Ufahamu kuhusu nyota za angani

Ufahamu kuhusu nyota za angani

Kama nilivyo ahidi ifuatayo ni ile nyongeza.

Nyota zinazaliwaje?
Kabla ya nyota kuzaliwa inaanza kama sayari ya kawaida wakati vumbi na hewa (sana sana hydrogen) ikijikusanya. Kadri hii hewa na vumbi vinavyoongezeka basi gravity nayo pia inaongezeka. Tukichukulia ukubwa/uzito wa jua letu kama kiwango (solar-mass) basi mkusanyiko wowote ule wa vumbi na hewa chini ya 0.013 solar-mass (1.3% ukubwa wa jua letu) hiyo itakuwa ni sayari (planet) tu. Kuanzia ukubwa wa 0.08 solar-mass na kuendelea gravity inakuwa kubwa sana (kilo moja hapa duniani ukiipeleka huko itakuwa na uzito wa kilo bilioni 100 na zaidi). Huu mgandamizo mkubwa wa gravity unafanya joto kupanda zaidi ya nyuzi milioni 15 celcius. Hili joto na mgandamizo wa gravity ndio kibiriti kinachofanya hydrogen ichanganyike ketengeneza helium na kutoa nguvu hizi za nyuklia (fusion). Hivi ndio jua linavyozaliwa.

Nyota zinakufaje?
Maisha ya nyota yanategemea sana na ukubwa wake. Nyota ndogo zinaishi muda mrefu sana (zinachoma hydrogen yake taratibu taratibu) kuliko nyota kubwa. Kwa mfano, nyota ndogo kama jua letu inategemewa kuwaka kwa miaka bilioni 10 wakati nyota kubwa sana kama Betelgeuse zinategemewa kuwaka kwa miaka million 10 tu.

Wakati nyota inawaka kunakuwa na uwiano (equilibrium) wa nguvu ya gravity na nyuklia. Gravity inakandamiza chini wakati milipuko ya nyuklia inasukuma vitu nje. Uwiano huu unaendelea hata baada ya hydrogen ikiisha. Baada ya hydrogen kuisha helium nayo italipuka kinyuklia kutengeneza Carbon na Oxygen. Baadae carbon nayo italipuka kunyuklia kutengeneza iron (chuma). Mara tu nyota inapoanza kutengeneza chuma (iron), mchezo umekwisha. Chuma ni kama maji yanayouzima huu mlipuko wa nyuklia mara moja. Milipuko ya nyuklia ikiacha, ule uwiano (equilibrium) wa gravity na nyukilia unakuwa haupo tena na gravity inashinda. Kila kitu huanguka chini na mlipuko mkubwa sana wa mwisho hutokea na mwanga mkubwa sana (super nova) huonekana.

Vitu viwili vinatokea wakati wa hii super nova. Kwanza, madini nzito zaidi ya chuma (iron) yanatengenezwa kama vile dhahabu, urani, nk. Hii ndio maana dunia yetu pamoja na sisi tunaitwa vumbi la nyota (star dust) kwa saababu kama hizi super nova zisingetokea basi dunia yetu na sisi tusingekuwepo. La pili linaliotokea baada ya kishindo (collapse) ni kuwacha tumba (core) ndogo sana lakini yenye uzito (density) mkubwa wa ajabu. Hii tumba ndio ijulikanayo kama BLACK HOLE.

(For correctness sake, not all stars die and turn into black holes. For instance, our sun is too small to turn into a black hole. When it dies it will collapse into a dense core with properties nowhere close to those of black holes)

Black holes na makaburi ya nyota.
Black holes zinazotokea baada ya nyota kubwa sana (super massive stars) ku-collapse ni vitu vya ajabu sana. Chupa moja ya bia (ujazo wa 0.5 lita) ya hii black-hole ina uzito wa zaidi ya tani 3,000,000,000,000. Gravity inayotokana na hizi black holes ni kubwa kiasi ya kumeza kitu chochote kile (majua, sayari, nk) kinachoikaribia. Hii gravity ni kubwa kiasi cha kumeza hata mwanga (even light cannot escape it) na ndio maana zinaitwa BLACKHOLE kwa sababu hazionekani (mwanga pia unamezwa). Kuwepo wa black hole kunajulikana tu kwa vitu inavyovimeza au vinavyo izunguuka. Usiku ukitoka nje angalia juu. Ukiona ukanda wa nyota nyingi basi huo ndio mkusanyiko wetu wa nyota (Galaxy yetu) unaoitwa MILKYWAY. Katikati ya hi
i galaxy yetu lipo hili black hole moja ambalo jua letu na nyota nyingine zote zilizopo kwenye hii galaxy yetu zinalizunguuka. Ukitaka kujua hii blackhole yetu iko wapi angalia juu na kama unaijua constellation ya Virgo basi usawa huo ndipo lilipo.

