji na mateso ya waMaasai zinavuja. Hata hivyo, vyombo vya habari hawatakikuzigusa na wanaharakati wakishachoka kupiga kelele.

***

Inasemekana serikali ya awamu ya sita ina mpango wa kuongeza maeneo ya hifadhi kutoka asilimia 30 ya ardhi yote ya nchi mpaka asilimia 50, yaani nusu ya ardhi yote ya nchi itageuzwa kuwa hifadhi ili watalii-matajiri na makampuni ya uwindaji waje bila kubughudhiwa na wenyeji. Nchi kama Ujerumani, Umoja wa Kifalme wa Kiaarabu (United Arab Emirates), Benki ya Dunia wanawekeza mabilioni ya dola katika miradi hii.

Vijiji vya KiMaasai pamoja na majengo yao ya shule na zahanati zinabomolewa kwa kisingizio cha kuhifadhi mazingira. Papo hapo wawekezaji wanaruhusiwa kujenga mahoteli na viwanja vya ndege ili wanawafalme kutoka Uarabuni waweze kuja na ndege zao kukaa katika mahoteli ya kianasa na kuwinda wanyamapori! Yaani nchini kwetu wanyamapori na wanawafalme kutoka nje wanathaminiwa zaidi kuliko wananchi wetu wenyewe. Kama kweli nusu ya ardhi ya nchi itageuzwa kuwa hifadhi kwa ajili ya uwindaji na utalii basi tunaelekea kuwa Jamhuri ya Hifadhi ( Republic of National Parks).

Jambo lingine la kusababisha uporaji wa ardhi ni uwekezaji katika maeneo makubwa ya misitu, eti kuhifadhi misitu na kupanda miti ili kuweza kuingia katika biashara ya kaboni. Mwaka jana Tanzania ilisaini mkataba wa maelewano na kampuni ya Dubai Blue Carbon. Chini ya mkataba huu Blue Carbon imepewa eneo la misitu lenye ukubwa wa hekta milioni 8 kuhifadhi misitu na kupanda miti kwa lengo la kushiriki katika biashara ya kaboni. Kampuni hii ya Dubai itauza carbon credits kwa nchi zinazozalisha mafuta na hewa chafuzi inayosababisha tatizo la mabadiliko ya tabianchi. Nchi mojawapo ambayo ni mchafuzi mkubwa wa hewa ni nchi za UAE zenyewe! Kwa hivyo, kampuni ya Dubai itauzia nchi za Kiaarabu carbon credit kusafisha jina lao kama mchafuzi wakati wakiendelea kuzalisha mafuta sambamba na hewa chafuzi! Na hayo yote kwa gharama ya watu wa Tanzania watakao poteza udhibiti na matumizi ya maliasili yao – misitu.

Kwenye hafla ya utiaji saini na Blue Carbon Mhe Waziri na watendaji wengine wa Serikali walisisitiza kwamba miradi ya hewa ukaa ni uchumi mbadala na inatoa fursa kwa Watanzania kukuza uchumi wao kwa kushiriki katika miradi ya biashara ya kaboni. Kwa maana nyingine, wazalishaji mazao ya chakula na mazao mengine yenye soko la ndani wanashawishiwa kudandia biashara ya hewa ukaa na kuachana na uzalishaji chakula. Ni rudio ya uchumi wa kikoloni unaofungamana na soko la kimataifa na kufanya wananchi kuwa wategemezi badala ya kujenga uchumi wa kitaifa unaosukumwa na mahitaji ya ndani. Tunarudia dhambi zilezile za uchumi tegemezi safari hii tukirubuniwa na mawakala wapya wa mabeberu. Wamawakala wapya wa mabeberu.

Mipango inayosukumwa kwa kisingizio cha hifadhi ya misitu na wanyapori ni mbinu mpya wa uporaji maliasili zetu, msingi wake ukiwa mama ardhi.

Suala la ardhi ni nyeti na lilikuwa nyuma ya mapambano na vita ya ukombozi kusini mwa Afrika. Hata mapambano ya mashuja wa Kenya wakiitwa eti MauMau yalikita kwenye uporaji wa ardhi na walowezi. (Wao wenyewe walijiita Jeshi la Kukomboa Ardhi, The Land Freedom Army). Suala la ardhi bado linaendelea kusumbua nchi za Namibia na Afrika Kusini. Sisi kwa sababu za kihistoria tuliepukana na tatizo la ardhi. Lakini sasa badala ya kujifunza kutoka historia, tuko mbioni kujitumbukiza katika kınaması (quagmire) ya tatizo la ardhi.

Suala la msingi kama ardhi (na rasilimali zinazopatikana chini na juu ya ardhi) hatuwezi kuliachia serikali. Watawala hawaoni mbali. Siasa zao ni za muda mfupi. Maono yao ni finyu. Matakwa yao ni ya kibanafsi. Hiki ni kizazi kipya cha watawala kilichokuzwa na mfumo wa uliberali mamboleo; sio tena kizazi kile cha kitaifa na kizalendo kilichotanguliza mbele maslahi ya nchi.

Ni juu ya wananchi wenyewe; wavujajasho wenyewe kulinda rasilimali zao na kuchukua hatma ya nchi yao mikononi mwao.


****************
Ccm wanauza tu rasilimali zetu alafu wanaenda kununua nyumba Dubai
Akili za kijinga hizi
 
Huyu jamaa ni mfuasi wa Karl Max ila kwa sasa ideas za kina adam smith ndio zimetamalaki hawezi kueleweka na viongozi wa zama hizi ambao wengi wao wapo zama za kutumia sana (consumerism) kulipo kutafuta, kupigania na kulinda.
 
