Udsm yaporomoka kiwango kutokana na siasa

Udsm yaporomoka kiwango kutokana na siasa

hahahahaha,naikubali SUA sana,hata elimu yao iko juu balaa tena kiukweli ilibidi iwe hata juu ya UDSM!
mimi nilicho mpinga elimukwanza ni kwamba siasa ndizo zinashusha chuo,sidhani kama kuna ukweli ndani yake maana kama ingekuwa ni kweli basi ghana university ingekuwa ya kwanza Africa!

Hata wakitoa elimu bure mtoto wangu hasomi udom,never

Ubora wa elimu ni nini? mbona hatujaona nchi ikipiga hatua pamoja na kuwa na vyuo hivyo mnavyoshabikia kuwa ni bora?
 
utashangaa graduate ca'nt construct a simple englis sentence. Najua wengine mtasema english ni lugha tu .I don't care . I know it has a role in the faliures.

hahahahaha,sikubishii mkuu kwani hata presentation tu ni adhabu kubwa sana kwa wengi!
Sasa sababu ni siasa vyuoni au ni mfumo mzima wa elimu toka chekechea?
 
Mh. Speaker, Mbona mkuu wangu nimesema Dar bado ipo juu! Au kwa vile nimesema Dar badala ya UDSM?Hahaha mimi ni MSUASO bwana! Hicho chuo cha Kata naangalia ustaarabu asije akasoma mtoto wangu kama hakitabadilika

Una utani na Mla Mbivu wewe , hakawii kuja juu
 
Safi elimu kwanza. Ud hawana ubunifu wa taaluma zao zaidi ya kujaza siasa kwenye vichwa vyao.utadhani kuna faculty of Politics and propaganda ,siku zote utadhani wanajiandaa na final project ya migomo na maandamano, uone walivyo punctual kwenye maandamano na migomo but hawafanyi hivyo kwenye projects na innovation. Niwaambieni nchi za wenzetu a big university kama Ud haiwi just source ya politicians kama ilivyosasa bali wanasayansi na chachu ya maendeleo kisayansi. tafiti zenye faida. Uchaguzi umeisha wamekosa cha kufanya ,sasa wanadai katiba mpya ,waulize ya zamani unaijua vizuri? atanukuu mapungufu ambayo Mnyika na Slaa wananukuu tu bila kuongeza hata mstari mmoja mwingine aliouona yeye pindi akiperuzi. nawaombeni vijana wenzangu hasa wasasa msiwe drived tu ,jaribuni kusoma, kutafiti na kutafuta ,msiwe na kauli za flani kasema , kila asemacho flani yes, na kila asemacho fulani no, no kuweni waerevu na mwerevu ni yule haamini kwa kurithi bali kwa kutafiti na kulinganisha. tuache uvivu .Chuo kinakufa taratibu ,najua mtatoa sababu kuwa ni mkandara ila kila mmoja wetu anahusika. jiulize mimi nafikiria nini zaidi. masomo , siasa,utafiti, maendeleo?

hivi nyie mmesoma wapi?
mmeifanyia nini tanzania?

maana msiwe watu wa kusoma kuja kukosoa wanaosoma udsm peke yake!
Kipi ambacho hata kwa ishara unaweza kutuambia umefanya wewe au as a project ya innovation uliyo ongelea?
aibu tupu,
 
Ubora wa elimu ni nini? mbona hatujaona nchi ikipiga hatua pamoja na kuwa na vyuo hivyo mnavyoshabikia kuwa ni bora?

nadhani ni topic ndani ya topic sasa,hapa mada ni "siasa zimeiporomosha udsm" ndicho ninacho pinga,...sina shaka ikianza mada ya wasomi wameifanyia nini nchi nitakwambia hakuna chochote!

Ni kwa sababu "wooooooote tuna fundishwa ufisadi na kutokuwa wazalendo" kila mtu anawaza asome sana,apate nafasi sehemu fulani ale kwa zamu yake
 
Wana jf kuna habari kuwa hadhi ya chuo kikuu cha dar es salaam inazidi kuporomoka kutokana na vyuo vya ardhi na mhimbili kujitenga.sasa imebaki engineering tu inachokibeba chuo.aidha inadaiwa kuwa tofauti na prof luhanga makamu mkuu wa sasa anaendekeza siasa badala ya taluma na utafiti.sua sasa wanashika nafasi ya 28 kwa ubora africa wakati mwaka jana walikuwa wa 78.

Source yako iko wapi tukaione kwanza???
 
