Ufahamu kuhusu nyota za angani

Ufahamu kuhusu nyota za angani

Tuanze hapa: Muda (time) ni relative na speed yako. Kadri speed inavyoongezeka ndio muda (Time) wako unavyozorota (slow-down). Dhana ni kuwa ukisafiri katika speed ya mwanga basi muda (au umri) wako unasimama ukilinganisha na uliowaacha duniani. Kwa hiyo ukirudi duniani wewe utakuwa kama ulivyoondoka (ki-umri) lakini dunia na watu wake watakuwa wamezeeka. Kwa hiyo wewe utakuwa unaona mambo ya siku za mbele ukilinganisha na umri wako (travel to the future). Hii ya kuwa ukisafiri kwa kasi umri wako unazorota imekwisha thibitishwa kisayansi kwa kuwatumia astronauts.

Sasa mkwara unakuja hapa. Kinadharia, kama utaweza kusafiri kwa kasi zaidi ya speed ya mwanga, basi muda (time) wako sio tu kuwa unasimama bali utakuwa unarudi nyuma (travel back in time). Tatizo hapa ni kuwa ukiweza kufanya hivyo na kukutana na wazazi wako walipokuwa watoto na ukaweza kuwaua, je wewe umepatikanaje. Hii ndio paradox ya kusafiri into the past.

Kwa maoni yangu ni kuwa kusafiri into the past haitawezekana. Sababu ya kwanza ni kuweza kusafiri kwa kasi kubwa zaidi ya kasi ya mwanga. Sababu ya pili ni hicho kiini-macho cha kuweza kubadilisha historia (mfano, umuue Hitler alipokuwa kichanga).

Mkuu travelin in to the future ina athiri vip umri wako wakati utakuwa umesafiri umbali mrefu kwa muda mfupi na kurudi? Kwa mfano Sehemu uliyokuwa usafiri kwa miaka 30 unasafiri kwa dakika tano kwenda na kurudi ita athiri vipi umri wako?
 
Mkuu travelin in to the future ina athiri vip umri wako wakati utakuwa umesafiri umbali mrefu kwa muda mfupi na kurudi? Kwa mfano Sehemu uliyokuwa usafiri kwa miaka 30 unasafiri kwa dakika tano kwenda na kurudi ita athiri vipi umri wako?
Imethibitika kisayansi kuwa ukisafiri kwa kasi kubwa basi aging process yako inazoroto. Na ukisafiri kwa kasi ya mwanga basi ukuaji wako unasimama kabisa .

Kwa hiyo ukisafiri masafa marefu ambayo yangekuchukua miaka 30 kwa kutumia dakika 5, wewe ndie utakaeona umetumia dakika 5 lakini sisi uliotuacha hapa tutaona umekwenda kwa miaka 30. Ukirudi, umri wako utakuwa umeongezeka kwa dakika 5 wakati sisi hapa duniani umri wetu utakuwa umeongezeka kwa miaka 30. Hii ndio maana ya traveling into the future.
 
Imethibitika kisayansi kuwa ukisafiri kwa kasi kubwa basi aging process yako inazoroto. Na ukisafiri kwa kasi ya mwanga basi ukuaji wako unasimama kabisa .

Kwa hiyo ukisafiri masafa marefu ambayo yangekuchukua miaka 30 kwa kutumia dakika 5, wewe ndie utakaeona umetumia dakika 5 lakini sisi uliotuacha hapa tutaona umekwenda kwa miaka 30. Ukirudi, umri wako utakuwa umeongezeka kwa dakika 5 wakati sisi hapa duniani umri wetu utakuwa umeongezeka kwa miaka 30. Hii ndio maana ya traveling into the future.

Mmhh hii bado ngumu kumeza mkuu..japo nimekuelewa vizuri..bado nahisi ni kuaminika zaidi ya uhalisia
 
Mmhh hii bado ngumu kumeza mkuu..japo nimekuelewa vizuri..bado nahisi ni kuaminika zaidi ya uhalisia
Mkuu, dhana ya kusafiri into the past ni ya kusadikika lakini kusafiri into the future inawezekana.

