Ufanisi wa madaktari wa Tanzania umeshuka, tatizo ni nini?

Ufanisi wa madaktari wa Tanzania umeshuka, tatizo ni nini?

Hahaha hamna mzee ukisema uzembe maanake unataka kuishi duniani miaka 200 , sisi tunapambana kunusuru maisha ya wanadamu ila inapofika hatua tunamwachia alieko juu afanye yake
Labda nitumie neno mistakes

Mistakes zinafanyika sana hospitalini, katika kumtibu mgonjwa.

Daktari nae ni binadamu anafanya mistake kama watu wengine.
 
Mwishoni mwa mwaka jana nilipoteza mtoto(still born) kwa uzembe wa madaktari na wauguzi, hii imetokea kwenye hospital kubwa ya private inayosifika nchi hii. Ni uzembe ambao niliujua,mama mtoto aliujua na maDr wenyewe waliujua na kujua nimegundua uzembe wao. Nilitaka niwashtaki ila nikashauriwa niachane nao. Inasikitisha sana Dr anaesifiwa ndio bingwa wa mambo fulani anafanya uzembe hadi kupoteza maisha ya mtu. Nawaheshimu sana madaktari nchi hii ila inabidi tuwe makini.
Dah!...pole sana boss.

Hii sekta ya afya inahitaji usimamizi making sana.
 
Hivi madaktari wa siku hizi wana shida gani! mbona kama ni hawajui kitu tena!? Yaani siku hizi ukienda hospitali utapata tiba ya haraka kama unaumwa magonjwa yaliozoeleka kama malaria,typhoid, u.t.i nk lakini kama unaumwa kitu ambacho hakijazoeleka unaweza ukafia hapo wanakuangalia.

Yaani imefika mahala mtu ukiumwa unaona hakuna umuhimu wa kwenda hospitali kwasababu unajua kabisa utakavyoambiwa na dawa utakazopewa.

Na wamekuwa wabishi sana hata ukijaribu kuwaelezea ni jinsi gani unaumwa na unavyojisikia wao wanaconclude mambo yao fasta fasta bila kujali hali ya mgonjwa.

NIliwahi kupata tatizo linaitwa Acute Pancreatitis miaka ya nyuma, nikashauriwa kuwa atleast kila mwaka nifanye check-up ya kongosho ili nijue utendaji kazi wake kama upo sawa au la...ili nisije kupata complications za kufeli kwa kongosho kama kupata ugonjwa wa kisukari ambao tayari nishaupata.

Nilijaribu kila mara kwenda kwenye hosp tofauti tofauti mikoani hadi kwenye hosp za rufaa za baadhi ya mikoa lakini cha ajibu utakuta umemuelezea daktari aina ya tatizo ulilopata inakuwa ni kama unamfundisha na yeye hajui chochote, yaaani uwe na historia ya acute pancreatits halafu daktari anakuandika ukapimwe u.t.i.

Are these doctors serious! maana hata afya yangu ilipofikia madaktari pia wamechangia kunifikisha cos ningefahamika mapema kuwa kogosho yangu haijakaa sawa basi ningeanza mapema matibabu huwenda nisingepata kisukari.
Sidhani kama Kuna daktari hamsikilizi mgonjwa,ni wachache mno madaktari wenye tabia hizo,Kila daktari anajitahidi kuhudumia mgonjwa wake apone vizuri,Tena wengine hata ukiwapigia simu ukamweleza tatizo lako la kiafya anakupatia maelezo mazuri kitu Cha kufanya,sema labda ulikutana na Mmoja ambaye naye anamatatizi yake,sio madaktari wote .
 
Mwishoni mwa mwaka jana nilipoteza mtoto(still born) kwa uzembe wa madaktari na wauguzi, hii imetokea kwenye hospital kubwa ya private inayosifika nchi hii. Ni uzembe ambao niliujua,mama mtoto aliujua na maDr wenyewe waliujua na kujua nimegundua uzembe wao. Nilitaka niwashtaki ila nikashauriwa niachane nao. Inasikitisha sana Dr anaesifiwa ndio bingwa wa mambo fulani anafanya uzembe hadi kupoteza maisha ya mtu. Nawaheshimu sana madaktari nchi hii ila inabidi tuwe makini.

