Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,307
- 25,932
Tangu Rais Dr. John Pombe Magufuli kuvunja Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na kuipandisha hadhi Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kuwa Jiji la Dar es Salaam, kumekuwa na mijadala kemkem kuhusu jambo hilo runingani, redioni na hata mitandaoni. Mjadala hasa unajikita katika kuelewa kilichofanyika jana. Wapo wanaosema kuwa kwasasa Mamlaka tu ya lililokuwa Jiji la Dar es Salaam ndiyo yaliyowekwa chini ya Ilala na jiji liko vilevile na pale pale.
Wapo wanaosema kuwa kwasasa Ilala ndiyo jiji na wengine ni Manispaa ndani ya Jiji la Dar es Salaam. Katika kuelewa jambo hili kuna mambo ya kuyafahamu. Mosi, kabla ya jana, Dar es Salaam kama mkoa ulikuwa na Halmashauri za Manispaa tano: Ilala, Kinondoni, Ubungo, Temeke na Kigamboni. Halafu, kulikuwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambalo kinadharia lilijumuisha Manispaa zote hizo.
Pili, hadhi ya juu kabisa ya kihalmashauri ni Jiji. Tatu, jana likavunjwa lililokuwa Jiji la Dar es Salaam (kwa maaa ya kuondolewa kwa iliyokuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam). Zikabaki Halmashauri za Manispaa tano. Moja ya Manispaa hizo-ya Ilala ikapandishwa hadhi kuwa Halmashauri ya Jiji na 'kubatizwa' jina la Dar es Salaam. Sasa kuna Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambayo kimsingi ni iliyokuwa Hamlmashauri ya Manispaa ya Ilala.
Ndiyo kusema, Jiji la Dar es Salaam kwasasa ni sehemu yote ya Wilaya ya Ilala na si vinginevyo. Wilaya za Kinondoni, Temeke, Ubungo na Kigamboni si sehemu ya jiji la Dar es Salaam. Hizo zimebaki kuwa Halmashauri za Manispaa. Katika kueleweka zaidi, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ya sasa imepakana na Halmashauri za Manispaa za Kinondoni, Temeke, Ubungo na Kigamboni. Kwahiyo, mtu wa Ubungo, Temeke, Kinondoni na Kigamboni hayupo ndani ya Jiji la Dar es Salaam.
Wapo wanaosema kuwa kwasasa Ilala ndiyo jiji na wengine ni Manispaa ndani ya Jiji la Dar es Salaam. Katika kuelewa jambo hili kuna mambo ya kuyafahamu. Mosi, kabla ya jana, Dar es Salaam kama mkoa ulikuwa na Halmashauri za Manispaa tano: Ilala, Kinondoni, Ubungo, Temeke na Kigamboni. Halafu, kulikuwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambalo kinadharia lilijumuisha Manispaa zote hizo.
Pili, hadhi ya juu kabisa ya kihalmashauri ni Jiji. Tatu, jana likavunjwa lililokuwa Jiji la Dar es Salaam (kwa maaa ya kuondolewa kwa iliyokuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam). Zikabaki Halmashauri za Manispaa tano. Moja ya Manispaa hizo-ya Ilala ikapandishwa hadhi kuwa Halmashauri ya Jiji na 'kubatizwa' jina la Dar es Salaam. Sasa kuna Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambayo kimsingi ni iliyokuwa Hamlmashauri ya Manispaa ya Ilala.
Ndiyo kusema, Jiji la Dar es Salaam kwasasa ni sehemu yote ya Wilaya ya Ilala na si vinginevyo. Wilaya za Kinondoni, Temeke, Ubungo na Kigamboni si sehemu ya jiji la Dar es Salaam. Hizo zimebaki kuwa Halmashauri za Manispaa. Katika kueleweka zaidi, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ya sasa imepakana na Halmashauri za Manispaa za Kinondoni, Temeke, Ubungo na Kigamboni. Kwahiyo, mtu wa Ubungo, Temeke, Kinondoni na Kigamboni hayupo ndani ya Jiji la Dar es Salaam.