Kubwajinga
JF-Expert Member
- Jan 23, 2008
- 2,193
- 299
P'SE STOP POSTING UNLESS UD STUDENTS CAN RESPOND
Kama hakuna wanafunzi wa UD wanaoweza kuleta habari, waungwana naomba tuachane na hii thread maana naona imeshaanza kuzua malumbano yasiyo na nywele. Angalia Mwafrika wa Kike vs Mama.
Ni maneno mazito haya mkuu na wenye ukweli ndani yake!However hata mimi nimeshapitia unyanyasaji kama huo!Na sidhani kama hoja peke yake vitawasaidia kusikilizwa!Almost all the times wanafunzi wamekuwa na hoja za msingi lakini ni hoja kama hizo ambazo viongozi wanaona ni hatari kwa maslahi yao na ya wale waliowapa vyeo hivyo!Nashangaa kwenye taifa huru viongozi wanasema wananchi ni huru wakati ukweli ni kwamba haki yenyewe bado inabidi ipiganiwe licha ya kwamba ni haki ya kibinadamu kuwa na haki na kuwa na uhuru!So why do we have to fight for what is rightsously ours?Jibu ni clash of interests..na sad enough ni personal ones!Sio zenye kujenga bali kubomoa!Ndio maana mara nyingi tumekuwa tuki resort kwenye migomo!Trust me been there done that!Kwanza ukiwa na hoja ya nguvu unapewa u"ring leader" na hapo wanakuflag kuwa wewe ndiyo kichocheo cha vurugu...bila kujali kuwa una hoja za nguvu..wanakuharibia masomo na unaswekwa lupango!I know that Masanja!
Hoja watu wanazo..nakuhakikishia kuwa kama ni politics watanzania we're very good at it!Tatizo ni ukiritimba!Haijalishi unasema nini!wao watatumia lugha fupi tu ya "wahuni hao"..i know this ni hard!Na watu wanaogopa kufuata process.kwa sababu process yenyewe haijwa kunstructed kutoa majibu na muafaka..badala yake ni kama staging point ya kuitokomeza hoja yako!Together with time..mnakuta msha graduate na kuwa hata na mke na watoto kabla ya solution kupatikana!Unajua sysytem ilivyo..hakuna anayefanya kazi bila maslahi..hakuna wazalendo wenye kuitumikia jamii na umma bila kujali whats their share!Kutokana na hilo milolongo ni mirefu na yenye kukatisha tamaa!I've been there bro..trust me!Mkuu Mushi, Me too I have been there at the HILL. I entirely agree with what you write here mkuu wangu. Lakini huoni kwamba hawa wanafunzi inabidi wajifunze njia sahihi za kutatua matatizo yao na ya JAMII? kama hoja zenu zimekataliwa, what else? ni kugoma, ni kuvunja nyumba, ni kupiga sympathizers wa watawala?? I dont think so. Unajua haki ni neno dogo sana lakini ni very wide na lina process ndefu sana kulitimiza.
Ofcourse kama haki ya mtu ingekuwa inatolewa automatically..Tusingekuwa na dunia tuliyonayo leo! Ndo maana dunia imejaa vita, umaskini nk..its all about HAKI na ningetegemea wanafunzi wa CHUO KIKUU wawe wa kwanza kulitambua hilo. Kama Mkandala hana msaada wana avenue ya kumuona Waziri etc..ni process ndefu na bureacratic, lakin hey ndo njia iliyopo unless kuna njia mbadala. Mgomo inabidi uwe last resort na watu wawe na justifications. Kwamba hatukuwa na njia nyingine. Kama swala la Mganda kunyanyaswa katika harakati za kugombea uongozi wangeenda mahakamani-simple. Unaweza sema ni process ndefu, but what about babu yangu kwimba anayeendesha kesi miaka kumi? sasa Msomi kama anaogopa hiyo process..what do you expect? He should work to change it for the better of him and my grand father in the village!
System yetu ni mbovu na very corrupt, lakini kama Mwanakijiji asemavyo, bila HOJA DUNIA HII HUWEZI KUAMBULIA KITU! NDO MAANA WAZUNGU MPAKA KESHO WATATUPIGA BAO..WANAENDA NA HOJA, SISI MARA NYINGI NI EMOTIONS ZA KUONEWA....WASOMI SHOULD KNOW BETTER!
hivi hushangai kwanini mtu anasomea mambo ya kilimo lakini hataki kwenda kuishi kwenye kilimo chenyewe yaaani kijijini?