Natumaini hii itasaidia pa kuanzia katika kuzijua nyota.

cc. Mwamba028, 2013 Globu
Iron Lady
Asante, elezea pia kuhusu Galax yetu ni kitu gani?
 
Mkuu nilikuwa na google Leo lakini cha kushangaza naambiwa kutoka duniani mpk Venus ni mbali zaidi kuliko kutoka duniani mpk kwenye jua hii imekaaje
Fikiria watu wawili mnaizunguka nyumba. Kama wewe uko mbele ya nyumba na mwenzio yuko nyuma ya nyumba basi umbali kutoka kwako hadi kwenye nyumba ni mdogo kuliko umbali toka kwako hadi kwa mwenzio.

Sasa hivi Venus iko upande mmoja wa jua na sisi tuko upande mwengine wa jua. Kwa hiyo Venus iko mbali sana kutoka hapa duniani kuliko jua lilivyo.
 
Ni kweli jua ndiyo nyota kubwa kuliko zote kwenye mfumo wetu wa jua (solar system) ambao una sayari 9 tu. Nyota unazoziona zinang'aa ziko mbali mno, wala haziko kwenye mfumo wetu huu wa kwetu, yaani ziko nje ya solar sytem. Jirani ya mfumo wetu, yaani jirani yetu aliye karibu sana na mfumo wetu wa jua (hayuko kwenye mfumo wetu) ni nyota inayoitwa alpha centauri, ambaye yuko umbali wa unaokadiriwa kuwa 4.4 light years kutoka hapa kwenye mfumo wetu wa jua, kwa maana kwamba umbali huo, ni umbali ambao ukiwa na ndege au chombo kingine chochote kile chenye uwezo wa kutembea kwa kasi ya km laki3 kwa sekunde moja (300,000km per second), au sawa na roundtrip zaidi ya 10 za kutoka Dar kwenda Mwanza (na kurudi), au zaidi ya 20 za Dar Mwanza, kwa sekunde moja tu, kinaweza kuchukua muda wa miaka 4.4 kufika kwa jirani yetu nyota ya alpha centauri ambaye ndiyo jirani aliye karibu zaidi na sisi. Mbali na hayo, jirani yetu kwenye galaxy yetu, yaani galaxy ambayo iko karibu sana na sisi kwenye universe inaitwa andromeda na iko umbali unaokadiriwa kufikia 2,000,000 light years (miaka-mwanga millioni mbili). Hii ndiyo galaxy iliyo karibu sana na sisi, hakuna nyingine ambayo ni jirani na sisi kuzidi hii. Hata hivyo, the entire universe ambayo ina millions of galaxies, inasemekana kwamba inatanuka kwa kiwango cha mara 300 trillion trillion kwa sekunde moja,..., jaribu ku-imagine hii scenerio, yaani possibly naweza kufananisha na kitu kilicho kidogo size ya mchanga kiwe kinatanuka na kuwa size ya tuseme, Tanzania nzima (mfano) kwa sekunde moja, halafu mtindo huo huo ndiyo uendelee kwa kutanuka namna hiyo kila umbile linalopatikana kila baada ya sekunde moja, you can imagine how incomprehensible the size of the universe is. Unaona maajabu haya ya ulimwengu huu tunaoishi? Who's behind all these mystical, miraculous and adventurous actions and creations? Are they really by coincidencial, randomly unorganised forces only? Really no thanks!
Ndugu yangu kusema ukweli mimi kuna kipindi nilikuwa naamini kuwa Mungu yupo, sasa hivi siamini tu ila pia nimeshahakikisha kwa evidence ambazo siwezi kuziprove kwa mtu mwingine, na hivyo nakusihi wewe uamini kuwa Mungu yupo and there is a day utahakikisha kama mimi nilivyohakikisha. You believe by hearing, you prove by seeing or experiencing. Kitu kikishakuwa knowledge maana yake kimeshadevelop beyond faith level!
Kuna sayari waliyoigundua miezi michache iliyopita ndani ya mwaka huu wakisema kuna uhai na akajitokeza tajiri mmoja kutengeneza chombo kitakachokuwa na speed ya mwanga ili kufika huko. Hiyo ndiyo iko karibu na solar system?
 
