UDSM: Tunaomba msaada wenu JF!


Nenda upate kikombe cha kahawa maana unahitaji some caffein
 
Mkuu Ben,

Hakuna ugomvi wowote kati yangu na mama. Mama ni mmoja wa memba wanaoheshimika sana hapa forum. Imekuwa tu yeye yuko upande wa kina Mkandala kwenye hii case na mimi niko upande wa wanafunzi.

Siko upande wa Mukandala tafadhali usitoe maneno from u ukayafanya yangu mdomoni mwangu. Nimepita mlimani, I have the feeling and I put myself on the students shoes now. Mimi sina chama jamani. Ninachoweka hapa hakifungamani na mambo ya CHADEMA,CCM, CUF, DP wala UDP.
However, sijasema wanafunzi wamekosea au utawala uko right, what I wanted to see are the explanations from Ant Ufisadi au wanafunzi kueleza kwa uwazi nini walitaka.
 

Ni makosa makubwa sana kwa uongozi wa chuo kikuu kuingilia uhuru wa wanafunzi wasomi wa kujichagulia viongozi wao. Kikwete sijui anafanya nini badala ya kunyakua simu na kumpigia Mkandala na kumuonya kuwa asimuaibishe.
 
Nimepigiwa simu sasa hivi na mwanafunzi wa mwaka wa pili wa IT,

hakuna kozi hiyo pale mlimani,navyojua kuna Bsc. in Computer science pekee,hauna haja ya kutupa namba.siye wenyewe tutajua.

Invisible fuatilia suala hili kwa ukaribu,



NDUGU YANGU UNA GUBU!! KWELI KWELI! SASA HUKIMALIZA HIYO KOZI YA COMPUTER SCIENCE UTAKUWA NANI?

AU HAUJUI? KITU KAMA UKIJUI BORA UNYAMANZE MIMI NIPO HAPOHAPO NI IT MTARAJIWA NA PIA NSHAKUWA IT, NIPO FIVE NA WAKATI FFU WANALETA WANAKUJA NILIKUWA NAPATA SAMAKI NA WALI CAFETERIA 1 WALIPO ZIDI KUSOGEA NILIKIMBILIA MAENEO YA HALL 1 ,

WAKATUKIMBIZA IKABIDI NIINGIE KWA AKINADADA PALE HALL1 WAKANIFUNGULIA NIKAPOA NOA KUWASIKILIZIA ,NDIO WAKAANZA KUPIGA MABOMU YAO TUKAWA NA MAJI TUKANAWA MACHO YAKAWA HAYAWASHI ILA SHIDA IKAWA KWENYE PUMZI TU HEWA ILIKUWA NZITO TU!,

MPAKA WALIPO MALIZA KUPIGA HAYO MABOMU YAO NDIO NIMETOKA HAPA,
WAKATI NAKUJA COET NA BASS ZA MABIBO HOSTEL ZIKAWA ZINAINGIA KUWACHUKUWA WANAFUNZI.

PIA NIKAONA DADA MMOJA KABEBWA KUTOKANA MSHITUKO PRESHA IKAPANDA HUYO DADA INAONEKA NI MPISHI WA CAFTERIA 1.

NIPO COET NIMECONNECT WIRELESS NAENDELEA NA MAMBO YANGU.
HAUNA POINT.
SIKUNYINGINE USIBISHIE WATU HOVYO.

MWANAHAKI ASANTE KWAKUTOA INFORMATION.
 


Lakini kwa nini afukuzwe kwa kuandamana kwa amani? Hii ndio issue yangu. Ni sawa kabisa nami najua kwamba ulihangaika sana kumsomesha mjukuu wako, lakini nani amesema ukishasoma kwa kuhangaika basi lazima uwe yes mzee?

Binafsi pamoja na kwamba napinga sana sababu za hawa vijana kuandamana, naunga mkono haki yao ya kuandamana na zaidi ya yote ninalaani sana na kwa nguvu zangu zote matumizi ya nguzvu yanayotumiwa na polisi. Kwa sababu ni vitisho vya namna hii vimetufanya sisi tuwe taifa la waoga, wanafiki na watu wa kujipendekeza. Nitaunga mkono vitendo vyovyote vya kutuondelea woga na unafiki watanzania.
 

