Keynez
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 2,428
- 3,937
Kumetokea mtindo wa kusambaa kwa video za ngono (maarufu kama connection) na ambazo muhusika au wahusika katika video hizo wanatajwa kuwa ni wanafunzi wa chuo fulani nchini, mara nyingi ni UDSM, IFM na hata UDOM.
Sijawahi kusikia mamlaka za vyuo hivi zikiongelea kuhusu video hizi, ni kama linaonekana ni jambo la kawaida.
Juzi nimekutana na video ambayo inavyosambazwa wanasema ni wanafunzi wa UDSM ila ukiwaona wahusika ni kama waethiopia au wanyarwanda na hata lugha wanayotumia siyo lugha zetu. Hili mimi nimegundua kwa sababu ni mfuatiliaji, ila wengi wanachukualia mambo juu juu bila kutafakari. Isije kuwa kuna njama za kuteketeza elimu yetu sisi tunabaki tu kushangilia connection mpya.
Hili jambo lina madhara makubwa kwa taasisi husika na kwa elimu yetu kwa ujumla. Tayari elimu yetu ina changamoto nyingi, tusiruhusu nyingine kama hizi ambazo zinaweza kabisa kukabiliwa kabla hazijawa sugu. Nasemaga siku zote, uhai wa taifa lolote upo katika mazingira yanayozunguka elimu inayotoa kwa watu wake.
Nashauri mamlaka husika liliangalie jambo hili kwa umakini unaostahili.
Sijawahi kusikia mamlaka za vyuo hivi zikiongelea kuhusu video hizi, ni kama linaonekana ni jambo la kawaida.
Juzi nimekutana na video ambayo inavyosambazwa wanasema ni wanafunzi wa UDSM ila ukiwaona wahusika ni kama waethiopia au wanyarwanda na hata lugha wanayotumia siyo lugha zetu. Hili mimi nimegundua kwa sababu ni mfuatiliaji, ila wengi wanachukualia mambo juu juu bila kutafakari. Isije kuwa kuna njama za kuteketeza elimu yetu sisi tunabaki tu kushangilia connection mpya.
Hili jambo lina madhara makubwa kwa taasisi husika na kwa elimu yetu kwa ujumla. Tayari elimu yetu ina changamoto nyingi, tusiruhusu nyingine kama hizi ambazo zinaweza kabisa kukabiliwa kabla hazijawa sugu. Nasemaga siku zote, uhai wa taifa lolote upo katika mazingira yanayozunguka elimu inayotoa kwa watu wake.
Nashauri mamlaka husika liliangalie jambo hili kwa umakini unaostahili.