Ufafanuzi tafadhali

Ufafanuzi tafadhali

Gurta

JF-Expert Member
Joined
Sep 17, 2010
Posts
2,233
Reaction score
532
1. Simu yangu imeibiwa
2. Nimeibiwa simu yangu.
3. Simu yangu imeibwa.
 
Sentensi zote tatu zina maana inayo lingana kimaana katika hali ya mazoea, na utofauti wake upo katika maumbo (mofolojia) au mpangilio wa maneno pekee, hata hivyo sentensi namba 1, ina utata kwa msomaji au msikilizaji kwa maana kwamba inaweza maanisha simu ilikuwa na kitu fulani inachokimiliki, ie. yaweza kuwa ni programau au vyovyote na imeibiwa (imetolewa) kutoka katika simu hiyo. Hivyo simu ndiyo iliyoingia hasara kwa kuibiwa kifaa au programu yake iliyokuwa ikimiliki. Hivyo basi, kwa mtazamo wangu sentensi hii hutumika kimazoea zaidi na si kwa kuzingatia utaalamu na mintalafu ya lugha, hususani lugha ya kiswahili.
Hivyo kwa maelezo hayo ni dhahiri kuwa sentensi #2 n#3 ndizo tungo sahihi zaidi kuelezea tukio la wewe kuibiwa simu yako, na hiyo #1, hutumika katika hali ya mazoea ya kutumia lugha, na inamakosa kimantiki na kisarufi.
MAOMBA KUWASILISHA....
 
1. Simu yangu imeibiwa
2. Nimeibiwa simu yangu.
3. Simu yangu imeibwa.

# 1 wakati uliopita lakini si jana wala juzi "kama dakika 5-10"
#2 tukio limetokea sasa hivi
#3 tukio limitokea jana ama zaidi ya jana

P.S ni maoni yangu ......
 
Sentensi zote tatu zina maana inayo lingana kimaana katika hali ya mazoea, na utofauti wake upo katika maumbo (mofolojia) au mpangilio wa maneno pekee, hata hivyo sentensi namba 1, ina utata kwa msomaji au msikilizaji kwa maana kwamba inaweza maanisha simu ilikuwa na kitu fulani inachokimiliki, ie. yaweza kuwa ni programau au vyovyote na imeibiwa (imetolewa) kutoka katika simu hiyo. Hivyo simu ndiyo iliyoingia hasara kwa kuibiwa kifaa au programu yake iliyokuwa ikimiliki. Hivyo basi, kwa mtazamo wangu sentensi hii hutumika kimazoea zaidi na si kwa kuzingatia utaalamu na mintalafu ya lugha, hususani lugha ya kiswahili.
Hivyo kwa maelezo hayo ni dhahiri kuwa sentensi #2 n#3 ndizo tungo sahihi zaidi kuelezea tukio la wewe kuibiwa simu yako, na hiyo #1, hutumika katika hali ya mazoea ya kutumia lugha, na inamakosa kimantiki na kisarufi.
MAOMBA KUWASILISHA....

big up! excellent! bravo! n many mo .....100%
 
uko sawa sawia...ulichonena hapa ni sahihi sina cha kuongezea
Sentensi zote tatu zina maana inayo lingana kimaana katika hali ya mazoea, na utofauti wake upo katika maumbo (mofolojia) au mpangilio wa maneno pekee, hata hivyo sentensi namba 1, ina utata kwa msomaji au msikilizaji kwa maana kwamba inaweza maanisha simu ilikuwa na kitu fulani inachokimiliki, ie. yaweza kuwa ni programau au vyovyote na imeibiwa (imetolewa) kutoka katika simu hiyo. Hivyo simu ndiyo iliyoingia hasara kwa kuibiwa kifaa au programu yake iliyokuwa ikimiliki. Hivyo basi, kwa mtazamo wangu sentensi hii hutumika kimazoea zaidi na si kwa kuzingatia utaalamu na mintalafu ya lugha, hususani lugha ya kiswahili.
Hivyo kwa maelezo hayo ni dhahiri kuwa sentensi #2 n#3 ndizo tungo sahihi zaidi kuelezea tukio la wewe kuibiwa simu yako, na hiyo #1, hutumika katika hali ya mazoea ya kutumia lugha, na inamakosa kimantiki na kisarufi.
MAOMBA KUWASILISHA....
 
1. Simu yangu imeibiwa
2. Nimeibiwa simu yangu.
3. Simu yangu imeibwa.

#1. Kuna kitu kilicho ibwa toka kwenye simu. Labda imeibiwa line au memory card ama credit! Hebu badili neno "Simu" kuwa "kaka, dada, mjomba, mpangaji, mtoto nk kisha weka "a" kwenye "i" ya kitenzi 'imeibiwa'
#2 & 3 Ina maana wewe ndo ulio ibiwa simu.
 
Back
Top Bottom