Hii ni hatari sana.

Mkandara ameshindwa kazi na sasa amepiga wanafunzi bila sababu yoyote. Common sense ingeweza tu kumwonyesha kuwa ni makosa makubwa kujaribu kuwachagulia wanafunzi wasomi viongozi. Yeye alidhani kuwa kila mara ccm wanavyoiba kura zanzibar na sehemu zingine na kisha kutumia mabomu na vipigo kunyamazisha watu ndio the only way.

Mkandara unatia aibu, unaaibisha chuo na taasisi yako ya demokrasia. Acha kupiga wanafunzi bila sababu. warudishe shule na uwaachie wachague viongozi wao kwa matakwa yao.
 
Nasikitika sana ninapoona wachangiaji ninaowaamini kama Mama anaposema tuwaache kwa kuwa walienda kupokea t-shirt na kofia kwa Mafisadi. Hivi kama mzazi unawatoto 4 na 1 ni mlevi hivi ni sahihi kwa wale wengine wakija kuomba fedha za karo uwatimue eti wataenda kulewa?
Kwa hali ilivyo sasa hivi pale Mlimani kama wanafunzi watarespond kwa FFU tunaweza kutengeneza tukio kama la Jan 27 pale Zanzibar
 
Ni makosa makubwa sana kwa uongozi wa chuo kikuu kuingilia uhuru wa wanafunzi wasomi wa kujichagulia viongozi wao. Kikwete sijui anafanya nini badala ya kunyakua simu na kumpigia Mkandala na kumuonya kuwa asimuaibishe.

Lakini si Kikwete alimpa kazi rafiki yake Mukandala baada ya yeye kumfanyia kazi nzuri na REDET? Tatizo ni kwamba Kikwete kote kaweka washikaji, na anawaamini, hasa wasomi kama mkandala hawezi kum-oppose! Hapo tusitegemee kitu.
Hata mimi nimewasikitika sana wanafunzi kuwa treated kama wahalifu!
 

Mama nimekuelewa, tuendeleze issues hapa maana taifa liko hatarini na watoto na vijana wenzetu wanaonewa mbele ya macho na masikio yetu.
 


Bandugu,
The situation is terrible at UDSM. Yataka ujionee na si kuadisiwa. Kama una gari kwa usalama usiende nalo kupita utawala.

Jamani, masikitiko yangu ni juu ya uwezo wa wasomi wetu watarajiwa. Fikra za watawala wetu juu ya mfumo wa elimu ni kuufanya uzalishe wataalamu wenye fikra mgando. Lakini kwa ulafi uliwafanya pofu wanashindwa kuona ndani ya zao la mfumo huo mbovu wanazalisha pia wapiganaji huku uchumi uzakomaza jeshi la wamachinga. Haya majeshi mawili yanazidi kukomaa na ipo siku yatakuwa "MUNGIKI"

Ushauri wa bure kwa Mkandala-VC: Naomba uweke rasmi MGOMO kama Course mojawapo itolewayo UDSM na wanafunzi wapewe course work marks. Hii itakuwa vema maana naona migomo inachukua sehemu kubwa ya masomo UDSM na kinachopiganiwa ni cha haki kuliko nadharia zisizo na tija zilizojaa ndani ya "MADESA"

Mh. Invisible naomba kutoa hoja.
 
Gembe acha chuki zako binafsi, kuna kozi inaitwa Computer Engineering and Information Technology (CIT) au hauna info nini kaka?
Kaka Ndege na wewe kwa leo umetokosa. Nina kijitabu hapa alikiletaga mjukuu wangu hata kozi hiyo inayoitaja wewe pia haipo. Kozi za kompyuta ni:-

B.Sc/ M. Sc ( Electronics and Information Technology)

B.Sc./M. Sc (Computer Scinece)

PGD (ICT Policy and Regulations)

Master of ICT Policy and Regulations

Kuna Department ya Computer and Systems Engineering.
 