Kubwa jinga tulia ndioa mwanzo tu huu..then watasoma na kupitia maoni haya na wao wataweza kuposti yao!
Ndio maana nilisema kwenye msafara wa mamba na kenge pia wapo sasa mama akawa mkali. Kila mwenye kutoa hoja ya kuwakandamiza wanafunzi atasema walifanya vurugu na kuvunja majengo. Ikumbukwe ule haukua mgomo bali ni kikundi cha "wanafunzi" wachache (hawazidi 50) waliokutana usiku wa manane kufanya vurugu. Lakini ikumbukbukwe katika hili la wanafunzi kusimamishwa masomo wanafunzi wa CoET waligoma kuingia madarasani for hours last Tuesday ili waongee na uongozi ili uwaeleze mustakabali wa mwenzao aliyesimamishwa bila kuwa na kosa. Na walifanya hivi bila kuwapigia kelele wengine.
wengine wanasema tusiwasaidie hoja kisa walienda kumsikiliza Makamba diamond. Japo hiyo nayo siyo hoja lakini bado walioenda kwa Makamba walikua ni sehemu ndogo sana ya wanafunzi.
Huyo Mukandala ambeye baadhi yenu mnahisi ni Mungu
i. Amemfukuza mwanafunzi kwa kumhusisha na vurugu ambazo wakati zinatokea yeye alikua kwenye kikao na mkuu wa kitivo chake
ii. Jumatatu iliyopita aliita waandishi wa habari akawatangaza kufukuza wanafunzi 16 kwa makosa mbali mbali ikiwemo kuvuta bangi na kubaka, jina la waziri mkuu wa DARUSO Mtatiro halikuwepo. J3 hiyo hiyo Mtatiro alionekana kwenye kipindi cha Jeneral on Monday akiwahimiza uongozi utimize wajibu wao kwa sababu wanafunzi wanauliza maswal ambayo yeye hana majibu na alikua amezuia mgomo siku hiyo na kwamba hata weza kuzuia kama watataka kugoma tena. J4 Mtatiro naye akapewa barua ya kusimamishwa akijumuishwa na wale 16
Ndugu zangu wana JF ni dhahiri tuka conclude kuwa hakuna anayeweza kuiweka kinagaubaga hapa issue ya UDSM, vijana wetu wameshindwa kujieleza, lakini kama ilivyoelezwa awali, wengi wetu tumepitia mlimani, tunaielewa situation, na kwa kwa kutumia uzoefu huo tunaweza kutoa mpendekezo ya suluhu mlimani. Nilikuwa mlimani miaka ya 2000 mwanzoni, enzi za akina Mkili, Zitto, Msando, Rugemalira, Ndaskoi etc.
Kwa ufupi hali ya demokrasia nchini mwetu inashabihiana kwa karibu na ile ya pale mlimani, kuna vitisho,ukandamizaji,rushwa,kubambikizana kesi na kila aina ya ufisadi baina ya wanafunzi wenyewe, ndani ya DARUSO na uongozi wa chuo. Wanafunzi wengi ambao ni potential kuwa viongozi na wenye ushawishi wanatafutwa au wanatafuta support ya makundi fulani ya nje yanayopambana na system nyingine ya utawala wa chuo ambayo imewekwa na system yenye wafuasi ndani ya jamii ya wanafunzi. Wakufunzi wao nao wamekuwa hodari wa kuzungumza kwenye forums za nje ya chuo ingawa wao wenyewe wako kwenye spoiled system ambayo wanaogopa kuisemea. Tutegemee nini sasa? Product ya hawa wakufunzi ndo sisi watanzania waoga na wajinga wa kujieleza. Ni kweli pia kuwa mtazamo kifikra miongoni mwa wanaharakati hawa wanafunzi umetofautiana na wakati mwingine kunakuwa na hoja zisizo na msingi zaidi kuliko zile za msingi, lakini all in all lazima tukubali kuwa kuna tatizo UDSM. Kwa hiyo ni mgogoro unaotakiwa kutazamwa kwa upana. Katika mazingira haya kuna walio neutral, wanaoona hakuna tatizo lakini kuna wanoona kuna tatizo.
