Kuna takwimu ya muhimu sana hukuionesha na labda ndo sababu ya kuzificha hizo table. Hii ni idadi ya walijiregister toka kila chuo (wangapi wamejiregister, wangapi wamefeli na wangapi ndo waliofaulu). Ukiangalia mathalani matokeo ya module F utaona walifaulu toka UDSM ni 112 ambayo ni sawa na 24.3% ya wote waliofaulu SIO YA WALIOJI-REGISTER, hivyo hivyo kwa IFM ni 90, TIA ni 44 na Mzumbe ni 39.
Hoja yangu ni ipi?
Ni kutaka kujua wamefaulu 112 (UDSM) kati ya wangapi?, 90 (IFM) kati ya wangapi? 44 (TIA) kati wa wangapi? etc. Ukicheza na percent huwezi ona mantiki hii lakini ukizichambua idadi kamili ndo utaelewa. Mfano kama IFM wamefaulu 90 kati ya 140 walijiandikisha na UDSM wamefaulu 112 kati ya 250 huwezi ukipiga percent kwa chuo (pass vs fail) utaona wenye wanafunzi wachache wana pass rate nzuri. So tulitee hizo table ili kuone enrollment ilikuwaje kama hatujamwaga sifa au kukosoa vigezo vilivyotumika