Pole sana Mkuu

Hii code kama naifaham hiv
 
Ni kweli hakuna kinachoshindika ila form failure waliopata alama D wanaishia uku uku level ya zahanati hawana nafasi zaidi ya hapo na ndio hao hao wanaozalisha matatizo sugu,,utakuta clinical officer au assistant clinical officer anatoa dawa kwa mtu ambaye hana history ya hypertension wala dalali za hypertension ghafla tu pressure ipo juu moja kwa moja anakurupuka anampa dawa za pressure hajacheck renal function test,liver,ecg,eco nk

Serikali/wizara ya afya inabidi iliangalie ili swala kwa makini sana afya za watu zipo hatarini
Da! Nikama yalionikuta. Nilipewa za
ikashuka haswa, nikapewa za kuipandisha, ikapanda kuwa karibu na normal . Nikajiuluza mbona mimi sina historia ya kuwa ma BP.
Mother akaniambya "babu yako alizitumia muda mrefu hatimae mishipa ikabast akafa" Nikaogopa na ikawa ndio mwisho wa kuzitumia mpaka sas nipo kawaida, nimegundua kumbe maumivu yapo kwenye misuli ya nje na sio ya ndani moyo.
Ukweli mwili wa binadamu unawasumbua sana madokta.
Tatizo langu nimepimwa hispitali tano + na kila mmoja katoa jibu lake tofauti na mwenzie, ie hawajawahi toa majibu yanayofanana., hospitali mojawapo iliniambia kuwa hawajaona chochote nikabaki kushangaa na kujouliza huyu physician yupo serious kweli!
 
Which hospital? Tuanzie hapo kwanza! Halafu waheshimu sana madokta, sawa? Isijekuwa umeenda kwa waganga sangoma, then unaleta stori nyingii.
Ujamuelewa mtoa mada au uelewa wako ni mashaka sana.
 
Sio udaktari tu nadhani sekta zote mambo hayako kama zamani na hii inatokana na kuangalia pesa kuliko vigezo vinavyotakiwa nenda muhas pale kuna watu wanasoma pale ila ufaulu wao haujakidhi vigezo vya kusomea udokta pesa yako tu ila ukienda kichwa kichwa unaambiwa hauna vigezo nadhani tatizo limeanzia hapo.
 
HONGERENI SANA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA YA MBEYA.



Wapendwa wana JF habarini za asubuhi?,Kama kichwa kinavyojieleza,Wiki iliyopita nilikwenda Hospitali ya Rufaa ya nyanda za juu kusini-Mbeya kwa lengo la kufanya Check up ya mwili mzima kutokana na kutojisikia vizuri,Ikumbukwe kuwa hiyo ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kwenda ktk hospitali hiyo.
Baada ya kuwasili hospitalini hapo nilipokelewa vizuri sana nikawa naelekezwa vizuri sehemu ambazo napaswa kupita,baada ya vipimo niligundulika na tatizo ambalo ilikuwa lazima kufanyiwa Upasuaji.Basi Daktari alinipa maelekezo kuhusu tatizo nililonalo, kisha akaniuliza ikiwa nipo tayari kufanyiwa operation siku ya pili asubuhi,nami nikakubali.
Baada ya kukubali kufanyiwa operation,nikalazwa;Nami nikaomba kuwekwa Wodi ya Private Usiku wote wakati Nasubiria kufanyiwa operation Madaktari walinitembelea na kunichukua vipimo mbalimbali na kunifariji kuwa nisiwe na wasiwasi kuhusu operation hiyoe.Ilipofika saa kumi na moja Alfajiri niliamshwa na kuambiwa kuwa nijiandae kwaajili ya operation,nikajiandaa kwaajili ya operation nikaenda Theater.Madaktari walinifanyia Operation kwa upendo mwingi huku Manesi wakinibembeleza kwa sauti nyororo, baada ya operation nikaanza kusikia maumivu makali lkn nilifarijiwa sana kwa huduma nzuri za Wataalamu wetu wa Afya.Nilipoanza kijisikia vizuri niliruhisiwa kurudi nyumbani,hivi sasa naendelea vema,bado natumia dozi ya dawa nilizopewa.

Hitimisho.
Binafsi nimevutiwa na kufurahishwa sana na huduma za Hospitali hii,kuna wakati nilimuuliza mke wangu aliyekuwa ananiuguza,"Hivi hii ni hospitali ya Private au ya Serikali?",Jibu likawa ni ya Serikali,niliuliza hivyo kutokana na kushangazwa na huduma zao bora sana.Hebu fikiria Daktari aliuenifanyia operation alinipigia simu saa nne usiku kuniuliza ninaendeleaje? Na akasema kupitia Namba yake hiyo nimpigie simu muda wowote ikiwa Kuna shida inanipata.Kwa kweli sikuona mhudumu aliyenijibu Vibaya au kutonijali.Ilifika wakati nikawaza kuwa ningekuwa Rais wa nchi hii ningeamuru Mshahara wa Watumishi wa wizara ya Afya uongezwe.Hongereni sana Madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Rufaa ya nyanda za juu kusini-Mbeya kwa Huduma yenu bora sana.Mwenyezi MUNGU awabariki sana.
 
Mods mnakera sana,sasa habari yangu kuhusu kuipongeza Hospitali ya Rufaa ya nyanda za juu kusini-Mbeya,inahusiana nini na Kushuka ufanisi wa Madaktari??.Dah mnakera sana.
 
Back
Top Bottom