Wana jf kuna habari kuwa hadhi ya chuo kikuu cha dar es salaam inazidi kuporomoka kutokana na vyuo vya ardhi na mhimbili kujitenga.sasa imebaki engineering tu inachokibeba chuo.aidha inadaiwa kuwa tofauti na prof luhanga makamu mkuu wa sasa anaendekeza siasa badala ya taluma na utafiti.sua sasa wanashika nafasi ya 28 kwa ubora africa wakati mwaka jana walikuwa wa 78.
Kife kabisa ili kizaliwe kingine. Ubabe wa maprofesa, wanafundisha kwa kiwango cha chini...udikteta.....
Kife tuu!
 
vigezo vilivyotumika,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,isijekuwa ni majengo
 
Tatizo Wana UDSM tunajisahau nakuendelea kushikilia dhana potofu kuwa UDSM ni Harvard ya Tanzania. Huu ni ushenzi ndo maana chuo kinaporomoka. Nimesoma pale miaka ya '90s kilikuwa tofauti sana na sasa, vijana wamekuwa wa kukalili tu madesa ili wafauru mitihani. Sishangai Mzumbe, St. Augustine, UDOM na hivyo vingine kuendelea kufanya vizuri zaidi ya UDSM.

Ni haibu sana kujiita Harvard ya Tanzania kwa sasa chuo kilivyo. Hiyo Harvard siyo jina na sifa tu kuwa ni chuo kikongwe bali watu/walimu wanafanya kazi za kueleweka kukifanya kuendelea vile kilivyo. Kama chuo hakifanyi research za kutosha kimepitwa na wakati. Walimu wanaendelea kutumia madesa yao ya mwaka 47 mpaka sasa kufundishia wanafunzi wakati mambo yanabadilika kila siku. Walimu wanahitaji kujiendeleza siyo tu kumaliza hizo PhD au Masters nakujiona ndo mwisho wa elimu.
 
BUT,hakuna chuo hapa tanzania,aidha cha umma au binafsi ambacho mhadhiri wake hajapita UDSM,kwa tanzania UDSM ni ACADEMIC BRIDGE,suala linakuja je nini kifanyike ili elim ya vyuo vye2 iendane na wakati,MAJAJI WOTE MNAOWAJUA,WAMEKATIZA UDSM,AKIWEMO WEREMA ANAEPNGANA NA UMMA
 
The FALL of UDSM is a continuation of the downfall of public institutions! Taasisi za umma zote iwe elimu, afya, huduma nyingine etc etc zinazotegemewa na Watanzania masikini walio wengi who have no alternative, zinazidi kuporomoshwa na no body cares coz kama elimu they can afford to send their kids somewhere to get quality education, and if it is health they can afford to go to South Africa, India etc etc Its just a continuation of the conspiracy to keep the poor people down! They'll get poor education, poor health services, poor living conditions,etc etc and remain poor forever! Watoto wa wakulima hawana mtetezi! Hawana accomadation ya kutosha iliyopo horrible, overcrowded, lecturers wachache,hawawezi kufanya kazi kwa lundo la wanachuo, library vitabu ishu, mazingira magumu kila kitu
 
Nabii hakubaliki nyumbani. Hakuna mahali popote ambapo siasa haingii hata katika dini swala ni siasa ipi au ya aina gani inayozungumziwa?
 
Tuseme kuwa kwa sasa watu tumekua wabinafsi na hatupendi uhalisia. Tuache majungu kike ejenge nchi yetu
 
We Speaker umesoma wapi wewe? Usikosoe tu wewe umefanya nini mpaka sasa ?
 
Sisi wana statistician tunasema (put them in a basket of only 2 unis) utaona UDSM kimeporomoka ki ubora ukilinganisha na SUA, mtu anatoka kuwa wa 78 hadi 28 wakati wewe miaka yote uko pale pale utakuwa unafanya nini, wangekuwa watoto wangu ningempongeza SUA zaidi ya UDSM kwa vile anaonekana anajituma zaidi ya mwenzake.


Umeona enheee!!! wewe kweli ni statistician manake nilikuwa nashangaa ni kwanini wote hao hawakuliona hilo!! Kama utaangalia SUA wamepanda kwa % ngapi, na UDSM wamepanda/kushuka kwa % ngapi basi hiyo margin ni mbingu na ardhi!
 
Udsm tunayoijua siyo ya sasa wewe angalia hata mijadala yao sikuhizi pumba tupu.raking wanaangalia vitu vingi ikiwemo hata uwezo wa wakufunzi lakini academically kwa uwezo wa kitaaluma kwa undergraduate UDSM imeshuka sana.Chuo akiwezi kuendelea kwa tafiti za quetionnaire kama Redet n.k.chuo lazima kiwe na tafti za kisayansi zinazotoa output

Dah, basi bana! Nilipomaliza SUA mwaka ule, ofisi niliyoajiriwa nilikutana tulipelekwa na washikaji wawili kutoka UDSM! Sio siri, kv washikaji walitoka UDSM na mimi toka SUA, (na kwa bahati mbaya watu wanaidharau sana SUA), nikajihisi kama jamaa watanifunika vibaya sana!!! my god, hadi pale nilipokuja kuona magamba yao ndipo nikaamini kumbe washikaji kweli wanatoka UDSM!!!!! in short niliwafunika kabisa!!!
 
I love the University of Dar es salaam, japo sijakisoma. Napenda hasa ile miti waliyo ipanda.
 
jamani mbona ni UDSM tu na SUA vipi kuhusu UDOM, MZUMBE? hat ST. AUGUSTINO-Mwanza. TUMAINI UNIV. hazipo kwenye ranking
 
Back
Top Bottom