Nakubaliana na wewe a thousand percent! Haikuwa na haja ya kuita polisi kama wanafunzi walikuwa kwenye maandamano ya amani. Ni wajuavyo hasa FFU huwa waomba vitu kama hivi vitokee at least waonekane wanafanya kazi maana huwa zoa zoa kama mtego wa panya. sijui ni kuwa exited na excess energy baada ya kutokufanya kazi kwa muda!
 

Poleni sana vijana wa mlimani kwa uonevu mnaopata toka kwa serikali ya ccm. Serikali isiyojali masilahi ya wananchi wake zaidi ya kutumia mabavu na kumwaga damu kuongoza nchi.
 
Angalia comment ya mwananchi mmoja kutoka Manzese hapo chini.

Muwasaidie vijana, vinginevyo mnakipeleka wapi chuo?? siasa za wanafunzi waachieni wenyewe
 

Ahh Ant ufisadi mwanangu! wapi nimetamka haya. By the way pole, nilikuwa nakuwaza sana, kwa kuona hii post yako nafarijika, hope you are okay
 

Susuviri,

Watu wengi hapa wamekuwa wanaongelea sana suala la Kikwete kumpa Mkandara uongozi wa juu kabisa hapo Mlimani. Ziara ya kwanza ya Kikwete hapa US alikuja na huyu Mkandara. Utakumbuka pia kuwa mwanzoni mwa uongozi wa Kikwete, Mkadandara alikuwa mmoja wa washauri wa Kikwete.

Katika hili, kama Kikwete anajali demokrasia na haki ya vijana wasomi nchini, achukue simu na kumpigia Mkandara na kumuonya kuwa aachane na uonevu huuu unaovuka kipimo cha kawaida cha kibinadamu.

Ooooppppssss nimesahau kuwa Kikwete hana ubavu wa kufanya maamuzi mazito kama haya!!!!
 
Hilo la uongozi wa chuo nalielewa, au kwa vile ni Mtatiro yumo basi nisihoji chochote. Sitaki malumbano period!

Kwa wanyonge njia rahisi ya kusikika mara nyingi huwa ni kuingia barabarani.

Ukifuata sheria ya mazungumzo ya amani hapa nchini utachelewa kufika kwa kuwa watakuweka kapuni na hawajali hata shida ya haraka au utakaa foleni ukome.

Baaada ya migomo kama huu hapo ndipo utaona baraza la chuo watamwita huyo makamu mkuu wa chuo na jopo lake na pia uongozi wa wanafunzi waawelekeze na kushauri cha kufanya.

Inasikitisha kuwa mgomo utokeapo eti ndipo wahusika wanatafuta kuzungumza pande zote.Toeni siasa vyuoni maana hiyo ni taasisi huru haifungamani na chama cha siasa

KUSOMA NI KUELIMIKA
 

Omutwale,

Huu uonevu lazima ukemewe kwa lugha kali kabisa. Kulikuwa hakuna sababu yoyote ya kupelekea FFU na kuanza kupiga wanafunzi ambao wanasoma na wengine wakiandamana kwa amani kabisa.

Kwanza kabisa, kulikuwa hakuna sababu ya kufukuza chuo viongozi wa wanafunzi kwa vile wamekataa suala la uongozi wa chuo kutaka kuwachagulia viongozi. Kila siku tunaongea kuhusu Kenya na Zimbwabwe kumbe tuna Zimbabwe zetu zinaendelea hapo Tanzania tena kwenye taasisi ya elimu ya juu.

Shame on you Mkandala!
 

COET

Faculty of ECSE kuna Depatments tatu

Department of Telecom

1:BSc Telecommunactions Engineering

Dertment of Electrical Power

2:BSc Electrical Engineering
3:BSc Electrical Power Engineering

Department Of Comp and system Engineering

4:BSc Computer Engineering and Information Technology (CIT)

Una lingine Mama?

Tafuta info kabla ya kukurupuka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…