Udhalilishaji: Video ya PNC akimuomba msamaha Ostaz Juma na Musoma

Udhalilishaji: Video ya PNC akimuomba msamaha Ostaz Juma na Musoma

kuomba msamaha ni jambo jema na la hekima. Ila kosa ni kupost picha hizo kwenye mitandao ya kijamii, kwa faida gani na sifa ipi hadi upost picha ukiombwa msahama. Hata mungu hapendi vibaya hivyo jamani#ostaz juma namusoma.
 
Kweli hakuna atakacho kufanyia binadamu halafu akose kukutangaza 2badilike ndugu zangu haya maisha ya kupita tu.
 
duh..inasikitisha sana wasanii wetu wa bongo wanavyonyanyasika
hakuna tofauti na wengine wanavofanyiwa na clouds fm
 
tumsubirie Joti na Mpoki watakvyotupa version yao ya tukio:smile-big:
 
Huyu kweli bado ana jiita Ustadh kabisa? Huyu ni mjinga sana. Kumdhalilisha mwenzie kiasi hiki kisa ana shida.
Kitendo alicho kifanya huyu jamaa Ustadh ni cha kulaaniwa na kukemewa.
Huyu ustadh ana akili kama za diaomond. Mpuuzi sana.

Hawa wasanii nao muda mwingine ni wajinga sana.

Asa hapa diamond kaingiaje!!kwani bila ya kutajwa domo story hainogi nn....acheni wivu wa kijinga
 
bora boss wangu anaendesha mambo yake kisasa..meneja yupo chin yake siyo yeye awe chini ya meneja..
yeye ndio kamwajiri meneja..si wa kumpelekesha pelekeshan kinjaa njaa

Heheee 😀 heaven on desert bana..

Huyo boss wako nae kapewa Gari ..Kasuburiwa apige nayo picha..Mwenye nayo akajitokeza Pedeshee..Ule ni udhalilishaji pia..

Tunalizungumzia kwa Mapana zaidi..Ili muelewe..

Shemeji yako Wema..Ule nao ni udhalilishwaji hata kama hajapiga magoti..

Tatizo lenu nyie wasanii starehe mnazithamini kuliko maisha..
 
Last edited by a moderator:
Sijasema naunga mkono kwa video hii kuwekwa hadharani, la hasha....mimi nimepingana na wanaombeza ustaadhi kwa jukumu alilojipa la kudili na wasanii.

Ingawa pia nashawishika kuhoji ni mazingira/sababu gani haswa zilizopelekea video hii kuwepo hapa.

Kwa uzoefu wangu juu ya wasanii wetu, huwa kweli wana tabia za "kisanii", kwa mfano....kufanya jambo fulani nyuma ya pazia na anapokuja hadharani (kwenye media) anaongea ya kwake..hasa kwa lengo la kuonekana yeye ni msafi na meneja ndio tatizo.....kwa mtindo huu hata wewe na mimi sidhani kama linapendeza....na wasanii kama kina Dogo janja ni mfano mzuri wa wakoroga mambo kwa mtindo huo....

Pili, ni hulka tuliyojijengea kuwa kuomba msamaha ni kujidhalilisha.....hizi ni hisia potofu ndio maana mnaona pnc amedhalilishwa/amejidhalilisha.......mimi sioni hivyo, na hii video haina tatizo lolote.

Anayempiga mwenzake picha ya uchi kwa maridhianao na baadae kuiweka mtandaoni, kwangu huo ndio udhalilishaji....lakini mtu kuomba msamaha ni jambo la kawaida.

Mkuu hapo kweli mi nawewe tuna View za kitofauti, kama kwako kudharirisha mpaka iwe picha za uchi duh???Je Waweza kushare nasi mtu mzima yeyote mwenye umaarufu aliyewahi omba msamaha kwa kumpiga mwenzie magoti na kuchukuliwa kwa video kisha kutupwa mitandaoni??One thing hapo kwa blue, U missed my point, SIJASEMA KUOMBA MSAMAHA NI KUJIDHARIRISHA/KUDHARIRISHWA maana hakuna ambaye hajawahi Omba msamaha kijana!!ila swala hapo ni kuchukuliwa video unaomba msamaha ukipiga magoti kisha isambazwe kwenye social N/W.
 
Asa hapa diamond kaingiaje!!kwani bila ya kutajwa domo story hainogi nn....acheni wivu wa kijinga
Sina wivu na Diamond na sina sababu hiyo.
Kwanza umekosa heshima una mkashifu mwenzio kama wewe umekalilika. Katika hili ubadilike hii si tabia nzuri na si utu kabisa na si tabia ya mtu mwenye umri juu ya 18.

Kilicho nifanya ni mtaje diamond hapa ni kwamba aicho fanya Stadh Juma ndicho alicho fanya Diamond kwa wema hata yeye ali mrekodi wema na kuweka kwenye mitandao ya kijamii na kwenye maradio hivyo katika wadhalilishaji Diamond hawezi kutotajwa.

Huu ndio ukweli sina chuki na mtu.
 
Mi nafikiri katika hili Pengine Ustadh Juma kakosa utu kabisa na ubinadamu.


Pengine kumrekodi PNC na kusambaza kwenye mitandao huu ni udhalilishaji kabisa na unatakiwa kukemewa na wasanii wenyewe na Baraza la Sanana Tanzania[BASATA], maana likiachwa hihivi lipite ni wasanii wengi watazidi kunyanyaswa na kudhalilishwa kabisa.

Nitamshangaa sana PNC akiendelwa kuwa mikononi mwa huyu mtu maana kufanya hivyo hitakuwa ana bariki udhalilishaji alio fanyiwa.

Katika hili BASATA hilibidi wamshughulikie Ustadh Juma maana kumuacha ni kupanda mbegu ya udhalilishaji kwa wasanii na nitashangaa kuona wana kaa kimya na nita jiuliza sana kazi yao nini.

Hili swala lime wadhalilisha sana wasanii na walitakiwa wajitokeze hadharani kulaani hichi kitendo.
 
huyu Ostaz Juma sijui anajiskiaje huko aliko....sijui hata alikua anawaza nn kupost picha na video hiyo
 
Mkumbuke pia Jaydee alishawahi kurusha kwenye kipindi chake cha Diary ya ladyjaydee, Mwinyi msanii wa machozi bendi akiombewa msamaa na mama yake kwa Gadner na Jide
 
Kama ni muangaliaji wa kipindi cha mkasi mr blue alishawahi sema kitu kuhusu huyu jamaa
 
Aisee kama ni mpenzi wangu tunaachanaa huyo ostadh ni Mungu,??nyau kabisaa heri angempigia magoti mama yake mbafu sana P
 
Back
Top Bottom