BlackPanther
JF-Expert Member
- Nov 25, 2015
- 9,185
- 8,715
Napoangaliaga angani wakati wa usiku huwa naona nyota zingine ambazo hazina mwanga wa rangi moja,yan inabadilika badilika mara nyekundu,kijan,bluu.
Je hizi nyota ni za aina gani? mana kuna mtu katika stori za utoto alinambia eti zile ni satelaiti
Pia nyota chanzo chake cha mwanga ni kipi?
Karibuni wadau wa Sayansi ya anga
Mkuu unaweza ukanifafanulia kuhusu Virgo?Ni maji tu (bahari) yaliyoganda
Kuna tofauti Kati ya sayansi ya Shule ya msingi, secondary Hata vyuoni na exploration, Nivea umekariri sayansi ya Shule ya msingi. Pole sanaUkichunguza utakuta Huyu ni mwalimu anayefundisha taifa la kesho.
VIRGO ni mkusanyiko wa nyota (constellation) unaofananishwa na mwanamwali alieshika mashuke ya ngano na wanajimu wa zamani. Hii ndio sababu ya huu mkusanyiko pia huitwa MASHUKE na wanajimu wa kiswahili.Mkuu unaweza ukanifafanulia kuhusu Virgo?
Madhumuni ya vyombo hivyo ni nini? Vimeenda kutafiti nini? Vimelenga kwenda sehemu moja au vinazunguka tu kupiga picha?Kwa sasa hatuweza kushuhudia tatizo kubwa ni kwamba mtu hawezi kupona na hizo radiation zilizopo kwenye outer space na vile vile chance ya kurudi duniani ni ndogo sana na wakiwa kwenye hicho chombo wanaweza kuwa machizi sababu watakuwa wamekaa sehemu moja ndogo kwa muda mrefu
Ila kupeleka chombo peke yake mpaka sasa hivi tumeweza kuna chombo kinaitwa voyager 1 and voyager 2 vimeishika toka nje ya solar system yetu, vilipelekwa angani mwaka 1977 na vitaendelea na safari mpaka itakapofika mwaka 2025,vimeisha tembea billions of kilometres kuna kipindi viliiona dunia kama kidoti kidogo cha blue, ila kwa sasa sidhani kama vinaiona dunia maana vipo mbali sana
Mkuu hapa umeeleza mambo makubwa sana mawili, hilo la radio signal sijalielewa na huo muda wa hizo signal mbona sijaelewa? Hiyo signal madhumuni yake ni nini? Na hao Aliens uliowataja wanategemewa wapatikane wapi ili wakione chombo hicho?Kwa sasa wanaanga wana madhumuni mengi tu, ila kubwa moja wapo ambalo wanalipigania ni kuweka space base kwenye mwezi,na pia kuweka camp na kuanzisha makazi kwenye sayari ya mars,na wameanza na hilo kwa ku tengeneza kituo cha utafiti maarufu kama international space station ( ISS) huko wanaanga wanafanya majaribio mengi yakiwepo binadamu atawezaje kuishi kwenye zero gravity,mimea itawezaje kukua kwenye zero gravity
Huwezi jua huenda kukawa na uhai kwenye mifumo mingine ya nyota maana kuna nyota nyingi sana, na kila nyota ila planet zake huenda kukawa na uhai somewhere wanaanga bado wanaendelea kufanya utafiti,voyager 1 na 2 zilivyotumwa mwaka 1977 zilikuwa na details kuhusu sisi ikiwepo DNA structure yetu na location ya solar system yetu ili endapo kama kuna aliens huko wakikiona chombo hicho au kikienda kuangukia sehemu walipo wapate hizo details na watutafute
Kuna mwaka wanaanga waliiona sayari moja siikumbuki jina lake ila. walituma radio signals ziende kwenye sayari wanasema ina possibility yakua na uhai, ila hizo signal zitachukua takribani miaka 25,000 kufika kwa hiyo kama tutapata majibu basi ni miaka mingi ijayo
Vimelenga kuuchunguza ulimwengu, binadamu kama binadamu ni muhimu kujua mazingira yanayotuzungukaMadhumuni ya vyombo hivyo ni nini? Vimeenda kutafiti nini? Vimelenga kwenda sehemu moja au vinazunguka tu kupiga picha?
Yani ni hivi wanaanga katika uchunguzi wao waliona kuna sayari inaweza kuwa na uhai ndani yake, yani kuna viumbe wanaishi sasa kwa kuwa sayari iko mbali sana na kuifikia kwa technology tuliyonayo sasa haita wezekana sababu sayari ipo umbali wa miaka 25,000 ya mwangaMkuu hapa umeeleza mambo makubwa sana mawili, hilo la radio signal sijalielewa na huo muda wa hizo signal mbona sijaelewa? Hiyo signal madhumuni yake ni nini? Na hao Aliens uliowataja wanategemewa wapatikane wapi ili wakione chombo hicho?