Fikiria hivi: Kama leo tukikugandisha (cryogenically) na kukuweka kwenye freezer kwa miaka 30. Tukikugandua (na ukiwa mzima) basi umri wako utakuwa uleule uliokuwa nao wakati ulipogandishwa (miaka 30 iliopita) wakati sisi tutakuwa tumezeeka kwa miaka 30. Kwa mantiki hii, ukiganduliwa utakuwa umesafiri into the future kwa sababu kila kitu kitakuwa miaka 30 older kuliko wewe.

Sasa kusafiri kwa kasi ya mwanga kuna effect kama ya cryogenics. Sio kwa kugandisha bali kwa kuzorotesha au kusimamisha muda.

Kugandishwa kwa cryogenics hutumika kila siku kuhifadhia mayai na mbegu za kiume za binadamu, au vimelea hai vinginevyo (bacteria, viruses). Kwa hiyo hii sio nadharia tena.
 
Mkuu, dhana ya kusafiri into the past ni ya kusadikika lakini kusafiri into the future inawezekana.

Fikiria hivi: Kama leo tukikugandisha (cryogenically) na kukuweka kwenye freezer kwa miaka 30. Tukikugandua (na ukiwa mzima) basi umri wako utakuwa uleule uliokuwa nao wakati ulipogandishwa (miaka 30 iliopita) wakati sisi tutakuwa tumezeeka kwa miaka 30. Sasa kasi ya mwanga ina effect kama ya cryogenics. Sio kwa kugandisha bali kwa kuzorotesha au kusimamisha muda.

Kugandishwa kwa cryogenics hutumika kila siku kuhifadhia mayai na megu za kiume za binadamu, au vimelea hai vinginevyo (bacteria, viruses). Kwa hiyo hii sio nadharia tena.

Duuh...mkuu unadhan teknolojia inaweza kuja kutengeneza chombo kinachokaribia light speed?
 
mkuu Kifyatu samahan naomba kufunzwa kuhusu hili
hivi kama mambo yoooooote kama nyota,sayari,galaxies etc vipo ndani ya universe,sasa je hiyo universe imo ndani ya nn? je nje ya universe kuna nini? nawaza mpaka nahisi kuwehuka
 
Duuh...mkuu unadhan teknolojia inaweza kuja kutengeneza chombo kinachokaribia light speed?
Nafikiri itawezekana. Lakini hata kama ukisafiri kwa kasi ya nusu ya speed ya mwanga umri wako utazorota, ikimaanisha utasafiri into the future japokuwa ni kidogo.

Ukisema travel into the future watu wanapata shida kuelewa lakini sio tatizo. Nimekupa mfano wa cryogenics. Tukiweza kukugandisha na cells zako zikabaki dormant kwa mwaka mmoja, tukikugandua utakuwa umesafiri into the future kwa mwaka mmoja. Sasa kama kasi inaweza kuzorotesha ukuaji wako, huko ndio kunakoitwa "traveling into the future".
 
nyota ni ndogo sana kuliko dunia, ni kama mwezi. zinategemea mwanga wa jua. na nyota ulizoona zinazobadilika kutoka rangi kutokea ya blue kwenda ya kijani ni kutokana na kuzibwa na miti na bahari .na ukiona nyekundu ujue hapo kuna radi na mvua inanyesha.

duh, no comment
 
mkuu Kifyatu samahan naomba kufunzwa kuhusu hili
hivi kama mambo yoooooote kama nyota,sayari,galaxies etc vipo ndani ya universe,sasa je hiyo universe imo ndani ya nn? je nje ya universe kuna nini? nawaza mpaka nahisi kuwehuka
Mkuu sasa ndio umefikia ukingoni walipo wanasayansi. Maswali kama, Je:
  • Kuna universe zaidi ya moja?
  • Kuna universe sambamba na hii yetu?
  • Inasemekana universe yetu inapamba kasi kutanuka - mwisho wake ni nini?
  • Big-bang ilikuwa ni mgongano wa universe mbili?
  • n.k.
Hapo ndio utamu wa sayansi unapoanza. Unakuwa na shauku ya kufanya utafiti wa haya madudu mpaka unawehuka.

