DOKEZO UDOM ni Chuo Kikuu kisichobadilika, ubora wa utawala bado uko chini

DOKEZO UDOM ni Chuo Kikuu kisichobadilika, ubora wa utawala bado uko chini

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Tangu mwanzo chuo hiki ni shiida tu! Mara ngono hovyo hovyo! Mara vyeti nje nje! mara marks za bura kwa kila mwanafunzi. Baada ya kuzoezwa haya yote, sasa naamini viongozi nao wamefuzu kwa ujinga-jinga, wanajiongeza kazi iendelee! Nao sasa wanaamua wayapendayo.
Udom wana CIVE,college nzuri sana kwa ICT,ila madudu ya pale ni hatari,hata hayo majina na matokeo yaliyopotea wanayo,si kwamba hawana hata hardcopies.

Nchi hii kwenye ICT bado tuko nyuma sana,bora hapo udom,ukienda SUA hata matokeo hayapo kwenye mfumo,eti wanapeana matokeo kwa kupiga picha,chuo kikuu au genge la wajinga watupu?

Kuhusu UDOM,uongozi wa juu hauko sawa kwenye ufatiliaji wa mambo.
 
Juzi nilikua kwenye graduation ya vijana wangu morogoro SUA,nikakuta wameweka jukwaa kule uwanjani,nikajiuliza,hivi chuo kikuu hakina ukumbi wa kufanyia sherehe kabisa?,Nikawasha gari jioni nafika mazimbu nikakuta ukumbi mzuri tu ila wezi wameweka watu juani EMC.

Baadae nikagundua kuna wezi wamepiga pesa ndefu kwenye hayo maandalizi ya mahafali,na hii ni baada ya kutonywa na mtu wa palepale kwa kunionyesha hao majizi wakiwa jukwaani na mzee wetu Warioba.

Ili kuhakikisha hilo,nikaomba wanaofanya mahafali wanipe niangalie mfumo wa matokeo ukoje,ndio nikakuta hata matokeo ya miaka iliyopita hayapo,yaani ni chenga tupu.

Wizi ndio unaua vyuo vyetu,sitegemei UDOM kufanya huo upuuzi bila wezi kuwepo,tuanze na hawa wa SUA huitaji ujuzi kujua wameiba.
 
Mimi nimesoma UDOM na hii changamoto kweli ipo, baadhi ya watu huwa hawaonekani kwenye kitabu Cha wahitimu hasa wale waliocarry baadhi ya masomo mwaka mwa mwisho.

Na sababu kubwa ni kwamba UDOM ni chuo chenye college Saba, walimu wa college moja huenda kufundisha college nyingine ambapo kila college Ina uongozi wake.


Inaonekana hakuna connection au mawasiliano mazuri baina ya colleges.

ila pia hata kwenye matokeo nasikia siku hizi wamerekebisha, Ila huwa yanashake unaweza ukapata somo B plain ukajikuta yamebadilika umekula sup.


Ishawahi kunitokea somo nimepata B+ ikaja kuwa C na hii ilikuwa kwa wanafunzi wote wa course hiyo, na malecturers wakakataa kubadilisha tena wakaweka notice kabisa, GIGO (garbage in garbage out), ulichokiona ndio ulichokipata.



Nadhani changamoto hizi (nyingi)itakuwa katika vyuo vingi au karibu vyote isipokuwa UDOM ni case study tu kwa ajili ya popularity yake.

Udsm hakuna kitu kama hiki
 
Ile ni takataka kama takataka zingine
NOw I got you! Nimedokezwa kwamba siku tatu zilizopita kuna mwanafunzi ameruka gorofani kwa lengo la kujiua. Sababu ni hii hii ya matokeo ya mitihani. Kwamba aliambiwa ameshinda, baadaye kaambiwa anafukuzwa. Hapa tulijadili kama mzaha vile lakini sasa inaharibu maisha ya wanafunzi. MBaya zaidi inafanywa kama siri ndani ya chuo.

Nadhani wanasheria wanastahili kusaidia tatizo kama hili llitokanalo na uzembe wa chuo. NI kama hawajali kuwa-frustrate wanafunzi.
 
Udom, malalamiko yanakuwa mengi sana, nadhani inabidi itafutwe kampuni ifanye management audit ya chuo, na ije na Suluhu ya kudumu
 
NOw I got you! Nimedokezwa kwamba siku tatu zilizopita kuna mwanafunzi ameruka gorofani kwa lengo la kujiua. Sababu ni hii hii ya matokeo ya mitihani. Kwamba aliambiwa ameshinda, baadaye kaambiwa anafukuzwa. Hapa tulijadili kama mzaha vile lakini sasa inaharibu maisha ya wanafunzi. MBaya zaidi inafanywa kama siri ndani ya chuo.

Nadhani wanasheria wanastahili kusaidia tatizo kama hili llitokanalo na uzembe wa chuo. NI kama hawajali kuwa-frustrate wanafunzi.
Ile ni takataka tu!
 
Back
Top Bottom