Popote pale chombo kitapo angukia baada ya mwaka 2025Yani ni hivi wanaanga katika uchunguzi wao waliona kuna sayari inaweza kuwa na uhai ndani yake, yani kuna viumbe wanaishi sasa kwa kuwa sayari iko mbali sana na kuifikia kwa technology tuliyonayo sasa haita wezekana sababu sayari ipo umbali wa miaka 25,000 ya mwanga
yani kama ukituma chombo chenye speed sawa na ya mwanga itachukua miaka 25,000 kufika kwenye hiyo sayari
wanaanga hao wakatuma radio signal kwenda kwenye hiyo sayari ili kama kuna viumbe wapate hizo signal na wajue kwamba kuna viumbe wengine sehemu fulani
Mfano labda hapa duniani itokee siku tupate signal kutoka anga za mbali kabisa, lazima tutajua kama kuna viumbe wengine wapo mahali fulani ndio wanatuma hizo signals ili tufahamiane lakini mpaka sasa hicho kitu hakijawahi kutokea, zaidi zaidi huwa tunapokea signals ambazo ziliachwa na mlipuko wa bing bang signal za bing bang zinapatikana kwenye TV za zamani zile hasa za chogo unapo washa zile chenga za makelele za mwanzo
mmh haya mambo kweli yana Mungu ndani yake maana huo mpangilio full complet
Mkuu Kifyatu kwa hapa umeniacha kabisa, hilo la kutozeeka sijakuelewa naomba ufafanuzi wa kina.Ilivyo ni kuwa kadri unavyokaribia kasi ya mwanga ndio ukuaji wako unavyozorota kutokana na contraction of space. Sasa kama ulimuacha pacha wako hapa duniani na kusafiri kwenye space kwa kasi ya mwanga, ukirudi hapa pacha wako atakuwa amezeeka kuliko wewe. Ukisafiri katika kasi ya mwanga basi kwako wewe muda (time) unasimama. Kama umesafiri kwa miaka 30 (ya hapa duniani) ukirudi utakuwa kama ulivyoondoka na kila uliemuacha atakuwa amezeeka kwa miaka 30.
Mkuu hili ndilo somo gumu zaidi kulielewa tangu nianze kujifunza physics na mathematics. Yaani sijui utanieleweshaje nielewe. Yaani chombo kiundwe kitakachotumia speed ya mwanga na kuweza kusafiri kwa kwa dakika 5, umbali ambao ningesafiri kwa miaka 30 kama ningetumia kifaa cha kawaida. Then baada ya dakika tano kuisha nikirudi nikute miaka 30 imepita? Inawezekana kweli?Imethibitika kisayansi kuwa ukisafiri kwa kasi kubwa basi aging process yako inazoroto. Na ukisafiri kwa kasi ya mwanga basi ukuaji wako unasimama kabisa .
Kwa hiyo ukisafiri masafa marefu ambayo yangekuchukua miaka 30 kwa kutumia dakika 5, wewe ndie utakaeona umetumia dakika 5 lakini sisi uliotuacha hapa tutaona umekwenda kwa miaka 30. Ukirudi, umri wako utakuwa umeongezeka kwa dakika 5 wakati sisi hapa duniani umri wetu utakuwa umeongezeka kwa miaka 30. Hii ndio maana ya traveling into the future.
Mkuu hili ndilo somo gumu zaidi kulielewa tangu nianze kujifunza physics na mathematics. Yaani sijui utanieleweshaje nielewe. Yaani chombo kiundwe kitakachotumia speed ya mwanga na kuweza kusafiri kwa kwa dakika 5, umbali ambao ningesafiri kwa miaka 30 kama ningetumia kifaa cha kawaida. Then baada ya dakika tano kuisha nikirudi nikute miaka 30 imepita? Inawezekana kweli?
Hivi katika ulimwengu kuna majini mapepo na mizimu, tunaviweka kwenye kundi gani hivi viumbe? Kuna tofauti gani na hao Aliens?Sikua nimeliona hili swali lako la jana.
Kuhusu aliens hata mimi nina shauku sana kujua ukweli uko wapi. Wacha hatua tulizopiga kitaaluma tangu 1950 lakini ukiangalia maajabu kama ya pyramids na accuracy ya ujenzi wake, technolojia za waMayans, Einstein alikuwa anaota nini mpaka kutuletea mahesabu yake ya relativity, nk. Utaona mara kwa mara kunakuwa na mlipuko wa elimu mpya inayotokea na inayotusogeza mbele kitaaluma na sijui ni kwa nini.
Mkuu inawezekana hata wewe na shauku zako za kujua mambo inawezekana unakamkono ka hawa aliens (jokes).
Mimi niko open kabisa kujuzwa kuhusu hawa eliens.
- Pengine ni malaika?
- Au ndio mkono wa Mungu mwenyewe?
- Hivi ni kweli katika universe yote hii hakuna viumbe wenye kufikiri na maarifa kama au zaidi ya sisi?
- Pengine aliens tunao lakini hatuwaoni (sio carbon-based kama sisi)?
- Inawezekana kuwa wanatubadilisha (wanatuumba) kwa kutufanyia genetic-mutations (kama jua letu linavyotufanyia) badala ya genetic cross-overs (yaani kuzaa na sisi) kama tunavyozaana?
Maswali ni mengi mkuu. Kuna mengi hatuyajui na ndio maana sipuuzii dhana yoyote ile nitakayoisikia.
Nyota ni jua na jua ni nyota....NYOTA ni kama jua lakini ziko mbali sana na dunia kushinda jua.NYOta ni kubwa kushinda jua.
Kuna nyota ni kubwa kuliko jua letu....ili tusichanganye watu. Our sun is also a star ikiwa na maana kama tutakuwa umbali wa zaidi ya 1 light year... basi jua letu litaonekana dogo sana kama tuonavyo nyota za mbali.Mkuu jua ndio nyota kubwa kuliko zote. So a sun is a star too
Msaada zaidi: just google ''Sun"
Mi nawaza hapo ndipo jehenam ya milelemkuu me naamini hapo kwenye black hole ndio source ya kila kitu,na pengine Mungu ndipo anapoishi