Karibu ulingoni. Sina jibu la swali lako lakini nimelipenda sana.
 
mkuu Kifyatu samahan naomba kufunzwa kuhusu hili
hivi kama mambo yoooooote kama nyota,sayari,galaxies etc vipo ndani ya universe,sasa je hiyo universe imo ndani ya nn? je nje ya universe kuna nini? nawaza mpaka nahisi kuwehuka


nimejaribu na Mimi kufanya research kdg lakini inaonekana hakuna kitu kinaitwa ' nje ya universe'

soma hapa

The Universe is all of time and space and its contents. [9][10][11][12] The Universe includes planets, natural satellites , minor planets , stars ,
galaxies, the contents of intergalactic space, the smallest subatomic particles , and all matter and energy . The observable universe is about 28 billion parsecs (91 billion light-years ) in diameter at the present time.[3] The size of the whole Universe is not known and may be either finite or infinite. [13] Observations and the development of physical theories have led to inferences about the composition and evolution of the Universe.
 
Mkuu Kifyatu nlisoma sehem kwamba galaxy zinaendelea kupanuka kwa speed kubwa kuliko speed ya risasi...je kuna phenomenon yoyote kwamba kuna possibility galaxy zikaja collide??...je ikitokea nini kitatokea maana kila galaxy ina black hole
 
Mkuu Kifyatu nlisoma sehem kwamba galaxy zinaendelea kupanuka kwa speed kubwa kuliko speed ya risasi...je kuna phenomenon yoyote kwamba kuna possibility galaxy zikaja collide??...je ikitokea nini kitatokea maana kila galaxy ina black hole
Universe yetu (pamoja na galaxies) inatanuka kwa kasi kubwa sana. Sasa sijui tunakwenda wapi.

Galaxies kugongana ni kitu cha kawaida sana. Zile gravitational vibrations tulizozungumzia awali zilitokana na blackholes za galaxies 2 kugongana. Galaxy yetu (milkway) iko mbele-kwa-mbele kuelekea kugongana na galaxy ya karibu iitwayo Andromeda. Zikigongana basi blackholes zake zitaungana na sio lazima solar system yetu iathirike isipokuwa tukipona basi nyota angani zinaweza kubadili positions zao (kazi kwao watabiri wa nyota).

Hapa chini ni simulation ya mgongano wa Milkway na Andromeda.