Fikiria watu wawili mnaizunguka nyumba. Kama wewe uko mbele ya nyumba na mwenzio yuko nyuma ya nyumba basi umbali kutoka kwako hadi kwenye nyumba ni mdogo kuliko umbali toka kwako hadi kwa mwenzio.

Sasa hivi Venus iko upande mmoja wa jua na sisi tuko upande mwengine wa jua. Kwa hiyo Venus iko mbali sana kutoka hapa duniani kuliko jua lilivyo.
Nimekupata mkuu
 
Kuna sayari waliyoigundua miezi michache iliyopita ndani ya mwaka huu wakisema kuna uhai na akajitokeza tajiri mmoja kutengeneza chombo kitakachokuwa na speed ya mwanga ili kufika huko. Hiyo ndiyo iko karibu na solar system?
Hapana. Hayupo anayeweza kutengeneza chombo kinachoweza kusafiri kwaa spidi ya mwanga. Mwanga unasafiri kilometa laki tatu kwa sekunde moja (300,000km/s), mwendokasi ambao chombo hicho kinaweza kwenda na kurudi kati ya Dar es salaam na Bukoba mara 15 ndani ya sekunde moja tu!
 
Majibu ni kama yafuatayo:

Vipi kuhusu wanasayansi je huwa wanakwenda anga za mbali au hutumwa vyombo tu?
Kati ya hapa duniani na mwezi wetu binaadamu wamesafiri sana. Hata hivi sasa kuna wanasayansi kadhaa kwenye kituo cha utafiti angani (International Space Station) wakiendelea na tafiti zao. Kituo hiki siku zote kina watu. Huwa wanabadilishana tu mara kwa mara.

Nilisikia kujengwa kwa vituo vya utafiti wa anga huko kwenye sayari nyengine je ni kweli?
Ni kweli lakini kwa sasa hakuna kituo chenye binaadam. Nitakupa mifano michache ya vyombo vya tafiti vilivyokwenda kwenye sayari.

Mars: Safari za kwenda Mars zilianza tangu 1960. Nyingi zilipeleka vyombo kupitia tu au kuizunguuka. Sasa hivi kuna magari 2 (Rovers zilizotua 2003 na 2011) yaliotua na kuendelea na utafiti. Lengo ni kuona kama baadae wanaweza kujenga kituo cha kudumu ili watu waende.

Saturn: Mwaka 2004 chombo kiitwacho Cassini-Huygens kilifika Saturn. Cassini kinaizunguuka hii sayari hata leo. Mdogo wake Huygens kilitua kwenye mwezi mmoja wa Saturn uitwao TITAN na kuona kuwa unafanana sana na dunia yetu na kuwa una mito, maziwa na mvua. Lakini mvua hii sio ya maji bali ya Methane (methane ni hewa hapa kwetu lakini ni kama maji kule kwa ajili ya baridi kali)

Kuna vyombo vingi sana vilivyopelekwa angani. Vingine vinazunguuka sayari, vingine vinatoswa ndani ya sayari kuona kuna nini, na vingine vinaendelea tu kusafiri na kuna vinavyotoka sasa kwenye solar system yetu lakini bado vinawasiliana nasi.

Vifaa na vyombo vinavyokuwa huko vinatumia power source ya aina gani?
Vyombo vyote viendavyo angani hasa kama vimepangiwa kwenda masafa marefu vinatumia vyanzo viwili vya nishati.