Nimewasiliana na baadhi ya vijana waliopo pale, ni kweli vijana wameamua kugoma ili wenzao takriani 25 waliosimamishwa masomo warudi. Kisheria mgomo huo ni batili maana viongozi wa DARUSO hawajaridhia. Kiini cha mgogoro wote huu ni Uchaguzi. Utata wa suala hili la uchaguzi wa rais ulioleta utata. Kumekuwa na matatizo ktk chaguzi nyingi za UD na wakati mwingine kumekuwa kuna attempt za kupindua serikali. imekuwa ikitokana na kupandikizwa kwa viongozi na utawala wa chuo, wengi waliowahi kuwa marais kwa kupandikizwa tumewaona wakipewa zawadi ya ajira na chuo, wapo akina Kusaja, Rugemalira alipewa zawadi ya scholarship, Kayombo alipewa zawadi ya ajira etc. Tuwaponde wanafunzi kwa kutokuwa na hoja lakini kuna tatizo mlimani linalohitaji attention yetu.
Mbona uishi kujichanganya changanyaMsomi wala usiwe na wasiwasi kabisa katika hili. Washauri wanafunzi wafuate ushauri wa Mwanakijiji na kuweka malalamiko yao kwenye maandishi. Wawe as precise as they can.
Meanwhile, vilio vyao vimesemwa hapa na wengi wameviona na sasa kinachofuata ni bango tu. Huyu Mkandara hawezi kukandamiza haki na demokrasia wakati ni yeye ndiye alikuwa ana-organize ya mambo ya demokrasia Tanzania kama sikosei.
Demokrasia lazima ioneshwe kwa vitendo na yote hayo yataanzia hapo chuoni. CCM hawawezi kuingilia chaguzi za wabunge (kama ule wa kiteto na kupiga watu) na wakawa hadi na ballz za kuingilia wasomi wetu.
Kwa hili waambie vijana kuwa wana bonge la support hapa JF na kilio chao kitasikiwa pia.
Mbona uishi kujichanganya changanya
Msomi wala usiwe na wasiwasi kabisa katika hili. Washauri wanafunzi wafuate ushauri wa Mwanakijiji na kuweka malalamiko yao kwenye maandishi. Wawe as precise as they can.
Kwa hili waambie vijana kuwa wana bonge la support hapa JF na kilio chao kitasikiwa pia.
ninadhani tunapoteza muda. kwanza tayari wameisha anza kugoma, alafu unawashauri waende mahakamani? ninaendelea kusikiliza hoja walizonazo ili nijue chimbuko lao kwa kinagaubaga.
ninawaombea success katika mgomo huo.
Mara chache sana migomo huleta mafanikio, bali mara nyingi sana migomo huleta mwanga wa kuonyesha mapungufu mengi kwa wanaogomewa. Ushauri binafsi, next time kabla ya kugoma leteni matatizo yenu hapa ili tuwashauri mfanye nini kutatua hayo matatizo.
Kwa kuwa mmeshagoma basi inabidi mshupalie hapo hapo. Nakumbuka enzi hizo "TOGETHER WE STAND" pamoja na pesa za SIGARA, tulikuwa tunagoma kwaajili ya kufichua VIJIFISADI, lakini ndo tukaambiwa kuwa tunataka pesa ya sigara. Ili muweze kufanikiwa lazima ktk hilo zoezi nyote mhusike, lakini mkishakuwa kwenye makundi basi ngoma imewalalie.
Nimekuja kukugua tunaweza kujenga taifa la watu wa ovyo kama tukiendelea kuwatetea watu ambao wanawatetea vijana wahuni,nimeongea na mmoja wa walimu wa chuo kikuu cha Dar es salaam,ambaye amenieleza kuwa wanafunzi waliosimamishwa wametokana na makosa mbalimbali ya utovu wa nidhamu,kama kufanya mapenzi hadharani maeneo ya Hosteli za mabibo,na wengine wamekutwa wakivuta bangi na kufanya mambo ambayo ni against students bylaws,sasa tuwatetee hawa??
hawa wanaleta motion hii ,kisa Kasimamishwa waziri Mkuu wa DARUSO.Hivi kweli mtu akiwa hana nidhamu aache chuo tu kisa yeye ni waziri mkuu??kisa yeye ana influence kubwa katika wabunge??hivi ndiyo kumaanisha kwamba hata Lowassa angeachwa hata kama anapendwa na baadhi ya wana CCM.
Mie nawashauri mtulie na Mkae Msome na mfanye uchaguzi kwa Amani,Uchaguzi wa DARUSO ni changamoto chache tu ambazo zina mwisho wake.
Ehe
Mkuu umegusia swala la mapenzi,kwani ni kosa kufanya mapezii ama mapenzi yepi hadharani??