Andromeda–Milky Way collision - Wikipedia, the free encyclopedia
 
Nia ya mada hii ni kuuweka muda na matukio kwa ufupi sana kama wataalamu wanavyouona ili tujifunze na kutafakari kwa akili zetu tunapochanganya na ufahamu kutoka vyanzo tofauti. Binafsi huu si msimamo wangu bali uchunguzi katika vyanzo ambavyo vipo siku zote kwenye vitabu, machapisho, digital information sources, habari za kuambiwa au kusikia, kujifunza na kadhalika. Kama tulitokea kwa bahati basi tuione bahati hii kwa upana wake na kama tulikusudiwa tutokeaa basi tuone kusudio hilo lilivyo na nguvu za kipekee kwa kuangalia matukio yanayoelezewa na wataalam wa fani husika.<br /><br />Pia katika kuupitia muda na matukio tunayoambiwa yalitokea na yatatokea, tunaweza kuona jinsi tulivyo muhimu au tusivyo muhimu katika muda huu mrefu wenye mambo makubwa yaliyotokea na yatakayotokea na hivyo kuufanya wakati huu kuwa wa kipekee sana. <br /><br /><b>Muda ni nini?<br /></b><br />Ni swali zito na la zamani sana kabla sisi wote hatujazaliwa tayari wataalam wa fani mbali mbali wamejaribu kulijibu kwa upeo wa juu sana. Bado swali hili lipo tu kwa kuwa bado tunaendelea kujifunza jinsi ulimwegu ulivyo na unavyofanya kazi. Na hasa ukitaka kufafanua muda ni nini ugumu unakuja lakini kila mtu hata mtoto mdogo anauona muda kwa namna yake mwenyewe. Hivyo kila mtu kwa nafasi yake anaweza kuu-define muda kwa maana kila mtu anau-experience na analo jambo fulani linalomfanya auone muda kwa namna yake. Sitajikita katika kutafuta maana ya muda inayokubaliwa na wengi kwa kuwa kuna majibu mengi sana kutoka kwenye dhana tofauti na hiyo si mada hii ila nitajikita katika kuangalia matukio na tofauti ya muda wake kwa kuwa ndio yanatupa ule mstari wa kufikirika wa muda wenye past, present and future.<br /><br />Kumbuka muda tumeamua wenyewe (binadamu) kuuweka katika vipimo (sekunde, dakika, mwaka etc) hivyo kuujengea kitu kama mstari ulionyooka katika fikra zetu. Kwamba mstari huu una uelekeo mmoja na sasa tuko katikati yake (tulipo) na yale yaliyopita yanajipanga upande mmoja wa tulikotoka na yajayo ambayo hatujayafikia yanajipanga katika upande mwingine wa mstari wa tunakoelekea.<br /><br />Matukio yanayo/yatakayo na yaliyotokea yanatupa uelewa wa muda uliopita, wa sasa na ujao. Kitu cha kukumbuka na cha ajabu ni kwamba mstari huu wa muda (arrow of time) wala haupo katika zile sheria za msingi za physics na wala hauna muunganiko wowote na sheria hizi. Hivyo mstari huu wa muda ni katika ufahamu wetu na uwezo wa kuuona au kuufikiri kwa kuangalia matukio hivyo ni wa kufikirika au psychological arrow. Tusiuchanganye na thermodynamic arrow na cosmological arrow hizi zinasimama kama dhana tofauti na sio mada yetu kwa sasa. <br /><br /><b>Muda kwa kuangalia tangu kutokea kwa ulimwengu (universe)<br /></b><br />NOTE. Kumbuka hapa baadhi ya maeneo theories, hypothesis na phenomena zenye ushawishi zinatumika. Wataalam wa theoretical phyisics, na Astrophicists wanashika hatamu hapa.<br /><br /><b>Umri wa sayari ya Dunia na Jua<br /></b><br />Wataalam hawa wanatuambia umri wa jua na dunia umekaribiana wakiwa na maana kuna tofauti ya miaka milioni 60. Lakini muda huu si kidogo kwetu sisi binadamu ambao dakika zinatumika hata kwenye misemo ya kila siku. Kama unakumbuka ule wa "Nipe dakika mbili tu ntakua hapo"<br /><br />Jua lilitokea katika wingu kubwa la gesi mbali mbali miaka bilioni 4.6 iliyopita (4.6 Ga). Baada ya hapo dunia ikatokea/tengenezwa kutoka kwenye mabaki ya milipuko ile ya gesi iliyokuwa iliyotengeneza jua. Baada ya hapa kikafuata kipindi kigumu sana ambacho dunia imewahi kupitia (<i>Hadean Eon</i>). Joto kali na lava katika uso wote wa dunia pamoja na milipuko mingi sana na kugongwa na mamilioni ya vimwondo, miale na mawe makubwa. Na hypothesis moja inasema katika kipindi hiki cha <i>Hadean Eon</i> ndipo mwezi ulipotokea baada ya dunia kugongwa na kitu kizito sana ambacho kinadhaniwa kuwa sayari ndogo au dwarf planet. Mkusanyiko wa mapande ya mawe, vumbi na madini yaliyosababishwa na mgongano huu wa dunia na aina fulani ya sayari ndogo ndio ulioutengeneza mwezi. Kumbuka ni process za muda mrefu sana hizi mamilioni ya miaka. Kipindi hiki cha Hadean Eon kinakadiriwa kuchukua takribani miaka bilioni moja(1 Billion) mpaka pale hali ya hewa ilipoanza kutulia taratibu na dunia kupoa.