  • Kwanza vinakuwa na solar panels kutengenezea umeme kutokana na mwanga wa jua.
  • Lakini chanzo cha muhimu sana kwa vyombo hivi ni nguvu za nyuklia. Hivi vyombo vinakuwa na nuclear reactors zinazotengeneza umeme na kuutumia moja kwa moja au kuuhifadhi kwenye batteries. Chanzo hiki cha nishati ni muhimu sana hasa ikifikia kuwa chombo kiko mbali sana na jua mpaka jua kuonekana kama nyota tu.
Kuna uhai kwenye huu mwezi unaofanana na dunia yetu?
 
Hapana. Hayupo anayeweza kutengeneza chombo kinachoweza kusafiri kwaa spidi ya mwanga. Mwanga unasafiri kilometa laki tatu kwa sekunde moja (300,000km/s), mwendokasi ambao chombo hicho kinaweza kwenda na kurudi kati ya Dar es salaam na Bukoba mara 15 ndani ya sekunde moja tu!
Duh mpk nimeogopa hiyo speed yake.
Lakini si kuna kule wamarekani walikituma kwenda Pluto walisema na karibiana kidogo speed na speed ya mwanga hicho kilikuwa kinaenda kilometers ngapi kwa sec?
 
Duh mpk nimeogopa hiyo speed yake.
Lakini si kuna kule wamarekani walikituma kwenda Pluto walisema na karibiana kidogo speed na speed ya mwanga hicho kilikuwa kinaenda kilometers ngapi kwa sec?
Hakijazidi 30,000km/h...........speed ya mwanga hata 10% bado hutajaweza kufikia
 
Mbona hamna cha ajabu hapo,ikumbukwe jua ni nyota ambayo ipo kwenye mzunguuko wa sayari zetu na mojawapo ya hizo sayari ni hio Venus,kwahio yes it is possible .

Jua ndio nyota pekee ilio karibu na sayari zilizo ktk mzunguuko wetu na pamoja na sayari yetu pia earth
 
Sasa hivi ikifika jioni wakati jua linazama ukiangalia magharibi utaona nyota inayowaka sana kabla ya nyota nyingine kutoka. Hii sio nyota bali ni sayari ya Venus. Na asubuhi kukipambazuka kuna nyota (ya mwisho kufifia) inayowaka sana mashariki, hii siyo nyota bali ni sayari ya Mercury.
Mi nilidhani tofauti ya sayari na nyota ni uzalishaji wa energy.
Kwamba nyota inajitegemea na sayari inategemea mwanga kutoka kwenye nyota!!
 
Mi nilidhani tofauti ya sayari na nyota ni uzalishaji wa energy.
Kwamba nyota inajitegemea na sayari inategemea mwanga kutoka kwenye nyota!!
upo sahihi mkuu, nyota inatengeneza energy yake yenyewe lakini sayari hazitengenezi energy zao ili kutoa mwanga ile yote ni reflection kutoka kwenye mwanga wa jua

Mfano sayari ya venus ambayo ina ng'aa sana usiku,mng'ao ule unatokana na anga ya venus kuwa na mawingu mazito yenye asidi ya sulphuric, ile sulphuric asidi ikikutana na gas inatengeneza crystals ambazo ni highly reflective

Kwa hiyo mwanga wa jua ukipiga kwenye venus asilimia 70 una bounce na ndio maana tunaiona venus ina ng'aa sana usiku
 
upo sahihi mkuu, nyota inatengeneza energy yake yenyewe lakini sayari hazitengenezi energy zao ili kutoa mwanga ile yote ni reflection kutoka kwenye mwanga wa jua

Mfano sayari ya venus ambayo ina ng'aa sana usiku,mng'ao ule unatokana na anga ya venus kuwa na mawingu mazito yenye asidi ya sulphuric, ile sulphuric asidi ikikutana na gas inatengeneza crystals ambazo ni highly reflective

Kwa hiyo mwanga wa jua ukipiga kwenye venus asilimia 70 una bounce na ndio maana tunaiona venus ina ng'aa sana usiku
Unataka kusema kuwa sio sababu ya ukaribu wetu na hiyo sayari ......???
 
Mi nilidhani tofauti ya sayari na nyota ni uzalishaji wa energy.
Kwamba nyota inajitegemea na sayari inategemea mwanga kutoka kwenye nyota!!
Ni sawa ulichosema. Lakini kama mwezi unavyotoa nuru kutoka kwenye jua ndiyo hivyo Venus, Mercury, na sayari zote tuzionazo angani hutoa nuru ya jua inayotua kwenye uso wake.