Shivji ni mpinga uwekezaji,huita kuuza
Yaani kwa akili yako finyu kabisa unadhani kila kinachofanywa na watawala wa serikali ya CCM kuanzia Mwinyi, Mkapa, Kikwete na huyu bibie Samia Suluhu Hassan ni uwekezaji?

Ndiyo maana humwelewi Prof. Issa Shivji kwa akili na mtazamo wako huu. Pole sana...

Rais aliyekuwa kinyume na sera na akili za udalali wa Maliasili za nchi kwa mabeberu alikuwa mwasisi wa Taifa hili pekee mzee Hayati Julius K. Nyerere na baadaye kuja kufuatiwa na Hayati John P. Magufuli pekee.

Hawa wengine wote ni madalali wa mabeberu wa waziwazi.

Na hali ya udalali huu kwa Sasa ni mbaya na hatari zaidi na ukifanyika katika namna ya ulafi na tamaa ya kijinga kabisa ya viongozi wa CCM na ya waziwazi kupita kiasi chini ya huyu Mama Mzanzibari Samia Suluhu Hassan.

Mbaya zaidi tena ni kuwa, maliasili zinazodalaliwa ni za Tanganyika tu huku za Zanzibar zikiwa salama!!
 
Yaani kwa akili yako finyu kabisa unadhani kila kinachofanywa na watawala wa serikali ya CCM kuanzia Mwinyi, Mkapa, Kikwete na huyu bibie Samia Suluhu Hassan ni uwekezaji?

Ndiyo maana humwelewi Prof. Issa Shivji kwa akili na mtazamo wako huu. Pole sana...

Rais aliyekuwa kinyume na sera na akili za udalali wa Maliasili za nchi kwa mabeberu alikuwa mwasisi wa Taifa hili pekee mzee Hayati Julius K. Nyerere na baadaye kuja kufuatiwa na Hayati John P. Magufuli pekee.

Hawa wengine wote ni madalali wa mabeberu wa waziwazi.

Na hali ya udalali huu kwa Sasa ni mbaya na hatari zaidi na ukifanyika katika namna ya ulafi na tamaa ya kijinga kabisa ya viongozi wa CCM na ya waziwazi kupita kiasi chini ya huyu Mama Mzanzibari Samia Suluhu Hassan.

Mbaya zaidi tena ni kuwa, maliasili zinazodalaliwa ni za Tanganyika tu huku za Zanzibar zikiwa salama!!
Halafu maisha yalikuwaje kipindi Cha Nyerere!?..viraka juu ya viraka,umasikini uliotopea,ukiwa na radio na baiskeli we tajiri,nilimsikia juzi redioni akihutubu,yaani alikua akichukia matajiri na kuwaita wanyonyaji,uwekezaji ni kumpa mtu mwenye mtaji afanye biashara ya bidhaa Fulani nchini kwako,watu wako watapata ajira, serikali itapata Kodi,tofauti na hapo ni akili za kimasikini na roho mbaya tu,huyo magu alilinda rasilimali gani!?
 
Baadhi ya watu mna shida kichwani. Mnajaribu kudokezwa mambo makubwa ya nchi yenu, yanavyokwenda mnampinga anayewajulisha!

HIli Taifa si la kuhoji viongozi wala kusimamia hizi rasilimali. Unamtoa Mmasai kwenye hifadhi, kwamba anaharibu mazingira, unakuja kuingia mkataba upate 10% unamuweka muarabu. Anafanya zaidi ya jamii ya kimasai kujenga mahoteli na kuwinda na tuko kimya!!!

Mimi ule mkataba wa misitu hekta milioni 8, ndiyo nilipochoka. Hii awamu itauza kila eneo. Itafikia wakati kila unapokanyaga utaambiwa huruhusiwi, ni eneo la Mfalme fulani ama nchi fulani, na uko ndani ya nchi yako. Yatafika tu tuombe uzima.
 
Baadhi ya watu mna shida kichwani. Mnajaribu kudokezwa mambo makubwa ya nchi yenu, yanavyokwenda mnampinga anayewajulisha!

HIli Taifa si la kuhoji viongozi wala kusimamia hizi rasilimali. Unamtoa Mmasai kwenye hifadhi, kwamba anaharibu mazingira, unakuja kuingia mkataba upate 10% unamuweka muarabu. Anafanya zaidi ya jamii ya kimasai kujenga mahoteli na kuwinda na tuko kimya!!!

Mimi ule mkataba wa misitu hekta milioni 8, ndiyo nilipochoka. Hii awamu itauza kila eneo. Itafikia wakati kila unapokanyaga utaambiwa huruhusiwi, ni eneo la Mfalme fulani ama nchi fulani, na uko ndani ya nchi yako. Yatafika tu tuombe uzima.

Hata mimi nimeshangaa kwa kweli.

Profesa anazungumza mambo makubwa ya nchi, watu wanaleta hoja za "lakini huyu mzee zamani kawahi kuwa na msimamo fulani". Sasa kwani lazima kila ishu tuidump katika kapu moja?. Kama zamani mtu alokosea ndo hivyo basi hana haki ya kupatia kwenye jambo jingine?.

Ndiyo maana Watawala wanaweza kufanya lolote nchini kwa sababu wanajua wabongo hawatajali kivile
 
Back
Top Bottom