<br /><b><br />Umri wa Ulimwengu (Universe)<br /></b><br />Umri wa ulimwengu au universe unakadiriwa kutokana na ile theory ya Big Bang kuwa ni miaka bilioni 13.8 toka mlipuko huo mpaka sasa. Hivyo toka jua li-form kutoka kwenye mawingu fulani ya gesi na baadae dunia mpaka sasa. <br /><br /><b>Mwisho wa Jua<br /></b><br />Na kama ulidhani muda unavyoenda mbele ndio mambo yanakuwa mazuri basi kaa vizuri uone muda ukiangaliwa huko mbeleni predictions za future zikoje. Baada ya miaka bilioni nane jua litapanuka mara 250 ya sasa na hivyo kumeza dunia na sayari zote. Lakini kabla ya hapo ndani ya miaka milioni mia nane (800yrs) kiwango cha carbondioxide kitashuka chini kabisa na kuisha na hii ina maana hakutakuwa na photosythesis na hivyo kukosekana kwa oygen ambayo ndio chanzo muhimu cha uhai. Baada ya miaka bilioni moja miale ya jua itakuwa mikali sana na kufanya maji yote katika dunia ya-evaporate na kupotelea anga za mbali.<br /><br /><b>Kabla ya universe<br /></b><br />Wataalam wanatuambia hata muda ulizaliwa hapo hivyo kabla ya Big bang hakukuwa na muda. Mvurugano na mraruano uliopo ni kwamba hakuna theory yoyote nzuri inayoendana na uwezo wa akili ya mwanadamu kwa hili. Lakini si kwamba hazipo theory zinazojaribu kueleza nini hii kitu inayoitwa "kabla ya Big Bang".<br /><br />Albert Eisten katika "<i>theory of relativity</i>" yeye anafafanua wazi jinsi muda ulivyozaliwa na kabla ya hapo muda ulikuwa umesimama au kwa lugha nyingine hauendi mbele wala nyuma. Na katika kipindi hiki ulimwengu mzima (universe) ulikuwa kitu kimoja kidogo sana zaidi ya sub-atomic particle yani huwezi kukiona hata kwa microscope.<br /><br /><i>Inflation theory </i>inasuggest kuwepo kwa universe nyingine iliosababisha hii tuliyomo wakati ile ya multiverse au chaotic inflationary ikipendekeza kuwepo kwa universes nyingi kama bubbles zisizohesabika na hii ya kwetu ni mojawapo. Kuna ile ya "Extra dimensional membranes" (<i>branes</i>), <i>White holes</i>, Our universe being inside a big black hole na models nyinginezo katika kujaribu kutafuta jibu lenye ushawishi. <br /><br /><b>Wakati ujao wa ulimwengu (universe)<br /></b><br />Baada ya jua kulipuka na kutoweka ama kuwa kitu kingine tofauti muda unaoendelea mbele ni wa kutisha na kusikitisha sana. Hapa sasa tunauangalia muda kwa kipindi kirefu sana kiasi kwamba namba zinazotumika kwa makadirio ili tuuone mwisho wa universe ni trillions za miaka (T).<br /><br />Baada ya muda wa kati ya miaka trilioni moja na trillioni mia (1-100T) nyota zitaacha kuumbika au ku-form katika pande zote za ulimwengu mzima. Kumbuka nyota zinakufa na kuzaliwa kila siku kwa sasa. Baada ya kati ya miaka trilioni 110 na 120 (110-120T), nyota ya mwisho kabisa kuwepo inaishiwa nishati yake na kuzima/kufa. Baada ya miaka 10^10 [SUP]76 [/SUP], matter katika ulimwengu au universe sasa imeliwa yote na black holes na ndiyo yamebakia yakiranda-randa na kumezana/kuungana.<br /><br />Baada ya miaka 10^10[SUP]120[/SUP] nishati yote katika ulimwengu(universe) imeisha hivyo hamna chochote kinachofanyika tena popote pale na inaitwa "Heat Death" wala haieleweki vizuri au mimi siielewi vizuri lakini ni model mojawapo yenye ushawishi kwa sasa.<br /><br /><b>Hitimisho:<br /> </b><br />Kutokana na information hizi za hawa wataalam, binadamu wa kawaida mwenye lugha na utamaduni (modern human) amekuwepo miaka 62,014 tu katika ulimwengu wenye miaka bilioni 13.8. Hii ni asilimia 0.000449% tu ya muda wote tangu kuanza kwa universe. <br /><br />Na wataalam hawa wanamaanisha kwa lugha nyepesi - katika muda huu mrefu na matukio yake chini ya sheria za kifizikia zilizojiweka zenyewe au zilizowekwa umefanya baadhi ya zile gas zijiangalie, zijitambue na kuanza kuulizana na kubishana zilitoka wapi na muda uendavyo mbele(kama unaenda mbele) imagine gas hizi zitafanya nin??.
Mada yake inajitegemea toka kwa @monstagala
Tafadhali kifyatu mchango wako
 