Ukiangalia kwa makini utaona nyota zote mwanga wake unameremeta (twinkle) lakini sayari mwanga wake haumeremeti.
 
Unataka kusema kuwa sio sababu ya ukaribu wetu na hiyo sayari ......???
Ukaribu unasaidia pia, lakini acidic cloud iliyocover Venus ndio sababu kuu kabisa inayofanya venus iwe na mwanga mkali vile

Mfano mwezi pale ulipo una reflect asilimia 12 tu ya mwanga wa jua ila kwa kuwa mwezi upo karibu zaidi ndio maana una ng'aa sana

Ingekuwa mwezi nao una acidic cloud au una reflect 70% ya mwanga wa jua kama venus, mwezi ungekuwa una ng'aa sana, ila kuwa mwezi hauna atmosphere wala clouds yeyote ile ni miamba tu ndio maana hau reflect mwanga mwingi wa jua

Ila kama venus ingekuwa karibu na dunia kama ilivyo kwa mwezi ingekuwa ina ng'aa sana kama vile mwanga wa mchana ulivyo
 
Ukaribu unasaidia pia, lakini acidic cloud iliyocover Venus ndio sababu kuu kabisa inayofanya venus iwe na mwanga mkali vile

Mfano mwezi pale ulipo una reflect asilimia 12 tu ya mwanga wa jua ila kwa kuwa mwezi upo karibu zaidi ndio maana una ng'aa sana

Ingekuwa mwezi nao una acidic cloud au una reflect 70% ya mwanga wa jua kama venus, mwezi ungekuwa una ng'aa sana, ila kuwa mwezi hauna atmosphere wala clouds yeyote ile ni miamba tu ndio maana hau reflect mwanga mwingi wa jua

Ila kama venus ingekuwa karibu na dunia kama ilivyo kwa mwezi ingekuwa ina ng'aa sana kama vile mwanga wa mchana ulivyo
Nimekusoma,vipi bro we unaamini ipo siku binadamu anaweza kuunda chombo cha kutembea kwa spidi ya mwanga .......???
 
Hivi sayari ya Venus na nyota ya Sirius IPI inangaa sana?
 
Nimekusoma,vipi bro we unaamini ipo siku binadamu anaweza kuunda chombo cha kutembea kwa spidi ya mwanga .......???
speed ya mwanga hatuwezi kufikia close na speed ya mwanga tunaweza tukafikia yaani speed ya 177,000 miles/ second ambapo kwa speed tukisema tukitume chombo kwenye alpha centauri( nyota iliyokaribu na mfumo wetu wa jua itatuchukua miaka 5 tu ila kwa kutumia chemical energy spacecraft itachukua zaidi ya. miaka 50,000 kufika kwenye hiyo nyota

sasa kazi ipo kwenye kutengeneza anti matter space vehicle

Mpaka sasa wanasayansi wameweza kutengeneza anti matter ambayo inafikia uzito wa nanograms 18

zimetengenezwa pale fermilab tevatron particle accerelator ni 15 nanograms,CERN ( 1 nanogram) DESY(Germany) 2 nanograms

Hicho kiwango cha antimatter kilichotengezwa mpaka sasa hivi dunia nzima nishati yake haiwezi hata kuchemsha kikombe cha chai, nanogram ni ndogo sana

1 gram ya anti matter inaweza kutengeneza mlipuko kama wa nuclear bomb
Kutengeneza gram 1 ya anti matter inahitajika 25 million billion kilowatt of energy na ina cost million billion dollars
Labda descendants wetu miaka ijayo wataweza kutengeneza anti matter

anti matter ikikutana na matter ya kawaida inatengeneza kiasi kikubwa cha energy, cosmic rays wanasayansi wanasema zina anti matter

Prolpusion system nyingine ambayo inaweza kufikia speed ya light ni warp drive ila bado sijaijua vizuri na bado ni science fiction kizazi hiki hatauweza kutengeneza

Labda mkuu kifyatu aje atuelezee wrap drive kama anaijua kiundani
 
Back
Top Bottom