Mkuu neo1 bandiko lako lina mambo mengi sahihi na mengine ni dhana. Hali hii ndio inayoifanya sayansi iwe tamu.

Nikupe mfano mdogo sana. BIG-BANG ni dhana tu na pengine sio kweli. Hii kuwa mlipuko ulitokea kutoka kwenye chembe ndogo sana (Singularity) ni kiini macho tu. Ukimsikia mwana sayansi anasema "SINGULARITY" basi ana maana "SIJUI NINACHOSEMA". Katika mahesabu ya mtanuko wa universe, ukifikia mwanzo mwa universe (yaani ukirudi nyuma) basi hesabu zinashindikana. Wakati wowote katika kukokotoa mahesabu kama utapata jibu kuwa ni NUMERATOR gawanya kwa SIFURI basi hiyo ndio Singularity. Hiki ndicho kinachotokea ukifanya mahesabu ya chanzo cha universe.

Kwa hiyo kusema ni nini kilikuwepo kabla ya Big-bang ni dhana tu na hakuna anaejua kwa uhakika. Ni vizuri kutafiti dhana tofauti (big-bang theory, string au M theory, n.k.) lakini kutafiti inamaanisha hujui kitu. Mara nyingi hii admission ya kuwa hujui inakupa mwanya au uhuru wa kujifunza mengi kutoka kwa watu wenye mtazamo tofauti - kama dini.

Muda (Time):
Kwa maoni yangu muda (time) ulikuwepo siku zote, na siku zote unakwenda mbele tu. Mtu anesafiri kwa kasi ya mwanga basi ni yeye, na yeye pekee ndie anaezorota ukuaji wake hivyo kwamba akirudi kwetu sisi tunakuwa tumezeeka lakini yeye ni kijana kama alivyoondoka. Anakuwa amedumaa wakati akisafiri katika kasi ya mwanga. Haimaanishi amekwenda mbele in time bali aliporudi amekuwa na umri alioondoka nao miaka 30 au 50 iliopita.

Kuna mengi ya kujifunza mkuu. Nimefurahi tu kuona watu kama wewe mkiwa na shauku ya kujua haya mambo. Mie pia ninajifunza mengi tu hapa jukwaani.
 
Ngoja nikupe mfano mmoja. Nyota ya karibu na sisi (Alpha Centauri) iko 4.4 light years kutoka hapa. Ina maana tunapoiangalia tunaona vitu vilivyotokea zamani (miaka 4.4 iliopita).

Sasa kama tungeweza kwenda kwa kasi ya ajabu na kufika kwenye hii nyota na kurudi mara moja, ina maana tungeona vitu ambavyo vitakujaonekana hapa duniani miaka 4.4 ijayo. Ina maana tutaweza kwenda into the future. Kuna katatizo kadogo tu hapa. Kwa sasa speed limit ya universe ni speed of light. Tukiweza kupata njia ya kusafiri kwa kasi kubwa zaidi ya speed of light basi usafiri kwenda future utawezekana.

Mkuu! hapa umenikanganya kidogo hivi ukitaka kwenda future uipite speed of light au uwe sawa na speed of light?
 
Mkuu! hapa umenikanganya kidogo hivi ukitaka kwenda future uipite speed of light au uwe sawa na speed of light?
Ukisafiri kwa kasi yoyote ile muda wako unatembea taratibu kuliko sisi tuliokaa. Ukiweza kusafiri katika kasi ya mwanga basi muda wako unasimama.

Ni kama uliegandishwa (yaani wenzio wanaendelea kukua lakini wewe unabaki na umri wako uleule). Kwa hiyo kama ukisafiri kwa kasi ya mwanga kwa miaka 50, kwako wewe utakuwa hujabadilika (itakuwa ni kama kufumba na kufumbua) lakini ukisimama (hapa duniani) basi itakuwa ni miaka 50 ya mbele. Uliotuacha hapa duniani tulikuwa tunapwaga tu kama kawaida na tunazeeka lakini wewe ulikuwa umedumaa na umri uleule ulioondokea nao. Hii ndio maana ya kusafiri into the future. Sasa kama kasi yako ni ndogo kuliko ya mwanga basi utazeeka lakini kwa rate ndogo kuliko uliotuacha.

Dhana ni kuwa ukiweza kusafiri kwa kasi kubwa kuliko kasi ya mwanga basi unaweza kurudi into the past. Hii sidhani kama itatokea au kuwezekana.
 
Back
Top Bottom